Jumapili, 24 Desemba 2017

ARE YOU EDUCATED OR JUST SCHOOLED? UMEELIMIKA AU UMESOMA TU?



ARE YOU EDUCATED OR JUST SCHOOLED?
UMEELIMIKA AU UMESOMA TU?

Neno ELIMU kwa watu wengi linafungamanishwa sana na neno SHULE. Yaani kwa watu wengi inaonekana mtu aliyekwenda shuleni ndo mwenye elimu. Ndiyo maana utasikia watu wakisema “Aah huyo jamaa kaenda shule huyo usimchezee”, na vitu vya aina hiyo.
Lakini kuihalisia kitu hiki tunachoita ELIMU tunakuwa tukimaanisha tu MFUMO RASMI WA ELIMU ama kwa lugha ya kiingereza FORMAL EDUCATION.

Na KUELIMIKA mtu anaweza kuelimika akiwa hata darasani hajaenda. Tafsiri yetu ya elimu ndo inatufanya tuone kama kwenda darasani ndo kuelimika.

Mfumo huu ambao sisi tumeurithi hasa kutoka kwa wakoloni ni mfumo ambao ulianzishwa ukiwa na malengo yake. Mfano wakati ambapo jamii ya watu waliofanikiwa huko Ulaya ilihitaji watu wa kuwatunzia pesa zao ilibidi taaluma zinazoshughuklikia mambo hayo zianzishwe yaani watu wa kutunza fedha za wengine. Hivyo wakaanza kufundishwa taratibu za ukitaka utunze pesa za mtu vizuri unatakiwa ufanyeje. Na ili kuthibitisha kuwa umeelewa kweli unapewa mitihani na ukifaulu unapewa cheti cha kwenda kumwonyesha mwenye hela zake zinazohitaji kutunzwa anakupokea unaanza kumsaidia mambo ya mahesabu yake.

 Hivyo hivyo wakati watu waliofanikiwa walipohitaji mtu wa kusaidia wafanyakazi wa huyu tajiri waishi vizuri kwa maelewano nk ilibidi watu wanaoitwa leo “Human Resource personnels” waibuke kama taaluma mpya.
Wakati ambapo watu wa kusaidia mitandao ya matajiri iende sawa wameibuka watu wa IT nk kama taaluma mpya.

Kwa hiyo kimsingi mfumo huu wa elimu ulianzishwa kwa ajili ya kumsaidia mtu aliyefanikiwa kiuchumi kuweza kupata watu #sahihi wa kumsaidia mambo yake #kitaalamu. Na siyo hasa kumsaida mtu maskini ili awe tajiri. No. Na nasema NO kwa sababu njia ya mtu kuwa tajiri haihusiani na kusomea uhasibu au IT au sheria nk. Sasa inawezekana kabisa mtu akasomea hivyo vitu na akawa tajiri lakini hatakuwa tajiri kwa sababu amesomea hivyo vitu bali kwa kuwa licha ya kusomea hivyo vitu amejihusisha na mambo mengine sahihi yaliyompelekea kuwa tajiri which means huyo mtu hata asingesomea hivyo vitu angeweza tu kuwa tajiri.

Bahati mbaya sana mfumo rasmi wa elimu (yaani formal education) umeonekana kwa sasa kuwa ndiyo ELIMU YENYEWE. Hiyo nasema ni bahati mbaya kwa sababu inaonekana tumesahau nini hasa MAANA (yaani kazi) ya kitu kinachoitwa ELIMU.

Tukijikita kwenye kujua maana halisi ya ELIMU yaani KAZI ya elimu ni nini tunaweza kuona hasa kuwa watu #wengi tuliopitia mfumo huo rasmi wa vidato na madarasa basi TUMESOMA tu na HATUJAELIMIKA per se. Yaani we are just schooled but not really educated.

Bahati mbaya mtu ukiongea vitu vya namna hii unaonekana eti unaiponda “elimu”. Mi sipondi kitu, Naeleza UKWELI as ninavyouona. Unaweza kupima maneno yangu kwa mizani ukaona kama yako sawa au hayako sawa na ukiona cha kukusaidia chukua. Ukiona hakuna cha maana pia Merry Christmas!
Nimeamua kuandika haya baada ya kuwa nimeongea na vijana wengi mno hasa walioko vyuoni na kugundua kuwa kuna tatizo kubwa mno la kimtazamo (a serious mindset problem) na ni kubwa kiasi kwamba tusipokuwa makini tutajenga jamii based on a LIE. Haina tofauti na hela za wakati wa JK ambapo zilionekana za bwerere na watu kudhani hayo ndo mafanikio YENYEWE wakati UKWELI WA MAMBO ni kuwa kama taifa tulikuwa tunaelekea kule wanyama aina ya DINOSAURS walikoelekea.


KAZI YA ELIMU

Sasa kimsingi kazi ya elimu (yoyote ile) ni kumuwezesha huyo anayeipewa hiyo elimu kuweza kufanya haya mawili:

(a)KUTAMBUA (to identify )
(b) KUKABILI/KUTATUA (to handle)

Sasa ni kutambua na kukabili nini? Jibu ni #kutambua na #kukabiliana na mambo haya matatu:

1.       WAJIBU WAKE
2.       CHANGAMOTO ZAKE
3.       MAFANIKIO YAKE

Hiyo ndo kazi ya elimu na hivyo definition yoyote ya neno EDUCATION  haitakuwa na maana kama hai-address mambo hayo hapo juu. Kwa hiyo kwa kifupi kama elimu uliyonayo haikusaidii kutambua na kukabili WAJIBU wako, CHANGAMOTO zako na MAFANIKIO yako basi hicho unachokiita elimu ni USELESS.

MFANO HAI
Jana nilikutana na binti mmoja anasomea mambo ya UFAMASIA katika chuo kimoja hapa jijini Dar es Salaam. Katika kuongea naye nikamuomba anitajie RESPONDIBILITIES zake angalau 5 hadi 10 kama mwanafunzi. Yaani yeye kama mwanafunzi anawajibu wa kufanya nini na nini. Huwezi kuamini alishindwa. Ina maana hajui huyu mtu kuwa wajibu wake ni nini. Unatarajia huyu mtu uje umpe hata hiyo ajira atajua wajibu huko kweli?

Wengi wanaoitwa WASOMI hawajui wajibu wao kabisa. Ndiyo maana si ajabu kuona amegraduate na anadhani wajibu way yeye kupata ajira ni wa SERIKALI.
Na ukijaribu kumwambia otherwise hamtoelewana kabisa. Yeye anajua akimaliza chuo kuna AJIRA. Yaani huko duniani yeye anajua kuna watu wana WAJIBU wa kumpa yeye ajira. Kuna watu wa kumpa yeye pesa.

Ni kwa sababu ya MINDSET hiyo ndo maana huyu mtu anamaliza chuo kikuu na akitaka kutembeza hata hizo CV anaamini mwenye wajibu wa kumpa nauli ya kusambazia CV zake ni MZAZI au MLEZI. Yaani yeye anadhani kazi yake ni kusoma tu basi. Vingine ni wajibu wa wengine. This is the challenge I’m addressing hapa.

Kuna wasomi wanadhani hawajafanikiwa kwa sababu serikali iliyopo ni ya CCM ...huyo anaamini Chadema wakishika dola tu kila kitu kitakuwa kama Ulaya. Kuna wasomi wanaamini hawajafanikiwa kwa sababu ya wazazi kutowaandalia “mazingira mazuri”. Sijui ndo yakoje mazingira hayo mazuri… kama kijana kutoka Tandale ambaye maneno “PENS DOWN” huenda hakumbuki lini mara ya mwisho ameyasikia na sasa anasambaza karanga zake NCHI NZIMA hadi nchi jirani. Yes Diamond Karanga.


na wewe unazinunua. Hivi huyu aliandaliwa mazingira gani na wazazi. Wewe bado unaendelea kusikia "pens down" mpaka leo na unalaumu wazazi bado?

Wasomi wengi wakiwaza kuanza biashara wanalalamika hawana MTAJI. Mchungaji wangu jana Jumapili akihubiri kanisani akasema hivi:

“Kama unashindwa kuanza biashara kwa sababu umekosa mtaji wa laki tano tu, yaani KAMA UTASHINDWA kuyaendea mafanikio yako kwa sababu ulikosa laki tano basi HUJITAMBUI KABISA!!”

What a powerful statement of fact and naked truth that was!!
Sasa mwambie "msomi" wa leo sentensi kama hiyo uone hizo sababu milioni moja atakazokupa kukupinga.

Msomi wa leo anadhani wajibu wa kupata mtaji ni wa MZAZI WAKE au NDUGU. Yaani haoni jinsi gani yeye kama yeye anawajibika kuupata huo mtaji. Ukimwambia hivyo anasema basi ngoja nitafute AJIRA KWANZA. Akiikosa ajira analaumu system. Hilo ndo tatizo la kusoma bila kuelimika. Maana wasomi walioelimika wapo wengi tu na wamefanikiwa kupiga hatua...







Wasomi wengi leo ndo wanaongoza kuikosoa na hata kuitukana serikali kwenye mitandao ya kijamii kwa nini hawana ajira. Seriously?

Kazi ya elimu ni kukusaidia kuujua WAJIBU WAKO kama msomi. Kama unadhani nauli ya kusambazia CV ni wajibu wa mzazi wako hivi utaacha kudhani mtaji wa biashara yako ni wajibu wake pia?
Sadly hiyo ndo MINDSET ya jamii ya wasomi walio wengi. Who shall deliver us from that mess kama tusipofundishana ukweli?

Nimeeleza pia kuwa kazi ya elimu ni kukuasaidia KUTAMBUA NA KUKABILI changamoto zako. Your challenges. Na ndo hapo unapokuta msomi changamoto yake hajui kama ni yake au hataki kukubakli kuwa ni yake. Mfano changamoto ya nauli niliyoiainisha hapo juu. Kumbuka kuwa walimu wako wana wajibu wa kukufundisha yale waliyofundishwa kukufundisha. Get it? Kwa hiyo wanakufundisha kwa LIMITATIONS za mitaala. Ndo maana kuna mambo yanaitwa EXTRA CURRICULA ndugu yangu. Na ndo maana pia kuna elimu nje ya madarasa yako ya chuo. Mfano elimu ya ujasiriamali.

So ni wajibu WAKO kuitafuta hiyo elimu popote ilipo. Huo siyo wajibu wa lecturer wako. Siyo wajibu wa lecturer wako kukufundisha jinsi ya kutunza pesa zako maishani na kuziwekeza nk. Hayo mambo kasome vitabu vya kina Kiyosaki na kina JIM ROHN ujifundishe mwenyewe.


Kama hutaki au unaona USUMBUFU sawa tu ni mindset yako iko flawed so good luck. But ukifikiri kuwa kazi ya kukufundisha kuhusu mafanikio kifedha ni ya mwalimu wako wa Book Keeping au Commerce basi unapoteza muda wako. Huyo kazi yake ni kukusaidia kujua kuhusu mahesabu ya matajiri ukaajiriwe upate kuishi angalau. Jim Rohn alisema “FORMAL EDUCATION WILL MAKE YOU A LIVING BUT SELF EDUCATION WILL MAKE YOU A FORTUNE” akimaanisha elimu hii ya madarasani na vidato nk inaweza kukutengenezea kipato cha kuishi lakini ukitaka utajiri basi tafuta elimu ya kujifunza kivyako nje ya madarasa.


Hiyo ndo nayosema kuhusu kusoma vitabu na kuhudhuria semina mbali mbali nk. Huo ni wajibu WAKO. Kama ulikuwa hujui nakukumbusha.
Sasa elimu ya miaka 17 darasani toka ulivyoanza chekechea yaani vidudu

hadi chuo kikuu kama haiwezi kutengeneza nauli tu ya kusambazia CV hiyo ni USELESS EDUCATION hata kama ukijisikia vibaya ninaposema hivyo. Elimu ya miaka 17 mfululizo yenye notes na notes ma-counter book na ma-counter book quire 1 mpaka quire 4 kama haiwezi kukusaida kujiajiri hadi uanze kulalamikia SERIKALI ina maana elimu hiyo haijakusaidia kutatua changamoto zako mwenyewe then tunachoweza kusema kuhusu hiyo elimu ni kuwa that "education" is USELESS.

Elimu ambayo ukipata ajira halafu bahati mbaya ukaambiwa cheti chako ni feki licha ya kwamba elimu ndiyo unayo lakini hiki cheti ulichakachua halafu badala ya kusonga mbele unataka kuishtaki serikali na unaanza kulalamika kwenye Jamii Forums kwa nini umefukuzwa kazi ujue elimu hiyo unayodai unayo ni USELESS.

Elimu inapaswa kukufanya kuwa #RESOURCEFUL.

Mojawapo ya vitu ninavyofundisha my business associates kwa sasa ni hiki. Kuwa resourceful. Yaani kuwa na majawabu ya changamoto zako wakati wote. Siyo kulalamika na kulaumu. Kulalamika na kulaumu ni dalili ya kuwa na USELESS EDUCATION. Yes maana kama umefukuzwa kazi kihalali halafu huoni wapi pa kuanzia na unasema umesoma basi hiyo elimu ni USELESS. Yaani siyo USEFUL. Bora ungekaa nyumbani ukachunga ng’ombe ungekuwa mmiliki wa ng’ombe lukuki saivi.

Vijana wengi wa vyuo wako kwenye mitandao ya kijamii wanalalamikia vitu vya ajabu. Mtu yuko chuo cha SAUT Mwanza halafu unakuta ameandika comment ya kulaumu serikali kuhusu EXPANSION JOINTS za hostel za UDSM. Ok naelewa ni kutoa maoni. But huyu huyu mtu hapo alipo ukimuuliza wajibu wake ni upi na changamoto zake atakapomaliza masomo ni zipi na amejiandaa vipi kuzikabili majibu hana kabisa. Halafu anasema ana majibu kuhusu expansion joints. Hapo ana mwaka wa 14 toka aanze kusoma madarasani tangu chekechea. Kesho tena akisikia serikali imepiga mnada ng’ombe analalamika tena. Keshokutwa akisikia sijui mbunge gani kahama chama analalamika tena. Wajibu wake hajui. Hajui hata akigraduate hela ya kupigia picha za kumbukumbu ya graduation itatoka wapi yeye anajua tu hiyo ni changamoto ya watu wengine yeye kazi yake ni kutoa maoni facebook na kutuma vikatuni WhatsApp. Badala muda huo angeutumia kusoma vitu vingine vya kimaisha na kupata maarifa na ujuzi wa KUPAMBANA NA HALI YAKE YA BAADAYE yeye haoni hilo. Mwisho elimu yake yote inakuwa USELESS tu.

Mnawapa wazazi wenu stress zisizo za msingi kwa sababu ya kutotambua wajibu wenu mapema. Unagraduate mzazi au mlezi badala apumzike but ndo anawaza kukupa tena nauli maana boom huna tena. Mzazi au mlezi anawaza kukulisha na kukuvisha na kukulipia umeme maji nk. Bado hata kuomba Mungu upige hatua huombi mzazi ndo apige magoti kukuombea. Hivi hiyo elimu kazi yake nini? That is why nikauliza UMEELIMIKA AU UMESOMA TU? ARE YOU REALLY EDUCATED OR JUST SCHOOLED?

Joho la graduation litakuwa na maana sana kama unaweza kutatua changamoto na kutimiza wajibu wako. Otherwise halina tofauti na dera tu!

Wasomi ambao ni just schooled hata wakienda serikalini au bungeni hawako RESOURCEFUL. Tatizo la jimboni kwake ambalo lingetakiwa akae na wananchi wake na madiwani wakalitatue na ingewezekana kabisa lakini yeye analipeleka Facebook kulalamikia serikali. Huyo elimu yake ni USELESS. Hawa ndo wabunge wasio na MAJIBU bali ni kulaumu na kulalamika from January to DECEMBER halafu January mosi wanaandika HAPPY NEW YEAR. Then wanaanza tena kulalamika!

Laiti kama wasomi wangetambua wajibu wao na kubuni njia za kutatua changamoto zao wenyewe kwanza sidhani kama nchi hii ingekuwa na changamoto zilizopo leo. Maana licha ya kuwa wasomi ni wachache lakini kama wakiwa na impact nzuri basi CHACHU KIDOGO ITACHACHUA DONGE ZIMA.

Binafsi niliona kuwa naweza kuchangia kwa kubadili fikra za vijana hasa walioko vyuoni bado ili waanze kujifunza jinsi ya kuwa RESOURCEFUL wao kwanza. Maana kama atamaliza chuo halafu elimu ya chekechea hadi chuo kikuu haiwezi kumzalishia nauli ya daladala sh 600/- mpaka apewe, sasa huyu ataweza kutatua changamoto za taifa lake kweli?

Hawa ndo wanawaza kuingia duniani kama ABIRIA. Yani anataka abebwe na mfumo. Akute nauli zipo, akute ajira zipo akute mishahara ni minono akitaka kuanza biashara akute mitaji ipo tu hapo inamngoja. Passenger mindset. (Makala inayofuata nitazungumzia hili. Be ready). Kwa kifupi elimu imemfanya asiweze kabisa KUFIKIRIA. And so imekuwa kwake ni useless education.

Elimu ikiwa useless haitakusaidia hata KUTAMBUA na KUHANDLE mafanikio yako. Kuna wasomi wengi walipata nyadhifa kubwa na kwa kuwa wana elimu ambayo huwa haimuandai mtu kujua kama sasa ndo kafanikiwa au la basi wamejikuta wakitolewa kwenye nyadhifa zao bila kutarajia. Ndo unashangaa mtu anatolewa kwenye uwaziri analalamika. Huyo elimu yake imekuwa useless kwake. Na ijapokuwa bado anaweza kuonekana yupo juu kimaisha lakini ni kwamba alishindwa kutambua kuwa sasa amefanikiwa na afanyeje ili mafanikio hayo yadumu – come what may, yaani afanyeje ili awe INDISPENSABLE. Nawafananisha na kijana mwanamuziki aliyetamba sana enzi hizo Mr. Nice ambaye bila shaka wakati ule hakujua kuwa ndo ilikuwa peak yake ya mafanikio na wengine wengi ambao leo wanaweza kuwa wanapitia kipindi kigumu kiuchumi na hawajui kilichotokea ni nini.

Elimu inapaswa ikufanye utambue kuwa sasa hapa ndo kilele cha mafanikio yangu kwa NJIA HII niliyoichagua mimi na ikusaidie kuhandle hiyo success yako.
Kuna wasomi wengi wazuri wamestaafu lakini huwezi kufananisha kiwango cha ELIMU yao na maisha yao ya kustaafu.

So sad, but so true.

Hapo ndo unaona tofauti ya SCHOOLING na REAL EDUCATION. Ngoja nikupe kashule kadogo tena hapa. Ni hivi kuna aina kadhaa za elimu:

1.       LITERACY EDUCATION.
Hapa unaandaliwa kujua kusoma na kuandika na kwa dunia ya leo na kuwa computer literate pia.. na ukishajua hayo unaanza kufundishwa mambo ya msingi kama URAIA, LUGHA, SAYANSI kidogo, HISTORIA nk. Hii hapa kwetu inaanza chekechea hadi High School. Miaka 14. Imagine!!

2.       PROFESSIONAL EDUCATION
Hii sasa ndo wanataka uwe MTAALAMU labda wa sheria, au wa utabibu, au ualimu au uhandisi nk. Hii ndo unapata vyuoni sasa. Miaka mitatu minne hadi mitano (mfano kwa madaktari).

3.       FINANCIAL EDUCATION
Hii ni elimu ya mafanikio kifedha hufundishwi shuleni hii.
Hii ndo unapaswa kutafuta mwenyewe sasa. Kwenye semina sijui Mwakasege anafundisha kuhusu fedha go and listen. Sijui James Mwang’amba anafundisha kuhusu uchumi nenda kajifunze au pata vitabu vyake. Sijui kaja Strive Masiyiwa kutoka Zimbabwe nenda kajifunze. Sasa kama wewe unataka tu matamasha-tamasha halafu vitu kama hivi hutaki basi bado hujatambua WAJIBU wako vizuri.

Sasa imagine ndo hujapata hii elimu ya tatu halafu umeajiriwa hadi ukastaafu… unadhani kitatokea nini hapo? Si ndo una miaka 60 ndo unawaza kuanza mradi wa kufyatua matofali mara mafundi wachakachue ule hasara mara roli lako la mchanga limekamatwa na nyara za serikali kwenye mchanga wako. Kwa sababu ya umri changamoto kama hizo zinakulemea kirahisi. Au ndo unaanza kuwaza kufuga kuku mara wanakufa na huku una mtoto yuko Chuo Kikuu naye hajitambui bado mpaka nauli anakuomba wewe mstaafu. Huku unasikia raisi kwenye TV anasema vyuma vitakaza hadi vitavunjika! Unaiangalia TV hata hujui uifanyeje.

Hiyo ndo hatari ya kufikiri hizo elimu za namba 1 na 2 zimekutosha kwa kuwa unapata mshahara ukasahau kuwa huna elimu namba 3 kwa kiwango kinachotakikana!

SO WHAT NOW?

Well..

Let’s be a bit practical now, shall we?

Kama wewe ni msomi especially kama bado upo masomoni hasa vyuoni basi angalia elimu yako mpaka sasa kama inaweza kukusaidia kupata vitu vifuatavyo bila kuajiriwa:

1.       Kodi ya nyumba angalau miezi sita.
Yaani hapo ulipo chuoni kwa elimu uliyowahi kupata toka chekechea hadi hapo ulipo sasa je unaweza kuitumia hiyo elimu bila kuajiriwa na ukazalisha kodi ya nyumba kwa miezi sita angalau? Kama huwezi basi elimu hiyo ya miaka 14 au zaidi mpaka sasa ni USELESS. Do something fast.

2.       Chakuka angalau cha wiki mbili mbele.
 Je elimu uliyonayo hadi sasa minus ajira inaweza kukufanya ukasurvive kwa upande wa kula kwa angalau wiki mbili mbele? Yani bila boom wala bila kuajiriwa wala bila kupewa hela na mtu. Wewe utumie elimu yako kugenerate income ya chakula. If not it is USELESS

3.       Vocha angalau mwezi mmoja.
Najua mawasiliano ni muhimu. Je elimu yako yaweza kukusaidia pia kutengeneza hela ya vocha kwa mwezi mmoja anagalau?

4.       Transport.
Je elimu uliyo nayo tukakuweka nayo mtaani utaweza kuzalisha nauli angalau nauli ya hata nusu mwezi bila kuomba mzazi?

5.       Mavazi.
Unaweza kuvaa nguo hizo hizo ukitaka but ukitamani kuvaa vizuri elimu uliyonayo unaweza kuigeuza pesa na ikakupa mavazi supposing kwamba ajira hupati wala hakuna wa kukupa?

See… najaribu tu kukusaidia kutambua kuwa hayo mambo ni WAJIBU WAKO. Na wewe kama msomi unapaswa kuwa mfano kwa ambao wanaitwa siyo wasomi. Sasa kama majibu yako hapo juu ni HAPANA kwa maswali yote hayo matano halafu bado unapoteza muda kwenye mitandao ya kijamii kuLIKE picha za Hamisa Mabeto na Zari au kubadili kwa nini watu wanahama vyama basi kuna tatizo kubwa kuanzia kwenye shingo yako kwenda juu!

Huwezi kuwa huna majibu ya maswali hayo hasa wewe msomi ambaye bado upo chuoni na bado hutaki kujifunza mambo EXTRA CURRICULA ya kukusaida kuanza mchakato wa kuwa msomi mwenye elimu USEFUL. Tambua wajibu wako, tambua changamoto zako, tambua mafanikio yako.
Hapo utakuwa UMEELIMIKA hakika.

Mtu aliyesoma tu anaweza kulalamika lakini mtu aliyeelimika anatoa majawabu ya changamoto. Mtu aliyesoma tu ana vitu vingi kichwani ambavyo havimsaidii yeye wala watu wanaomzunguka. Kichwa chake always kikiona changamoto kinajishughulisha na kutafuta nani wa kulaumu. Kichwa cha mtu aliyeelimika (BILA KUJALI KAISHIA DARASA LA PILI AU KAFIKA CHUO KIKUU PIA) kinajishughulisha na kutafuta njia ya kutatua changamoto ya kwake au za watu wengine kabisa. Ndo maana watu wamegundua M-PESA kutatua matatizo ya watu wengine badala ya kulalamikia foleni za benki kila siku. Hiyo ndo namaanisha kuwa #resourceful.

Bottomline: Never complain.

If you are not solving the problem you are not being helpful.


  1. Be EDUCATED, not just SCHOOLED.

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
WhatsAPP +255 788 366 511
Merry Christmas!

Jumanne, 12 Desemba 2017

CONFIDENCE WITHOUT KNOWLEDGE: LEARN FROM SIMON PETER (KUJIAMINI BILA MAARIFA: JIFUNZE KWA SIMON PETRO)


*****
Naongelea biashara na ujasiriamali.
*****

Shalom!

Namshukuru Mungu kwa kutuwezesha kuwa pamoja tena. Nawapenda sana.

Leo tujifunze pia jambo jingine muhimu katika ulimwengu wa biashara na ujasiriamali.

Katika kusoma Biblia ukikutana na habari za mtu aitwaye Petro aliyekuwa mmoja wa wanafunzi wa Yesu unaweza ukahisi huenda jamaa alikuwa kimbelembele sana.

Kwanza alipenda sana kujibu maswali kabla ya wengine. Ilikuwa ni kama tabia hivi.

Pili alipenda kutoa suggestions bila kuuliza wenzake wala nini. Mfano pale mlimani alipomwambia Yesu: "ukitaka NITAJENGA vibanda vitatu..."
(Mathayo 17:4)

Yaani anasema NITAJENGA wakati pale yuko na wenzake wawili. Kuna watu wanadhani alipanic labda. Lakini kama nilivyosema ukisoma habari zake zote utajua ilikuwa kama tabia yake pia kutaka kuwa tofauti.

Tatu alikuwa na uwezo wa kuchukua maamuzi magumu papo kwa hapo bila kuuliza mtu. Mfano alivyomkata mtu sikio akijaribu kuzuia Yesu asikamatwe.
(Yohana 18:10)

Nne alikuwa anaweza kutaka afanyiwe kitu cha tofauti na wengine bila kuhofia watawazaje kuhusu yeye.  Mfano kukataa kuoshwa miguu kisha "alipopigwa mkwara" akaona isiwe tabu wala nini ila kama vipi basi aoshwe na kichwani na mikono siyo miguu tu!
(Yohana 13:9)

Kwa kifupi wengine wanaweza kusema labda Petro alikuwa akifanya vitu kwa kukurupuka!

Lakini ukichunguza hayo mambo niliyoyataja na ukachunguza namna alivyokuwa akifanya mambo yake na ukizingatia kazi aliyokuwa akiifanya maishani kabla ya kumfuata Yesu (yaani UVUVI); unaweza kutambua kuwa Petro alikuwa mtu mwenye KUJIAMINI kupita kiasi. Uvuvi si kazi nyepesi. Kukaa macho usiku baharini mara mvua mara mawimbi tena uko kwenye kachombo kadogo lazima uwe ngangari! Kwa hiyo jamaa alikuwa anajiamini sana.


KUJIAMINI KWA PETRO

Na unaweza ukaona kujiamini huko wakati Yesu alipotokea juu ya maji halafu Petro akamwambia Yesu kama ni wewe kweli hebu niamuru na mimi nitembee juu ya maji! Yesu alipompa go-ahead jamaa hakufikiria mara mbili akatoka chomboni na kutembea juu ya maji! Aisee. Usifikiri ilikuwa rahisi. Ilikuwa ni confidence kubwa sana.
(Mathayo 14:29)


Ilikuwa tabia yake kabla hata ya kuongelea imani. Na Yesu alichagua WAVUVI makusudi akijua hawa siku wakielewa somo watapiga kazi bila woga. So Petro kwa confidence ileile akaingia baharini akitembea JUU YA MAJI pia.

Lakini mfano wa pili kusisitiza nature yake ya kujiamini kupita kiasi ilikuwa wakati Yesu alipowatabiria kuwa watamkimbia wote. Petro akasema (natumia maneno yangu hapa:) "AH WAPI..! LABDA HAWA WAOGA WAOGA. SIYO MIMI WEWEE. MIMI!?? MIMI BANA HATA KUFA NA WEWE NITAKUFA NA WEWE HATA WAKIKIMBIA WOTE HAWA! WE HUNIJUI KUMBE?"
(Story nzima pale Marko 14:29-30 uone maneno yake mwenyewe)


TATIZO LA PETRO

Lakini kumbe Petro alikuwa anajiamini YEYE KAMA YEYE. Yaani aliamini uwezo wake wa kuhimili mambo ya siku zote akasahau kuwa sasa alikuwa katika BUSINESS MPYA ambayo ilihitaji maarifa mapya ambayo alikuwa HANA!


MIMI NA WEWE

Hivyo ndivyo watu wengi tulivyo. Tunajiamini bila maarifa sahihi. Matokeo inakuwa ni DISASTER ingawa kwa neema ya Mungu tunasonga mbele.

Mojawapo ya kitu nilichoweka katika kitabu changu kitakachowajia baadaye ni kuwa wakati nilipoacha kazi ili kuanza safari ya kibiashara na ujasiriamali miaka kadhaa iliyopita nilikuwa najiamini kweli kweli!  Yaani ungenikuta wakati ule "ungenipisha njia" tu utake usitake. Nilikuwa najua mi noma. Nilikuwa najiamini kuwa kila kitu kitaenda sawa tu. Ndo maana nilikuwa tayari kushuka chomboni (ajira) na kutembea juu ya maji  (ujasiriamali). Na nikawa nasema yani mimi hata kampuni yangu isipoenda vizuri "Nitakomaa mpaka kieleweke tu maana mi noma."

Lakini kumbe nilikuwa natembea katika ujinga  (IGNORANCE) uleule wa ndugu yetu Petro tu, wa kujiamini bila kuwa na MAARIFA SAHIHI. Miaka miwili tu baada ya kuanzisha kampuni yangu nilikuwa na changamoto nyingi mno tofauti na nilivyokuwa nimetarajia. Nilijikuta ni wakati wa kulipa kodi na pesa hakuna, nilikuwa na wateja kadhaa lakini hawakuwa wakilipa kwa wakati na wengine kutolipa kabisa tofauti na matarajio yangu. Wafanyakazi wanahitaji mishahara inabidi nikope pesa kwa rafiki zangu kulipa baadhi ya mishahara nikitarajia wateja wakilipa nitarejesha. Wateja hawakulipa! Nina madeni. Ninadai watu pia. Nikajikuta ninapata stress ambayo sikuwahi kufikiria ingewahi kuwa hivyo. Hapo nikama nishatembea juu ya maji sasa uhalisia umetokelezea kuwa kumbe sijawa tayari kutembea juu ya maki kama nilivyodhani. Nilipata chest pains ambazo zilinipeleka Muhimbili bila kutarajia kwa mara ya kwanza katika maisha yangu. Hizo ni baadhi tu ya changamoto ambazo naweza kusema kwa sasa. Ziko nyingi.

Hii historia yangu kila mara huwa inanikumbusha ile story ya Petro alivyoanza kutembea juu ya maji kabla hajapata maarifa sahihi kuhusiana na IMANI YAKE. Alianza kuzama maana mashaka yaliibuka.

Hakuwa na maarifa sahihi kwa nini WENGINE (Yesu) waliweza kutembea juu ya maji.


UNATARAJIA KUANZA BIASHARA? JIFUNZE HAPA

Nimekuwa nikikutana na vijana mbali mbali everyday kuongea nao kuhusu biashara na ujasiriamali. Wengi wao hawana tofauti sana na Petro kwa mantiki hiyo niliyoieleza. Kama ilivyokuwa kwangu wakati naanza pia. Vijana wengi wanadhani mafanikio ni kama kutuma 'SMS'. Kwamba unatype tu kidogo kisha unabonyeza SEND afu tayari. Ndo maana wamekuwa WALEVI WA BETTING.

Ukweli ni kwamba mafanikio hasa katika biashara na ujasiriamali yanahitaji kupata MAARIFA sahihi ya kitu unachotaka kufanya. Kujiamini ni kuzuri lakini kudhani kuwa kujiamini kwako ndo kutaleta mpenyo kibiashara bila kuwa na maarifa sahihi ni kachumbari ya disaster! Biblia inasema Watu #wanaangamizwa kwa kukosa MAARIFA! Umeona ee?

So bila msaada sahihi UTAANGAMIA KIBIASHARA. Utasingizia biashara yako imerogwa na shangazi au na mpemba au shetani ameiinukia kumbe shetani yuko zake Brazil huko ni wewe tu huna maarifa sahihi. (Shetani hana uwezo wa kuwa kila mahali kwa wakati mmoja...he is not omnipresent).
Maarifa rafiki.
Kuwa mtu wa kufundishika.


Miezi kadhaa iliyopita niliandika makala iliyosema ukitaka kufanikiwa kibiashara epuka pesa za NDUGU, MARAFIKI na MAJIRANI. Na nikaeleza sababu na kutoa mifano. Nashukuru iliwasaidia watu wengi mno kupata maarifa SAHIHI kuhusu eneo la wateja na sasa wanasonga mbele.
Maarifa ni muhimu usijiamini tu ukaishia hapo.


MWONE PETRO TENA

Wakati Yesu anasema wote watamkimbia na Yesu akijua kuwa Petro kwa kujiamini kwake atasema YEYE HATOFANYA HIVYO. Yesu akaona amsaidie Petro maarifa kiduchu ya kumsaidia. Akamwambia Simoni "Shetani amewataka ninyi (ni kama ameomba ruhusa) apate kuwapepeta kama vile ngano lakini ninekuombea wewe ili imani yako isitindike"
(Luka 22:31 na kuendelea)

Lakini kwa kujiamini zaidi ndo hapo Petro akasema hatamwacha Yesu hata baada ya kupata information ambayo alikuwa hana.

Kumbe!

Yesu alitaka kumwonyesha Petro kuwa kujiamini kwako kutakwama tu mahali maana kuna vitu bado hujui. Na kama huamini ngoja uone muda wa jogoo kuwika ukifika kabla hajawika utakuwa umeshanikana mara tatu wewe huyo huyo.

Kumbe shetani alikuwa na ruhusa ya kuwapepeta kina Petro na Petro hajui.

Kumbe Yesu alikuwa ameshamwombea Petro ili asiache njia na Petro hajui.

Ila anajiamini balaa!
Wakati hajui kinachoendelea.


UNAJIFUNZA KITU?

Kuna vijana ukikaa naye anakwambia mimi nataka kufuga kuku. Au kulima mananasi. Au kufanya biashara fulani. Lakini anaishia tu kujiamini sababu labda ana amepata mtaji wa pesa anadhani amemaliza kila kitu.
Au kwa sababu alifaulu Chuo kwenye masomo magumu anahisi hakuna ugumu tena zaidi ya ule.
Anahisi yeye noma.

Mimi nilipoanza nilikuwa nadhani kampuni yangu itasambaa nchi za jirani ndani ya miaka mitano tu. Lakini mpaka mwaka wa pili unafika bado tuna ofisi moja Mbezi Beach na hatuna mawazo ya kwenda hata Morogoro tu hapo. Hahaaaa. Stress za kutosha. Kujiamini bila maarifa ndo huko.

Stress zikianza unaanza kujiona mjinga. Umeajiri watu bila kuwa na KNOWLDEGDE ya kutosha ya mambo. Unazama nao kwenye maji.


BUT WHAT TO DO?

Bila Petro kupata msaada wa kuombewa na Yesu imani yake ingetindika HAKIKA.
Ama bila kuokolewa pale majini alipoanza kuzama story yake ingeishia pale.


WHEN A STUDENT IS READY....THE TEACHER WILL SHOW UP.

Msaada huwa upo tu always. Baada ya kuanza bila maarifa ilifikia hatua nikasema sasa nataka maarifa sahihi. Wachina wana msemo unaosema siku zote mwanafunzi akishakuwa tayari basi mwalimu huwa anatokea. So nilikutana na watu walionisaidia MAARIFA SAHIHI na hayo ndo yamenisaidia kusimama hadi leo.

Kama unataka kujifunza pia hasa kwa mtu unayeanza kufanya biashara njoo tuongee. Hakika hitakuwa bure. Utajifunza mengi ya kukufaa. Leo mimi najiamini kwa sababu ya maarifa siyo kwa kuwa nilifaulu darasani no. Nimejenga imani juu ya KNOWLEDGE SAHIHI. Thats why ninachokifanya sasa kimesimama miaka minne na kimeanza kuzaa MATUNDA mengine sasa.

Usifanye biashara tu kwa kuamini utafanikiwa. Watu wa Mungu wengi wanadhani kwa sababu ya kutoa zaka na kufunga sana ndo unaweza kuwa KICHWA na si mkia katika biashara. Uhalisia ni kwamba wanaoongoza kibiashara (vichwa) katika nchi nyingi wana MAARIFA na SKILLS (UJUZI) ambayo wewe unayefunga tatu kavu kila mwezi hujajishughulisha sana kuyapata. Kanuni inasema ukikosa maarifa #unaangamizwa. Full stop.

Vijana wengi wanaanza biashara kwa "MZUKA" tu. Wako very pumped up. Na wanaweza kutengeneza mpaka pesa za kupiga nazo picha. Wanahisi tayari wamefanikiwa. Lakini sustainable financial success hawaipati. Why? Hawatafuti maarifa sahihi.

Kama ilivyokuwa kwa Petro kufanya mambo kwa kujiamini tu bila maarifa kulimfanya asikitike sana imekuwaje akamkana Yesu tena hata baada ya kupewa warning! Kwamba ilikuwaje KUJIAMINI KOTE kukayeyuka tena mbele ya #kijakazi wa kike?

Inanikumbusha wanaume ambao huwa wanasema wao siku wakioa basi mwanamke hawezi kuwaambia kitu. Watafute baada ya kuoa utashangaa sana walivyo "wapole" mbele ya wake zao. Ishu ni kuwa waliamini CONFIDENCE zao kabla ya kupata maarifa kuhusu mambo ya ndoa yalivyo na dynamics za mahusiano zilivyo.



Biashara na ujasiriamali vinafanana na maisha ya ndoa tu in a way. Kuna dynamics zake. Usione ukadhani. Confidence zako ni nzuri  lakini ukifikiri kuwa ndo unachohitaji ili kudumisha ndoa unaweza kushangaa sana. Na ndivyo na ujasirimali ulivyo. Unahitaji MAARIFA SAHIHI.

Confidence zilimliza Petro na akajifunza.
Usije kupata stress zisizo za lazima katika safari yako ya ujasiriamali na biashara bure kisa hukutaka kujifunza vitu muhimu.

Karibu sana kujifunza kama utakuwa interested. Good luck God bless you always!


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa
#WhatsApp +255 788 366 511