.
KIPI HUNA KATI YA PESA NA MUDA? PESA? MUDA? VYOTE?
Soma kidogo hapa.. Kuna watu wa aina NNE tunapoongelea pesa na muda.
1. WANA MUDA MWINGI ILA HAWANA PESA
Watu ambao hawana pesa ila wana muda wa bwerere. Hawajui thamani ya muda. Hawa ndo wale ambao hawajui cha kufanya. Anaamka mpaka analala usiku hana specific timetable. Unaweza kumkuta anaenda dukani ukamwambia nisindikize saluni na akakubali. Yupo yupo tu. Unaweza kuta ameingia Facebook hajui hata kwa mini. Basi tu kwa sababu ana bando. Akiperuzi akaona mahali wanaongelea mpira yumo. Akiscroll post za chini akakuta kuna mtu kapost kuhusu UKAWA yumo. Akikuta kuna mtu kapost mtu ana uvimbe mkuuubwa watu wameambiwa wacomment AMEN na yeye huyo anacomment AMEN. Kundi hili ni kundi lenye watu wengi mno. Watu wa aina hii kufanikiwa ni bahati nasibu. Labda kwa bahati tu akutane na post nzuri kama hii na post zingine nzuri huenda ikamsaidia. Otherwise hawa ndo hawaelewi maisha yanaenda wapi maana hawana kitu fulani specific wanachofanya. Wakisikia tu kuna kitu kiko kama dili hivi wanaenda. Wakikuta kumbe kinahitaji bidii na kujituma wanaondoka. Wanataka maisha mazuri yaje tu yenyewe. Hawa huwa na maisha magumu zaidi. Ukimwambia njoo nikuonyeshe njia bora zaidi anakuja. Coz muda anao. Hana shughuli maalumu. Wanahudhuria matamasha na semina nyingi mno lakini hawafanyii kazi chochote. Wamezoea kuishi bila mpangilio maalumu. Ndiyo default life yao. Wanarejea maisha yale Yale ya muda mwingi bila cha kufanya
2. WANA PESA ILA HAWANA MUDA
Hili ni kundi la watu wenye shughuli fulani ya kiuchumi. Labda ameajiriwa au amejiajiri. Wako busy kweli kweli. Na ukweli pesa inaonekana. Hawa huwezi kumwambia njoo tuonane akaja hapo hapo. Huyu lazima apange kwanza ratiba zake. Maana yupo busy. Au lazima aombe ruhusa kazini. Au labda atoroke ndo anaweza kupata muda wa kufanya mambo yake binafsi. Au asubiri weekend ambapo kila ratiba itategemea siku hizo mbili, kama ni ibada, usafi, kutembelea wagonjwa au ndugu kwenda mahali kuona labda kiwanja kinauzwa au kuona ujenzi au mradi wake unaendeleaje nk. Mara nyingi watu wa kundi hili hushindwa kufanya vitu vingi vinavyohusu maendeleo yako binafsi mfano kujisomea, kuhudhuria semina zinazofundisha mambo yanayoweza kuwa na manufaa kwake nk. Sababu ana ratiba iliyobana. Ukiwa na sherehe ukamwomba mchango hashindwi kukuchangia angalau chochote kile lakini muda wa kuja kujumuika na wewe ni vigumu akaupata.
Hili ni kundi ambalo kuna watu wanaitwa MIDDLE CLASS people. Watu wa maisha ya kati. Mambo yako si mabaya sana lakini si kwamba ni mazuri. Wasomi wengi na watafutaji wengi wapo hapa. Na wengi wao huishia kupata changamoto za kiafya ukubwani au uzeeni kama stress na maradhi mbali mbali nk. Sababu ya kutokuwa na muda hata wa kuangalia afya zao, mazoezi, kupumzika vizuri nk kwa kuwa walikuwa busy siku zote. Maisha ya watu hawa middle class mwishoni huja kuwa magumu kwa kuwa hata kuwa na muda na majirani tu ilikuwa ishu. Kwa kuwa wengi wana magari (mengi ni mkopo. Wengine gari la kazini) na kwa kuwa wanaweza kulipa kodi ya nyumba au hata kupata kakiwanja na Kuanza kujenga huko Malamba Mawili basi wanaridhika. Hawawezi kuota kumiliki nyumba Masaki au kununua kiwanja Upanga. Kama upo kundi hili lazima uanze kutafuta mbinu mbali mbali za kuyakabili maisha vizuri siku za usoni. Waangalie wastaafu ambao walikuwa busy zamani. Saivi utasikia mgongo, miguu, macho nk vinasumbua. Hawa ndo ukimkuta social media wengi wao wako critical kwa kila kitu. Maana haoni kama ana shida yoyote. Lakini siku akiambiwa kazi imeisha hata kama ana PHD utasikia "nimekosa mimi nimekosa sana".
Wakati alipokuwa akipewa mbinu mbadala alikuwa critical. Ukimwambia kitu anakuuliza wewe una nini? Default picture yake ni average life. Not extraordinary life.
3. HAWANA MUDA WALA HAWANA HELA
Ulishasikia mtu anaambiwa "busy for nothing"? Ni kitu kama hicho. Yani mtu unakuta labda ni kibarua tu mahali anatumwa kazi asubuhi mpaka jioni. Labda ameajiriwa kazi ya ulinzi, au gereji, au kwenye mradi wa ujenzi anabeba zege au kupaka rangi. Hashindi njaa ni kweli lakini ukweli hana hela. Wala hatamani kuendelea kuwa hivyo. Kuamka alfajiri kulala saa tano usiku. Hela anayopata inatosha kula kwa mama ntilie tu na nauli. Basi.
Hawezi kuota hata gari. Hata ya mkopo. Maana hata hakopesheki. Huyu hata muda wa Facebook ni nadra akiingia ni kupitisha macho afu anatoka. Au hata simu ya Facebook hana.
4. WANA MUDA NA WANA PESA
Hapa ndo utakuta wale ambao hana tena shida ya pesa. Pesa iko. Hana tena shida ya muda. Akihitaji kwenda mahali haombi ruhusa wala kuaga mtu labda kumuaga mwenza wake tu. Anaweza kusikia kuna shamba linauzwa mahali na hahitaji kutafuta hela tena ili akalinunue bali anaanza michakato ya kisheria pale pale kununua kama amelipenda. Kuna siku nilienda Morocco Square hapo Kinondoni jirani na Airtel kuna Apartments zinajengwa nikaonana na watu wa NHC waliokuwa wanakagua ujenzi unaendeleaje. Nikawauliza hizo apartments zinauzwaje wakasema kuna za milioni 600 na za milioni 800. Na unatakiwa kulipa cash 10% (yaani aidha milioni 60 au 80 cash) halafu inayobakia unaweza kuimalizia ndani ya miezi 12. Na kuna watanzania kadhaa wamenunua tena kwa hela halali. Hawa wako kundi hili hapa. Hela ipo. Muda upo.
Kuna watu walienda kutembea Marekani kibiashara walipokuwa njiani kurudi wakapita mahalinchi nyingine wakakuta kuna mnada wa nyumba kwenye nchi hiyo. Hawakujiuliza mara mbili wakanunua. Kuna wazee fulani wana mtoto wao alikuwa akisoma Canada. Alipograduate wakamuuliza unataka kuishi wapi akasema huku huku Canada wakamnunulia nyumba Canada. Ukisikia hivyo unaanza kuwaza ni mafisadi. Mawazo yako ninkuwa bila ufisadi watu hawanunui nyumba Canada. Kwa taarifa yako Hawa siyo waajiriwa serikalini wala popote ni wafanya biashara.. Kundi la watu kwenye pesa. Na muda. Wanaweza kuamua kesho wakaenda kutembea visiwa vya Comoros. Watu wanaoishi kundi hili wana discipline kubwa ya maisha. Hawa ni watu wanaopenda kujifunza kila siku. Ukimwambia una idea hakatai kukusikiliza. Coz anaamini kuwa hata mafanikio yake yalitokana na kujifunza vitu vipya.Na watu wengi wanatamani kufika kundi hili. Lakini HAWANA discipline ya kujifunza tabia zinazoweza kukufikisha huko.
Swali muhimu tu la kujiuliza tu ni kuwa je, wewe upo kundi lipi.
Una muda mwingi lakini huna hela? = fukara
Una hela nyingi lakini huna muda? = middle class
Huna muda wala huna hela.. Vijisenti unavyopata vinaishia nauli kula kodi ya nyumba nk? = maskini
Au una muda mwingi na hela siyo shida tena? = tajiri.
Jibu unalo mwenyewe. Hakuna mchawi. Shida siyo Magufuli shida ni wewe kuamua kujifunza how utoke hapo ulipo au uendelee kusubiri Tanzania ya Viwanda.
Sisi tupo katika program ya kusaidiana mawazo tu. Nini unaweza kufanya kufika kundi hilo la nne. Kama unataka kujifunza karibu.
WhatsApp #o788366511 au #o752366511. Mafunzo ni bure ila tu uwe *serious.* So kama unaona unahitaji kujifunza au una ndugu yako rafiki yako mdogo wako nk unayetaka aanze kujifunza mapema mambo muhimu badala ya kupoteza muda mtandaoni mpatie namba hizo.
Semper Fi
Andrea G. Muhozya
Darbes Salaam, Tanzania
East Africa
Jumatano, 21 Septemba 2016
Jumatatu, 12 Septemba 2016
UKIFA MASKINI HILO NI KOSA LAKO
Zamani nilikuwa nashangaa kwa nini Bill Gates anasema "kama ulizaliwa maskini hilo si kosa lako ila ukifa maskini hilo ni kosa lako" mpaka nilipogundua #makosa mengi ambayo watu #maskini hufanya. Makosa ya watu maskini ni mengi nitataja machache:
1. KUNA MTI WENYE MZIZI MMOJA?
Ulishawahi kuona mti wowote wenye mzizi mmoja? Hili nilifundishwa jana na mdogo wangu Josinah Leonard. Sasa maskini wengi wameshikilia ajira (au kibarua, au labda ana kakitu anauza) kama njia PEKEE ya kuwaingizia kipato wakati hata mwembe tu au mpapai au mti wowote ule una mizizi mingi tofauti tofauti ya kupata chakula na maji kutoka ardhini.
Ndo maana hakuna tajiri yeyote mwenye mkondo mmoja wa kipato. Wengi wanadhani Bill Gates anamiliki Microsoft tu. Ana vyanzo lukuki vya mapato. Kama wewe una chanzo kimoja cha mapato basi uko mbioni kufa maskini.
2. MAWAZO MGANDO
Kisha nikakumbuka pia maskini wengi wanafanya kosa la kuishi kwa mawazo ya zamani. Yani unakuta akiwaza biashara anawaza duka. Kwani kuna tajiri yoyote mwenye duka au vibanda 1000 vya MPESA? Hujiulizi?. Dunia imebadilika maskini hawabadiliki kichwani. Kampuni kubwa ya TAXI duniani (yani UBER) haimiliki gari hata moja. Lakini ndo kampuni kubwa ya usafiri wa TAXI duniani. Anatumia taxi za watu wengine. Wewe bado unawaza kununua bajaji na boda boda! Things have changed. You must also change. Kuna mengi ya kueleza hapa ngoja niendelee na mengine. Lakini hapo pia palinifanya nielewe kauli ya Bill Gates.
3. PERSONAL DEVELOPMENT
Maskini wengi hawasomi vitabu. Sikia hakuna tajiri asiyesoma. Bill Gates ana wiki mbili kwa mwaka ambazo yeye huzitumia kusoma vitabu vipya ambavyo hajawahi kusoma maishani
. Hebu jiulize Bill Gates anajifungia kusoma vitabu ili iweje? Wewe ukijifungia ndani ujue unaangalia series. Ukiulizwa umesoma vitabu vingapi mwaka huu hadi sasa January to September... Usikute labda hujasoma kabisa hata kimoja. Lakini message za WhatsApp ulizosoma mwaka mzima huu zinatosha kuchapisha magazeti ya Nipashe ya kujaa kwenye kabati lako la nguo! I mean that's a shame mate. Vitabu hutaki. Ukifa maskini hapo utakataa kuwa si kosa lako? Si unaona sasa kuwa utakubaliana na Bill Gates pia. Listen, SOMA VITABU. Acha kuishi kwa knowledge ya Mzumbe University sijui UDSM ya miaka mitano au 7 iliyopita sijui bachelor of nini? Soma vitabu huko ndo kuna maarifa. Mtaani hela hazifati Ph.D ya mtu. Kama ni hivyo maprofessor wangekuwa ndo matajiri. Knowledge ya pesa ina maarifa yake tofauti na Masters of Arts au Ph.D ya mambo ya mazingira. Kama chanzo chako cha taarifa za mafanikio bado ni Tumaini University au ni magroup ya WhatsApp utachelewa sana kujua habari za mafanikio. Hakuna tajiri asiyefanya personal development. Hata ungekuwa na elimu kubwa kiasi kipi kama hufanyi personal development utabakia kuwa significant katika maeneo mengine lakini si eneo la fedha. Kwa hiyo vitabu ni sehemu ya hiyo personal development. Kuna seminars, nk. Sasa jiulize semina ngapi zinazoongelea mafanikio umehudhuria mwaka huu.? Ngoja nikwambie kitu usipofanya Personal Development thamani yako itabaki kuwa ile ile ya miaka 7 iliyopita. Jana nilikuwa na kiongozi wangu mmoja katika biashara yetu. And akasema amepata fursa ya kualikwa sehemu kwenda kufanya TRAINING (mafunzo) kwa watu fulani wa "maana". Jumla ya hao watu ni 165. Jumla ya siku ambazo atatoa hayo mafunzo ni siku 5. Na kila mtu katika hao watu 165 atalipa sh 300,000/- kwa siku. Sasa fanya mahesabu sh laki 3 mara 165 hiyo ni hela yake ya siku halafu zidisha mara siku tano!! Umepiga hiyo hesabu? Sasa wewe unataka tu ukalime vitunguu au matikiti uwe milionea kesho. Maarifa unayo? Maarifa hujengwa taratibu. Siku nyingine ntaongelea vizuri zaidi kuhusu hiyo personal development.
4. TIME MANAGEMENT
Kosa jingine maskini wanafanya ni kupoteza muda. Time management mbovu. Hasa vijana. Aisee. Hawana ratiba. Ratiba pekee waliyonayo baadhi ya vijana ni ratiba ya mechi za premier league anajua ratiba za Manchester hadi mwakani. Lakini ratiba yake ya kila siku kwamba akiamka anaenda wapi hakuna. Hana hata kadiary au ka notebook hata kale ka sh elfu moja. Angalau awe anaandika vitu muhimu maishani nk.. Nothing. Ana magroup ya WhatsApp ya mpira, ya siasa yani moja linaitwa UKUTA 1 jingine UKUTA MAKAMANDA, UKUTA KANDA YA MAGHARIBI, UKUTA ORIJINO, mtu huyo huyo mmoja bado yuko magroup ya waliosoma pamoja na waliofanya kazi pamoja ambayo yote hayo habari kuanzia asubuhi hadi jioni ni UKUTA uleule. Anacopy message za huku anapeleka huku. Haya. Mwingine ana magroup HAPA KAZI TU, WATASOMA NAMBA, MAGUFULI JEMBE, CCM KAMPENI, UMOJA WA VIJANA, CCM VYUONI, ukimwona yuko busy utadhani karani wa chama. Wengine wako kwenye magroup ya NGONO TU maana huku Facebook na instagram kuna watu wanatangaza kutafuta namba ili wakuunge kwenye hayo magroup na unakuta namba 900 au zaidi. Unabaki unashangaa hawa watu muda huo wanaupata wapi? Hapo mtu akishindwa kufanikiwa ni kosa la mzazi? Au la mwenyekiti wa mtaa? Au Naibu Spika? Au la Kubenea? Kweli? Yani Kubenea anahusikaje kukufanya wewe ufanikiwe kiuchumi. Sipatagi connection. Sikia. Linda muda wako kwa WIVU MKALI na ujitenge na kila kitu kinachoiba muda wako. Time is MONEY.
5. KUTOFIKIRIA VIZAZI VIJAVYO
Kosa jingine maskini hufanya ni kutofikiria vizazi vijavyo. Sasa hii sijui laana? Maana wenzetu hawako hivyo.Mtu hafikirii kuwekeza kwa ajili ya watoto na wajukuu. Muda wako ukiutumia vizuri leo utawafanya watoto wako na wajukuu watumikiwe na mataifa. Lakini kwa style ya wengi wetu hii ya kujifikiria wenyewe ilimradi wewe unamudu kulipa kodi na kula na kuvaa basi watoto Mungu ataleta riziki. Khaaa? Kwa taarifa yako Mungu alisema unapaswa kuacha urithi mpaka kwa wana wa wanao (yani wajukuu). Sasa jiulize hiyo shughuli yako rasmi kwa sasa mwanao anaweza kuja kuiendeleza baada yako. Kwa ajira hiyo ni impossible. Mungu akikuchukua wanaweka tangazo moja kwenye notice board la kifo chako jingine kwenye gazeti la kutafuta mtu wa kujaza nafasi yako. Hiyo ndo reality. Hapo Kubenea hahusiki. Jamani msishangae namtaja sana Mhe. Kubenea ni mbunge wa jimbo langu na namtaja kuwakilisha wabunge wote. Sasa ukianza kuwaza kuhusu vizazi viwili baada yako utajiona jinsi ulivyo nyuma mno. Watu wanajifikiria wenyewe tu. Ndo maana ni rahisi kuridhika na vihela vidogo. Hutaki kuhangaika ili wajukuu waje wafaidi. Unataka ufaidi wewe kwanza eti unasema "kwa nini nijitese". Kwani kwa nini Yesu "alijitesa"? Ukiambiwa hivyo unasema" kwani mi Yesu?" shauri yako. Watoto wako au wajukuu watafukua kaburi lako afu watatoa hiyo skeleton waitandike bakora weee afu waizike tena. Omba ujengewe kaburi lako kwa nondo na zege. Wengi wanabaki maskini kwa mawazo ya ubinafsi wa kutowaza watakaokuja after you.
6. KUFIKIRI KUWA KUANZA BIASHARA INAHITAJI UWE NA MTAJI KWANZA
Wengi wamekwama hapa. Anafikiri kuwa inabidi atafute mtaji kwanza afu ndo atafute cha kufanya. Wakati anautafuta mtaji fursa zinaendelea kumpita. Akija kuupata anapata matatizo hela tena inatumika kutatua matatizo ya kifamilia. Anaanza upya tena. Mwisho anaamua kusema basi nahisi "Mungu hapendi". Maskini wengi wana kauli rahisi rahisi tu. "Si wote lazima tuwe matajiri". Anajijumlisha kwenye neno *wote*. Mtu anayefanikiwa anajua mtaji wa kuanza biashara ni kitu cha mwisho na ni kitu chepesi mno kuliko vingine vyote. Lakini wengi wanawaza mtaji. See? Kitu cha mwisho na *chepesi* anakifanya kiwe cha kwanza na kigumu.
Sasa hivi naielewa sana kauli hiyo hapo juu ya Bill Gates. Ukifa maskini hilo ni kosa lako. Anyway.. Kama unataka kujifunza zaidi mambo ya aina hii ama shida yako ni hapo kwenye namba 6 au namba 4 au namba 1 labda unawaza kuwa na vyanzo vingi vya mapato afu hujui unaanzia wapi na unatamani kupata ushauri au una biashara haiendi kokote mwaka wa sita sasa huenda kuna mahali unakosa basi njoo WhatsApp #o788366511 au #o752366511 ujifunze zaidi.
UKIBADILIKA, KILA KITU KITABADILIKA.
Semper Fi,
Andrea G Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
USHAURI WA BURE KWA WANAOWAZA KUFANYA BIASHARA
MAMBO YA KUZINGATIA KAMA UNATAKA KUINGIA KWENYE ULIMWENGU WA BIASHARA
Kuna mambo mengi ya kuzingatia kabla hujajiingiza kwenye biashara. Nimekuwekea baadhi ya mambo hayo hapa chini. Haya ni yale niliyojifunza on the ground ndani ya miaka yangu michache hii ya ujasiriamali toka mwaka 2011 katika biashara mbali mbali nilizofanya. Ukiyazingatia utaona faida yake.
1. HAKIKISHA UNA ELIMU YA BIASHARA
Simaanishi diploma sijui certificate ya chuo au zile notes za Commerce. No. Hiyo siyo elimu ninayomaanisha. Namaanisha aina ya elimu kwa vitendo kama vile apprenticeship. Yaani kujifunza kwa mtu taratibu uone jinsi biashara inavyofanyika. Kama hilo ni gumu kulingana na mazingira basi hakikisha biashara unayotaka kuifanya au mradi unaotaka kuanzisha una watu wanaofanya kitu hicho hicho walio tayari kukupa elimu kila siku hasa miaka miwili ya kwanza katika jambo hilo. Watu watakaokuwa tayari kukupa siri za mafanikio bila kukuficha. Watu watakaokuwa tayari kukushika mkono kwa dhati mpaka ufikie malengo yako.. Ukijifanya "gangwe", wewe ndo sijui "godzilla" kwa sababu shuleni ulipataga B+ ya Business Law itakula kwako mpaka upate mvi za kope kabla ya muda. Labda kama shida yako ni kufanya show off. Lakini kama shida yako ni kufanikiwa katika ulimwengu wa biashara unahitaji mtu anayejua hicho kitu vizuri ambaye yuko tayari kukupa information za wapi pa kukanyaga wapi pa kukwepa. Hii ndo elimu nayoiongelea.
2. USIDHARAU MWANZO MDOGO.
Usianze kitu kipya kwa gharama kubwa hususan kwa mara ya kwanza. Ukajikuta unakopa milioni 5, 10, 50, nk ili ukafanye biashara mpya ambayo hata hayupo mtu wa kukuelekeza kwa dhati namna ya kuifanya. Utaishia kupoteza hela za watu na kudaiwa na labda kupata stress au hata heart attack. Na kama utakuwa umeajiriwa bado utaathiri hata ajira yako sababu ya stress. Haya ninayasema kwa experience. Ukipenda chukua huu ushauri kwa umakini sana. Anza kitu chenye mtaji mdogo. Hata Biblia inasema si busara kudharau mwanzo mdogo. Usitake kuanza alipo Shigongo leo. Au Dewji. Kubali kuanza kidogo. Halafu ukue taratibu taratibu. Itakupunguzia stress zisizo za lazima. Nilijifunza hilo pia ndani ya miaka hii mitano ya ujasiriamali na biashara.
3. FANYA UTAFITI LAKINI JALI MUDA.
Fanya research kuhusu chochote ambacho unataka kufanya. Huenda umeshauriwa ufanye biashara fulani. Chochote ambacho mtu atakwambia ukafanye. Google kama ikibidi. Angalia information kuhusu hicho kitu. Tafuta walioifanya WAKAFANIKIWA. Yaani mfano unataka kuanza ufugaji kwa nini uende kwa walioanza wakashindwa wakati walioifanya wakafanikiwa wapo? Ukitaka kujiunga na chuo unauliza walio disco au waliofaulu? Fanya utafiti na kusanya zaidi information kutoka kwa waliofanikiwa kuliko waliofeli hiyo biashara. Bottomline is fanya utafiti wa kina. Ili ujiridhishe. Usisisimke tu.
Na utafiti usifanye miaka nenda rudi. Unataka kufanya biashara au kuumba dunia nyingine? Muda haukungoji. Na kuna vitu ukichelewa kuvifanya katika umri fulani au katika msimu fulani itakugharimu sana. Mfano kama ulikuwa unafanya utafiti wa kufungua Internet Cafe toka mwaka 2002 mpaka leo hivi hata ukiamua kufanya hiyo biashara leo si utakuwa unapoteza muda tu bure? Season yake ilishapita. Maisha hayakusubiri. Fanya utafiti ila jali sana muda.
4. KAMA HUTAKI KUOGA UMEVUA NGUO ZA NINI?
Nimeongelea ufanye utafiki. Sasa kama baada ya utafiti wako utaona moyoni mwako kuwa kuna manufaa ya kuifanya hiyo biashara au kufanya huo mradi basi usijiulize mara mbili. Fanya mara moja. Maana ukianza kujiuliza na wakati umeshafanya research yako vizuri ni dalili tu ya moyo wenye woga woga na wasiwasi ambao kwenye biashara itakuwa kikwazo cha mafanikio. Jifunze kuamini utafiti wako mwenyewe. Watu wengi wamekwama hapa eti. Woga woga tu. Woga si moja ya kitu cha kuja nacho huku ndugu yangu. Huku inabidi ujifunze kujiamini. Watu wengi huwa wanakwama hapa. Keshaona kuwa kitu anachotaka kufanya ni sahihi lakini anakuwa bado tu anasitasita. Yupo kama hayupo. Mwisho hela ya mtaji anakula na ule moto aliokuwa nao wa kuanzisha mradi au biashara unazimika anarudi nyuma hatua 50. Mpaka arudishe tena ule moyo wa kuanza tena miaka mingi ijayo na wengine ndo basi tena. Anabaki mtazamaji na mkosoaji wa wengine wakati yeye hata kuanza alishindwa.
5. NANI ANAIFAHAMU VEMA HIYO BIASHARA?
Labda unataka kuanza kilimo tena cha matikiti labda. Je unamfahamu mtu yeyote ambaye anaijua vizuri biashara hiyo nje ndani? Kuanzia mbegu, aina (species) za hayo matikiti, misimu ya mauzo, wadudu shambulizi, nk. Usiombe ushauri kwa mtu asiyejua hiyo biashara kwa namna moja au nyingine. Mfano umeamua kuuza nguo. Unaenda kuomba ushauri kwa muuza magazeti kuhusu biashara. Yeye biashara yake ni leo kwa leo. Yaani leo kama habari UKUTA na kesho habari ikawa kupanda miti basi mambo ya jana yanakuwa siyo dili tena. Sasa unadhani atakushauri nini? Au unataka kuanza biashara ya kuuza mafuta ya mzeituni (Olive Oil) unaenda kuuliza kwa mama ntilie eti akwambie kama yana soko wakati yeye anapikia mafuta ya kuchakachua. Unadhani atakwambia ukafanye hiyo biashara? So don't ask the wrong people. Eti unakuta mtu anasema "mimi mama yangu ndo my best friend lazima nikamuulize". Wakati hana ufahamu nayo. Mbona ulikuwa humuulizi ALGEBRA ulipokuwa shule? Si unaona ee? So..Tafuta mtu anayeijua.
6. UNA NGOZI YA FARU?
Ukitaka ku excel kwenye biashara lazima uwe na ngozi ya faru. Niliwahi kujifunza mahali kuwa Faru ana ngozi ngumu mno. Na kwamba zamani wakati wa zana duni za uwindaji walikuwa wakitumia mishale kwa ngozi ya Faru ilikuwa ikishindwa kupenetrate ile ngozi yake. Na pia kuwa faru anaweza kuwa na ndege mgongoni kwake wanakula wadudu au wanarukaruka pale mgongoni na wala asifeel kama wapo. Inabidi uwe na ngozi ngumu. Kuna watu watakukatisha tamaa, kunachangamoto na mishale mingi itarushwa hakikisha una ngozi ngumu na utashinda hiyo mikikimikiki.
7. NINI TAFSIRI YA MAFANIKIO KWAKO?
Kwa wengi mafanikio ni kupata pesa nyingi. Wengine hata ukimuuliza pesa nyingi kwako ni sh ngapi hana idea. Wengine mafanikio kwao ni magari na majumba wengine mafanikio ni starehe, wengine mafanikio ni kutoa sadaka na kusaidia wengine zaidi wengine mafanikio ni kuajiri watu wengi, wengine mafanikio ni kusomesha watoto international school wengine mafanikio ni kuwa na vitega uchumi wengine mafanikio ni kuwa na akiba kubwa benki nk wengine mafanikio ni kula vizuri na kuwa na afya bora nk. Wewe kwako mafanikio ni nini? Ili ufanikiwe lazima kwanza uwe na definition ya mafanikio yenyewe. La sivyo unaweza kupata kila kitu katika biashara na bado ukawa unahisi hujafanikiwa kabisa. Hii imewasumbua wengi.
Kuomba Mungu ni jambo constant wala sina haja kukwambia. Ni sawa na kuoga. Mpaka uambiwe? Nadhani unanielewa.
So if unapenda kujua zaidi biashara sahihi katika zama hizi karibu kwa WhatsApp #o788366511 au #o752366511 kujifunza.
Semper Fi,
Andrea Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
Kuna mambo mengi ya kuzingatia kabla hujajiingiza kwenye biashara. Nimekuwekea baadhi ya mambo hayo hapa chini. Haya ni yale niliyojifunza on the ground ndani ya miaka yangu michache hii ya ujasiriamali toka mwaka 2011 katika biashara mbali mbali nilizofanya. Ukiyazingatia utaona faida yake.
1. HAKIKISHA UNA ELIMU YA BIASHARA
Simaanishi diploma sijui certificate ya chuo au zile notes za Commerce. No. Hiyo siyo elimu ninayomaanisha. Namaanisha aina ya elimu kwa vitendo kama vile apprenticeship. Yaani kujifunza kwa mtu taratibu uone jinsi biashara inavyofanyika. Kama hilo ni gumu kulingana na mazingira basi hakikisha biashara unayotaka kuifanya au mradi unaotaka kuanzisha una watu wanaofanya kitu hicho hicho walio tayari kukupa elimu kila siku hasa miaka miwili ya kwanza katika jambo hilo. Watu watakaokuwa tayari kukupa siri za mafanikio bila kukuficha. Watu watakaokuwa tayari kukushika mkono kwa dhati mpaka ufikie malengo yako.. Ukijifanya "gangwe", wewe ndo sijui "godzilla" kwa sababu shuleni ulipataga B+ ya Business Law itakula kwako mpaka upate mvi za kope kabla ya muda. Labda kama shida yako ni kufanya show off. Lakini kama shida yako ni kufanikiwa katika ulimwengu wa biashara unahitaji mtu anayejua hicho kitu vizuri ambaye yuko tayari kukupa information za wapi pa kukanyaga wapi pa kukwepa. Hii ndo elimu nayoiongelea.
2. USIDHARAU MWANZO MDOGO.
Usianze kitu kipya kwa gharama kubwa hususan kwa mara ya kwanza. Ukajikuta unakopa milioni 5, 10, 50, nk ili ukafanye biashara mpya ambayo hata hayupo mtu wa kukuelekeza kwa dhati namna ya kuifanya. Utaishia kupoteza hela za watu na kudaiwa na labda kupata stress au hata heart attack. Na kama utakuwa umeajiriwa bado utaathiri hata ajira yako sababu ya stress. Haya ninayasema kwa experience. Ukipenda chukua huu ushauri kwa umakini sana. Anza kitu chenye mtaji mdogo. Hata Biblia inasema si busara kudharau mwanzo mdogo. Usitake kuanza alipo Shigongo leo. Au Dewji. Kubali kuanza kidogo. Halafu ukue taratibu taratibu. Itakupunguzia stress zisizo za lazima. Nilijifunza hilo pia ndani ya miaka hii mitano ya ujasiriamali na biashara.
3. FANYA UTAFITI LAKINI JALI MUDA.
Fanya research kuhusu chochote ambacho unataka kufanya. Huenda umeshauriwa ufanye biashara fulani. Chochote ambacho mtu atakwambia ukafanye. Google kama ikibidi. Angalia information kuhusu hicho kitu. Tafuta walioifanya WAKAFANIKIWA. Yaani mfano unataka kuanza ufugaji kwa nini uende kwa walioanza wakashindwa wakati walioifanya wakafanikiwa wapo? Ukitaka kujiunga na chuo unauliza walio disco au waliofaulu? Fanya utafiti na kusanya zaidi information kutoka kwa waliofanikiwa kuliko waliofeli hiyo biashara. Bottomline is fanya utafiti wa kina. Ili ujiridhishe. Usisisimke tu.
Na utafiti usifanye miaka nenda rudi. Unataka kufanya biashara au kuumba dunia nyingine? Muda haukungoji. Na kuna vitu ukichelewa kuvifanya katika umri fulani au katika msimu fulani itakugharimu sana. Mfano kama ulikuwa unafanya utafiti wa kufungua Internet Cafe toka mwaka 2002 mpaka leo hivi hata ukiamua kufanya hiyo biashara leo si utakuwa unapoteza muda tu bure? Season yake ilishapita. Maisha hayakusubiri. Fanya utafiti ila jali sana muda.
4. KAMA HUTAKI KUOGA UMEVUA NGUO ZA NINI?
Nimeongelea ufanye utafiki. Sasa kama baada ya utafiti wako utaona moyoni mwako kuwa kuna manufaa ya kuifanya hiyo biashara au kufanya huo mradi basi usijiulize mara mbili. Fanya mara moja. Maana ukianza kujiuliza na wakati umeshafanya research yako vizuri ni dalili tu ya moyo wenye woga woga na wasiwasi ambao kwenye biashara itakuwa kikwazo cha mafanikio. Jifunze kuamini utafiti wako mwenyewe. Watu wengi wamekwama hapa eti. Woga woga tu. Woga si moja ya kitu cha kuja nacho huku ndugu yangu. Huku inabidi ujifunze kujiamini. Watu wengi huwa wanakwama hapa. Keshaona kuwa kitu anachotaka kufanya ni sahihi lakini anakuwa bado tu anasitasita. Yupo kama hayupo. Mwisho hela ya mtaji anakula na ule moto aliokuwa nao wa kuanzisha mradi au biashara unazimika anarudi nyuma hatua 50. Mpaka arudishe tena ule moyo wa kuanza tena miaka mingi ijayo na wengine ndo basi tena. Anabaki mtazamaji na mkosoaji wa wengine wakati yeye hata kuanza alishindwa.
5. NANI ANAIFAHAMU VEMA HIYO BIASHARA?
Labda unataka kuanza kilimo tena cha matikiti labda. Je unamfahamu mtu yeyote ambaye anaijua vizuri biashara hiyo nje ndani? Kuanzia mbegu, aina (species) za hayo matikiti, misimu ya mauzo, wadudu shambulizi, nk. Usiombe ushauri kwa mtu asiyejua hiyo biashara kwa namna moja au nyingine. Mfano umeamua kuuza nguo. Unaenda kuomba ushauri kwa muuza magazeti kuhusu biashara. Yeye biashara yake ni leo kwa leo. Yaani leo kama habari UKUTA na kesho habari ikawa kupanda miti basi mambo ya jana yanakuwa siyo dili tena. Sasa unadhani atakushauri nini? Au unataka kuanza biashara ya kuuza mafuta ya mzeituni (Olive Oil) unaenda kuuliza kwa mama ntilie eti akwambie kama yana soko wakati yeye anapikia mafuta ya kuchakachua. Unadhani atakwambia ukafanye hiyo biashara? So don't ask the wrong people. Eti unakuta mtu anasema "mimi mama yangu ndo my best friend lazima nikamuulize". Wakati hana ufahamu nayo. Mbona ulikuwa humuulizi ALGEBRA ulipokuwa shule? Si unaona ee? So..Tafuta mtu anayeijua.
6. UNA NGOZI YA FARU?
Ukitaka ku excel kwenye biashara lazima uwe na ngozi ya faru. Niliwahi kujifunza mahali kuwa Faru ana ngozi ngumu mno. Na kwamba zamani wakati wa zana duni za uwindaji walikuwa wakitumia mishale kwa ngozi ya Faru ilikuwa ikishindwa kupenetrate ile ngozi yake. Na pia kuwa faru anaweza kuwa na ndege mgongoni kwake wanakula wadudu au wanarukaruka pale mgongoni na wala asifeel kama wapo. Inabidi uwe na ngozi ngumu. Kuna watu watakukatisha tamaa, kunachangamoto na mishale mingi itarushwa hakikisha una ngozi ngumu na utashinda hiyo mikikimikiki.
7. NINI TAFSIRI YA MAFANIKIO KWAKO?
Kwa wengi mafanikio ni kupata pesa nyingi. Wengine hata ukimuuliza pesa nyingi kwako ni sh ngapi hana idea. Wengine mafanikio kwao ni magari na majumba wengine mafanikio ni starehe, wengine mafanikio ni kutoa sadaka na kusaidia wengine zaidi wengine mafanikio ni kuajiri watu wengi, wengine mafanikio ni kusomesha watoto international school wengine mafanikio ni kuwa na vitega uchumi wengine mafanikio ni kuwa na akiba kubwa benki nk wengine mafanikio ni kula vizuri na kuwa na afya bora nk. Wewe kwako mafanikio ni nini? Ili ufanikiwe lazima kwanza uwe na definition ya mafanikio yenyewe. La sivyo unaweza kupata kila kitu katika biashara na bado ukawa unahisi hujafanikiwa kabisa. Hii imewasumbua wengi.
Kuomba Mungu ni jambo constant wala sina haja kukwambia. Ni sawa na kuoga. Mpaka uambiwe? Nadhani unanielewa.
So if unapenda kujua zaidi biashara sahihi katika zama hizi karibu kwa WhatsApp #o788366511 au #o752366511 kujifunza.
Semper Fi,
Andrea Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
Jumamosi, 25 Juni 2016
KUTIMIZA NDOTO ZAKO INAKUPASA KUONA MBALI ZAIDI YA WANAOKUZUNGUKA
KUTIMIZA NDOTO ZAKO INAKUPASA KUONA MBALI ZAIDI YA WANAOKUZUNGUKA
Naitwa Andrea Muhozya na nina ndoto kubwa za kutimiza maishani. Nimeokoka, nampenda Yesu. Ni Mtanzania kwa kuzaliwa, mwenyeji wa Ukerewe, mkoani Mwanza. Kwa sasa ninaishi Dar es Salaam. Nina taaluma ya sheria (holder wa LL.B) ambayo niliipata kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 2008. Lakini kwa sasa najishughulisha na biashara hususan biashara ya mtandao (Network Marketing) kupitia kampuni ya Forever Living Products yenye makao makuu nchini Marekani lakini ikiwa imesambaa nchi zaidi ya 150 duniani
Kampuni hii pia ipo hapa Tanzania.
Safari yangu ya maisha ambayo ndo kwanza imekucha imeanza mbali kama ilivyo kwa watu wengi wenye ndoto maishani na imejaa kona kona (Waingereza wanaita TWISTS & TURNS).
Nikiwa kama mtoto wa mwisho kuzaliwa katika familia ya kawaida sana ya watoto watatu tulikuzwa na mzazi mmoja ambaye ni mama (single-parent family) na maisha hayakuwa mepesi sana kutokana na hali halisi ya kuwa mzazi alikuwa mwalimu wa shule ya msingi kijijini akiwa mwaminifu kazini na hatukuwa na miradi ya biashara ya kusaidia kuongeza kipato hivyo mshahara wake ndiyo ulikuwa kila kitu kwetu na hata kwa ndugu zetu wengine. Sikujua sana mzigo aliokuwa akiubeba mama mpaka aliposhindwa kunilipia ada nikiwa kidato cha pili nikiwa Seminari ya Makoko mjini Musoma, ambapo nilipata ufadhili wa walimu wangu kuanzia hapo na mtu mwingine ambao walinisomesha hadi namaliza kidato cha sita. Mungu awabariki siku zote. Nikiwa Seminari mzazi wangu akitamani nisomee upadre mimi nikawa na ndoto ya kuwa mwanasheria. A twist in the tale. Kama yule Obi Okonkwo wa kitabu NO LONGER AT EASE cha Chinua Achebe alivyoamua kusoma Lugha wakati ametumwa kusomea sheria. Wakati mwingine inabidi uangalie ndani ya moyo wako Mungu ameweka nini. Usije ukapishana nacho.
Nilipoingia Chuo Kikuu nikaamua kusoma sheria nikiwa na ndoto ya kuja kuingia kwenye siasa za kimataifa kwa ajili ya mambo ya haki za binadamu, watoto na mazingira lakini baada ya kumaliza chuo nikaona kuwa moyoni mwangu siasa haukuwa mwelekeo wa kutimiza ndoto zangu za maisha na za kusaidia wengine.
Another twist, another turn.
Baada ya Chuo Kikuu kama ilivyo kwa wanafunzi wengi huwaza ajira kama njia ya kutimiza ndoto zao. So nikaingia kwenye mfumo wa ajira kupitia benki ya Stanbic Tanzania. Nilidumu katika ajira hiyo kwa miaka miwili tu kuanzia 18 July 2008 hadi 18 July 2010 nilipositisha ajira yangu (resign) wakati ndo imeanza kunoga ili nikaangalie njia nyingine ya kutimiza ndoto zangu baada ya kuona kuwa mfumo wa ajira usingenifikisha mahali nilipokuwa nataka kufika maishani. Kumbuka ninatoka familia ya mzazi aliyeajiriwa hadi kustaafu na nilikuwa nikiwaza pia nikisubiri hadi kustaafu itakuwaje. Japo ajira yangu ilikuwa nzuri niliamua kufumba macho na kuzitazama ndoto zangu kubwa mbele yangu.
Another twist another turn.
Kwa kuwa sikuwa na UZOEFU wa biashara wa uhakika hapo kabla niliamua kuanza chini kabisa ambapo si wengi walinielewa. Na hapa ndipo ningependa usikilize kitu. Usifikiri lazima ueleweke na kila mtu ndipo uwe sahihi. Mimi nilijua sitaeleweka but nilijua nilikuwa nafanya nini. Nilienda kuanza na biashara ndogo ambayo kwa akili ya mtu wa kawaida kuona msomi wa Chuo Kikuu unaacha kazi Benki tena Makao Makuu halafu unaenda kuuza Popcorn (bisi) stendi ya Mwenge nadhani hata wewe unaweza ukahisi mawazo ya watu yalivyosumbuka kunitafsiri. Kila mtu alisema chake. Wengine huyu kadata, amerogwa, mpelelezi, hajielewi, nk. Kwa kuwa nilijua nilichokuwa nafanya niliamua kuifanya. Nilijua mpaka SIDO ni wapi, mahindi yanatoka wapi, mafuta gani yanafaa, nilifika mpaka Century Cinemax Mlimani City kujua wao wanapata wapi mahindi na mashine na mafuta gani na sukari gani wanatumia ndo nikajua kwa nini wanauza bei wanayouza. Tembea ujifunze. So watu hawakunielewa lakini mimi ni mtu nayependa sana kujifunza📄. Biashara ya Popcorn ilinifanya nijue wale vijana pale Mwenge wanatengeneza mpaka Tsh elfu 70 kwa siku moja. Hebu piga mara siku saba za wiki afu mara wiki nne za mwezi afu unaona mtu mwenye mshahara wa laki nne anavyomdharau muuza bisi bila kujua tofauti kati yao. Story short, nilijifunza vitu vingi sana na baada ya kuwa nimejifunza vingi nikaamua kuanza biashara nyingine pale pale Mwenge. Nilikuwa nshajua wapi watu wanapita kwa wingi nk. Wapi kodi ni ndogo wapi kodi kubwa pale stendi. Nani dalali nani dalali wa dalali. Nk. Nikaingia kufanya biashara ya kuuza vitabu. Nilifanya kwa miaka miwili bila mafanikio hadi nikafunga duka baadaye. Lakini kabla sijafunga duka nilikuwa nimeshaiupgrade na kuanza biashara nyingine ya kampuni ya Ulinzi. Nikawa na ofisi Mbezi Beach mimi na wenzangu wachache. Miaka miwili baadaye biashara hiyo ilikuwa umetupatia wakati mgumu na mimi personally iliniingiza kwenye madeni mengi hasa na marafiki zangu wa karibu kitu ambacho niliona kinaathiri mahusiano yangu nk. Kumbuka huko kote sikuwa na mtu ananiita kunifundisha cha kufanya ni wachache sana ambao walikuwa na utayari wa kunipa tips za mafanikio. Kikubwa tu ni kuwa kila biashara ilinipa experience tofauti tofauti lakini matokeo yanayofanana. Kwamba sikuona ikinipeleka kutimiza ndoto zangu.
Wakati nawaza nifanye nini kusonga mbele... Ndoto bado ninazo. Njia mbali mbali bado hazinisogezi walau kupiga hatua... Basi hapo ndipo nikashirikishwa mfumo wa Biashara ya Mtandao na rafiki yangu Edwin Simon Ndege na nikauelewa vizuri na kuamua kuanza kufanya rasmi biashara hii ya Mtandao kupitia kampuni hii ya Forever Living Products Jumamosi ya October 23, 2013, saa moja jioni. Na namshukuru sana Mungu kunikutanisha na Edwin maana alinionyesha wanasema THE THING ITSELF. Yaani alibonyeza reli 😀😀.
Niliona ni biashara ambayo ingenipatia ndoto zangu zote. Kifupi niliona *vitu 10* ambavyo ningevipata katika biashara hii. Ngoja ni vitaje halafu uone kwa nini sikuiachia hii fursa ukizingatia hisitoria ya biashara nilizotangulia kufanya:
1. Kuja kuwa mmiliki wa biashara KUBWA
2. Kipato cha ziada
3. Uhuru wa kipato
4. Afya bora (kampuni hii inajihusisha na bidhaa za afya na urembo)
5. Uhuru wa muda
6. SAFARI za kimataifa. Napenda kusafiri sana.
7. Kupanuka kifikra maana mafunzo ni mengi kwa waliotangulia. Nilipenda sana hii. Maana siku ya Kwanza tu nilijifunza kwa watu zaidi ya sita! Napenda kujifunza unakumbuka ee?
8. Kusaidia watu wengine.
9. Kustaafu kwa wakati nitakaotaka siyo sababu ya umri. Tamu sana hii
10. Kuacha urithi. Biashara hii inarithishwa kwa vizazi viwili mfululizo baada yangu.
Mimi sijui wengine huona nini wanapoonyeshwa hii fursa! Labda wanaona kitu kimoja. Mimi niliona hayo kumi mbele yangu. Hebu fikiria! Ningewezaje kukataa aina hiyo ya future.
NINI KIMETOKEA TANGU HAPO
Mengi yametokea na sijajutia kuianza hii biashara. Afya yangu imeboreka mara 100. Mfano tu kutokana na bidhaa nzuri za hii kampuni sijaumwa malaria tena toka nimeanza hii biashara. Afya ni muhimu sana. Kuna watu wanapata pesa lakini kila siku hospitali. Hili ni jambo kubwa sana ukizingatia mimi nilikuwa napatikana na malaria kila baada ya miezi minne hivi hapo kabla. What a business. Kumbe nilikuwa na weak immunity.
Pia nimekuwa mtu mwenye mtazamo *mkubwa* mno na ndoto zangu zimepanuka zaidi. Mfano zamani nilikuwa na ndoto ya kumiliki gari zuri (lolote). Sasa hivi naona PORSCHE MACAN. Hiyo ndo tofauti. Nawaza kumiliki boti, private jet nk.
Treni hapana. Hahahaaaaa
Mafanikio ya kifedha je?
Wengi huniuliza swali hili. Kama nilivyosema kwanza kabisa nimefanikiwa sana kubadili mtazamo wangu kuhusu maisha na kuhusu mafanikio. Unajua watu wengi hudhani kuwa kufanikiwa lazima uwe na uwezo wa kuonyesha pesa nyingi mkononi au benki. Ndiyo maana wengine wanapiga picha na noti za elfu kumi nyingi nyumbani kwao. Hujawahi kuona watu kama hao? Hata wanamuziki wanaofanya hivyo kwenye nyimbo zao.
Lakini sasa hivi mtazamo wangu umebadilika sana! Nimetambua na nazidi kutambua kuwa mafanikio yangu kifedha ni matokeo ya kuwasaidia watu wengine kufanikiwa kwanza. Yaani Bakhressa anafanikiwa sana sababu ni matokeo ya yeye kuwasaidia watu wengine KWANZA. Mfano anawapa watu chakula, ajira (yaani mshahara), kodi kwa serikali nk, nk. Kwa kuwa anafanya hayo kwanza ndiyo anapata mafanikio kama malipo ya kuwasaidia wengine kufanikiwa.. Huo ndiyo mtazamo wangu mpya. Ndiyo maana niko tayari kusaidia kila mtu katika biashara yangu. Kadri nitakavyosaidia wengi kwa moyo wote bila kuchoka wala kulalamikia wingi wa watu ndivyo nitakavyofanikiwa zaidi kifedha.
Hivyo mafanikio makubwa niliyonayo ni FIKRA ZANGU KWANZA. Sasa hivi mimi ni mtu mwenye kuona mbali na kuwaza makubwa zaidi ya hapo zamani. Biashara hii imenipanua sana fikra kwa sababu ya mafunzo kuwa mengi. Hivyo ninajua mafanikio makubwa ya kifedha yapo njiani.
Hata hivyo siyo kwamba sipati fedha. Ninapata. Kwa kuwa biashara hii haina mshahara kipato changu kinategemea MIMI mwenyewe nimefanya kazi kiasi gani. Kwa mfano je ni kweli nimemtafuta wateja? Je ni kweli nimewashirikisha watu wapya fursa hii ili iwasaidie pia? Kumbuka kama sisaidii wengine siwezi pia kufanikiwa. Kwa hiyo kuna miezi nasaidia watu na kuongea na wateja na ninatengeneza laki 6 hadi laki 8 kwa mwezi kwa cheo changu cha Supervisor. Najua wengi huwa hawastushwi na fedha ndogo kama hizi.Wala hawaoni mbali zaidi (beyond) ya kipato cha aina hii. Hata hivyo hicho kipato ni bonus tu ya kujenga team hakihusiani na bidhaa ninazouza kwa wateja wangu. Nina nyakati nauza bidhaa za thamani hiyo ama zaidi kwa mwezi. Still bado siyo pesa ya kumshtua mtu. Na lengo langu siyo kushtua watu ni kubadili maisha yangu na kuwasaidia wengine kuishi ndoto zao. Ndiyo maana naona beyond kipato hicho. Kwa sababu kuna watu walio mbele yangu wenye vipato mara 40 ya hicho. Na namshukuru Mungu sana kwa hilo maana ninajua KUMBE INAWEZEKANA.
Lakini lazima nipige kazi. Sasa vipi nikikaa nyumbani bila kushirikisha watu biashara? Anhaaa. Nikifanya hivyo ukweli sitopata pesa kwa kuwa hata Biblia inasema ASIYEFANYA KAZI NA ASILE. Na kama nilivyosema mfumo huu siyo kama ajira. Mfumo huu unahitaji nidhamu kubwa na kujifunza kila siku kwa waliofanikiwa na kujituma kwa dhati bila kusukumwa sukumwa. Kwa kuwa nimeshatambua kuwa napaswa kusaidia watu wengi mno nimeamua kufanya hivyo kwa nguvu zangu zote kusaidia kila aliye tayari kusaidiwa. Nashukuru kuona naweza kushika mkono wengine pia.
Lengo langu ni kwamba ndani ya mwaka mmoja toka sasa niwe nimeongeza kipato changu mara 10 ya hiki ninachopata kwa sasa. Kwa kuwa mindset yangu imepanuka najua nitafikia lengo hilo. Je, kwa mfano mwezi kama huu mwakani nikiwa na kipato mara 10 ya hicho nilichokutajia itakuwa ni kidogo? Na pia ndani ya kipindi hicho nataka kuwasaidia watu watano kupata kipato mara 10 ya wanachopata sasa. Na mwakani ninataka kusafiri miji mikubwa ya nchi saba tofauti kupitia hii kampuni. Miji hiyo ni Dubai, Johannesburg, Barcelona, Monte Carlo, Rome, London na New York. Miji mitatu katika hiyo (Barcelona, Monte Carlo na Rome) nitaizuru kupitia Merikebu ya Kifahari (Cruise Ship). Hebu pata picha!!
Furaha iliyoje! Ilikuwa ndoto yangu ya muda mrefu lakini sasa inaelekea kutimia kupitia mpango wa hii kampuni kuwezesha kila mtu kutimiza ndoto zake. Utapata wapi biashara ya aina hii dunia ya leo? Nitafurahia kipato changu na kuwa na muda wa kuibariki familia yangu kufurahi pamoja katika safari hizo. Vipi kama siku moja ukiweza kusafiri pia katika Cruise Ship? Si watu wengi hupata hiyo fursa duniani, ndiyo maana naichukulia biashara hii kama zawadi kutoka kwa Mungu hasa nikiangalia itakavyowafaa watoto na wajukuu zangu baada yangu.
Nazidi kujifunza kila siku. Sitaacha kujifunza. Najua nitatimiza ndoto zangu zote kupitia kujifunza.
SWALI FUPI: Je, unahisi ni biashara yenye kutimiza ndoto zako pia? Kumbuka kama una ndoto na unataka kuzitimiza kuwa tayari kutoeleweka na wengi na hata kupitia majaribu mbalimbali. Usisubiri kueleweka na kila mtu. Ndiyo ujumbe uliopo katika picha hii ifuatayo..
Huko nje kuna watu wengi wasioijua hii biashara vizuri. Njoo kwetu ujifunze kwa usahihi na kuielewa fursa hii na pamoja tutawasaidia watanzania wengi sana kujikwamua kiuchumi na kuishi maisha ya ndoto zao.
Karibu sana utajifunza mengi mno ambayo wengi hawayajui kuhusu biashara hii. Kujifunza zaidi WhatsApp #o788366511 au #o752366511.
Semper Fi.
AGM
Dar es Salaam, Tanzania
East A
Naitwa Andrea Muhozya na nina ndoto kubwa za kutimiza maishani. Nimeokoka, nampenda Yesu. Ni Mtanzania kwa kuzaliwa, mwenyeji wa Ukerewe, mkoani Mwanza. Kwa sasa ninaishi Dar es Salaam. Nina taaluma ya sheria (holder wa LL.B) ambayo niliipata kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka 2008. Lakini kwa sasa najishughulisha na biashara hususan biashara ya mtandao (Network Marketing) kupitia kampuni ya Forever Living Products yenye makao makuu nchini Marekani lakini ikiwa imesambaa nchi zaidi ya 150 duniani
Kampuni hii pia ipo hapa Tanzania.
Safari yangu ya maisha ambayo ndo kwanza imekucha imeanza mbali kama ilivyo kwa watu wengi wenye ndoto maishani na imejaa kona kona (Waingereza wanaita TWISTS & TURNS).
Nikiwa kama mtoto wa mwisho kuzaliwa katika familia ya kawaida sana ya watoto watatu tulikuzwa na mzazi mmoja ambaye ni mama (single-parent family) na maisha hayakuwa mepesi sana kutokana na hali halisi ya kuwa mzazi alikuwa mwalimu wa shule ya msingi kijijini akiwa mwaminifu kazini na hatukuwa na miradi ya biashara ya kusaidia kuongeza kipato hivyo mshahara wake ndiyo ulikuwa kila kitu kwetu na hata kwa ndugu zetu wengine. Sikujua sana mzigo aliokuwa akiubeba mama mpaka aliposhindwa kunilipia ada nikiwa kidato cha pili nikiwa Seminari ya Makoko mjini Musoma, ambapo nilipata ufadhili wa walimu wangu kuanzia hapo na mtu mwingine ambao walinisomesha hadi namaliza kidato cha sita. Mungu awabariki siku zote. Nikiwa Seminari mzazi wangu akitamani nisomee upadre mimi nikawa na ndoto ya kuwa mwanasheria. A twist in the tale. Kama yule Obi Okonkwo wa kitabu NO LONGER AT EASE cha Chinua Achebe alivyoamua kusoma Lugha wakati ametumwa kusomea sheria. Wakati mwingine inabidi uangalie ndani ya moyo wako Mungu ameweka nini. Usije ukapishana nacho.
Nilipoingia Chuo Kikuu nikaamua kusoma sheria nikiwa na ndoto ya kuja kuingia kwenye siasa za kimataifa kwa ajili ya mambo ya haki za binadamu, watoto na mazingira lakini baada ya kumaliza chuo nikaona kuwa moyoni mwangu siasa haukuwa mwelekeo wa kutimiza ndoto zangu za maisha na za kusaidia wengine.
Another twist, another turn.
Baada ya Chuo Kikuu kama ilivyo kwa wanafunzi wengi huwaza ajira kama njia ya kutimiza ndoto zao. So nikaingia kwenye mfumo wa ajira kupitia benki ya Stanbic Tanzania. Nilidumu katika ajira hiyo kwa miaka miwili tu kuanzia 18 July 2008 hadi 18 July 2010 nilipositisha ajira yangu (resign) wakati ndo imeanza kunoga ili nikaangalie njia nyingine ya kutimiza ndoto zangu baada ya kuona kuwa mfumo wa ajira usingenifikisha mahali nilipokuwa nataka kufika maishani. Kumbuka ninatoka familia ya mzazi aliyeajiriwa hadi kustaafu na nilikuwa nikiwaza pia nikisubiri hadi kustaafu itakuwaje. Japo ajira yangu ilikuwa nzuri niliamua kufumba macho na kuzitazama ndoto zangu kubwa mbele yangu.
Another twist another turn.
Kwa kuwa sikuwa na UZOEFU wa biashara wa uhakika hapo kabla niliamua kuanza chini kabisa ambapo si wengi walinielewa. Na hapa ndipo ningependa usikilize kitu. Usifikiri lazima ueleweke na kila mtu ndipo uwe sahihi. Mimi nilijua sitaeleweka but nilijua nilikuwa nafanya nini. Nilienda kuanza na biashara ndogo ambayo kwa akili ya mtu wa kawaida kuona msomi wa Chuo Kikuu unaacha kazi Benki tena Makao Makuu halafu unaenda kuuza Popcorn (bisi) stendi ya Mwenge nadhani hata wewe unaweza ukahisi mawazo ya watu yalivyosumbuka kunitafsiri. Kila mtu alisema chake. Wengine huyu kadata, amerogwa, mpelelezi, hajielewi, nk. Kwa kuwa nilijua nilichokuwa nafanya niliamua kuifanya. Nilijua mpaka SIDO ni wapi, mahindi yanatoka wapi, mafuta gani yanafaa, nilifika mpaka Century Cinemax Mlimani City kujua wao wanapata wapi mahindi na mashine na mafuta gani na sukari gani wanatumia ndo nikajua kwa nini wanauza bei wanayouza. Tembea ujifunze. So watu hawakunielewa lakini mimi ni mtu nayependa sana kujifunza📄. Biashara ya Popcorn ilinifanya nijue wale vijana pale Mwenge wanatengeneza mpaka Tsh elfu 70 kwa siku moja. Hebu piga mara siku saba za wiki afu mara wiki nne za mwezi afu unaona mtu mwenye mshahara wa laki nne anavyomdharau muuza bisi bila kujua tofauti kati yao. Story short, nilijifunza vitu vingi sana na baada ya kuwa nimejifunza vingi nikaamua kuanza biashara nyingine pale pale Mwenge. Nilikuwa nshajua wapi watu wanapita kwa wingi nk. Wapi kodi ni ndogo wapi kodi kubwa pale stendi. Nani dalali nani dalali wa dalali. Nk. Nikaingia kufanya biashara ya kuuza vitabu. Nilifanya kwa miaka miwili bila mafanikio hadi nikafunga duka baadaye. Lakini kabla sijafunga duka nilikuwa nimeshaiupgrade na kuanza biashara nyingine ya kampuni ya Ulinzi. Nikawa na ofisi Mbezi Beach mimi na wenzangu wachache. Miaka miwili baadaye biashara hiyo ilikuwa umetupatia wakati mgumu na mimi personally iliniingiza kwenye madeni mengi hasa na marafiki zangu wa karibu kitu ambacho niliona kinaathiri mahusiano yangu nk. Kumbuka huko kote sikuwa na mtu ananiita kunifundisha cha kufanya ni wachache sana ambao walikuwa na utayari wa kunipa tips za mafanikio. Kikubwa tu ni kuwa kila biashara ilinipa experience tofauti tofauti lakini matokeo yanayofanana. Kwamba sikuona ikinipeleka kutimiza ndoto zangu.
Wakati nawaza nifanye nini kusonga mbele... Ndoto bado ninazo. Njia mbali mbali bado hazinisogezi walau kupiga hatua... Basi hapo ndipo nikashirikishwa mfumo wa Biashara ya Mtandao na rafiki yangu Edwin Simon Ndege na nikauelewa vizuri na kuamua kuanza kufanya rasmi biashara hii ya Mtandao kupitia kampuni hii ya Forever Living Products Jumamosi ya October 23, 2013, saa moja jioni. Na namshukuru sana Mungu kunikutanisha na Edwin maana alinionyesha wanasema THE THING ITSELF. Yaani alibonyeza reli 😀😀.
Niliona ni biashara ambayo ingenipatia ndoto zangu zote. Kifupi niliona *vitu 10* ambavyo ningevipata katika biashara hii. Ngoja ni vitaje halafu uone kwa nini sikuiachia hii fursa ukizingatia hisitoria ya biashara nilizotangulia kufanya:
1. Kuja kuwa mmiliki wa biashara KUBWA
2. Kipato cha ziada
3. Uhuru wa kipato
4. Afya bora (kampuni hii inajihusisha na bidhaa za afya na urembo)
5. Uhuru wa muda
6. SAFARI za kimataifa. Napenda kusafiri sana.
7. Kupanuka kifikra maana mafunzo ni mengi kwa waliotangulia. Nilipenda sana hii. Maana siku ya Kwanza tu nilijifunza kwa watu zaidi ya sita! Napenda kujifunza unakumbuka ee?
8. Kusaidia watu wengine.
9. Kustaafu kwa wakati nitakaotaka siyo sababu ya umri. Tamu sana hii
10. Kuacha urithi. Biashara hii inarithishwa kwa vizazi viwili mfululizo baada yangu.
Mimi sijui wengine huona nini wanapoonyeshwa hii fursa! Labda wanaona kitu kimoja. Mimi niliona hayo kumi mbele yangu. Hebu fikiria! Ningewezaje kukataa aina hiyo ya future.
NINI KIMETOKEA TANGU HAPO
Mengi yametokea na sijajutia kuianza hii biashara. Afya yangu imeboreka mara 100. Mfano tu kutokana na bidhaa nzuri za hii kampuni sijaumwa malaria tena toka nimeanza hii biashara. Afya ni muhimu sana. Kuna watu wanapata pesa lakini kila siku hospitali. Hili ni jambo kubwa sana ukizingatia mimi nilikuwa napatikana na malaria kila baada ya miezi minne hivi hapo kabla. What a business. Kumbe nilikuwa na weak immunity.
Pia nimekuwa mtu mwenye mtazamo *mkubwa* mno na ndoto zangu zimepanuka zaidi. Mfano zamani nilikuwa na ndoto ya kumiliki gari zuri (lolote). Sasa hivi naona PORSCHE MACAN. Hiyo ndo tofauti. Nawaza kumiliki boti, private jet nk.
Treni hapana. Hahahaaaaa
Mafanikio ya kifedha je?
Wengi huniuliza swali hili. Kama nilivyosema kwanza kabisa nimefanikiwa sana kubadili mtazamo wangu kuhusu maisha na kuhusu mafanikio. Unajua watu wengi hudhani kuwa kufanikiwa lazima uwe na uwezo wa kuonyesha pesa nyingi mkononi au benki. Ndiyo maana wengine wanapiga picha na noti za elfu kumi nyingi nyumbani kwao. Hujawahi kuona watu kama hao? Hata wanamuziki wanaofanya hivyo kwenye nyimbo zao.
Lakini sasa hivi mtazamo wangu umebadilika sana! Nimetambua na nazidi kutambua kuwa mafanikio yangu kifedha ni matokeo ya kuwasaidia watu wengine kufanikiwa kwanza. Yaani Bakhressa anafanikiwa sana sababu ni matokeo ya yeye kuwasaidia watu wengine KWANZA. Mfano anawapa watu chakula, ajira (yaani mshahara), kodi kwa serikali nk, nk. Kwa kuwa anafanya hayo kwanza ndiyo anapata mafanikio kama malipo ya kuwasaidia wengine kufanikiwa.. Huo ndiyo mtazamo wangu mpya. Ndiyo maana niko tayari kusaidia kila mtu katika biashara yangu. Kadri nitakavyosaidia wengi kwa moyo wote bila kuchoka wala kulalamikia wingi wa watu ndivyo nitakavyofanikiwa zaidi kifedha.
Hivyo mafanikio makubwa niliyonayo ni FIKRA ZANGU KWANZA. Sasa hivi mimi ni mtu mwenye kuona mbali na kuwaza makubwa zaidi ya hapo zamani. Biashara hii imenipanua sana fikra kwa sababu ya mafunzo kuwa mengi. Hivyo ninajua mafanikio makubwa ya kifedha yapo njiani.
Hata hivyo siyo kwamba sipati fedha. Ninapata. Kwa kuwa biashara hii haina mshahara kipato changu kinategemea MIMI mwenyewe nimefanya kazi kiasi gani. Kwa mfano je ni kweli nimemtafuta wateja? Je ni kweli nimewashirikisha watu wapya fursa hii ili iwasaidie pia? Kumbuka kama sisaidii wengine siwezi pia kufanikiwa. Kwa hiyo kuna miezi nasaidia watu na kuongea na wateja na ninatengeneza laki 6 hadi laki 8 kwa mwezi kwa cheo changu cha Supervisor. Najua wengi huwa hawastushwi na fedha ndogo kama hizi.Wala hawaoni mbali zaidi (beyond) ya kipato cha aina hii. Hata hivyo hicho kipato ni bonus tu ya kujenga team hakihusiani na bidhaa ninazouza kwa wateja wangu. Nina nyakati nauza bidhaa za thamani hiyo ama zaidi kwa mwezi. Still bado siyo pesa ya kumshtua mtu. Na lengo langu siyo kushtua watu ni kubadili maisha yangu na kuwasaidia wengine kuishi ndoto zao. Ndiyo maana naona beyond kipato hicho. Kwa sababu kuna watu walio mbele yangu wenye vipato mara 40 ya hicho. Na namshukuru Mungu sana kwa hilo maana ninajua KUMBE INAWEZEKANA.
Lakini lazima nipige kazi. Sasa vipi nikikaa nyumbani bila kushirikisha watu biashara? Anhaaa. Nikifanya hivyo ukweli sitopata pesa kwa kuwa hata Biblia inasema ASIYEFANYA KAZI NA ASILE. Na kama nilivyosema mfumo huu siyo kama ajira. Mfumo huu unahitaji nidhamu kubwa na kujifunza kila siku kwa waliofanikiwa na kujituma kwa dhati bila kusukumwa sukumwa. Kwa kuwa nimeshatambua kuwa napaswa kusaidia watu wengi mno nimeamua kufanya hivyo kwa nguvu zangu zote kusaidia kila aliye tayari kusaidiwa. Nashukuru kuona naweza kushika mkono wengine pia.
Lengo langu ni kwamba ndani ya mwaka mmoja toka sasa niwe nimeongeza kipato changu mara 10 ya hiki ninachopata kwa sasa. Kwa kuwa mindset yangu imepanuka najua nitafikia lengo hilo. Je, kwa mfano mwezi kama huu mwakani nikiwa na kipato mara 10 ya hicho nilichokutajia itakuwa ni kidogo? Na pia ndani ya kipindi hicho nataka kuwasaidia watu watano kupata kipato mara 10 ya wanachopata sasa. Na mwakani ninataka kusafiri miji mikubwa ya nchi saba tofauti kupitia hii kampuni. Miji hiyo ni Dubai, Johannesburg, Barcelona, Monte Carlo, Rome, London na New York. Miji mitatu katika hiyo (Barcelona, Monte Carlo na Rome) nitaizuru kupitia Merikebu ya Kifahari (Cruise Ship). Hebu pata picha!!
Furaha iliyoje! Ilikuwa ndoto yangu ya muda mrefu lakini sasa inaelekea kutimia kupitia mpango wa hii kampuni kuwezesha kila mtu kutimiza ndoto zake. Utapata wapi biashara ya aina hii dunia ya leo? Nitafurahia kipato changu na kuwa na muda wa kuibariki familia yangu kufurahi pamoja katika safari hizo. Vipi kama siku moja ukiweza kusafiri pia katika Cruise Ship? Si watu wengi hupata hiyo fursa duniani, ndiyo maana naichukulia biashara hii kama zawadi kutoka kwa Mungu hasa nikiangalia itakavyowafaa watoto na wajukuu zangu baada yangu.
Nazidi kujifunza kila siku. Sitaacha kujifunza. Najua nitatimiza ndoto zangu zote kupitia kujifunza.
SWALI FUPI: Je, unahisi ni biashara yenye kutimiza ndoto zako pia? Kumbuka kama una ndoto na unataka kuzitimiza kuwa tayari kutoeleweka na wengi na hata kupitia majaribu mbalimbali. Usisubiri kueleweka na kila mtu. Ndiyo ujumbe uliopo katika picha hii ifuatayo..
Huko nje kuna watu wengi wasioijua hii biashara vizuri. Njoo kwetu ujifunze kwa usahihi na kuielewa fursa hii na pamoja tutawasaidia watanzania wengi sana kujikwamua kiuchumi na kuishi maisha ya ndoto zao.
Karibu sana utajifunza mengi mno ambayo wengi hawayajui kuhusu biashara hii. Kujifunza zaidi WhatsApp #o788366511 au #o752366511.
Semper Fi.
AGM
Dar es Salaam, Tanzania
East A
Jumatatu, 21 Desemba 2015
"Just A Stick"
START WHERE YOU ARE WITH WHAT YOU HAVE
Many years (in fact many millennia) ago a shephard was called by his Master and given a difficult assignment: to go and confront a foreign King with a critical message - to free the slaves he had so they could go their way for that Master. Puzzled, the shephard-cum-servant wondered how he could confront the foreign king without any "special tools" and any "strategic plan" and "specific presentation skills", etc. And thus this servant had to confront the sender with a clever question: "What if they don't believe me?" He queried.
And then the powerful sender asked him "What do you have in your hand?"
And the guy was like, "Ammm.. A stick... Jus a stick. Yeah"
And the sender says, "Toss it down"
The guy did and boy! Stick turns into a snake! What? He had to run away for fear.. "What's going on here?", I believe he was so wondering when the sender told him to "Keep Calm and take the snake by its tail". Are you kidding me? But he did. Story short, Moses (yes the Moses of the Bible) went and confronted King Pharaoh with "just a stick" and his brother and the slaves were freed.. Not because of the stick though.
I have come to learn that most people would like to do something grand with their lives..but they want to be grand first before they can do it. Kind of they want "to be Picasso first before they can be Picasso". And most of them for "good" reason – they they're wondering how on earth they can get it done with "just a stick" in their hand. I was one of them. Until I learnt how detrimental to success that can be.
You might have a big dream or vision yourself and you are probably wondering how "well prepared you need to be" first. And that is a good thing. Look, Abraham Lincoln said he would spend the first four hours sharpening the axe if he was to chop down a tree in six! Smart man. Preparation is extremely important. It makes the execution smooth and even faster.
Nevertheless it is critical that you don't despise meagre beginnings in the guise of preparing yourself. It seems to be a Godly principle to bless abundantly those who accept small beginnings. Those who don't belittle starting where they are with what they have. This is not a Bible class here, but there's a verse in the Bible that reminds us mortals not to despise humble beginnings.
There are people who either out of ignorance or a wish to have that grand entrance have waited to be ready all their lives. You shouldn't. Get started where you are with what you have. Even if it's just a stick.
See I grew up thinking to be big you have to start big. Starting small was never an option for me. Whatever I wanted to do I wanted it started big, huge if you will.
One day I met a local entrepreneur at a seminar. He was talking about all these topics: confidence, adding value, etc, etc. After the seminar I approached him and asked him what I was to do to be a motivational speaker. Guy looks me in the eye and asks "So how long have you been doing the talk?"
"Excuse me?", I asked, quickly adding: "Amm.. I haven't started out yet.." Wasn't that why I eas asking him what should I do to get started in the first place? I wondered.
You know what he told me? "It's not what you don't have but what you do have. You must start speaking. Speak to your friends, your neighbours. School children, folks at church, your neighbours, etc etc! You are not "going to be" a speaker.. You either are or you aren't! You must start speaking and then get to perfect the hussle as you go along.."
Waooh!!
What a paradigm shift that was for me?
So I picked my stick by the tail and went home and started practicing alone. Recording myself on my mobile phone. Listening later and laughing really hard at my own "talk".. How it sounded. But I got confident and I started sending the audios to a few friends. Some would laugh. Some would give me their feedback. I didnt tell them why I was sending them the audios anyway. But as I grew more cinfident I started visiting nearby Secondary Schools and asked for a chance to speak to students. No school turned me down, to my surprise. I had nothing except bus fare and a book I would carry, any book, and a notebook, plus the message I had in my mind. That was my " just a stick". Then surprisingly some students started asking me if I could document my messages and sell those to them. I worked it out somehow. And they started buying the document, unprofessional as it looked. And that was when it occurred to me that if I had waited to be Robin Sharma or Tony Robbins first, I would have waited forever. I hadn't started the talks as a serious venture but just to try but I learnt enormous lessons. I am on my way to resuming the talks in the coming days and I believe I will have even greater contributions to make and a bonus of a little experience too.
So what about you? Do you have a dream? Are you waiting until you can get hold of the $5 million dollar loan before you embark on your Real Estate dream? Are you waiting until you have everything before you start that football team of your own? Are you waiting until you are a CPA or Ph.D before you start your own enterprise? Has God called you to ministry and you are trying to get all prepared first - whatever that means. Think again...
How did Bill Gates start?
What about Mandela?
Richard Brandon?
Lionel Messi?
How did Shania Twain start?
Do you know how Silvester Stallone started? You'd be surprised?
What about Agatha Christie or that creative mind behind Harry Potter?
Most successful people that you admire today started out with "just a stick in their hand". God blesses those who have faith! The daring ones.
Start where you are my friend. Pick your stick and start that business.
Unless of course you too like Dangote have a rich grandpa who can give you "additional seed money" of 500,000 naira or you too like Trump has a rich dad who can give you "a small loan of a million dollars"!. Otherwise just start small and grow big as you go.
If you wait to have everything you need you might wait till forever comes. What you have with you, a dream, the confidence and, the passion and your faith in God, are more than enough to fuel you to get started. Don't let the gas run out for nothing. Get started now.
[Well this is one of the things I have addressed thoroughly in my upcoming book... Stay tuned..)
Thanks for reading and God bless you.
I welcome your thoughts in the comment section below.
Many years (in fact many millennia) ago a shephard was called by his Master and given a difficult assignment: to go and confront a foreign King with a critical message - to free the slaves he had so they could go their way for that Master. Puzzled, the shephard-cum-servant wondered how he could confront the foreign king without any "special tools" and any "strategic plan" and "specific presentation skills", etc. And thus this servant had to confront the sender with a clever question: "What if they don't believe me?" He queried.
And then the powerful sender asked him "What do you have in your hand?"
And the guy was like, "Ammm.. A stick... Jus a stick. Yeah"
And the sender says, "Toss it down"
The guy did and boy! Stick turns into a snake! What? He had to run away for fear.. "What's going on here?", I believe he was so wondering when the sender told him to "Keep Calm and take the snake by its tail". Are you kidding me? But he did. Story short, Moses (yes the Moses of the Bible) went and confronted King Pharaoh with "just a stick" and his brother and the slaves were freed.. Not because of the stick though.
I have come to learn that most people would like to do something grand with their lives..but they want to be grand first before they can do it. Kind of they want "to be Picasso first before they can be Picasso". And most of them for "good" reason – they they're wondering how on earth they can get it done with "just a stick" in their hand. I was one of them. Until I learnt how detrimental to success that can be.
You might have a big dream or vision yourself and you are probably wondering how "well prepared you need to be" first. And that is a good thing. Look, Abraham Lincoln said he would spend the first four hours sharpening the axe if he was to chop down a tree in six! Smart man. Preparation is extremely important. It makes the execution smooth and even faster.
Nevertheless it is critical that you don't despise meagre beginnings in the guise of preparing yourself. It seems to be a Godly principle to bless abundantly those who accept small beginnings. Those who don't belittle starting where they are with what they have. This is not a Bible class here, but there's a verse in the Bible that reminds us mortals not to despise humble beginnings.
There are people who either out of ignorance or a wish to have that grand entrance have waited to be ready all their lives. You shouldn't. Get started where you are with what you have. Even if it's just a stick.
See I grew up thinking to be big you have to start big. Starting small was never an option for me. Whatever I wanted to do I wanted it started big, huge if you will.
One day I met a local entrepreneur at a seminar. He was talking about all these topics: confidence, adding value, etc, etc. After the seminar I approached him and asked him what I was to do to be a motivational speaker. Guy looks me in the eye and asks "So how long have you been doing the talk?"
"Excuse me?", I asked, quickly adding: "Amm.. I haven't started out yet.." Wasn't that why I eas asking him what should I do to get started in the first place? I wondered.
You know what he told me? "It's not what you don't have but what you do have. You must start speaking. Speak to your friends, your neighbours. School children, folks at church, your neighbours, etc etc! You are not "going to be" a speaker.. You either are or you aren't! You must start speaking and then get to perfect the hussle as you go along.."
Waooh!!
What a paradigm shift that was for me?
So I picked my stick by the tail and went home and started practicing alone. Recording myself on my mobile phone. Listening later and laughing really hard at my own "talk".. How it sounded. But I got confident and I started sending the audios to a few friends. Some would laugh. Some would give me their feedback. I didnt tell them why I was sending them the audios anyway. But as I grew more cinfident I started visiting nearby Secondary Schools and asked for a chance to speak to students. No school turned me down, to my surprise. I had nothing except bus fare and a book I would carry, any book, and a notebook, plus the message I had in my mind. That was my " just a stick". Then surprisingly some students started asking me if I could document my messages and sell those to them. I worked it out somehow. And they started buying the document, unprofessional as it looked. And that was when it occurred to me that if I had waited to be Robin Sharma or Tony Robbins first, I would have waited forever. I hadn't started the talks as a serious venture but just to try but I learnt enormous lessons. I am on my way to resuming the talks in the coming days and I believe I will have even greater contributions to make and a bonus of a little experience too.
So what about you? Do you have a dream? Are you waiting until you can get hold of the $5 million dollar loan before you embark on your Real Estate dream? Are you waiting until you have everything before you start that football team of your own? Are you waiting until you are a CPA or Ph.D before you start your own enterprise? Has God called you to ministry and you are trying to get all prepared first - whatever that means. Think again...
How did Bill Gates start?
What about Mandela?
Richard Brandon?
Lionel Messi?
How did Shania Twain start?
Do you know how Silvester Stallone started? You'd be surprised?
What about Agatha Christie or that creative mind behind Harry Potter?
Most successful people that you admire today started out with "just a stick in their hand". God blesses those who have faith! The daring ones.
Start where you are my friend. Pick your stick and start that business.
Unless of course you too like Dangote have a rich grandpa who can give you "additional seed money" of 500,000 naira or you too like Trump has a rich dad who can give you "a small loan of a million dollars"!. Otherwise just start small and grow big as you go.
If you wait to have everything you need you might wait till forever comes. What you have with you, a dream, the confidence and, the passion and your faith in God, are more than enough to fuel you to get started. Don't let the gas run out for nothing. Get started now.
[Well this is one of the things I have addressed thoroughly in my upcoming book... Stay tuned..)
Thanks for reading and God bless you.
I welcome your thoughts in the comment section below.
Alhamisi, 17 Desemba 2015
Is The Window Of Opportunity Still Open? Then Use It Fast!
HOW DO YOU KNOW IF THE SUN HASN'T VANISHED?
Answer: YOU CAN'T KNOW.
Well, at least until after some time.
'How much time', you may ask. Well after exactly 8 minutes according to scientists for according to science it takes 8 minutes for the light from the sun to reach our beloved planet. So we'll still see the sun for 8 minutes. Interesting, no?
For 8 good minutes we can all be walking, swimming, farming, driving, chatting, or just "chilling" out somewhere and then whoop!!! Night time all of a sudden. Complete darkness.
Well, can you imagine that? Drivers crushing in trees and houses, people falling into pits, school children screening, airplanes losing sight of runways, everybody panicking and all that? Just imagine. Don't worry it's not gonna happen. God is in control....
Just make believe!
How important the sun will suddenly become all important as both TVs and social media terrorists and clerics alike will unite to discuss what has befallen us mortals!
But now no one talks about such a thing. Because it seems not a possibility on our plate. And rightly so. Why would it vanish? It's been there since..well, since time immemorial! Why would it want us all fall into 'kingdom come' all of a sudden?
In many ways that's how most people look at many things. We don't really appreciate things until they're gone. Maybe you too are one of them. You don't appreciate your job, spouse, business, children, team, leaders, etc, just because you think its their duty to do what they are supposed to do or to even please you. You don't appreciate "your sun" because you think it's its duty to shine on you whether it likes or not. And you want it to shine on you the way you want it to: not too hot not too bright..but just "perfectly".
There are opportunities you have now and they seem to have always been there. Maybe an opportunity to serve others well at your job..opportunity to visit your parents...opportunity to take your spouse or children to vacation..opportunity to visit the orphanage and homeless people... opportunity to serve God by singing, preaching, writing, etc.. opportunity to start a business...opportunity to buy assets... opportunity to start investment schemes such as buying shares etc... opportunity to go for your dreams...well they all seem to have always been there... They all seem to still be there now — just like the sun!
But are you sure the 'sun of your opportunities' will still be there tomorrow? Are you sure it will still be there next year? Are you even sure if its still out there at all???
Finding that out after "8 minutes" can be so tragic and chaotic for your life. You might not be able to handle the shock. And even if you could you certainly won't be able to replace the sun. Don't think all unsuccessful people were lazy, some just "found themselves in total darkness"
If yo have read WHO MOVED MY CHEESE? by Dr. Spencer Johnson you know what I'm talking about?
Don't be Hem who was shocked to find no cheese and hollered "who moved my cheese" cheese which wasn't HIS in the first place! And then yelled "it's not fair" as if life was meant to be fair at all. Yet that's how most people react when they go to the office one morning only to be told "You employment has been terminated" which to me is harsher than "YOU ARE FIRED". That's how people react when the opportunity to invest in something is all of a sudden barred by law for reasons best known to the government. That's what happens when you discover your talent in the evening hours of your life. With most people it becomes so chaotic and then they may become so agitative and dramatize everything to everyone's 'discomfort'. Look, even the opportunity to "serve" God is better taken in your youthful years, according to the Bible. "Remember your creator in the days of your youth..." proclaims Ecclesiastes 12:1! Before the sun has vanished, you bet right.
Be wise enough to look out for your sun, your opportunity, or your CHEESE. Don't be caught unawares. Most people don't recover from the shock. Ask for God's guidance and strength to take on every opportunity that you have always thought of taking.
Before the sun vanishes!
For when it does you may really not know. And when you know it may be too late.
Take your opportunities seriously!
My next article will be on "starting where you are, with what you have"
Thanks for visiting my blog.
I hope this was helpful.
Let me know your thoughts.
Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
Answer: YOU CAN'T KNOW.
Well, at least until after some time.
'How much time', you may ask. Well after exactly 8 minutes according to scientists for according to science it takes 8 minutes for the light from the sun to reach our beloved planet. So we'll still see the sun for 8 minutes. Interesting, no?
For 8 good minutes we can all be walking, swimming, farming, driving, chatting, or just "chilling" out somewhere and then whoop!!! Night time all of a sudden. Complete darkness.
Well, can you imagine that? Drivers crushing in trees and houses, people falling into pits, school children screening, airplanes losing sight of runways, everybody panicking and all that? Just imagine. Don't worry it's not gonna happen. God is in control....
Just make believe!
How important the sun will suddenly become all important as both TVs and social media terrorists and clerics alike will unite to discuss what has befallen us mortals!
But now no one talks about such a thing. Because it seems not a possibility on our plate. And rightly so. Why would it vanish? It's been there since..well, since time immemorial! Why would it want us all fall into 'kingdom come' all of a sudden?
In many ways that's how most people look at many things. We don't really appreciate things until they're gone. Maybe you too are one of them. You don't appreciate your job, spouse, business, children, team, leaders, etc, just because you think its their duty to do what they are supposed to do or to even please you. You don't appreciate "your sun" because you think it's its duty to shine on you whether it likes or not. And you want it to shine on you the way you want it to: not too hot not too bright..but just "perfectly".
There are opportunities you have now and they seem to have always been there. Maybe an opportunity to serve others well at your job..opportunity to visit your parents...opportunity to take your spouse or children to vacation..opportunity to visit the orphanage and homeless people... opportunity to serve God by singing, preaching, writing, etc.. opportunity to start a business...opportunity to buy assets... opportunity to start investment schemes such as buying shares etc... opportunity to go for your dreams...well they all seem to have always been there... They all seem to still be there now — just like the sun!
But are you sure the 'sun of your opportunities' will still be there tomorrow? Are you sure it will still be there next year? Are you even sure if its still out there at all???
Finding that out after "8 minutes" can be so tragic and chaotic for your life. You might not be able to handle the shock. And even if you could you certainly won't be able to replace the sun. Don't think all unsuccessful people were lazy, some just "found themselves in total darkness"
If yo have read WHO MOVED MY CHEESE? by Dr. Spencer Johnson you know what I'm talking about?
Don't be Hem who was shocked to find no cheese and hollered "who moved my cheese" cheese which wasn't HIS in the first place! And then yelled "it's not fair" as if life was meant to be fair at all. Yet that's how most people react when they go to the office one morning only to be told "You employment has been terminated" which to me is harsher than "YOU ARE FIRED". That's how people react when the opportunity to invest in something is all of a sudden barred by law for reasons best known to the government. That's what happens when you discover your talent in the evening hours of your life. With most people it becomes so chaotic and then they may become so agitative and dramatize everything to everyone's 'discomfort'. Look, even the opportunity to "serve" God is better taken in your youthful years, according to the Bible. "Remember your creator in the days of your youth..." proclaims Ecclesiastes 12:1! Before the sun has vanished, you bet right.
Be wise enough to look out for your sun, your opportunity, or your CHEESE. Don't be caught unawares. Most people don't recover from the shock. Ask for God's guidance and strength to take on every opportunity that you have always thought of taking.
Before the sun vanishes!
For when it does you may really not know. And when you know it may be too late.
Take your opportunities seriously!
My next article will be on "starting where you are, with what you have"
Thanks for visiting my blog.
I hope this was helpful.
Let me know your thoughts.
Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
Jumanne, 15 Desemba 2015
Who Are Your Associates..?
THE LAW OF ASSOCIATION..
Can you clearly see yourself living your dreams?
Can you see yourself getting there by the company you keep, the friends you have?
There are 4 categories of associates you may have:
1. Your CONFIDANTS
2. Your CONSTITUENTS
3. Your COMRADES
4. Your COMPATRIOTS
Your confidants are those you can share inner things even secrets.. They love you UNCONDITIONALLY. They love you for the long haul. They are people who will come bail you out of jail. They don't care about your money, status, weight looks or future. These are usually few, maybe one or two.
Your constituents are people who are with you because what you are for is what they are for. What you want is also what they want. They see you for the complimenting effect you have on them.
Your comrades are not for you and even not for what you are for. But they are AGAINST WHAT YOU ARE AGAINST.. These are people who JUST SHARE a common enemy with you...once the enemy is eliminated everyone goes on with their life. They were never for you or what you were for. This can be so deceiving especially in politics.
Your compatriots are people who can die for you but only for a season. That is when you want to eliminate what they think should be eliminated. Once the season is over don't expect them. In the right season these can be as many as ever! When the season is gone you'll have trouble locating any.
Now.... which associates do you have?
It's dangerous to associate with a comrade thinking they are a confidant. It's worse to treat your compatriots like your confidants!
You must know where your friends fall. Look at your closest 5 friends... Which category do they fall in?
Can the friends you have take you where you want to go? Can you get there with them?
If you can't then change your friends. Associate with other people who can take you there. It's not sinful to do so. Don't associate with people simply because you say "tumetoka mbali" [we've come a long way together].
Ask yourself this: are they going WHERE you are going?? Be sure they are.
Be sure they aren't just against what you are against! You may "toka mbali" all you want but if all they want in life is to start a tour company to operate in Arusha and what you want is to become the African real estate mogul you better part ways! If their mission is to preach in the villages and yours is to preach to the nations part ways for God's sake!
Don't associate with people who are going to Namanga whereas you are headed to the Philippines!
Don't even invite them in your team or else you surely will be frustrated big time.
So look at your associates today and ask yourself OBJECTIVELY:
~ Are they seeing what you are seeing?
~ Are they making you a big dreamer and big thinker?
If you are the best and smartest person in the group get out fast (while you still can), coz you can't learn anything by being told you are the best.
Associate yourself with people who think you "ain't nobody" as the Americans would put it.
Don't throw your dreams away by pleasing people. You are not here to please anyone. Even God doesn't concern Himself with pleasing anyone. He "goes about His business" as though no one is watching. Humans or no humans, angels or no angels, heaven or no heaven He is still God. He knows He can't please all his creatures. Give them sunshine some won't like it..rain some won't like it.. Give them peace in their land some will say they want war for progress.. Let them have war some will ask where is God when people are suffering like this. Be silent some will say there's no God. Answer them by thunder and lightning and some will say what kind of God scares his own children...etc.. See God Himself cant please everyone. Don't try to outsmart Him. Don't stay in a group because you want to please people. Be yourself.
Value your dreams and vision enough to walk away from associates who aren't adding value to you. Who aren't challenging you to become more. Who aren't challenging you to work harder and sleep less.
Be sure where you are going is WHERE your current associates are also headed. Or you won't get there.
Above all ask God for guidance. Seek and ye shall find. People who are waiting to associate with you are available if you look for them. There's no point to lose your dreams because you wanted your friends to b there with you. Sometimes God doesn't want them near you for a good reason. Find new friends. Where would you be really if you associated with your best kindergarten or pre-school friends?
Look at your dreams today and look at your associates. Then determine if their feet are headed where you are. If not, its time to say good-bye, or, even adieu!
All in my upcoming book....
Watch this space..
Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa
Can you clearly see yourself living your dreams?
Can you see yourself getting there by the company you keep, the friends you have?
There are 4 categories of associates you may have:
1. Your CONFIDANTS
2. Your CONSTITUENTS
3. Your COMRADES
4. Your COMPATRIOTS
Your confidants are those you can share inner things even secrets.. They love you UNCONDITIONALLY. They love you for the long haul. They are people who will come bail you out of jail. They don't care about your money, status, weight looks or future. These are usually few, maybe one or two.
Your constituents are people who are with you because what you are for is what they are for. What you want is also what they want. They see you for the complimenting effect you have on them.
Your comrades are not for you and even not for what you are for. But they are AGAINST WHAT YOU ARE AGAINST.. These are people who JUST SHARE a common enemy with you...once the enemy is eliminated everyone goes on with their life. They were never for you or what you were for. This can be so deceiving especially in politics.
Your compatriots are people who can die for you but only for a season. That is when you want to eliminate what they think should be eliminated. Once the season is over don't expect them. In the right season these can be as many as ever! When the season is gone you'll have trouble locating any.
Now.... which associates do you have?
It's dangerous to associate with a comrade thinking they are a confidant. It's worse to treat your compatriots like your confidants!
You must know where your friends fall. Look at your closest 5 friends... Which category do they fall in?
Can the friends you have take you where you want to go? Can you get there with them?
If you can't then change your friends. Associate with other people who can take you there. It's not sinful to do so. Don't associate with people simply because you say "tumetoka mbali" [we've come a long way together].
Ask yourself this: are they going WHERE you are going?? Be sure they are.
Be sure they aren't just against what you are against! You may "toka mbali" all you want but if all they want in life is to start a tour company to operate in Arusha and what you want is to become the African real estate mogul you better part ways! If their mission is to preach in the villages and yours is to preach to the nations part ways for God's sake!
Don't associate with people who are going to Namanga whereas you are headed to the Philippines!
Don't even invite them in your team or else you surely will be frustrated big time.
So look at your associates today and ask yourself OBJECTIVELY:
~ Are they seeing what you are seeing?
~ Are they making you a big dreamer and big thinker?
If you are the best and smartest person in the group get out fast (while you still can), coz you can't learn anything by being told you are the best.
Associate yourself with people who think you "ain't nobody" as the Americans would put it.
Don't throw your dreams away by pleasing people. You are not here to please anyone. Even God doesn't concern Himself with pleasing anyone. He "goes about His business" as though no one is watching. Humans or no humans, angels or no angels, heaven or no heaven He is still God. He knows He can't please all his creatures. Give them sunshine some won't like it..rain some won't like it.. Give them peace in their land some will say they want war for progress.. Let them have war some will ask where is God when people are suffering like this. Be silent some will say there's no God. Answer them by thunder and lightning and some will say what kind of God scares his own children...etc.. See God Himself cant please everyone. Don't try to outsmart Him. Don't stay in a group because you want to please people. Be yourself.
Value your dreams and vision enough to walk away from associates who aren't adding value to you. Who aren't challenging you to become more. Who aren't challenging you to work harder and sleep less.
Be sure where you are going is WHERE your current associates are also headed. Or you won't get there.
Above all ask God for guidance. Seek and ye shall find. People who are waiting to associate with you are available if you look for them. There's no point to lose your dreams because you wanted your friends to b there with you. Sometimes God doesn't want them near you for a good reason. Find new friends. Where would you be really if you associated with your best kindergarten or pre-school friends?
Look at your dreams today and look at your associates. Then determine if their feet are headed where you are. If not, its time to say good-bye, or, even adieu!
All in my upcoming book....
Watch this space..
Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)