Ijumaa, 23 Machi 2018

USIPOFANIKIWA KIUCHUMI KIPINDI KAMA CHA JPM BASI UTAJILAUMU SANA MBELENI!

[....Kwa wanafunzi wa mafanikio tu....]

USIPOFANIKIWA KIUCHUMI KIPINDI KIGUMU KAMA CHA JPM BASI UTAJILAUMU MBELENI!

Wiki takribani tatu ziliopita niko zangu mitaa ya Mlimani City mle ndani maeneo ya duka la vitabu pale nikakutana na rafiki yangu mjasiriamali anayejua maana ya kushikilia ndoto na maono kaka Prosper Mwakitalima. Kuonana kwetu ilikuwa bahati kwa kila mmoja wetu maana tulishapanga kuonana ili kubadilishana mawazo mara kwa mara lakini majukumu yakawa yanatubana lakini nahisi Mungu akaaamua atukutanishe tu kwa lazima, lol.

So salamu za hapa na pale na kutaniana kidogo then tukabadilishana mawazo kidogo na licha ya muda kuwa mfupi lakini conversation yetu ikaanza kuwa deep kidogo kadri tulivyozidi kuzungumza. Prosper ni mtu ambaye ukibarikiwa kuwa naye karibu hakika utagundua kuwa nchi hii imebahatika kuwa na vichwa adimu sana na very soon dunia italitambua jambo hilo.
Huwezi kuelewa ninachosema kama huna kawaida ya kukutana na watu wenye vichwa vilivyotulizana.

Tarehe 28 February niliandika Makala kuhusu umuhimu wa kuwa na AKILI ILIYOTULIA (possessing a quiet mind) kama unataka kufanikiwa. Pro ni mmoja wa watu wenye akili inayoweza kutulia katikati ya kelele. Mafanikio yake kwa kiasi kikubwa mno yanatokana na hilo.

So back to mimi na Prosper katika mambo niliyomuuliza ni anaonaje hali ya uchumi wa nchi kwa sasa. Prosper aliniangalia kwa  jicho kavu sana na bonge la smile na kusema very unapologetically, na namnukuu: “KAKA, USIPOFANIKIWA KIUCHUMI KIPINDI HIKI CHA JPM BASI HUENDA USIFANIKIWE KABISA TENA!”

Wow! What a powerful statement! Ni watu wachache mno nchi hii wanaoweka kuwa na guts tu za kukwambia kauli kama hiyo kipindi hiki.

Well mimi na Pro tulizidi kupeana tips mbali mbali za jinsi ya kufanikiwa fursa mbali mbali za kuwekeza, namna ya kuanza biashara haraka na kwa nini vijana wengi hawapigi hatua hata ndogo tu kuelekea mafanikio kiuchumi. Then tukaagana na kuahidiana kukutana tena kwa ajili ya "kikombe cha kahawa". Kaka Prosper, bado nakumbuka bro. Mbingu zinajua we have to meet again and again.

So kama nilivyosema ni wiki takribani tatu zimepita na nimetafakari sana kauli ile na kufikiria ni vijana wangapi wanaona na kusema kitu cha aina hiyo katikati ya makelele yanayoendelea hivi sasa katika taifa letu kuhusu uchumi kuwa mgumu. Nimefikiria na kuona jinsi gani vijana wengi wasivyoona kabisa kipindi hiki kama kipindi cha kufanikiwa kiuchumi bali wanachoona ni hali ngumu na kudorora kwa uchumi. Well Makala hii haikulazimishi kuona ninachoona mimi ama anachoona Prosper ama mtu mwingine. Ndiyo maana juu kabisa nimesema hii ni Makala kwa “Wanafunzi wa Mafanikio” na siyo kwa ajili ya any Tom, Dick and Harry. So una uhuru wa kuona unachokiona.

Lakini kwa wewe ambaye ni mwanafunzi wa mafanikio basi nakualika upitie machache hapa chini na kuzidi kujifunza mambo yanayoweza kubadili maisha yako hasa katika kipindi hiki kinachoitwa KIGUMU.

Hebu naomba tuanzie hapa.
Hivi unafahamu kitu kinachoitwa RIPOTI YA UTAJIRI DUNIANI ambayo hutolewa kila mwaka? Kama ndiyo mara ya kwanza unasikia kuhusu kitu hiki basi tambua kuwa ulikuwa umechelewa sana kujua jambo muhimu mno la kukusadia kuyaendea mafanikio yako. Mwalimu wangu wa mafanikio (my mentor) aliniambia kama nataka kufanikiwa basi nistop kusikiliza ripoti za vifo vingapi vimetokea, ajali ngapi zimetokea, na mambo mengine ya aina hiyo na badala yake nianze kujaza kichwani mwangu taarifa za mambo ya mafanikio na ripoti zinazozungumzia mambo ya mafanikio zaidi. Na namshukuru sana. Jambo hilo limenibadili share sana!

Sasa hii Ripoti ya Utajiri wa dunia ya kila mwaka hutolewa na Kampuni (firm) muhimu sana duniani iitwayo KNIGHT FRANK. Yafuatayo ni mambo machache kuhusu hali ya uchumi wa dunia kutokana na ripoti za kampuni hii kutoka mwaka 2012 hadi mwaka huu 2018 na projection zake hadi mwaka 2022. Na ninavyoandika Makala hii pembeni yangu kuna hiyo Wealth Report ya mwaka huu 2018 nimetoka kuipitia tena kwa mara nyingine.

Sasa ni hivi…

Kwa mujibu wa Kampuni hiyo ya Knight Frank, mwaka 2017 na 2018 utajiri wa mataifa ya Amerika, Asia na Ulaya Magharibi unashuka katika miaka hii miwili (japokuwa bado wako juu mno zaidi yetu licha ya kushuka kwao lakini wameshuka) na utajiri wa Mashariki ya Kati umebaki jinsi ulivyokuwa bali utajiri wa Urusi na bara la Afrika unakua kutoka 54% hadi 69% kwa nchi ya Russia na kutoka 57% hadi 76% kwa bara letu la Afrika. Sasa nikuulize. Wewe mwaka jana na mwaka huu ulikuwa unaona Afrika kama sehemu ambayo matajiri wanaongezeka?

Habari ndiyo hiyo. Sasa mpaka hapo bado una mawazo ya kukimbia Afrika ukaajiriwe Ulaya??
Think again.

Kwa upande wa Tanzania sasa, Ripoti ya mwaka 2012 ilionyesha kuwa Tanzania ilikuwa na mabilionea 160 tu. Yaani watu wanaoitwa dollar millionaires. Nataka ujifunze kitu muhimu hapa na uone kwa nini narudia sana kukukumbusha umuhimu wa kuwa na akili iliyotulia katikati ya kelele nyingi zinazoendelea. Soma kwa umakini sana nachosema hapa. Nimesema mwaka 2012 kwa mujibu wa ripoti ya mwaka huo ya Utajiri wa Tanzania kulikuwa na mabilionea 160 tu. Kumbuka kipindi hicho ndo Rais Kikwete ana miaka 7 madarakani na ndicho kipindi wanachosema watu kuwa hali ilikuwa nzuri.

Miaka mitatu baadaye wakati utawala wa Rais Kikwete unaondoka yaani mwaka 2015 mabilionea 30 zaidi walikuwa wameongezeka Tanzania na kufikia idadi ya mabilionea 190.

So wakati JPM anaingia madarakani kulikuwa na mabilionea takribani 190 hivi. Sasa mwaka mmoja tu baadaye yaani 2016 Tanzania ilikuwa na mabilionea 210. Ni kama mabilionea wapya 20 ndani ya mwaka mmoja tu wa utawala wa JPM. Je wewe ulikuwa unahisi unaongezeka kiuchumi au hapana.

Nadhani ukisoma ripoti kama hizi kama akili yako haijatulia unaweza kuona ni propaganda za kisiasa. How come mabilionea waongezeke wengi hivyo katika kipindi ambacho uchumi tunaambiwa unashuka kwa kasi?

Lakini kama umeshtuliwa na idadi hiyo ya mabilionea wapya wa mwaka 2016 basi jiandae kushtuka zaidi. Maana Wealth Report ya mwaka jana 2017 inaonyesha kuwa mwaka jana pekee mabilionea wapya waliozalishwa Tanzania walikuwa 40 ndani ya mwaka mmoja tu wa 2017!!! Yaani ni wengi mno ndani ya mwaka jana tu kuliko miaka miaka minne ya utawala wa Rais Kikwete ambapo wewe unasema ati hali ilikuwa nzuri.

Again how come watu wote hao 40 kuwa mabilionea wapya kwa mwaka ambao tunaambiwa hali ilikuwa mbaya na uchumi unakaribia kufa? Hapo ndo maneno ya rafiki yangu Prosper yanapo-make sense. Na point yangu hapa ni kwamba ukiendelea kulalamika na kulaumu na kusubiri mambo yabadilike utendelea kushangaa ripoti za aina hii kila mwaka.

Projection zinaonyesha kuwa kufikia mwaka 2022 yani miaka minne tu ijayo basi idadi ya mabilionea Tanzania itakuwa watu 460 kutoka 250+ wa sasa. Kwa maana hiyo kuna watu kama 200 siyo mabilionea sasa hivi lakini ndani ya miaka minne ijayo watakuwa mabilionea. Bado unasikiliza story za uchumi unakufa? Ngoja nikupe mfano. Hoteli ya Landmark Ubungo ilibadilisha operation ikawa Hostel na watu wakasema unaona uchumi unakufa? Lakini baadaye kidogo ikarudina kuwa hoteli tena na hakuna aliyesema kuwa swali uchumi unakua. Swali ni je huyu mwenye hoteli ni mjinga?  No. Ni kawaida kubadili biashara. Huku sikia mwenye mabasi ya Sumry  aliuza yote na sasa yuko serious kwenye kilimo? Jifunze kufanya utafiti binafsi. Inakufanya uone vitu visivyoonekana.

Sasa watu 200 kuwa mabilionea wapya ndani ya miaka minne ijayo. Na wewe si angalau uwe milionea wakati huo?

Lakini tatizo unapenda kulisha akili yako habari za umbea na maandamano na kusahau kuwa una nafasi ya kutuliza akili na kusaidia jamii yako kwa kufanikiwa ndani ya miaka tajwa hii na ukaweza kutoa ajira na kusaidia wasiojiweza. Habari unazopenda kufatilia ni nani katoa wimbo gani na kwa nini hajamshirikisha nani. Kweli?
Eti nani kahamia chama fulani na je amehama au amenunuliwa? Again nazungumza na mwanafunzi wa mafanikio. Hayo mambo ya umbea na maisha ya watu hayapaswi kuwa sehemu ya fikra zako na muda wako hata kidogo. Unapaswa kutumia muda wako kusoma vitabu na kupata taarifa sahihi kuhusu mambo ya mafanikio yako. Hizo habari zingine zinachelewesha mno juhudi zako za mafanikio. Najua si rahisi kuziacha lakini jitenge nazo na utaanza kuona utakavyopiga hatua haraka na kuanza kuona fursa  nyingi mno za mafanikio zilizokuzunguka mpaka utajiuliza kama ulikuwa kipofu zamani au?

Nikasoma ripoti moja hivi karibuni iliyosema mauzo ya hisa katika soko la hisa na Dar es Salaam yani Da es Salaam Stock Exchange (DSE) yalipanda kutoka hisa laki 7 hadi hisa milioni 3 ndani ya wiki moja kutokea tarehe 9 Machi hadi tarehe 16 Machi na kusababisha mauzo yatoke Tsh milioni 518 hadi Bilioni 5 ndani ya wiki hii moja. So wakati wewe unasubiri kujua hatma ya maandamano kama yapo au hayapo unahangaika kutafuta nani anasapoti na nani anapinga wenzako wanahangaika kusubiri hisa zao kama zinapanda bei wauze wapige pesa wakawekeze kwenye miradi mbali mbali. Halafu ukisikia mabilionea wanaongezeka unapanic na kubisha.

Jiulize ulikuwa unajua habari hizo za soko la hisa kufanya vizuri hivyo? Kipindi taarifa hizo zinatolewa kipindi hicho hicho kuna taarifa za polisi wamemkamata nani sijui msanii gani analalamika sijui uchawi umetokea wapi watu sijui wakawaje. Sasa wewe nawe unakuta upo na hizo habari. No huwezi fanikiwa.

My friend wewe ni mwanafunzi wa mafanikio. Zingatia kuwa una muda mchache sana wa kuishi hapa duniani na uutumie tu kwa mambo ya msingi yanayohusiana na hatma ya maisha yako. Na kama una mpango wa kufanikiwa basi huna luxury ya kufatilia umbea hata kidogo. Narudia, kama una mpango wa kufanikiwa kiuchumi basi huna luxury ya kufatilia umbea hata kidogo. Don’t fool yourself na kutaka kufurahisha ubongo wakati mafanikio hayawezi kuja bila kuusumbua ubongo. Haiwezekani kichwa cha Bakhresa kinasumbuka kuwaza azalishe nini zaidi na auze nini au abuni biashara gani mpya halafu wewe cha kwako kinawaza nani kakamatwa au nani kaachiwa au nani anataka kuandamana au nani anapinga maandamano halafu unataka na wewe uwe kama Bakhresa. Jambo hilo linawezekanaje?
Hebu kuwa serious.

Gazeti la THE GUARDIAN la Jumapili ya tarehe 11 mwezi huu Machi liliandika tena FRONT PAGE habari za ripoti hii ya Utajiri ya Knight Frank ya mwaka huu 2018 hasa kwa Tanzania. Lakini ni watanzania wangapi wenye kujua kusoma kiingereza wanaopenda kufatilia habari kama hizi. Wewe unayesema hujui kiingereza haya haya hapa nimekuewekea kwa Kiswahili sasa usijesema hukuwa na hizo taarifa.

Kwa mujibu wa gazeti hilo (The Guardian Jumapili 11 Machi) likinukuu ripoti kwa sehemu na pia kutoa observation yake lilisema kuwa Matajiri wakubwa Tanzania hawafiki 20. Yaani watu wenye utajiri wa $50 milioni na zaidi (Bilioni 110 na kuendelea), Hawafiki 20 nchi hii na kwamba idadi yao itaendelea kuwa ndogo hivyo hivo kwa miaka mitano ijayo. Miongoni mwa waliotajwa katika kundi hili ni:

Mohamed Dewji
Said Salim Bakhresa
Rostam Aziz
Reginald Mengi
Ally Awadh (Lake Oil Group)
Shekhar Kanabar (Synarge Group)
Shubash Patel (Motisun Group)
Ghakib Said Mohamed (GSM Group)
Fida Hussein Rashid (Africarriers Group)
Salim Turky (Turky’s Group of Companies)
Yogesh Manek (MAC Group)
Abdulaziz Abood (Abood Group)
Haroon Zakaria (Murzah Oils)

(Watoto wa UFALME mpo?)

Ewe mwanafunzi wa mafanikio kiuchumi ulikuwa unajua majina mangapi katika haya?

Unadhani watu hawa wanapitisha taarifa gani katika vichwa vyao kila siku?
Nataka kukupa challenge kidogo. Unadhani taarifa ulizonazo wewe kichwani ndizo hizo hizo walizo nazo wao pia?
So ukianza kufikira hivi vitu hutapata kamwe muda wa kupoteza kujadili mambo yasiyo na tija katika safari yako ya mafanikio kiuchumi. Nimejaribu kwa siku kadhaa kuandika makala hii toka nionane na kaka Prosper lakini nimekuwa natingwa na shughuli mbali mbali lakini ikabidi sasa nisimamishe shughuli zingine nikuandikie wewe rafiki yangu haya mambo upate mwanga zaidi katika safari yako ya mafanikio kiuchumi. Hivi ninavyoandika hapa ni saa saba za usiku. Nakuandikia hadi usiku hivi kwa kuwa nakupenda na nakutakia mafanikio makubwa kiuchumi kuliko mtu yeyote maana yumkini ukawa wewe ndiyo jibu la ajira ya vijana wengi mno nchi hii. Kwa nini tumsubiri Dangote atoke Nigeria kuja kutupa ajira wakati tunaweza kukuandaa wewe na ukapunguza mno tatizo la ajira nchi hii.

So kama itanilazimu kukuandikia makala saa saba za usiku ili zikusaidie nitafanya hivyo mpaka mwisho wa uhai wangu. Ila sasa usiniangushe! Taarifa hizi uzitumie vizuri.

Turudi kwenye mada. Je ulikuwa unamjua huyo Yogesh Manek?

Slim Turky?

Shekhar Kanabar?

Take it as a challenge. Nakuandikia vitu adimu sana. Tumia vizuri taarifa hizi uone chochote cha kujifunza jifunze andika kwenye notebook yako ili uwe unajikumbusha mara kwa mara.

Kulingana na ripoti nyingine ya Utajiri kutoka kampuni ya Credit Suisse inasema utajiri wa dunia nzima kwa sasa ni thamani ya $280 trilioni. Na 0.7% tu ya watu duniani inacontrol asilimia 46% ya utajiri huu wakati 70% ya watu wanaofanya kazi duniani inacontrol 2.7% tu ya utajiri huo. So unaweza kuona ni wapi unatakiwa kusimama ili uweze kuleta tofauti duniani. Kwenye KUAJIRIWA ama kwenye KUAJIRI wengine.

Hakuna kipindi ambacho fursa za kufanikiwa kiuchumi zimeongezeka na kuwa wazi mno kama kipindi hiki ch JPM. Kwa sababu ya uwajibikaji kubadilika kidogo basi fursa ambazo zamani usingeweza kuzisikia hata kidogo mpaka umjue mtu sasa hivi unaweza kuwa na access nazo kirahisi kabisa na kuzifanyia kazi kama wengine.

Hivi unajua sasa hivi ukiwa na pesa kidogo mno unaweza kuuziwa ardhi kwa bei rahisi kuliko wakati wa JK? Kwa kifupi huu ndo wakati wa kumiliki ardhi kirahisi zaidi na kihalali kuliko kipindi kingine chochote.

Taifa letu kwa sasa ni kama limemka usingizini na ndo maana unaona walioamka nalo wanazidi kuongezeka kiuchumi. Tambua kuwa hakuna mtu atakayeleta pesa nyumbani kwako wewe ukiwa Instagram unalike picha za Wema Sepetu. Lazima kwanza uachane na mambo ya kijinga kisha uamke usingizini tatu uache kusikiliza taarifa mbaya uanze kusikiliza taarifa nzuri.

Unajua kila kitu kikizidi unakuwa addicted nacho. Au hata kama hujawa totally addicted unakuwa kwenye dependence level. Yani huwezi kufunction vizuri bila hicho kitu. Unajua kuna mtu asipovuta sigara akili haichangamki. Dependency level. Na kuna mtu asipopata umbea wa Instagram naye akili haikai sawa wakati kuna mwenzako asipoona post za Strive Masiyiwa yeye ndo akili haikai sawa anaweza kuanza kurudia za nyuma tu kama Masiyiwa hajaandika kitu kipya.

So wewe ungependa uwe addicted na habari mbaya na za umbea na watu wanaodhalilishana au habari nzuri na za mafanikio?
It's your choice!
Lakini kama kweli wewe ni mwanafunzi wa mafanikio basi hapo choice iko very clear.

Kila mwaka kuna ripoti zinazokwambia biashara ngapi zinafungwa watu wangapi hawana ajira wanafunzi wangapi wamekosa mkopo, miradi mingapi inayofungwa nk. Na ingawaje ripoti hizo zinatolewa tambua kuwa kuna ripoti zingine zinatolewa pia kuhusu biashara zinazokuja juu, vijana wanaopiga hatua kimafanikio, matajiri wanaoongezeka, miradi inayofunguliwa na jinsi inavyoweza kushiriki katika miradi hiyo.

Ukichagua kujaza taarifa za kundi la kwanza la ripoti basi very soon utaanza kuamini kuwa mafanikio kiuchumi hayawezekani kipindi hiki. Na utaanza kupenda habari negative negative na ripoti tu za vifo na ajali na magonjwa na matusi ya Instagram.

Lakini ukijaza kichwa chako na taarifa za kundi la pili la taarifa but soon utaanza kujiona kama mtu anayefanikiwa katikati ya watu wanaolalamila usiku na mchana.

Kumbuka wewe ni mwanafunzi wa mafanikio. Hupaswi kamwe kuonekana wala kusikika ukilalamika.  Ondoka kundi hilo la wanaolalamila haraka. Ingia kundi la wanaochukua hatua. Yes. Take Action. Hilo ndiyo kundi la waliobarikiwa siyo suala la dini hapa. Hilo ndo kundi la watu ambao Mungu anasubiri waombe halafu awaonyeshe mwanga zaidi. Hilo ndiyo kundi la wanaoleta mabadiliko ya kweli. Hilo ndiyo kundi la watu ambao wakiamka asubuhi mbingu zinajua na dunia inatambua.

Ningependa wewe uwe miongoni mwa watu hao wanaoleta mabadiliko chanya. Lakini kama hutapenda kuacha taarifa zisizo na tija kwako hakika hutafanikiwa kipindi hiki chenye fursa nyingi mno za wazi kwa wale wenye UTHUBUTU wa kujaribu. Na kama kakangu Prosper alivyosema basi kama hufanikiwi katika kipindi cha namna hii ambacho ukitaka kununua ardhi mwenye nayo anakubembeleza badala ya kuringa kama enzi za JK basi huenda usije kufanikiwa tena.

Na kama itakuwa hivyo hakika utajilaumu sana.

Acha wengine walalamike na kupiga umbea. Wewe choose bo be different.
Miaka minne ijayo waweza kuwa miongoni mwa mabilionea wapya waliosemwa na Knight Frank.

Tukutane katika makala nyingine ya mafanikio Mungu akitupa neema tena.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa
www.andreamuhozya.blogspot.com
WhatsApp +255 788 366 511

Ijumaa, 2 Februari 2018

TABIA TATU ZA MTU ALIYE USINGIZINI (AU JAMII ILIYO USINGIZINI AU TAIFA LILILO USINGIZINI)

MINDSET ni kitu muhimu cha kwanza katika kuleta maendeleo kuliko hata NGUVU KAZI.
Twende taratibu tu utanielewa.

Ulishawahi kujiuliza iliwezekanaje UINGEREZA nchi ndogo kabisa tena ya kisiwa iliyo kwenye baridi huko na yenye watu wachache sana iliwezaje kutawala almost dunia nzima ikiwemo Marekani bila kelele na kwa muda mrefu?
(Juzi kwenye ukurasa wangu wa Facebook niliongelea suala la Israel watu wakaanza kuleta sababu za dini. Ooh imebarikiwa. Oh taifa teule. Lakini mimi nilikuwa naongelea MINDSET. Leo nimeanza na Uingereza)

So back to my example. Tafakari pamoja na mimi. Unadhani Uingereza ilitawala nchi zoote hizo sababu ya kuwa na nguvu kazi kubwa au jeshi kubwa au pesa nyingi au nayo taifa teule lenye mki Mtakatifu? Au leo bado ina influence kubwa kiaasi kwamba Queen Elizabeth akisema leo anakuja kutembea Tanzania huenda ikawa sikukuu unadhani hiyo power ni kwa kuwa yeye mzungu au mwanamke au malkia. Kwani kuna malkia wangapi duniani mbona wengi? Ni sababu ya MINDSET yake na yetu ni tofauti. Yeye anatuona watawaliwa sisi tunamuonaje inategemea na tutakavyobehave aisema chochote kuhusu Tanzania au akisema anakuja kutembea. Na sisi kiongozi wetu akisema anaenda kutembea. Mindset.


Tatizo la mindset ni kubwa ndo maana leo mtu akiwaza utajiri wa watu kama Dewji na Manji na Mengi utasikia anasema eti "Mwenzako karithi huyo" au "Kaanza zamani huyo" na kama ni mchungaji utasikia "Sadaka za waumini hizo". Mindset ya aina hiyo haioni anything beyond sababu nyepesi nyepesi.
Ndo maana nilipoongelea Israel watu wakasema "Imebarikiwa hiyo". Hizo ni akili za kivivu na kishirikina. Hazitaki kuwa responsible.

Unadhani Uingereza walimanage kutawala almost dunia nzima sababu ya ngekewa au eti baraka?

Jibu ni walijenga MINDSET YA TOFAUTI. Mindset ya KUTAWALA. Listen to me Mungu alituumbia mindset ya utawala..so usipoitumia utajikuta umejenga default mode ya KUTAWALIWA TU.

Kuna watu wana MINDSET ya kutawaliwa. Hawawezi KUJITAWALA. By default.

Na kabla hatujafika mbali jiulize wewe binafsi mindset yako ni ya KUTAWALA au KUTAWALIWA? Mtu mwenye mindset ya kutawaliwa hupenda aambiwe cha kufanya. Atafutiwe solution. Asaidiwe kupata majibu ya matatizo yake mwenyewe. Hata akiomba nafasi ya AJIRA mahali hafikirii nje ya anachofanya na akikwama anataka akwamuliwe. Mfano akikwama kifedha anaomba mkopo. Si mbaya but mkopo siyo kuwa ndo solution sahihi ya matatizo ya kiuchumi. Mi zamani nilikuwa teja wa mindset hii. Mpaka nilipoamka usingizini. So naongea nachofahamu.

Watu wengi bado wana mindset ya KUTAWALIWA na kwa sababu hao ni wengi kwenye jamii basi jamii hiyo mwisho huwa na mindset ya KUTAWALIWA na kwa sababu jamii za aina hii ni nyingi katika taifa basi mwisho taifa husika huwa na mindset ya kutawaliwa na mataifa ya aina hii yawapo mengi katika bara fulani basi bara zima kwa ujumla wake litakuwa na mindset ya KUTAWALIWA! Mpaka leo vijana wetu wanatamani kwenda Ulaya hata wakafagie tu. Ukimwambia huku atafute kazi hata ya kufagia hataki. Ila mwambie kuna kazi ya kufagia Ulaya utamkuta Libya akiwa anasubiri boti za kwenda Ulaya. Halafu wakiuzwa kama kuku ndo tunaanza kulaumu kwa nini Marekani haiingilii. With due respect Marekani ndo imewapeleka Libya? Naongea vitu vigumu kidogo so usipanic! Kama unataka kupanic subiri kule chini utapanic tu. So tusilaumu wengine kwa matatizo yetu na mindset zetu. Hata kama US ilidestabilize Libya but what if watu hao wangetesewa Morocco? Au vipi kuhusu wadada wa kazi waliosemekana kutesewa Uarabuni. Tatizo ni mondsetnza KUTAWALIWA.

Ni tatizo la MINDSET hili siyo tatizo la imani wala dini. The problem is watu wameweka mbele imani na dini katika vitu vinavyohitaji AKILI. Mchungaji wangu husema kwamba kuwa na imani siyo mbadala wa kutotumia AKILI na husema kama ni hivyo Mungu asingetupatia akili kama imani ndo mbadala. Najaribu kuwasaidia religous fanatics ambao hawawezi kutazama kitu au kukijadili bila kuingiza imani zao.

Umeshawahi kujiuliza kwa nini North Korea imeendelea kupita sisi hadi ina Nuclear Weapons na hawana dini lukuki kama huku. Wamewezaje kujenga mji mzuri namna hii katikati ya aftermath za vita mbaya iliyowaacha bila chakula na katika kipindi hicho wao wanawekewa vikwazo na sisi tunapewa misaada?
China mpaka dini zinapigwa marufuku kwa kuwa sisi tulionazo dini tumeonekana kusubsitute dini for brain. Nchi kama China zinahofia mambo mengi lakini hilo likiwa mojawapo pia. Dini walizoleta wakoloni walizidilute ili kututawala. Zina mapungufu mpaka tutakapoanza kustudy ndo tutagundua. Nchi za Asia zimetupita katika kudevelop mindset ya KUJITAWALA.

Ndo nakukumbusha ya North Korea kupiga hatua kuliko sisi. Shida hapo ni dini pia? Au nao ni taifa teule? Hawatumii Android wala sijui Microsoft wamedevelop softwares za kwao wenyewe na systems za computers za kwao na maisha yanasonga na ndo wanaongoza kwa ku-hack mitandao duniani. Japo si jambo zuri. Ila nalitumia kama mfano maana wanahack kwa maslahi ya taifa lao. Hata Marekani wanafanya hivyo. Kama utakumbuka mwaka 2014 North Korea ilishutumiwa kuhack mtandao wa Sony na kurelease Movies ikiwemo ya THE INTERVIEW ambayo ilikuwa ikiandaliwa bado iliyokuwa na maudhui yaliyosemekana "kuidhalilisha" North Korea.

Point yangu hapa ni kuwa uwezo wa North Korea katika mambo ya computers ni mkubwa mno kiasi kwamba hata Marekani INAUHOFIA. Soma makala hii fupi ya The New York Times uone mambo ya hawa watu.. https://mobile.nytimes.com/2017/10/15/world/asia/north-korea-hacking-cyber-sony.html?referer=https://www.google.com/

Inawezekanaje North Korea kufikia level za kubishana na Marekani hadharani wakati sisi tunaitwa "sh*thole" countries na tunajichekeshachekesha tu na wengine kufikia hatua ya KUKUBALI hadharani kuwa sisi kweli ni sh*ithole countries. Unaona tatizo la MINDSET ya kutawaliwa?

Mwaka 2017 nilienda kutembea kikijini kwetu Ukerewe na kujifunza upya maisha ya watawala wa zamani. (Babu yangu alikuwa karani wa chief wa Ukerewe na hata nyumbani ni kwenye eneo alilopewa na chief jirani na makazi ya chief). Mojawapo ya vitu nilivyojifunza ni kuwa Chief alikuwa na uwezo wa kukukanya (reprimand) muda wowote tena hadharani au kuchukua mkeo hadharani au kukuadhibu na ULITAKIWA umwambie ASANTE  ili kuonyesha utii. Na wengi walizoea hivyo siyo kwa woga no ilifikia hatua ikawa ndo MINDSET ya kila mtu kusema asante kwa chochote atakachofanya OMUKAMA.

Leo ni miaka mingi imepita machief hawapo lakini "WAPO" bado vichwani mpaka mwa wajukuu ndo maana hata leo ukitembelea nyumbani kwa chief yoyote wa zamani awe Marealle au Mkwawa utapaswa kuingia na kutoka kwa respect. Why? Mindset. Wakoloni walikuja na kuondoka lakini WAPO bado vichwani mwetu. Na wanalijua hilo. In fact walilijua kabla hata hawajaondoka. Wakagundua kumbe kubaki huku hakuna tija bora wabaki vichwani mwetu hata wasipokuwepo tutaendelea kuishi kama vile wapo. Ulishaona ile picha ya farasi amefungwa kwenye kiti?
Wengi mlishaiona. Unakuta mtu anasema tusiguse maslahi ya WAZUNGU kwamba WATATUSHTAKI.

Seriously?

Hii ndo akili ya farasi kwenye kiti. Au ndo ile kuwa jambazi akija kwako akisema lala chini mnaweza kulala hapo mpaka saa nne asubuhi kwa hofu tu kumbe jambazi huenda muda huo keshafika mkoa mwingine. Woga.

Lakini ndivyo watu wengi walivyo. Ndivyo jamii zetu nyingi zilivyo. Ndivyo mataifa yetu mengi ya Afrika yalivyo. Afrika Kusini "wakadanganyishiwa" kupewa Mandela kuwaongoza wazungu wakijua huyu atatawala muda mchache tu lakini hawa watu wana mindset ya kutawaliwa tu. Nenda SA leo uone nani anamiliki uchumi huko mpaka leo? Watu wengi weusi wa Afrika Kusini hawataki kufanya kazi. Wanataka starehe. Unadhani ni bahati mbaya kuwa na maambukuzi ya HIV kuliko nchi zingine?
Wakiona hii watapanic pia.

Tatizo nini? Jibu ni:  USINGIZI.

Na sasa twende kwenye kichwa cha article yangu ya leo.

Kuna TABIA (CHARACTERISTICS) 3 za mtu au jamii au taifa lililoko usingizini.

1. MTU ALIYE USINGIZINI HUWA HAJUI KUWA AMELALA MPAKA AKISHAAMKA

Hii ni tabia ya kwanza.
Hujawahi kuona mtu amelala sebuleni kisha akiamka ndo anashangaa kumbe alikuwa keshalala kwenye kochi. Kisha kuamka ndo anainuka na kwenda kitandani.

Ndivyo watu wengi walivyo. Wako usingizini. Ndivyo jamii nyingi zilivyo. Ziko usingizini na wala hazitambui hilo. Ndivyo mataifa ya Afrika yalivyo yapo usingizini na hayajui.

Mtu aliyeko usingizini na halafu hajui kuwa yupo usingizini unafanyaje ili kumsaidia. Wazungu wanachokifanya wanatumia ile methali yetu ya USIMWAMSHE ALIYELALA ila wao wanaimodify kidogo wanaongeza MUWASHIE NA FENI NA UMFUNIKE NA SHUKA HAPO HAPO SEBULENI.

Ndo wanachofanya. Wanajua nchi zetu zimelala wanachofanya kwanza wanatuwashia feni ili mwili uhisi kaubaridi (mfano wanaiba rasilimali nk) kisha wanatuongezea kashuka (misaada).
Hapo mataifa yetu yananogewa na usingizi.
I pity my continent!

Kuna mahali nilisoma kuwa ukitaka kumtawala mtu mtengenezee problem ambayo hakuwa nayo kabla kisha uje na solution kabla yake. That's what is happening.

Mtu aliyelala huwa hajui kuwa amelala hadi akishaamka. Huyu anahitaji KUAMSHWA ndipo afundishwe njia ya kuendea. Ukimfundisha mtu aliye usingizini utapoteza muda bure. Kuna mawili either tuwasubiri watu wetu hadi watakapoamka wenyewe au tuwaamshe kwa lazima.


2. MTU ALIYE USINGIZINI KUNA VITU VINGI ANAFANYA AMBAVYO ASINGEWEZA KUVIFANYA KAMA ANGEKUWA MACHO.

Ulishaona mtu amelala mpaka mate yanatiririka kwenye kona za midomo. Waliosoma kitabu cha THE BEAUTYFUL ONES ARE NOT YET BORN wanakumbuka yule main character alivyolala kwenye basi kwa style hii.

Ok mtu aliyelala anaweza kukoroma kama mashine ya kusaga lakini akiamka (akiwa macho) mashine inazima. Uliwahi kuota unakimbia au kukimbizwa sijui na nini wengine huota anakimbizwa na nyoka mwingine na mgambo wa manispaa mwingine hata anakimbizwa na vitu vingi labda mchepuko. Anakimbia hadi anaanza kutoka jasho usingizini. Lakini akiamka (akiwa macho) haoni kilichokuwa kinamkimbiza.
Tatizo lilikuwa USINGIZI na wala siyo mgambo wala mchepuko.

Kwa hiyo ukikuta mtu amelala huku anaongea mwenyewe sijui "Hapana... nisamehe.. mgambo jamani..." we utamwelewaje? Si utajua shida siyo kuna mgambo ila ni USINGIZI?

Watu wengi wamelala. Vijana wengi wamelala. Facebook ni sehemu ya biashara leo hii lakini vijana wengi kwao ni kijiwe tu cha kubishania mpira na betting au siasa au dini au kulike picha za makalio au kujadili size ya sehemu za siri za mtu fulani. Hawana tofauti na mtu aliyelala na anatoa mate mdomoni.

Siku wakiamka usingizini hakika hutaona wakibishana tena kama leo.

Kuna watu wamebishana kuhusu Lowassa toka 2015 hadi itafika 2020 bado wanabishana.

Kuna watu wamejadili Manchester toka mwaka 2000 na wachezaji huenda waliokuwepo washatoka wote labda huyu bado anajadili Manchester.

Amejadili Zitto Kabwe toka yuko Chadema hadi leo ana chama chake bado anamjadili kwa kisingizio cha kutoa maoni. Mwenzio ni mwanasiasa na maisha yake mengine yanaendelea.


Tatizo nini hapo?

Jibu ni USINGIZI. Na wanasiasa wanajua. Wakikuona UMELALA sebuleni wanakuwashia feni na kukuletea shuka. Kwa ujinga wako unahisi unasaidiwa kumbe unapotea bila kelele.

Ukiongea leo kuhusu watu walioajiriwa wajifunze kujiajiri hata part time majibu utakayopewa na kejeli nzito nzito ukiwa huna wito na mambo haya ya kuelimisha watu unaacha. Lakini kumbe sisi wengine tumetoka familia za wazazi waliotegemea ajira hadi kustaafu na tumeona yaliyojiri LIVE. Tunajua machungu ya kusubiri pension ya mzazi ndo ilipe ada yako. Ndo maana tunajaribu kuamsha wengine yasiwakute.

Juzi nimekutana na mama mmoja mstaafu anajiuliza afanyeje kujikwamua kifedha maana hali yake inazidi kuwa mbaya watoto wake wako chuo wawili mmoja undergraduate mwingine Masters na yeye ndo amewalipia ada kwa kukusanya pension na kukopakopa huku na kule maana hawakupata mkopo wa serikali. Fikiria maisha ya mzazi kama huyu halafu mtoto wake ukimshauri kuwa huko chuo ajitafutie kipato asimtegemee mzazi wake mzee mstaafu huyo mwanafunzi hatakuelewa kabisa! Why?

Yuko USINGIZINI tena kawashiwa feni na kufunikwa kashuka kazuri.

It's sad kuona vijana wetu wengi wanatumia muda kubishania CHAMPIONS LEAGUE au NDONDO CUP au makalio ya WEMA SEPETU. Na wanamuziki wanatumia advantage ya watu kulala wanakufunika na shuka wanakuimbia ANGALIA SHEPUUUUU na wewe unaitikia "AEEE..."
Yaani unakuta kwenye daladala sauti juu na wanafunzi wanaenda shule na ndo wimbo huo. Hivi hawa kama ndo fikra hizo wanazoimbiwa na kuimba watawaza nini kwenye kipindi cha hesabu sijui unafundisha LOGARITHM. Lakini ukijaribu kuwaambia hizo nyimbo wakae nazo mbali weeee! Utaulizwa wewe BASATA?

Tatizo la usingizi hilo.

Lakini hatuachi kusema kwa kuwa tunajua hawa wamelala sebuleni na wamefunikwa shuka. Sasa wewe unataka kumzimia feni unatarajia areact vipi?

Na hizo reaction mbaya zinatokana na hili la tatu hapa chini:


3. MTU ALIYELALA HUWA HAPENDI KUAMSHWA

Hii ndo tabia ya tatu na ya mwisho (for purposes of this post) ya mtu aliyelala. Wengi tunakumbuka utotoni ilikuwaje tukiamshwa kwenda shule. Weee!! Nani aamke? Hadi uimbiwe nyimbo..maana kuna watoto wanaamshwa kwa raha sana utasikia "Junior please wake up my sweet boy". Lakini kwa kina sisi kama ulikuwa na mama kama wa kwangu mwenzangu kibao kimoja kitafanya siyo tu uamke bali ndani ya dakika10 utakuwa ushamaliza maandalizi yote na uko mlangoni unaelekea shule tena kwa kukimbia.

Umenuna. Kumbe ni kwa faida yako. Lakini kuamka ulikuwa hupendi.

Wengi tunajua kuwa tabia mojawapo ya watu wanaotaka kufanikiwa ni kuamka mapema. Jiulize wewe unapenda kuamka saa 10 alfajiri kila siku?
Jibu ni HAPANA.

Ndivyo watu wengi walivyo. Ndivyo jamii nyingi zilivyo. Ndivyo na mataifa mengi Afrika yalivyo. Hayataki kuamshwa.

Hujasikia wahubiri wakisema ni siku za mwisho tumrudie Mungu? Nani anataka kusikia hizo habari? Nani anaziamini kwanza? Ndo ilivyo katika kila eneo la maisha yetu kielimu kiuchumi, nk.

Watu wetu hawataki KUAMSHWA. Wanataka mambo yawe hivi hivi. Jana nilienda sehemu inaitwa Kimanzichana Mkuranga  huko kuna mashamba mashamba ndani ndani huko. Wakati narudi nikakutana na mama mmoja pale Mbagala akiwa amebeba "dishi" lina mihogo mibichi na karanga na vipande vya nazi..ni wale wanaotembezaga kama huyu hapa kwenye picha
 


Nikasogea karibu naye kidogo kudadisi kidogo..

Mimi:
Habari yako dada naona umebeba "kifurushi". (Ndo jina hilo hapa mjini)

Yeye:
Haaahaa ndiyo nikupe cha 4G? (4G ndo kipande cha kassava na cha nazi na karanga mbichi kwa pamoja. Hahaaa. Mambo hayo)

Mimi:
Asante bana nimekuona nikataka nikuulize kitu maana nimetoka shambani huko Kimanzichana so nikaona huenda siku za usoni naweza kuwa nakuuzia mihogo kwa bei rahisi.

Yeye:
Aah ya Mkuranga hiyo siyo mizuri. Ya Kibiti ndo mizuri.

Mimi:
(Nikapotezea hilo la sehemu)
Kwa hiyo unauzia hapa Mbagala?

Yeye:
Hapana nasimamaga Ubungo pale mataa mitaa hiyo ndo navuka barabara nikapande gari hivyo.

Mimi:
(Huku nikitoa hela hivi ili kuonyesha simpotezei muda) Sasa hapo Ubungo umekuwepo kwa muda gani?

Yeye:
Muda mrefu sana.

Mimi:
Sasa flyover ikikamilika magari yakawa hayasimami yanapitiliza utafanyaje?

Yeye:
Aah yatasimama tu. Yasiposimama basi mipango ya Mungu kakangu. Nikupe vipande vingapi?

Mimi:
(Huku nikiwaza usafi wa hiyo mihogo yenyewe nk.) Nipe kipande kimoja. Sasa dada akitokea mtu wa kukupa mawazo jinsi ya kuboresha hiyo biashara yako na kujiandaa kwa mabadiliko ya barabara nk utapenda kujifunza?

Yeye:
Aah. Mi nshajizoelea hivi hivi. Yakibadilika tutarudi hata kijijini tukalime tu kakamgu mambo mengine ni mipango ya Mungu sa mi ntawambia wasijenge hizo flaiova?

Mimi:
Asante dadangu nakuelewa... kazi njema dada.

Yeye:
(Akivuka barabara) Haya asante kwa heri pia.

Unaona kazi ya kumwamsha mtu ambaye amenogewa na USINGIZI ilivyo? Na keshaongezewa shuka.

Measures nyingi zinazotolewa na serikali kwa watu wa aina hii ni sawa na kuwawashia feni na kuwafunika shuka ili walale vizuri sebuleni either kwa kuhofia kupoteza muda kuamsha mtu asitetaka kuamka au kwa kutaka wazidi kulala ili kusiwe na maswali mengi kwenda serikalini.

In any case hawa wanahitaji KUAMSHWA KWA LAZIMA.

Ndo maana tumepata president ambaye akitaka kukuamsha haijalishi umelala masaa mangapi ila kama umelala sebuleni atakuamsha tu kwa kuzima feni na kuvuta hilo shuka wakati bado umenuna anakumwagia na maji usingizi ukutoke vizuri na wakati unazidi kuchukia anakwambia: "Hivi ulisali kabla ya kulala kweli? Hebu piga magoti kwanza hapo uniombee na mimi baba yako maana hii kazi ya kukuamsha kila siku inahitaji moyo!"

Hahaaaa.

Ni utani lakini naamini unaweza kuelewa jinsi ilivyo ngumu kuamsha mtu aliyelala. Na jibsi anavyochukia kuamshwa. Nimesema aliyelala huwa HAPENDI KUAMSHWA. Usingizi ni mtamu mno. Trust me. Hasa usingizi wa KIFIKRA na KIMAWAZO.

Lakini taifa haliwezi kupiga hatua kwa kuwa na jamii iliyo usingizini.

Walichokifanya wenzetu ni kuhakikisha watu wanaamshwa..Kila mtu apewe mtu wa kuamsha. Marekani haijafika hapo kwa kuchekacheka no. Kasome historia wakati wanajenga taifa lao uone ilikuwaje. Walilazimisha kila mtu kujitambua.

Sisi huku we don't care. Mtu anakula ndizi ganda anatupa hapo hapo kama nyani. Seriously. Zebra cross inawekwa mtu anavuka pembeni yake sehemu yenye hatari. Nenda Mlimani City mpaka wavuka kwa miguu wamewekewa taa ambazo ni wao wanaweza kuzicontrol yani ukitaka kuvuka una uwezo wa kubonyeza taa zikasimamisha magari na ukishavuka unabonyeza tena upande wa pili unabonyeza kuruhusu magari lakini watu wanakimbia katikati ya magari. Akili gani hii. Buguruni waliwekewa daraja kuvuka kuokoa maisha yao lakini mpaka walipowekewa uzio ndo wakaanza kupanda daraja kuvuka barabara.

Bodaboda hawataki kuheshimu sgera za usalama na mamlaka zinawa"potezea" sasa si ndo kuwawashia feni huku? Na wenyewe wanaona raha.

Dereva anapita kwenye kivuko cha waenda kwa miguu afu hakuna anayejali. Fanya hivyo US uone adhabu yake! Mlioenda US tusaidieni adhabu ya kupita taa nyekundu au zebra crossing bila kusimama tafadhali nadhani unaweza kupewa adhabu ambayo huwezi kuisahau maishani.

Sisi mpaka mtoto wa shule agongwe ndo tuweke tuta. No forward thinking watu wamepewa dhamana serikalini lakini they are not leaders. Wanasubiri shida ndo waamke. Tena wakiamka shukuru Mungu. Dereva akiona tochi ndo anapunguza mwendo. Mkitaka muone kuna tatizo kubwa la mindset nchi hii ondoeni tochi wiki moja muone. Watu hawajabadilika FIKRA. Bado wamelala. Akipigwa tochi analalamika eti tochi zimezidi. Hajui ni kwa faida ya wengi na ya kwake.

Matokeo yametoka ndo tunaangalia shule zilizofanya vibaya.

Why now?
Hamkujua zitafanya vibaya kweli? Au mnatuchora tu? Hii ndo shida ya Afrika.

Watu wamelala. Ukikosea ukawapa ubunge unatarajia utapata mawaziri wa aina gani huko mbeleni?

So tatizo linaanzia kwa kila mmoja wetu. Wewe UMEAMKA? Nesi umeamka au uko usingizini. Daktari. Mwalimu. Mkulima umeamka au unasubiri Mungu alete mvua kila mwaka huku miti unachoma mkaa na mingine hupandi. Kwani Mungu ni mganga wa kienyeji? Mungu anatumia systems alizoweka. Ukizi disturb inakula kwako tu.

Askari umeamka ndugu yangu au uko usingizini. Kwa nini mtu apite nje ya ATM akute umelala na bunduki umeweka chini tena mchana eti unasema kuna kaupepo? Hahaaa. Unaijua sehemu inayoitwa DMZ -au Dimilitarised Zone huko Korea? Hebu google uone maaskari hao kama wanaweza hata kupiga kope.

Huku kwetu askari anachat muda wa kazi. I mean WHAT A COUNTRY! Msinipige mawe. Nasema tu. Like seriously?

So wewe umeamka msomaji wangu? Binti umeamka au nikuonyeshe wenzako kama Amina Sanga ambaye ni tunu kubwa ya taifa hili na ingekuwa uwezo wangu ningempatia Ubalozi hata akisomea diplomasia akiwa kazini sawa tu.
  

Si kila siku rais analalamikia balozi zetu nyingi?
Kuna watu huko wamelala. Wanadhani ni 1982 saivi wakati tuna watu walio macho huku kwa nini tusiwatumie?

Kijana wa kiume umeamka? Kama hujaamka basi utaisha kukalamika kila siku kila ukiamshwa na kulaumu serikali haijakupa hela na kutamani kwenda kufagia Ulaya. Shame on you.

Mwajiriwa unapiga umbea tu kazini. Akipita bosi wako akakuhamisha kituo au kukupa adhabu unaanza kusema huyu naye anajipendekeza cheo chenyewe haongezwi.
Hutaki kuamshwa.

Israel ni nchi ya watu walioamshana. Wengi wameamka. Siyo sijui dini. North Korea wameamshana. China wameamshana. Siyo dini hapo.

Afrika imelala na kila tukitaka kuamka feni inaongezwa au tunawashiwa na AC kabisa ili kelele za feni zisije kutuamsha. Lol.

Juzi nikasema inawezekanaje Bara zima la Afrika kukubali nchi moja ya China kutujengea ofisi za Makao Makuu ya AU ati msaada?
Are we even serious? Sijawahi kuona usingizi wa namna hii. Tunadumaza our intellect na wenzetu are taking advantage of that.
Tunataka tu UNAFUU. Watu wanaotuwakilisha humu mjengoni tuna uhakika WAKO MACHO?

Dah........ nimejizuia kuandika kitu kwa kweli. Inasikitisha sana.

That is insulting ourselves. Ndo sasa unakuta nchi zetu za Afrika hizi tunapewa msaada wa kuchimbiwa kisima na serikali ya JAPAN au kujengewa choo cha shule fulani na nchi fulani. Hivi wanatufikiriaje sisi. I mean with all due respect. Hivi Tanzania inaweza kukubaliwa hata kusaidia kujenga chochote Marekani hata kama hela zimetoka kwa wadau binafsi? Unaona sisi tunakubali kwa sababu ya mindset ya KUTAWALIWA.

Mtanzania akitaka kujenga choo cha shule kwa kujitolea mahali fulani anaweza hata kukataliwa na hao shule au halmashauri kisa ataonekana anatafuta umaarufu. Lakini balozi wa nchi fulani atakubaliwa na ITV taarifa tunaweza kuona choo kimejengwa kwa msaada wa nchi fulani.

Seriously?

Shida ni tumelala! That's why hatuoni shida kujengewa choo na kuchimbiwa visima na tuna watu wengi na resouces nyingi kuliko huyo anayetuchimbia.

Wake up Africa!

Serikali haitaweza kutatua tatizo la uchumi kwa kuleta tu viwanda. Haya nawapa mawazo adimu. Myasikilize myaelewe. Tunahitaji PRIVATE sector iwe imara mno. Nafurahi napoona Zantel wamechimba visima TBL wamejenga kitu fulani. Mwakasege amejenga kituo cha polisi. Nk.
Huko ndo kujitambua.

Viongozi wa dini na madhehebu wasiishie kuwekea watu mikono na kutamka baraka kwa watu walioko usingizini. Mnasababisha IMANI nzuri ionekane kama mazingaombwe sasa. Kama nimelala halafu wewe umefumbua macho kabisa na  unaniambia NIPOKEE UTAJIRI kwa kuitikia AMEN basi wewe umelala zaidi yangu. Na kama hujalala basi unajua kuwa UNANIPOTOSHA na unafurahi kuniwashia feni na kunifunika shuka. Injili ya kweli ni ile inayohakikisha NIMEACHA dhambi kwanza kabla ya mengine. Kama hujui wala hutaki kujua kama  nimeachana na dhambi kweli ila kila tukikutana tunaimba na kuruka na unaniambia NIMEBARIKIWA huo usingizi wako hata Yeremia nahisi hakuuona enzi zake. Utanipoteza papa. Kwa kweli hapa don't go deeper papa. No. .

Kama unataka ku go deeper katika hili sasa unashangaa nini China na North Korea wakipiga marufuku imani ya aina hii?

We have to change.

Only the TRUTH has the POWER to change our destiny as a nation and as a continent. Tena siyo ukweli wa kuambiwa na mtu wa nje bali wa kuambizana wenyewe.

Lakini leo akionekana kiongozi kati yetu anayejaribu kuamsha watu usingizini hiyo vita atakayopata ataisoma namba. Shida siyo kutawaliwa shida ni akili za yule farasi aliyefungwa kwenye kiti. Hazitaki kujaribu kuondoka kwenye kifungo cha fikra

Uingereza ilitawaliwa na ROMAN EMPIRE mpaka walipoamka usingizini. Lakini walipoamka wanatutawala hadi leo tunaenda kucheza michezo inayoitwa JUMUIYA YA MADOLA. Ya nini? Mashindano ya nchi zilizowahi kutawaliwa na Uingereza. Hatujajitambua. Eti tunaendeleza umoja. Kweli?

Marekani ilitawaliwa na Uingereza mpaka ilipojitambua kama taifa. Vita iliyozuka si ya kitoto. Kujitambua kuna gharama zake yes. But leo USA is a superpower.

Afrika imetawaliwa na kila mtu na HAIJAJITAMBUA mpaka leo. Hatujioni kama WATAWALA sisi. That's why tupo tu hapa. Hatuna UJASIRI wa kuwa pioneers at anything great.

Waarabu walitoka kwao wakaja hadi Afrika...

Wahindi wakatoka wakaja...

Waingereza wakaja...

Wareno na Wajerumani na Wafaransa wakaona isiwe tabu tugawane hili bara tusigombanie fito. Wakaja nao...

Wachina nao sasa wamekuja...

Sisi tupo tu hapa hapa Afrika tunaogopa hata kutoka nje. Bado tunakariri HOW EUROPE UNDERDEVELOPED AFRICA.

Kweli??

Singapore imefika mbali siyo sababu ya eti ni taifa teule. Walijitambua. Walitawaliwa kama sisi. Nilibahatika kusoma kitabu cha Rais wao wa kwanza FROM THIRD WORLD TO FIRST na kuona safari yao ilivyokuwa ngumu.
Leo hii ukiangalia Singapore utashangaa.  Rwanda imejaribu. Inazidi kujaribu. Na hata mindset ya vijana wa Rwanda imebadilika.  Mwezi uliopita nilikutana na kijana mmoja wa Rwanda yuko UDSM anasomea kozi fulani hivi baada ya kuongea naye kidogo akashangaa eti kuwa mimi ni Mtanzania. Namuuliza kwa nini anashangaa anasema anashangaa kwa sababu wanafunzi watanzania walioko naye Hostel vitu wanavyojadiliana ni vya kitoto hadi haamini kama ni wanafunzi wa CHUO KIKUU ambao ndo picha ya taifa baadaye.

Imagine!

Kwa style ya USINGIZI huu Tanzania kama taifa hatuwezi kuwaza hata siku moja kutuma WAHANDISI wetu Haiti au India wakajenge kitu nao. Safari wanazowaza wao ni waende semina wakale per diem na kupiga picha kwenye majengo mazuri yaliyojengwa na WAHANDISI wa nchi zingine! Wamelala hadi waamshwe kwa lazima. Labda kigezo cha kumaliza course ya UHANDISI kiwe kutengeneza mashine fulani au kama ni Ardhi University lazima mtu abuni jengo la Wizara fulani alete mchoro wa MAANA kwa kila mtu!

Lakini nani anataka hizo shida? Ukifanya hivyo yule mama wa haki za binadamu utasikia anasema nyie serikali kama mmeshindwa KUTULETEA maendeleo msiwatese watoto wetu.
Lol. Nimewaza tu.

Maana walio macho kumbe hawako macho kwa faida ya aliyelala ila wako macho ili waendelee kupata chochote au ili isile kwao. Yani mfano unakuta mtu kapewa nafasi serikalini lakini anafanya kazi ili asitumbuliwe siyo ili alete tija mahali alipo.
Wazungu wanaongeza feni tu taratiibu.

Ndo shida ya USINGIZI HIYO. Tutatawaliwa milele.
Coz hatutaki kuamka. Wenzetu wana THINK TANKS kibao kwa kuzingatia talents na abilities za watu. Sisi huku hata ikianzishwa inazingatia KNOW WHO.

Ndo tatizo la usingizi. In summary:

1. Tumelala na hatujui kama tuko usingizini

2. Siku tukiamka kuna vitu tunavyofanya sasa  hatutafanya tena milele

3. Tatizo ni hatuko tayari kuamka.

Siku nyingine ukisikia kama umelala afu kuna mtu anawasha feni ogopa sana tena amka.

Lakini ukiamshwa basi na wewe amka.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
WhatsApp: +255 788 366 511

Jumatano, 17 Januari 2018

ARE YOU A TRAVELLER OR JUST A PASSENGER? (FIVE FUNDAMENTAL DIFFERENCES BETWEEN THE TWO)... WEWE NI MSAFIRI AU ABIRIA TU? (JIFUNZE MAMBO MATANO MUHIMU YANAYOWATOFAUTISHA WATU HAWA).



Ahadi ni deni.

Niliahidi kuwa makala yangu inayofuata itazungumzia suala la Traveller's mindset Vs. Passenger's mindset so nashukuru Mungu nimetimiza ahadi licha ya mambo kuwa mengi na hii ikiwa makala yangu ya kwanza ya mwaka huu mzuri wa 2018 toka Yesu aje dunia hii.

Tuendelee...
:::::::::::::::::::::::::::::::  ::::::::::  :::::::::::::::::::::::::::::::::

Mwanzo!

September 2017.

Ni Jumamosi.
Alarm ya simu yangu inaita kwa nguvu mida ya saa 10 na robo alfajiri. Naamka papo kwa hapo ili mlio usivuruge usingizi wa mke wangu maana alikuwa amefanya kazi kubwa jana yake kuniandalia vitu muhimu kwa safari yangu ya simu hii.

Ninazima alarm nashukuru Mungu kwa kuniamsha salama (ningekuwa nimekufa nisingesikia alarm au siyo?)

Nikakimbia bafuni chap chap kujimwagia maji ili kuondoa kabisa uchovu na usingizi. Well mwezi huo bado asubuhi kulikuwa na kibaridi sana hata hapa Dar es Salaam. Nilimaliza kujisafi na kuelekea chumba kingine ambapo nilikuwa nimeweka begi langu ili pia maandalizi yangu ya mwisho yasiondoe usingizi wa mke wangu.

Begi la size ya kati hivi lilikuwa tayari nguo kadhaa za kutosha kubadili huko niendako, mashuka mawili, taulo, viatu na sandals, begi lilijaa hadi likafunga kwa shida kidogo. Begi la mgongoni (backpack) lilikuwa na notebook, na vitabu viwili, biblia laptop na scarf nzito ya kufunga shingoni ikitokea hali ya baridi. Maji ya kunywa dawa chache muhimu mswaki nk.

Nikamuaga mke wangu nikampigia bajaj fasta huyo Ubungo.. Safari ya Mwanza ikawa imeiva. Kaubaridi ka alfajiri kalinifanya nivae shati na kuweka na koti juu yake.

Safari ikaanzia Shekilango na ilikuwa nzuri tu licha ya kuonekana kama kulikuwa na hitilafu kiaina kwenye gari (kwa mtu anayejua gia zinavyopaswa kuingia kwenye gari) lakini ilikuwa salama na kiyoyozi kizuri kikipuliza na kuubembeleza mwili.

Lakini baada ya kukaribia tu Chalinze basi likaharibika kabisa tatizo tukiwa tunadhani ni dogo kumbe gear box..!

"What the.....????"

Sauti kadhaa zikasikika.

Well wa kulalamika walikuwepo wa kupiga simu walikuwepo wa kupiga selfie pia walikuwepo. Wa kununa kimya kimya walikuwepo.

Wa kulaumu kiwanda lilichotengeneza basi nao walikuwepo. Wa kulaumu dereva walikuwepo wwa kulaumu mmiliki walikuwepo wa kulaumu SUMATRA walikuwepo. Wa kulaumu serikali walikuwepo. Na wa kujilaumu kwa nini hawakusafiri jana yake pia walikuwepo.

Wa kuchukulia poa pia walikuwepo.

Tatizo lililodhaniwa na wengi kuwa litachukua muda mfupi likachukua nusu saa lisaa mara masaa. Kutoka saa mbili hadi saa sita kasoro ndipo tulipoondoka kwa basi la kukodishiwa.

Lakini katika kipindi hicho cha masaa takribani matatu nilijifunza jambo muhimu mno ambalo ndilo hasa chimbuko la makala yangu hii. Nilijifunza kumbe kuna tofauti kubwa kati ya MSAFIRI na ABIRIA tuwapo safarini.

Nianzie lilipoharibika basi....

Kwa kuwa sasa basi liliharibika na likazimwa engine AC pia ilizima. Kwa hiyo hali ya hewa ndani ya basi haikuwa rafiki sana. Wengi walifungua madirisha.

Binafsi niliamua kutoka nje ambako tayari kulikuwa na watu kadhaa wamekaa pembeni wengine kwenye miti nk. Lengo langu nitafute sehemu ya peke yangu nisome kitabu angalau kuliko kupoteza muda kulalamika tu kama everybody else. Muda ni mali au siyo?

Nimevaa cadet na shati na koti. Pembeni ya barabara kama mita 10 hivi kulikuwa na gogo kuna kijana mmoja tuliyekuwa naye kwenye basi wa miaka kama thelasini hivi nilivyomuona amevaa pensi na yeboyebo (zile wanavaa sana wachina) na tshirt na amevaa miwani ya jua amelala kwenye gogo moja kubwa lilikuwe mahali pale kama mtu anayeota jua. Amekaa kama vile alikuwa pale toka jana yake usiku.

Nilipomuana nikaona ni mtu tofauti sana na watu wengine wote waliokuwepo hasa kwa alivyovaa.

Nilisogea nikamsabahi akatoa miwani yake ya jua na kuining'iniza kichwani ili tuonane. Well tukateta mawili matatu (mi hupenda sana kusikia kutoka kwa watu wengine naamini ndo njia bora ya kujifunza)

So nikamuuliza:

"Unaelekea wapi kiongozi?"

Yeye: "Mwanza"

Mimi: (huku nikimuangalia juu hadi chini) Anhaa Okay mimi pia naelekea Mwanza. Unafanya kazi Mwanza?

Yeye: No naenda kutembea tu.

Mimi: Oh safi sana. Napenda kusafiri sana pia. Naelekea Mwanza pia japo naenda kibiashara na kumsalimia mama.

Yeye: Wewe huonekani kama MSAFIRI.  Unaonekana kama ABIRIA tu.
(Dah jibu lake lilinifanya niwaze huyu jamaa amenionaje kwanza. Kwanza nimevaa vizuri kuliko yeye au hajioni? Na ina maana kusafiri kote huku nchi hii bado kaniona mshamba au??🤔)
Wakati naandaa cha kusema akaendelea. Na hapa ndo shule ilipo.

Yeye: Ndo maana sasa hivi kuna joto lakini umevaa vest na shati na koti na "moka" wakati siyo mazingira yake.
(Nilitamani nijiangalie juu hadi chini. Nikajikausha. Kiukweli jua lilikuwa linazidi kuwa kali na joto kuzidi kuongezeka. Lakini nilikuwa bado nimevaa koti. Well nikaona siyo tabu. Nikatoa koti nikaweka mkononi. Akacheka kidogo.

Yeye: Watu wengi unaowaona hapa nje wanalalamika ni kwa sababu ni ABIRIA. They are not TRAVELLERS. Maana wangekuwa wasafiri wangeweza kuwa na uzoefu nini kinaweza kutokea safarini na kikitokea ukiwa karibu na makazi ya watu ubehave vipi na ikiwa porini pia uta survive vipi au kwa ujumla tu ufanyeje kama huna solution.

Mimi: Aisee. That's very interesting. I guess sijawahi kuwaza  haya mambo licha ya kusafiri kwa muda mrefu.

Yeye: No bro wewe hujasafiri kwa muda mrefu ila umekuwa ABIRIA kwa muda mrefu.
(Ulishawahi kumtazama mtu kwa jicho fulani hivi? Ilikuwa kidogo nimwangalie kwa hasira lakini desire ya kujifunza ilikuwa kubwa. Nikajikausha.
Ila dah. Yaani hilo neno liliingia akilini mwangu kwa nguvu utafikiri analigongelea kwa nyundo)

Yeye: Mtu akiwa abiria concern yake ni kufika anakoenda. Hapo katikati hata kitokee nini yeye anawaza KUFIKA TU wakati kumbe chenye maana ni ile SAFARI na siyo destination.

Dah! Yaani I was TRANSFIXED. Sikuwa naamini masikio yangu. Nikamuangalia tena nikakosa cha kumuuliza wala kumsemesha. Kuna nyakati akili yako huwa inajua kuwa sasa hapa niko DARASANI sitakiwi kujitingisha. Hii ni shule adimu. So niliamua kumpa attention yangu yote.

Akakaa vizuri kwenye gogo lile akaendelea....


Yeye: Kwa mfano hii safari yetu imesimama hapa. Lakini watu wengi wanalalamika badala ya kushukuru Mungu kuwa wamepewa chance ya kuinteract ambayo wasingeipata kama basi lisingeharibika. Hapa ndipo kuna connection muhimu za baadhi yao. Hapa ndo kuna muda wa kutafakari mambo muhimu kwa baadhi yao lakini wengi wanalalamika tu. Why? Kwa sababu ni ABIRIA siyo WASAFIRI.

(Wow! Nikasema huyu kijana naona yuko vizuri sana kichwani)

Akaendelea...

Yeye: Eneo hili tulilopo sasa hivi huu ni ukanda wa wanyama kupita kutoka Mikumi kuelekea mpaka Saadani. Kila baada ya miaka kadhaa huwa wanyama wanapita maeneo haya haya na kwenda mbuga zingine. Na zamani kabla ya barabara hizi na kabla ya watu kujenga makazi eneo hili lilikuwa na wanyama wengi wakipita.

::::::::::::::::::::::::::::::::

Kwa kifupi alinieleza kuhusu wanyama ambayo nilikuwa sijui. Alinieleza mambo mengi kuhusu safari na wasafiri na kuhusu abiria na siku nyingi sana zimepita baada ya safari ile lakini mambo niliyojifunza hayajapita kabisa.

Alinifanya nikajifunze upya kuhusu tofauti ya msafiri na ABIRIA na nimekuandalia tofauti chache kati yao kama ifuatavyo:

1. ABIRIA ANATAMANI KUFIKA TU MSAFIRI ANATAMANI HATA SAFARI ISIISHE JAPO ANAJIKUTA INAISHA TU AFANYEJE

Anachotaka ABIRIA ni KUFIKA tu. Mengine yote ni usumbufu kwake na upotezaji wa muda. MSAFIRI pia anataka kufika lakini awe ameifurahia safari yake hapo katikati.
Ujiangalie pia katika maisha. Je wewe unatamani tu KUFIKA? Unatamani tu kumaliza shule, au kupata degree. Au kuoa/kuolewa. Au kufanikiwa. Ila mchakato hapo katikati unaona usumbufu. Binafsi ninakutana na watu wengi katika kufundisha kwangu ujasiriamali lakini wengi wanataka tu kupata pesa basi. Process hawataki. Usije kwenye ulimwengu wa biashara kama ABIRIA. No. Be a traveller. Mchakato ndo muhimu. Siyo mamilioni utakayopata.

So wewe je ni MSAFIRI au ABIRIA?
Unatamani chuo kiishe tu upate degree au pia unaenjoy hayo maisha yako ya chuoni?

Unatamani tu upate ajira au unaenjoy interviews unatamani hata isingeisha? Ndo utajijua wewe ni abiria au msafiri. Ukienda ibadani unatamani iishe uondoke au ikiisha unasema dah imeishajeishaje hii kitu.

Kwa ABIRIA kuchelewa kufika ni usumbufu au mkosi lakini kwa msafiri kuchelewa kufika ni sehemu ya safari. Wasikilize watu waliochelewa kufika Moshi wakati wa Christmas utajua nachosema kulingana na wanavyosimulia.

Ndivyo ilivyo.

Mtu anaanza biashara akichelewa kufanikiwa anaacha. Huyo ni ABIRIA. Msafiri ataona hiyo ni sehemu ya kuyafikia mafanikio yake.
Wewe una mindset ipi?

2. ABIRIA HUBEBA KILA KITU LAKINI MSAFIRI HUBEBA VICHACHE TU VYA MAANA

Again. Ukikumbuka story yangu niliposafiri nilibeba mpaka mashuka taulo nk. Seriously??? Lol.

Ndivyo ilivyo kwa wengi wetu. Tumekuwa ABIRIA for a long time maishani. Abiria atabeba mabegi mawili, simu mbili, chaja, powerbank, nguo kibao, laptop, viatu tofauti tofauti, pesa taslimu tena nyingi, na nyingine nyingi kwenye MPESA, kadi za benki, nk.

Ndugu yangu unaenda Mwanza au sayari ya Mars?? Ulishaona movie ya *Coming To America* jinsi Eddie Murphy na msaidizi wake walivyotua Marekani na rundo la mabegi meeengi na kwanza yote yalipotea (stolen).



Lakini msafiri hubeba vitu  muhimu tu. Tena vichache. Camera. Nguo chache mno. Taulo la nini wakati anaweza kupata huko aendako na asipopata poa tu atakauka tu hata iweje. See?
Hawa watu watatumia fedha kiwango tofauti sana.

Sasa katika maisha tuna a lot of baggages tumejifunza nyumbani, shuleni na kwenye jamii. Ukiishi maisha yako umebeba hizo baggage zooote kama kina Eddie Murphy utaingia gharama nyingi sana na stress zisizo na msingi kwa sababu you are moving with things you don't need. Watu wengi wamejaza vitu unnecessary vichwani mwao. Sasa lazima tu uchelewe kufika unakotaka kimaisha maana unarudishwa nyuma na mzigo mkuubwa wa vitu ambavyo havihitajiki katika safari ya mafanikio yako.

Mwaka jana 2017 July niliandika makala fupi kuwa ukimwambia Bakhressa kuwa MIHOGO ni biashara kubwa atakuita boardroom muongee vizuri. Wakati ukimwambia mtu msomi na elimu zake atakwambia hiyo  achana nayo. Kwa sababu msomi amebeba mawazo ya vitabuni yooote kama yalivyo. Bakhressa hana hiyo mizigo so ukimpa idea kichwa inaichuja haraka kuliko msomi ambaye yeye anataka idea yako ieandane kwanza na definitions alizosoma kitabuni.

Be a traveller!! Acha kubeba "mataulo na mashuka na maviatu na mahela" nk. Namaanisha acha kutembea na mawazo yasiyokusaidia sana. Unayo tu. Vitu vingi tulivyojifunza maishani havitusaidii zaidi ya kuwa mzigo tu kwetu. Jiulize mambo uliyojifunza toka chekechea hadi labda degree mangapi unayahitaji ili kutimiza kusudi la kuishi kwako? Be a traveller. Ndiyo maana vitu alivyofanya Yesu viliandikwa vichache vya MUHIMU.

3. IKITOKEA SHIDA CHA KWANZA KWA ABIRIA NI KULALAMIKA CHA KWANZA KWA MSAFIRI NI KUJIFUNZA NI NINI KIMETOKEA (KWA USAHIHI WAKE) NA YEYE ANAWEZAJE KUWA SEHEMU YA SULUHISHO IF POSSIBLE

Katika maisha ndivyo ilivyo pia. Ikitokea shida katika ndoa mwanandoa ambaye ni abiria tu ataanza kwa kulalamika. Lakini ambaye ndoa kwake ni safari ataanza kwa kujiuliza WHAT HAPPENED, WHY EXACTLY and WHAT TO DO.

Katika masomo hivyo hivyo. Ukifeli ukalalamikia Waziri au NACTE au lecturer, wewe ni abiria. Jiulize why umefeli kiukweliukweli. Then tafuta solution ya *kiukweliukweli.*

Biashara ikiwa ngumu jiulize why kwako imekuwa NGUMU. What exactly is the reason. Then how can you fix it.

Umekosa mkopo chuo cha kwanza ni nini kulalamika? Au kufikiria why exactly umekosa kwanza. Hao waliokunyima mkopo ni kama basi lililoharibika njiani. Tuna assume hutabaki hapo milele. But sasa while uko hapo unajifunza nini? TRAVELLERS NEVER COMPLAIN.. IF YOU DO YOU ARE NOT A TRAVELLER.

4. ABIRIA HUJIPIGA PICHA YEYE LAKINI MSAFIRI HUPIGA PICHA MATUKIO.

Wengi wetu tumekuzwa kama abiria. Ni jukumu lako kujifunza kuwa msafiri badala ya kulalamikia ulivyokuzwa.

Kwa kifupi abiria akiwa hata kwenye ndege angani atajipiga picha kwenye ndege. Lakini msafiri atapiga picha za matukio. Msafiri anaamini zaidi kuwa kumbukumbu nzuri zaidi ni matukio na siyo sura yake. Mfano abiria atapiga selfie akiwa kwenye basi au ndege
 lakini muda huo huo jua linachomoza au kuzama lina mwanga fulani mzuri abiria haoni kabisa hilo tukio ila msafiri hawezi kumiss hilo tukio.

Akienda mbuga za wanyama abiria utamjua tu hata alivyovaa hafanani kama yuko mbugani. Lakini hata picha abiria atajipiga picha nyingi za yeye akiwa mbugani kuliko alichokikuta mbugani.

Katika maisha ni hivyo hivyo. Unapitia moments nyingi hapo shuleni au nyumbani au kazini au katika biashara yako. Weka rekodi ya matukio muhimu siyo kingine.

Abiria hata notebook hana lakini msafiri ana JOURNAL.

Unakutana na watu wengi kila siku. Je kichwani mwako inabaki kumbukumbu ya sura za watu au tukio lililotokea. Kumbuka  kinachokufundisha ni tukio siyo sura ya mtu.

Weka rekodi za matukio muhimu. Ni tukio gani muhimu katika biashara yako. Usipige picha tu uko ofisini unakunywa chai. Piga matukio muhimu pia kama lift imekwama, nk. Utajifunza katika hayo kuliko chai ambayo mchana tu ushaisahau.

Ulishawahi kuona mtu akienda nje ya nchi. Picha nyingi anapiga kwenye vitu common. Huyo ni abiria. Msafiri ni mtu ambaye mindset yake ni katika vitu vipya. Hata akipiga picha katika sehemu common ataipiga kitofauti sana na huenda sura yake isiwepo.

Abiria hupenda kupiga picha na watu maarufu. Lakini  msafiri hupenda #kukutana na watu maarufu hata wasipopiga picha. Ukikutana na Dewji muhimu ni nini kwako: Picha ya ukumbusho au kitu ulichojifunza kwake?

Watu wengi wamepoteza fursa muhimu kwa sababu ya kung'ang'ana kupata selfie na Mengi badala ya kukaa pembeni umuulize kitu ambacho jibu lake litafungua njia yako even wider.

Kupiga picha na Bill Gates ni nzuri lakini je ndicho unachohitaji ili ufanikiwe kimaisha? Yeye alifanikiwa kwa kupiga picha na watu maarufu kwani?

Abiria anachotaka ni akifika awe na sura yake kwenye picha zaidi ya 20 alizopiga. Msafiri anataka akifika ana picha 20 pia lakini ni za matukio muhimu yaliyojiri safarini.
Be a traveller.

5. ABIRIA HATAKI KITU KIPYA.... LAKINI MSAFIRI ANAKITAMANI

Hili ndo limewashinda wengi wanaojaribu kufanikiwa wakiwa na mindset ya ABIRIA.

Abiria akikuta kuna njia mpya tofauti na aliyoizoea anaona usumbufu. Msafiri ndo hufungua macho ili aone mambo mapya. Na ajifunze.

Ukiwa abiria hata serikali ikianzisha utaratibu fulani wewe unataka mambo yawe kama yalivyokuwa siku zote. Hauko open-minded kujifunza mambo kwanza uyaelewe. Kanisani wakiweka utaratibu mpya unaona usumbufu hata nyumbani mzazi akiweka utaratibu mpya unaona usumbufu. Kina Ben Carson walizoea wakitoka shule ni kucheza, kuangalia TV na kula afu ndo homework. Mama yao akabadilisha gia. Akasema kuanzia sasa ni homework kwanza kisha kucheza, kisha ndo TV tena TV ni mara mbili tu kwa wiki. Tena mtaangalia vipindi nitakavyochagua mimi viwili tu wiki nzima. Weeeee! Mbona ilikuwa shughuli. Lakini fast forward miaka mingi sana baadaye sasa hivi Ben Carson ni Waziri  wa Nyumba na Maendeleo ya Miji huko Marekani!!


Hajawa waziri kwa kuachwa kuangalia TV bali kwa kunyimwa huo uhuru. Kwa kulazimishwa kuwa MSAFIRI badala ya kuachwa kuwa ABIRIA tu kama wengine.

Nimejifunza kuwa watu wanaofanikiwa ni watu wenye kupenda kujifunza vitu vipya. Siyo lazima wavifanye no. Ila wanajifunza tu. Lakini wakiona vinaanufaa wanajaribu na mwisho wanafanikiwa sana. Yani ukija na idea mpya anakwambia njoo tuongee nikusikilize. Kisha ataamua baada ya kukusikiliza.

Lakini mtu mwenye mindset ya kiabiria abiria atakwambia NO usije. Niko busy. Sina muda. Nk. Anabaki na level ya ufahamu aliyonayo. Anajua barabara ya zamani tu. Basi likichepuka kupita njia mpya anasinzia. Waulize madereva taxi wa zamani jinsi ambavyo walikataa kujifunza kuhusu vitu kama UBER na TAXIFY na kuviona kama usumbufu na uone sasa hivi walivyoanza kuelewa dunia inakoelekea.

Usiwe ABIRIA. Utakosa vingi maishani. Kijana mwenzetu Diamond angekuwa na akili za kiabiria (passenger mindset) asingekubali kujaribisha perfume wala karanga.

Kwanza angesema "Niko busy saivi hiyo idea ngoja kwanza nimalize album hii inayokuja". But unadhani wasanii wengine waliomtangulia kupata pesa unadhani hawakupewa ideas kama hizo? Walipewa. But labda walizidharau.
Wakawa na mindset za passenger tu. Leo wamepotea.

"Professa Jay" alipopewa idea ya kuingia siasa akaona ajaribu. Huyo hapo anasema mwenyewe anaongoza binadamu na wanyama.


Anyway point ni kuwa alikuwa na mindset ya TRAVELLER. Wanamuziki waliobaki na mindset za kipassenger huenda wakaja kupotea kabisa.

Mtazame P. DIDDY. Traveller huyo siyo passenger. Anaskiliza idea mpya. And look wapi yupo sasa.


Kama unataka kufanikiwa na idea mpya hutaki hata kusikiliza tu ujue UNAJIDANGANYA. Usiamini maneno yangu. Fanya utafiti wako kuhusu wote waliofanikiwa uone kama walijataa kusikia idea mpya na ngeni.




So lazima ujifunze hilo pia. Usikariri barabara. Kuwa tayari ku explore new arenas. Hilo nalo ni tofauti kubwa kati ya MSAFIRI na ABIRIA.

Wewe ni yupi kati ya hao?

:::::::::::::::::::::::::::::::::::

Yako mambo mengi mno niliyojifunza kuhusu tofauti ya mtu ambaye ameishi kama ABIRIA na yule anayeishi kama MSAFIRI.

Nimeshea na wewe hayo machache niliyoona yanaweza kukufaa pia.

Toka nisafiri na huyo kijana aitwaye MATHIAS SAGUTI (instagram @mathias_cyclist_official_page)

sijawahi kubaki the same.

Namshukuru Mungu kila siku kunikutanisha na watu walionifanya kuzidi kujua vitu vipya vya manufaa.

Nakuombea wewe pia ya kwamba maandishi haya yasikuache jinsi yalivyokukuta.

Nikushukuru kusoma mpaka hapa. Kama umejifunza chochote cha kukufaa nitafurahi kusikia kwenye comment section.

Barikiwa sana!


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa
WhatsApp +255788366511


*MWISHO*
:::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::

Jumapili, 24 Desemba 2017

ARE YOU EDUCATED OR JUST SCHOOLED? UMEELIMIKA AU UMESOMA TU?



ARE YOU EDUCATED OR JUST SCHOOLED?
UMEELIMIKA AU UMESOMA TU?

Neno ELIMU kwa watu wengi linafungamanishwa sana na neno SHULE. Yaani kwa watu wengi inaonekana mtu aliyekwenda shuleni ndo mwenye elimu. Ndiyo maana utasikia watu wakisema “Aah huyo jamaa kaenda shule huyo usimchezee”, na vitu vya aina hiyo.
Lakini kuihalisia kitu hiki tunachoita ELIMU tunakuwa tukimaanisha tu MFUMO RASMI WA ELIMU ama kwa lugha ya kiingereza FORMAL EDUCATION.

Na KUELIMIKA mtu anaweza kuelimika akiwa hata darasani hajaenda. Tafsiri yetu ya elimu ndo inatufanya tuone kama kwenda darasani ndo kuelimika.

Mfumo huu ambao sisi tumeurithi hasa kutoka kwa wakoloni ni mfumo ambao ulianzishwa ukiwa na malengo yake. Mfano wakati ambapo jamii ya watu waliofanikiwa huko Ulaya ilihitaji watu wa kuwatunzia pesa zao ilibidi taaluma zinazoshughuklikia mambo hayo zianzishwe yaani watu wa kutunza fedha za wengine. Hivyo wakaanza kufundishwa taratibu za ukitaka utunze pesa za mtu vizuri unatakiwa ufanyeje. Na ili kuthibitisha kuwa umeelewa kweli unapewa mitihani na ukifaulu unapewa cheti cha kwenda kumwonyesha mwenye hela zake zinazohitaji kutunzwa anakupokea unaanza kumsaidia mambo ya mahesabu yake.

 Hivyo hivyo wakati watu waliofanikiwa walipohitaji mtu wa kusaidia wafanyakazi wa huyu tajiri waishi vizuri kwa maelewano nk ilibidi watu wanaoitwa leo “Human Resource personnels” waibuke kama taaluma mpya.
Wakati ambapo watu wa kusaidia mitandao ya matajiri iende sawa wameibuka watu wa IT nk kama taaluma mpya.

Kwa hiyo kimsingi mfumo huu wa elimu ulianzishwa kwa ajili ya kumsaidia mtu aliyefanikiwa kiuchumi kuweza kupata watu #sahihi wa kumsaidia mambo yake #kitaalamu. Na siyo hasa kumsaida mtu maskini ili awe tajiri. No. Na nasema NO kwa sababu njia ya mtu kuwa tajiri haihusiani na kusomea uhasibu au IT au sheria nk. Sasa inawezekana kabisa mtu akasomea hivyo vitu na akawa tajiri lakini hatakuwa tajiri kwa sababu amesomea hivyo vitu bali kwa kuwa licha ya kusomea hivyo vitu amejihusisha na mambo mengine sahihi yaliyompelekea kuwa tajiri which means huyo mtu hata asingesomea hivyo vitu angeweza tu kuwa tajiri.

Bahati mbaya sana mfumo rasmi wa elimu (yaani formal education) umeonekana kwa sasa kuwa ndiyo ELIMU YENYEWE. Hiyo nasema ni bahati mbaya kwa sababu inaonekana tumesahau nini hasa MAANA (yaani kazi) ya kitu kinachoitwa ELIMU.

Tukijikita kwenye kujua maana halisi ya ELIMU yaani KAZI ya elimu ni nini tunaweza kuona hasa kuwa watu #wengi tuliopitia mfumo huo rasmi wa vidato na madarasa basi TUMESOMA tu na HATUJAELIMIKA per se. Yaani we are just schooled but not really educated.

Bahati mbaya mtu ukiongea vitu vya namna hii unaonekana eti unaiponda “elimu”. Mi sipondi kitu, Naeleza UKWELI as ninavyouona. Unaweza kupima maneno yangu kwa mizani ukaona kama yako sawa au hayako sawa na ukiona cha kukusaidia chukua. Ukiona hakuna cha maana pia Merry Christmas!
Nimeamua kuandika haya baada ya kuwa nimeongea na vijana wengi mno hasa walioko vyuoni na kugundua kuwa kuna tatizo kubwa mno la kimtazamo (a serious mindset problem) na ni kubwa kiasi kwamba tusipokuwa makini tutajenga jamii based on a LIE. Haina tofauti na hela za wakati wa JK ambapo zilionekana za bwerere na watu kudhani hayo ndo mafanikio YENYEWE wakati UKWELI WA MAMBO ni kuwa kama taifa tulikuwa tunaelekea kule wanyama aina ya DINOSAURS walikoelekea.


KAZI YA ELIMU

Sasa kimsingi kazi ya elimu (yoyote ile) ni kumuwezesha huyo anayeipewa hiyo elimu kuweza kufanya haya mawili:

(a)KUTAMBUA (to identify )
(b) KUKABILI/KUTATUA (to handle)

Sasa ni kutambua na kukabili nini? Jibu ni #kutambua na #kukabiliana na mambo haya matatu:

1.       WAJIBU WAKE
2.       CHANGAMOTO ZAKE
3.       MAFANIKIO YAKE

Hiyo ndo kazi ya elimu na hivyo definition yoyote ya neno EDUCATION  haitakuwa na maana kama hai-address mambo hayo hapo juu. Kwa hiyo kwa kifupi kama elimu uliyonayo haikusaidii kutambua na kukabili WAJIBU wako, CHANGAMOTO zako na MAFANIKIO yako basi hicho unachokiita elimu ni USELESS.

MFANO HAI
Jana nilikutana na binti mmoja anasomea mambo ya UFAMASIA katika chuo kimoja hapa jijini Dar es Salaam. Katika kuongea naye nikamuomba anitajie RESPONDIBILITIES zake angalau 5 hadi 10 kama mwanafunzi. Yaani yeye kama mwanafunzi anawajibu wa kufanya nini na nini. Huwezi kuamini alishindwa. Ina maana hajui huyu mtu kuwa wajibu wake ni nini. Unatarajia huyu mtu uje umpe hata hiyo ajira atajua wajibu huko kweli?

Wengi wanaoitwa WASOMI hawajui wajibu wao kabisa. Ndiyo maana si ajabu kuona amegraduate na anadhani wajibu way yeye kupata ajira ni wa SERIKALI.
Na ukijaribu kumwambia otherwise hamtoelewana kabisa. Yeye anajua akimaliza chuo kuna AJIRA. Yaani huko duniani yeye anajua kuna watu wana WAJIBU wa kumpa yeye ajira. Kuna watu wa kumpa yeye pesa.

Ni kwa sababu ya MINDSET hiyo ndo maana huyu mtu anamaliza chuo kikuu na akitaka kutembeza hata hizo CV anaamini mwenye wajibu wa kumpa nauli ya kusambazia CV zake ni MZAZI au MLEZI. Yaani yeye anadhani kazi yake ni kusoma tu basi. Vingine ni wajibu wa wengine. This is the challenge I’m addressing hapa.

Kuna wasomi wanadhani hawajafanikiwa kwa sababu serikali iliyopo ni ya CCM ...huyo anaamini Chadema wakishika dola tu kila kitu kitakuwa kama Ulaya. Kuna wasomi wanaamini hawajafanikiwa kwa sababu ya wazazi kutowaandalia “mazingira mazuri”. Sijui ndo yakoje mazingira hayo mazuri… kama kijana kutoka Tandale ambaye maneno “PENS DOWN” huenda hakumbuki lini mara ya mwisho ameyasikia na sasa anasambaza karanga zake NCHI NZIMA hadi nchi jirani. Yes Diamond Karanga.


na wewe unazinunua. Hivi huyu aliandaliwa mazingira gani na wazazi. Wewe bado unaendelea kusikia "pens down" mpaka leo na unalaumu wazazi bado?

Wasomi wengi wakiwaza kuanza biashara wanalalamika hawana MTAJI. Mchungaji wangu jana Jumapili akihubiri kanisani akasema hivi:

“Kama unashindwa kuanza biashara kwa sababu umekosa mtaji wa laki tano tu, yaani KAMA UTASHINDWA kuyaendea mafanikio yako kwa sababu ulikosa laki tano basi HUJITAMBUI KABISA!!”

What a powerful statement of fact and naked truth that was!!
Sasa mwambie "msomi" wa leo sentensi kama hiyo uone hizo sababu milioni moja atakazokupa kukupinga.

Msomi wa leo anadhani wajibu wa kupata mtaji ni wa MZAZI WAKE au NDUGU. Yaani haoni jinsi gani yeye kama yeye anawajibika kuupata huo mtaji. Ukimwambia hivyo anasema basi ngoja nitafute AJIRA KWANZA. Akiikosa ajira analaumu system. Hilo ndo tatizo la kusoma bila kuelimika. Maana wasomi walioelimika wapo wengi tu na wamefanikiwa kupiga hatua...







Wasomi wengi leo ndo wanaongoza kuikosoa na hata kuitukana serikali kwenye mitandao ya kijamii kwa nini hawana ajira. Seriously?

Kazi ya elimu ni kukusaidia kuujua WAJIBU WAKO kama msomi. Kama unadhani nauli ya kusambazia CV ni wajibu wa mzazi wako hivi utaacha kudhani mtaji wa biashara yako ni wajibu wake pia?
Sadly hiyo ndo MINDSET ya jamii ya wasomi walio wengi. Who shall deliver us from that mess kama tusipofundishana ukweli?

Nimeeleza pia kuwa kazi ya elimu ni kukuasaidia KUTAMBUA NA KUKABILI changamoto zako. Your challenges. Na ndo hapo unapokuta msomi changamoto yake hajui kama ni yake au hataki kukubakli kuwa ni yake. Mfano changamoto ya nauli niliyoiainisha hapo juu. Kumbuka kuwa walimu wako wana wajibu wa kukufundisha yale waliyofundishwa kukufundisha. Get it? Kwa hiyo wanakufundisha kwa LIMITATIONS za mitaala. Ndo maana kuna mambo yanaitwa EXTRA CURRICULA ndugu yangu. Na ndo maana pia kuna elimu nje ya madarasa yako ya chuo. Mfano elimu ya ujasiriamali.

So ni wajibu WAKO kuitafuta hiyo elimu popote ilipo. Huo siyo wajibu wa lecturer wako. Siyo wajibu wa lecturer wako kukufundisha jinsi ya kutunza pesa zako maishani na kuziwekeza nk. Hayo mambo kasome vitabu vya kina Kiyosaki na kina JIM ROHN ujifundishe mwenyewe.


Kama hutaki au unaona USUMBUFU sawa tu ni mindset yako iko flawed so good luck. But ukifikiri kuwa kazi ya kukufundisha kuhusu mafanikio kifedha ni ya mwalimu wako wa Book Keeping au Commerce basi unapoteza muda wako. Huyo kazi yake ni kukusaidia kujua kuhusu mahesabu ya matajiri ukaajiriwe upate kuishi angalau. Jim Rohn alisema “FORMAL EDUCATION WILL MAKE YOU A LIVING BUT SELF EDUCATION WILL MAKE YOU A FORTUNE” akimaanisha elimu hii ya madarasani na vidato nk inaweza kukutengenezea kipato cha kuishi lakini ukitaka utajiri basi tafuta elimu ya kujifunza kivyako nje ya madarasa.


Hiyo ndo nayosema kuhusu kusoma vitabu na kuhudhuria semina mbali mbali nk. Huo ni wajibu WAKO. Kama ulikuwa hujui nakukumbusha.
Sasa elimu ya miaka 17 darasani toka ulivyoanza chekechea yaani vidudu

hadi chuo kikuu kama haiwezi kutengeneza nauli tu ya kusambazia CV hiyo ni USELESS EDUCATION hata kama ukijisikia vibaya ninaposema hivyo. Elimu ya miaka 17 mfululizo yenye notes na notes ma-counter book na ma-counter book quire 1 mpaka quire 4 kama haiwezi kukusaida kujiajiri hadi uanze kulalamikia SERIKALI ina maana elimu hiyo haijakusaidia kutatua changamoto zako mwenyewe then tunachoweza kusema kuhusu hiyo elimu ni kuwa that "education" is USELESS.

Elimu ambayo ukipata ajira halafu bahati mbaya ukaambiwa cheti chako ni feki licha ya kwamba elimu ndiyo unayo lakini hiki cheti ulichakachua halafu badala ya kusonga mbele unataka kuishtaki serikali na unaanza kulalamika kwenye Jamii Forums kwa nini umefukuzwa kazi ujue elimu hiyo unayodai unayo ni USELESS.

Elimu inapaswa kukufanya kuwa #RESOURCEFUL.

Mojawapo ya vitu ninavyofundisha my business associates kwa sasa ni hiki. Kuwa resourceful. Yaani kuwa na majawabu ya changamoto zako wakati wote. Siyo kulalamika na kulaumu. Kulalamika na kulaumu ni dalili ya kuwa na USELESS EDUCATION. Yes maana kama umefukuzwa kazi kihalali halafu huoni wapi pa kuanzia na unasema umesoma basi hiyo elimu ni USELESS. Yaani siyo USEFUL. Bora ungekaa nyumbani ukachunga ng’ombe ungekuwa mmiliki wa ng’ombe lukuki saivi.

Vijana wengi wa vyuo wako kwenye mitandao ya kijamii wanalalamikia vitu vya ajabu. Mtu yuko chuo cha SAUT Mwanza halafu unakuta ameandika comment ya kulaumu serikali kuhusu EXPANSION JOINTS za hostel za UDSM. Ok naelewa ni kutoa maoni. But huyu huyu mtu hapo alipo ukimuuliza wajibu wake ni upi na changamoto zake atakapomaliza masomo ni zipi na amejiandaa vipi kuzikabili majibu hana kabisa. Halafu anasema ana majibu kuhusu expansion joints. Hapo ana mwaka wa 14 toka aanze kusoma madarasani tangu chekechea. Kesho tena akisikia serikali imepiga mnada ng’ombe analalamika tena. Keshokutwa akisikia sijui mbunge gani kahama chama analalamika tena. Wajibu wake hajui. Hajui hata akigraduate hela ya kupigia picha za kumbukumbu ya graduation itatoka wapi yeye anajua tu hiyo ni changamoto ya watu wengine yeye kazi yake ni kutoa maoni facebook na kutuma vikatuni WhatsApp. Badala muda huo angeutumia kusoma vitu vingine vya kimaisha na kupata maarifa na ujuzi wa KUPAMBANA NA HALI YAKE YA BAADAYE yeye haoni hilo. Mwisho elimu yake yote inakuwa USELESS tu.

Mnawapa wazazi wenu stress zisizo za msingi kwa sababu ya kutotambua wajibu wenu mapema. Unagraduate mzazi au mlezi badala apumzike but ndo anawaza kukupa tena nauli maana boom huna tena. Mzazi au mlezi anawaza kukulisha na kukuvisha na kukulipia umeme maji nk. Bado hata kuomba Mungu upige hatua huombi mzazi ndo apige magoti kukuombea. Hivi hiyo elimu kazi yake nini? That is why nikauliza UMEELIMIKA AU UMESOMA TU? ARE YOU REALLY EDUCATED OR JUST SCHOOLED?

Joho la graduation litakuwa na maana sana kama unaweza kutatua changamoto na kutimiza wajibu wako. Otherwise halina tofauti na dera tu!

Wasomi ambao ni just schooled hata wakienda serikalini au bungeni hawako RESOURCEFUL. Tatizo la jimboni kwake ambalo lingetakiwa akae na wananchi wake na madiwani wakalitatue na ingewezekana kabisa lakini yeye analipeleka Facebook kulalamikia serikali. Huyo elimu yake ni USELESS. Hawa ndo wabunge wasio na MAJIBU bali ni kulaumu na kulalamika from January to DECEMBER halafu January mosi wanaandika HAPPY NEW YEAR. Then wanaanza tena kulalamika!

Laiti kama wasomi wangetambua wajibu wao na kubuni njia za kutatua changamoto zao wenyewe kwanza sidhani kama nchi hii ingekuwa na changamoto zilizopo leo. Maana licha ya kuwa wasomi ni wachache lakini kama wakiwa na impact nzuri basi CHACHU KIDOGO ITACHACHUA DONGE ZIMA.

Binafsi niliona kuwa naweza kuchangia kwa kubadili fikra za vijana hasa walioko vyuoni bado ili waanze kujifunza jinsi ya kuwa RESOURCEFUL wao kwanza. Maana kama atamaliza chuo halafu elimu ya chekechea hadi chuo kikuu haiwezi kumzalishia nauli ya daladala sh 600/- mpaka apewe, sasa huyu ataweza kutatua changamoto za taifa lake kweli?

Hawa ndo wanawaza kuingia duniani kama ABIRIA. Yani anataka abebwe na mfumo. Akute nauli zipo, akute ajira zipo akute mishahara ni minono akitaka kuanza biashara akute mitaji ipo tu hapo inamngoja. Passenger mindset. (Makala inayofuata nitazungumzia hili. Be ready). Kwa kifupi elimu imemfanya asiweze kabisa KUFIKIRIA. And so imekuwa kwake ni useless education.

Elimu ikiwa useless haitakusaidia hata KUTAMBUA na KUHANDLE mafanikio yako. Kuna wasomi wengi walipata nyadhifa kubwa na kwa kuwa wana elimu ambayo huwa haimuandai mtu kujua kama sasa ndo kafanikiwa au la basi wamejikuta wakitolewa kwenye nyadhifa zao bila kutarajia. Ndo unashangaa mtu anatolewa kwenye uwaziri analalamika. Huyo elimu yake imekuwa useless kwake. Na ijapokuwa bado anaweza kuonekana yupo juu kimaisha lakini ni kwamba alishindwa kutambua kuwa sasa amefanikiwa na afanyeje ili mafanikio hayo yadumu – come what may, yaani afanyeje ili awe INDISPENSABLE. Nawafananisha na kijana mwanamuziki aliyetamba sana enzi hizo Mr. Nice ambaye bila shaka wakati ule hakujua kuwa ndo ilikuwa peak yake ya mafanikio na wengine wengi ambao leo wanaweza kuwa wanapitia kipindi kigumu kiuchumi na hawajui kilichotokea ni nini.

Elimu inapaswa ikufanye utambue kuwa sasa hapa ndo kilele cha mafanikio yangu kwa NJIA HII niliyoichagua mimi na ikusaidie kuhandle hiyo success yako.
Kuna wasomi wengi wazuri wamestaafu lakini huwezi kufananisha kiwango cha ELIMU yao na maisha yao ya kustaafu.

So sad, but so true.

Hapo ndo unaona tofauti ya SCHOOLING na REAL EDUCATION. Ngoja nikupe kashule kadogo tena hapa. Ni hivi kuna aina kadhaa za elimu:

1.       LITERACY EDUCATION.
Hapa unaandaliwa kujua kusoma na kuandika na kwa dunia ya leo na kuwa computer literate pia.. na ukishajua hayo unaanza kufundishwa mambo ya msingi kama URAIA, LUGHA, SAYANSI kidogo, HISTORIA nk. Hii hapa kwetu inaanza chekechea hadi High School. Miaka 14. Imagine!!

2.       PROFESSIONAL EDUCATION
Hii sasa ndo wanataka uwe MTAALAMU labda wa sheria, au wa utabibu, au ualimu au uhandisi nk. Hii ndo unapata vyuoni sasa. Miaka mitatu minne hadi mitano (mfano kwa madaktari).

3.       FINANCIAL EDUCATION
Hii ni elimu ya mafanikio kifedha hufundishwi shuleni hii.
Hii ndo unapaswa kutafuta mwenyewe sasa. Kwenye semina sijui Mwakasege anafundisha kuhusu fedha go and listen. Sijui James Mwang’amba anafundisha kuhusu uchumi nenda kajifunze au pata vitabu vyake. Sijui kaja Strive Masiyiwa kutoka Zimbabwe nenda kajifunze. Sasa kama wewe unataka tu matamasha-tamasha halafu vitu kama hivi hutaki basi bado hujatambua WAJIBU wako vizuri.

Sasa imagine ndo hujapata hii elimu ya tatu halafu umeajiriwa hadi ukastaafu… unadhani kitatokea nini hapo? Si ndo una miaka 60 ndo unawaza kuanza mradi wa kufyatua matofali mara mafundi wachakachue ule hasara mara roli lako la mchanga limekamatwa na nyara za serikali kwenye mchanga wako. Kwa sababu ya umri changamoto kama hizo zinakulemea kirahisi. Au ndo unaanza kuwaza kufuga kuku mara wanakufa na huku una mtoto yuko Chuo Kikuu naye hajitambui bado mpaka nauli anakuomba wewe mstaafu. Huku unasikia raisi kwenye TV anasema vyuma vitakaza hadi vitavunjika! Unaiangalia TV hata hujui uifanyeje.

Hiyo ndo hatari ya kufikiri hizo elimu za namba 1 na 2 zimekutosha kwa kuwa unapata mshahara ukasahau kuwa huna elimu namba 3 kwa kiwango kinachotakikana!

SO WHAT NOW?

Well..

Let’s be a bit practical now, shall we?

Kama wewe ni msomi especially kama bado upo masomoni hasa vyuoni basi angalia elimu yako mpaka sasa kama inaweza kukusaidia kupata vitu vifuatavyo bila kuajiriwa:

1.       Kodi ya nyumba angalau miezi sita.
Yaani hapo ulipo chuoni kwa elimu uliyowahi kupata toka chekechea hadi hapo ulipo sasa je unaweza kuitumia hiyo elimu bila kuajiriwa na ukazalisha kodi ya nyumba kwa miezi sita angalau? Kama huwezi basi elimu hiyo ya miaka 14 au zaidi mpaka sasa ni USELESS. Do something fast.

2.       Chakuka angalau cha wiki mbili mbele.
 Je elimu uliyonayo hadi sasa minus ajira inaweza kukufanya ukasurvive kwa upande wa kula kwa angalau wiki mbili mbele? Yani bila boom wala bila kuajiriwa wala bila kupewa hela na mtu. Wewe utumie elimu yako kugenerate income ya chakula. If not it is USELESS

3.       Vocha angalau mwezi mmoja.
Najua mawasiliano ni muhimu. Je elimu yako yaweza kukusaidia pia kutengeneza hela ya vocha kwa mwezi mmoja anagalau?

4.       Transport.
Je elimu uliyo nayo tukakuweka nayo mtaani utaweza kuzalisha nauli angalau nauli ya hata nusu mwezi bila kuomba mzazi?

5.       Mavazi.
Unaweza kuvaa nguo hizo hizo ukitaka but ukitamani kuvaa vizuri elimu uliyonayo unaweza kuigeuza pesa na ikakupa mavazi supposing kwamba ajira hupati wala hakuna wa kukupa?

See… najaribu tu kukusaidia kutambua kuwa hayo mambo ni WAJIBU WAKO. Na wewe kama msomi unapaswa kuwa mfano kwa ambao wanaitwa siyo wasomi. Sasa kama majibu yako hapo juu ni HAPANA kwa maswali yote hayo matano halafu bado unapoteza muda kwenye mitandao ya kijamii kuLIKE picha za Hamisa Mabeto na Zari au kubadili kwa nini watu wanahama vyama basi kuna tatizo kubwa kuanzia kwenye shingo yako kwenda juu!

Huwezi kuwa huna majibu ya maswali hayo hasa wewe msomi ambaye bado upo chuoni na bado hutaki kujifunza mambo EXTRA CURRICULA ya kukusaida kuanza mchakato wa kuwa msomi mwenye elimu USEFUL. Tambua wajibu wako, tambua changamoto zako, tambua mafanikio yako.
Hapo utakuwa UMEELIMIKA hakika.

Mtu aliyesoma tu anaweza kulalamika lakini mtu aliyeelimika anatoa majawabu ya changamoto. Mtu aliyesoma tu ana vitu vingi kichwani ambavyo havimsaidii yeye wala watu wanaomzunguka. Kichwa chake always kikiona changamoto kinajishughulisha na kutafuta nani wa kulaumu. Kichwa cha mtu aliyeelimika (BILA KUJALI KAISHIA DARASA LA PILI AU KAFIKA CHUO KIKUU PIA) kinajishughulisha na kutafuta njia ya kutatua changamoto ya kwake au za watu wengine kabisa. Ndo maana watu wamegundua M-PESA kutatua matatizo ya watu wengine badala ya kulalamikia foleni za benki kila siku. Hiyo ndo namaanisha kuwa #resourceful.

Bottomline: Never complain.

If you are not solving the problem you are not being helpful.


  1. Be EDUCATED, not just SCHOOLED.

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
WhatsAPP +255 788 366 511
Merry Christmas!