Jumamosi, 13 Mei 2017

DUNIA HAITOKUKUMBUKA KWA MAMBO UTAKAYOJISIKIA KUFANYA BALI KWA MAMBO #UTAKAYOSUKUMWA KUYAFANYA


Mungu katuwezesha kukutana tena. Basi Jina lake lizidi kuinuliwa maana kuwa hai ni za zawadi kubwa mno.

Leo nina jambo muhimu kuongea na wewe.


Katika kipindi cha miaka saba ambayo nimeitumia kujifunza na kupractice ujasiriamali na kujifunza kwa watu walioacha ALAMA duniani nimeweza kujifunza mambo mengi. Mojawapo ni kuwa dunia haina muda na mambo unayokuwa COMFORTABLE kuyafanya hata kama utafanikiwa nayo vipi. Ukifa yanaishia hapo na jina lako linabaki kwenye kaburi pale. Born 19.... died 20... hivyo yani.

Dunia inamkumbuka mtu ambaye alitii sauti ya MSUKUMO wa ndani wa kufanya kile alicholetwa hapa duniani kukifanya. Unaweza kuwa effective and successful kwenye jambo fulani hapa duniani lakini kama ukifa na jina lako likafa ni dalili kuwa ulikuwa mbinafsi na ulitaka mafanikio BINAFSI tu wala hukujali kuwa unapaswa uguse watu wengine kabla hujaondoka duniani. Ni vizuri kuangalia sana mambo unayoyafanya kama unayafanya tu kwa kuwa ndicho ULICHOSOMEA au ndicho KIRAHISI KUFANYA au unakifanya kwa kuwa kuna MSUKUMO NDANI YAKO wa kukifanya?

Yaani uligombea ubunge kwa kuwa ULISUKUMWA moyoni au sifa tu au ulitaka kuonyesha watu kuwa wewe ni "kiboko"? Usipoangalia hili jambo utakuwa maarufu kweli kweli lakini siku ukimaliza muda wa ubunge na jina lako linaishia hapo tena ukiwa bado hai. Hivi kila aliyewahi kuwa mbunge mashuhuri au waziri bado anatajwa leo na kukumbukwa?
Ask yourself.

Unafanya biashara kama fashion au una MSUKUMO ndani kuwa ufanye? Kama huna msukumo ndani wa biashara basi utakuwa unaendesha gari kwenye njia ya treni. Kitakachotokea hata wewe mwenyewe hutajua yani. Usifanye biashara ili uwe kama Dewji. Yeye ana msukumo wa kwake. Wewe nawe UNAO?

Umeajiriwa sababu "watoto watakula nini" au umeajiriwa sababu una MSUKUMO kuwa inatakiwa uwepo hapo ulipo ili huduma yako iwanufaishe watu wa Mungu watakaokuja kazini kwako? Usifurahie kuitwa ofisa wa benki au meneja masoko au head mistress nk huku una IGNORE sauti fulani inayokusukuma kutokea ndani kuhusu jambo jingine kabisa. Ukiendelea kuiignore hiyo sauti ipo siku ITANYAMAZA kimya haitazungumza tena kwa kipindi kirefu tu. Lakini ujue utakuwa umeignore kitu ambacho Mungu alikuwa anataka ufanye. Utashangaa umekaa kazini miaka mingi na mpaka unastaafu lakini huna amani moyoni na ukistaafu basi jina linaishia hapo pia. Halafu ile sauti ndo itarudi sasa. How sad.

Unasoma Chuo kwa ajili CV ionekane ina neno "University" au ili ukue-kue kidogo kabla hujaolewa...au unasoma sababu una kitu kinakwambia moyoni kuwa unapaswa kusoma hicho kitu. Au ulichagua kozi kwa kuwa ni nyepesi au kwa sababu "ina AJIRA" au sababu rafiki au anko alisema engineering ndo kozi ya "vichwa" kama wewe. Sasa kichwa gani unaambiwa pa kwenda.

Point ya msingi hapa ni kuwa mahali popote ulipo jitahidi sana kusikiliza sauti ya ndani yako. Siyo maneno ya mzazi tu au mume au mke sijui auntie ambao sauti ya ndani yako hawajui inafananaje. Za ndani kwao zenyewe hawajazisikiliza wataelewaje kuwa huwa kuna sauti ndani ya mtu!? So BE YOU. It's YOUR life. Life is really more than money and fame.

Dunia huyapa heshima kubwa majina ya wale waliofanya vitu vilivyotokana na MSUKUMO fulani ndani yao na siyo waliofanya tu sababu ya fashion au kutaka kujulikana na certainly haiwapi heshima wale waliodharau sauti iliyowaambia ACHA HIKI KAFANYE KILE.

Ni ngumu  kuacha kitu ambacho ni popular machoni pa wengi ili ukafanye kitu ambacho unasukumwa moyoni kufanya hata kama hakieleweki kwa wengine. Lakini ukiweza hilo basi jina lako litakumbukwa miaka mingi hata ukiwa umeondoka.

Ngoja nikupe mifano michache tu ya majina yanayotajwa na kukumbukwa sana na dunia.


1. WILLIAM BOEING

Ilikuwa jioni majira ya saa moja kasoro hivi. Mwangaza wa jua la mwezi wa July uling'arisha anga la magharibi kwa rangi nzuri iliyotulia na jua likaanza kudondoka na kuruhusu giza kuufunika uso wa nchi. Nikiwa futi 30,000 kutoka usawa wa bahari ilikuwa ndiyo mara yangu ya kwanza kushuhudia jua likizama nikiwa angani mbali kiasi hicho. Kuzama kwa jua (sunset) ni mojawapo ya mambo ninayopendelea sana kuyatazama.

Masikioni mwangu kulikuwa na headphones nikisikiliza muziki wa kusindikizia safari yangu ya kwanza ndani ya ndege aina ya BOEING 737.. Baada ya kutazama jua likiwa limeishia kabisa juu ya mawingu akili ikanirudisha kwenye dirisha la ndege kushoto kwangu lilivyokuwa zuri na lilivyotengenezwa kwa ustadi mkubwa. Na kisha akili yangu ikanileta kwenye ndege yenyewe - BOEING 737.

Muda kidogo baadaye jina la mwanzilishi wa kampuni kubwa ya Boeing likaja kichwani. Huyu ni bwana William Boeing. Nikaanza kutafakari kidogo kuhusu alipoanzia, alichoamua kufanya, ALICHOSUKUMWA kufanya, na dunia inamkumbuka kwa lipi katika hayo.

Akiwa amezaliwa familia "bora" baba yake akiwa mhandisi wa mambo ya madini William alisomeshwa shule za maana mno kwanza Uswizi kisha kwao Marekani kwenye Chuo Kikuu maarufu cha YALE UNIVERSITY. Kama hujui kuhusu Chuo hiki Google tu kidogo uone kusomesha mtu hapo inakuwaje.

Lakini William akakatisha masomo yake YALE UNIVERSITY na AKAAMUA kwenda kufanya biashara ya MBAO!! Dah!.  Kuna watu wana maamuzi magumu. Huwa nasema ni rahisi kuacha VETA ili ukafanye mambo yako. Lakini kuacha YALE UNIVERSITY ukauze MBAO? Hiyo ni level nyingine ya maamuzi. Trust me.

Lakini akafanikiwa sana katika hiyo biashara na kupata fedha nyingi mno. Akajulikana kama muuza mbao maarufu.

 Lakini katika safari zake kibiashara siku moja akatembelea maonyesho ya kibiashara huko Seattle na kuona watu wametengeneza mashine fulani ambayo waliirusha angani IKIWA NA MTU.  Moyo wake ukapiga PAAP! Akapata MSUKUMO mpya kabisa wa kuunda NDEGE yake. Na akaacha kila kitu na hela zake akazielekeza kwenye hilo jambo lililompa msukumo mpya.

Alipitia mengi lakini akafanikiwa. Na leo hii dunia inamkumbuka kwa jambo hilo. Ukitazama leo ndege aina ya BOEING zilivyo leo ni mwendelezo tu wa alichokianzisha. Dunia haikumbuki mbao ngapi aliuza. Ukitaja jina/neno Boeing watu hawalihusishi na mbao bali na kampuni kubwa ambayo imegusa maisha ya watu wengi mno. Na hakuna siku inayoenda leo ambapo hagusi maisha ya watu dunia hii. Na hayupo.

What about you? Think about your end. Forget the comfort. Work on your legacy. Utakumbukwa kwa kipi? Kwamba ulikuwa polisi au mhasibu afu basi? Kuna mapolisi au wahasibu wangapi dunia hii hadi ukumbuke ukumbuke wewe? Gusa maisha ya watu hasa wasikokujua kabisa.


2. FRANCIS SCOTT KEY

Huenda hili likawa jina geni kwako. Huyu alikuwa mwanasheria maarufu tu huko Marekani zamani za kale. Alifanya kazi kubwa mno kama mwanasheria hadi akafikia kuwa DISTRICT ATTORNEY hiki ni cheo cha heshima mno katika kila jimbo la Marekani. Kumbuka Marekani kila jimbo ni nchi. Yeye alikuwa District of Columbia. Yani "jikoni". Hivi Mungu akupe nini?

Lakini kuna jambo lilitokea kati ya mwaka1812 hadi 1815. Nalo ni vita kati ya Marekani na Uingereza. Kuna wamarekani wakakamatwa na Jeshi la Uingereza. Yeye kama mwanasheria akawa amepelekwa kwenda kuNEGOTIATE hao watu waachiliwe. Bahati mbaya naye akashikiliwa. Akakaa kwenye kambi ya adui kwa muda mrefu mno huku akishuhudia nchi yake ikidondoshewa mabomu na hana cha kufanya. Lakini siku moja alfajiri mapema mno mapambazuko yakianza na usiku kucha eneo la Marekani lililokuwa karibu na ile kambi likiwa limeshushiwa "mvua" ya mabomu usiku kucha huyu bwana Francis Scott Key huku akitazama kwa masikitiko eneo la nchi yake lililopigwa mabomu usiku kucha akashangaa kuona bendera ya Marekani ikiwa ipo kwenye mlingoti ikipepea. Kitu hicho kilimpa MSUKUMO wa ajabu mno moyoni. Akapata faraja kubwa kuwa licha ya mabomu yote yale lakini bendera ya nchi yake ilikuwa bado ikipepea vizuri kabisa. Akapata MSUKUMO wa kuandika SHAIRI kuhusu hilo tukio. Kichwa cha hilo shairi ni: THE STAR-SPANGLED BANNER (banner=flag)

Miaka kadhaa baadaye Bunge la Marekani (Congress) likapitisha resolution ya shairi hilo kuwa WIMBO WA TAIFA WA MAREKANI!

Leo hii Francis Scott Key hakumbukwi kwa kesi nyingi alizosimamia kwa kazi aliyosomea bali kwa kitu alichoandika bila kusomea. Popote pale wimbo wa TAIFA wa Marekani unapoimbwa  kila siku anagusa maisha ya watu wengi mno wa nchi yake na nje ya nchi yake wanaoguswa na shairi lake.

Usikute wewe unaweza kuchora picha moja tu au kutunga kitabu kimoja tu na dunia ikakukumbuka kwa hilo ila unang'ang'ana uwe maarufu kama Tundu Lissu.
Think about that.


3. NELSON MANDELA

Mwanamasumbwi na mwanasheria pia msomi kutoka Chuo Kikuu cha FORT HARE na kile cha WITWATERSRAND. Na akiisha kupikwa huko katika vyuo AKAAMUA kufanya kazi kama mwanasheria jijini JOHANNESBURG.

Lakini serikali ya watu wazungu ilipopitisha sheria ya ubaguzi wa rangi Mandela akapata  MSUKUMO mpya ndani yake siyo wa kuwa hakimu au jaji no. Ulikuwa ni msukumo wa kupigania USAWA na kupinga sera za kibaguzi kwa moyo wake wote. Msukumo wa kuwa mwanaharakati.

Alipitia magumu mengi, ndoa yake ya kwanza na bi Evelyn Mase ikafa.
Akaanza kufatiliwa na serikali na kukamatwa mara kwa mara. Mwisho akapewa kesi nzito na kuhukumiwa kifungo cha maisha jela ambacho alikitumikia katika magereza matatu tofauti ikiwemo la Robben Island.

Miaka 27 baada ya kufungwa akaachiwa. Dunia haikumbuki gloves zake au kesi alizosimamia bali UANAHARAKATI WAKE na KUPIGANIA KWAKE USAWA. Pia dunia inamkumbuka Mandela kama mtu aliyekuwa hana kinyongo na mtu. Mfano licha ya yeye kuachana na mke wake wa kwanza kwa sababu za Evelyn kumtuhumu Mandela kutokuwa mwaminifu na Evelyn kubadili dini na kuolewa na mtu mwingine na nk lakini Evelyn alipokufa Mandela na familia walihudhuria msiba vizuri kwa hisia zote. Lakini pia alipotolewa gerezani alimsamehe mtu aliyeidhinisha Mandela afungwe maisha!!
Dunia inakumbuka hilo.

What about you?


4. ABRAHAM LINCOLN

Mwanasheria mwingine huyu. Tena huyu alikuwa mwanasheria kwa KUJIFUNDISHA mwenyewe na kisha kwenda kufanya BAR EXAM (wanasheria wanajua hii kitu..siku hizi kuna LAW SCHOOL)

So huyu ni kichwa sana acha wewe ambaye umefundishwa na maprofessa wazuri na maktaba unayo na computer na internet na hao waliokufundisha wanakupa mtihani na bado unafeli afu unasema eti profesa kanifelisha! Ungejifundisha mwenyewe nyumbani kama Lincoln afu ndo ukapewe mtihani ungeelewa hata swali linahusu nini kweli? Nataka uone tofauti yako na Abbe! Alikuwa kichwa si mchezo.

Alisimamia kesi kadha wa kadha na kupata ushindi mnono hasa kwa kutumia kipawa chake cha kuongea vizuri.

Hata hivyo dunia leo haimkumbuki kama mwanasheria nguli na kichwa bali kama mojawapo ya maraisi bora kabisa wa Marekani na hasa kwa kuzuia umiliki wa watumwa huko Marekani na kuzuia nchi kusambaratika ilipoingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na mgogoro wa umiliki wa watumwa ambao ulizalisha chama cha Republicans mwaka1854. Baada ya Congress kupitisha sheria ya KANSAS-NEBRASKA ACT ambayo ilitaka kila jimbo liamue lenyewe endapo litaruhusu watu wake wamiliki watumwa au la. Majimbo kadhaa yakapinga hiyo sheria yakitaka sheria isiwepo suala la kuchagua kumiliki au kutomiliki. Ndipo Republican Party ilipoanzia hapo na LINCOLN akapata MSUKUMO mkubwa wa kuachana na sheria na kuingia kwenye siasa za uongozi wa juu rasmi akijiunga na chama cha Republican mwaka 1856 na kuwa raisi miaka minne tu baadaye!

Wajasiriamali na watafuta mafanikio wanamkumbuka Lincoln kwa jinsi alivyopambana bila kuchoka kutoka level za chini hadi kufikia kuwa raisi wa Marekani. Sheria ilikuwa tu mahali alipoanzia lakini uongozi wa nchi ukawa ni msukumo wa ndani. Msukumo mkali mno wa ndani uliomvusha kwenye changamoto za vipindi vigumu vya kushindwa uchaguzi kupoteza mke kupata nervous breakdown nk hadi akaja kuwa raisi.

Usidharau msukumo wa ndani. Lincoln angeweza kubaki mahakamani lakini jina    lake lingeishia siku yake ya kufa kama maelfu ya wanasheria wenzake huko ambao hakuna anayewajua wala kuwakumbuka.


5. TAIKICHIRO MORI

Kila mtu anamjua Bill Gates hasa kwa kuwa ni tajiri namba moja duniani. Lakini ni vizuri kupitia historia na kujifunza kwa waliowahi kumtangulia katika nafasi hii.
Taikichiro Mori ni mmoja wapo na alikuwa tajiri namba moja duniani mwaka 1992 utajiri wake ukiwa net worth $13 billion.

Na dunia inamkumbuka hivyo yani licha ya kuwa alikuwa academician mzuri huko Japan na mwenye mafanikio katika eneo hilo.

Alipata mafanikio mazuri katika masomo yake hadi kufikia kuwa mwalimu wa Chuo Kikuu.  Na huko katika kufundisha akafanikiwa hadi kufikia level ya DEAN wa KITIVO CHA BIASHARA katika Chuo kiitwacho YOKOHAMA CITY UNIVERSITY. Ukiwa dean wewe ni mtu mkubwa. Alidumu katika nafasi hiyo kwa miaka mitano hadi alipostaafu mwaka 1959.

Ni baada ya kustaafu ndo alipopata MSUKUMO mpya wa kufanya biashara ya REAL ESTATE. Nadhani hela zake mafao hizo. Lol. Alifanya hiyo biashara kwa miaka mingi na akafanikiwa mno ndo hadi kufikia 1992 akawa tajiri wa kwanza duniani. Dunia inajua alipoanzia lakini inakumbuka na kuheshimu ilichomsukuma kufanya.

Sasa kustaafu ualimu au uhandisi au unesi au chochote siyo mwisho wa maisha. Kama kuna sauti ndani inakwambia kagombee udiwani au kafungue mgahawa tii sauti usifanye mgumu moyo wako. Usiseme miye mzee. Kuna mstaafu mwenzako mzee alitajirika uzeeni. Huyu si mwingine bali.....


6. HARLAND SANDERS (a.k.a Colonel Sanders)



Huyu naye alikuwa mwanasheria lakini sheria ikagoma "kumtoa" baada ya miaka mingi. Akaona afanye vingine kama kuuza insurance covers nayo ikagoma. Akaamua kuuza taa tu sasa. Taa nazo zikampa headache tu. Mpaka anastaafu anapata mafao anayaangalia hivi anaona ujinga kabisa bora akajiue tu.

Lakini kabla ya kujiua akiwa mahali anapanga mipango ya kujiua akapata msukumo mdogo tu ndani kwamba kabla hajajiua aandike kwenye karatasi vitu vyote ambavyo hajawahi kufanya. Akiwa anaandika akakumbuka kuwa yeye alikuwa ni bonge la mpishi. Na kwamba alikuwa ametengeneza formula  (recipe) ya kupika kuku kwa kumchanganya na viungo zaidi ya 10 tofauti tofauti ambavyo ni yeye tu alikuwa anavijua na kuku alikuwa mtamu asikwambie mtu. Khaaa. Akaahirisha kujiua akaenda kuanza kupika kuku ili sasa badala ya kula mwenyewe akawauzie wengine. Lol. Akaanza kuuza kwenye sehemu watu wanakojaza mafuta kwenye gari. Anawaambia huyu kuku ukimla lazima utampenda maana nimeweka recipe ya viungo vingi vizuri vya asili. Kama mchezo akaanza kuingiza vijisenti. Akiwa na umri wa miaka 62 akapata MSUKUMO mwingine wa kuisajili biashara yake kama franchise business akiwa anaiita KENTUCKY FRIED CHICKEN. Kuku wa kukaanga kutoka jimbo la  KENTUCKY. Hiyo ilikuwa mwaka 1952.

Miaka 12 tu baadaye mwaka 1964 biashara ilikuwa imechanganyia akaiuza kwa $2 million. Bilioni kama nne za kitanzania leo. Fikiria mtu mwenye hela aina hiyo mwaka 64!!! Akiwa mzee wa miaka 74.

Kwa hiyo kama umepigika huoni mbele unataka ufe tu mwambie shetani hivi: NAAHIRISHA KUJIUA SITAKUFA BALI NITAISHI NA NITAFANYA KITU HAKIJAWAHI KUTOKEA HATA KAMA NI KUKAANGA DAGAA UPYA.

Ilimradi usikilize sauti ya ndani yako kwa utulivu. Tulia sikiliza. Mungu akiongea utajua tu I tell you. Utashangaa hakuna atakayekufundisha cha kufanya utahangaika huku na kule wewe mwenyewe utajishangaa hutakuwa na muda na critics na wanaokucheka wala hutatafuta kuonewa huruma tena. Utashangaa mifupa yako ina nguvu akili yako imeamka. Huo nao ni kama ubatizo mpya kabisa nakwambia. Na dunia haitataka kujua sijui ulisoma wapi au ulifanya kazi wapi. Dunia itataka kutangaza jina lako kupitia mambo uliyoyafanya kupitia MSUKUMO NDANI YAKO. Kitabu kinasema UTII NI BORA ZAIDI... Ndo maana Sprite wanasema TII KIU YAKO. Sasa mi nasema TII SAUTI YA NDANI YAKO na utashangaa toka hapo hutajitaji alarm ikuamshe utaamka mwenyewe tu.  Kwani jogoo huwa anaamshwa na alarm? Yeye ndo alarm clock. Sasa ukitii sauti ya ndani utashangaa wewe ndo unakuwa ALARM CLOCK.

Usifanye kitu kwa kuogopa watu watakuonaje kama hutafanya. Kuna watu wakiona RANGE ROVER inapita huwa wanasema: DAH MUNGU ALIUMBA VICHWA AISEE. Utukufu unaenda kwa Mungu. Kuna watu wakila KFC huwa wanamtukuza Mungu. Kuna watu wa wakipanda ndege au wakiimba wimbo wa TAIFA au wakilala hoteli nzuri nzuri au wakinunua iPhone huwa wanajisemea dah Mungu aliumba vichwa. Hayo yote na mengine ni zao la watu WALIOTII SAUTI YA NDANI MWAO. Kuna watu wanapaswa waogeee au kusafishia nyumba sabuni yako halafu ile harufu tu mtu anaisikilizia anamtukuza Mungu. Lakini wewe unataka kukata tamaa. Eti huwezi kuuza sabuni.

Kuna mtu mwingine.. Robin Sharma.. aliacha sheria pia baada ya sheria kumpa stress za kutosha akapata MSUKUMO  kuandika kitabu kinaitwa MEGA LIVING ili kusaidia watu jinsi ya kumanage stress. Kisha akaandika THE MONK WHO SOLD HIS FERRARI

na THE LEADER WHO HAD NO TITLE na akagusa maisha ya mamilioni ya watu na baadaye kukodiwa na mpaka makampuni makubwa duniani kama NIKE, MICROSOFT, PwC, HP ili afundishe viongozi wa hayo makampuni na wafanyakazi wao. Unakuta analipwa hadi dola laki tano kwa saa na anafundisha masaa matano.  So siku hiyo moja anakuwa ameingiza dola milioni moja na nusu.  Yani bilioni tatu za kitanzania kwa siku moja. Hiyo ndo THAMANI anayopewa mtu aliyetii sauti ya muumba wake kutoka ndani.

Ndege huimba kwa msukumo ulio ndani yao. Siyo kwa kuwa ndege wenzake watamwonaje asipoimba. Wewe unafanya vitu ili watu wakuelewe? Yesu hawakumwelewa watakuelewa wewe? Mimi huwa naandika tu sijali atakayeshindwa kuelewa nachosema. Naangalia msukumo ulio ndani ukiniambia andika kuhusu hiki naandika. Hata ikiwa saa saba za usiku.

Ukitazama watu wangapi wanaafiki ndo ufanye kitu wakati moyoni mwako tayari kuna mwafaka ujue hiyo ni dalili ya WOGA na kutotii.  Kumbuka kitabu kinasema UTII NI BORA.
TII SAUTI YA NDANI YAKO


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.
WhatsApp #o788367511
All Calls and SMS #o752367511
Blog: www.andreamuhozya.blogspot.com

Jumatatu, 24 Aprili 2017

WANT SUCCESS? BE A STUDENT OF NATURE TOO. (UNATAKA MAFANIKIO? KUWA MWANAFUNZI WA ASILI PIA)



WANT SUCCESS? BE A STUDENT OF NATURE TOO.

UNATAKA MAFANIKIO? KUWA MWANAFUNZI WA ASILI PIA


Kwa muda mrefu nimekuwa mwanafunzi wa mafanikio hasa kutoka kwa watu mbali mbali ambao ninahisi kwao nina mengi ya kujifunza mambo mbali mbali. Ninajifunza kwa kusoma kwenye vitabu mbali mbali, kukutana na watu face to face, pia kwenye Internet hasa YouTube videos, na pia kufuatilia wasemayo watu mbali mbali (ambao naamini Mungu aliwekeza kitu muhimu ndani yao) kwenye kurasa zao katika mitandao ya kijamii kama hapa Facebook, LinkedIn, Twitter na Instagram.  
Kwa mfano Facebook kina ninapo-login kabla sijasoma chochote huwa napitia kurasa 10 kwanza kuona walichoandika zikiwemo za wafuatao:
1.       James Mwanga’mba
2.       Mohamed Dewji
3.       Grant Cardone
4.       Robin Sharma
5.       Strive Masiyiwa
Na zinginezo....

Nimejifunza mengi na ninamshukuru Mungu kwa kunipa fursa ya kujifunza kutoka kwao kwa kweli. Kama ni chakula ninapata ladha tofauti tofauti na virutubisho tofauti tofauti ili afya yangu kuanzia shingoni kwenda juu izidi kukaa sawa. Najifunza pia kupitia comments mali mbali za watu wanapita katika kurasa hizo. Mfano juzi Cardone alipost akiuliza watu waseme MALENGO YAO MAKUBWA waliyowahi kuyaweka ni yapi and ukipitia comments niliweza kujua binadamu wenzangu duniani wana malengo yapi makubwa na hivyo kujifunza binadamu wenzangu wanawaza nini kuhusu maisha haya mafupi ambayo tumekodishwa na Mungu kwa kitambo.

Nawaombea wote wanaoshirikisha mawazo yao mema Mungu azidi kuwabariki na kuwawezesha kufanya hivyo ili waweze kuhuisha yale yaliyokufa ndani ya watu na kuchochea yale yaliyo hai.
Kutokana na kujifunza kwangu kutoka huko kote na kwa uzoefu wangu wa kuupitia mchakato wa mafanikio nimetambua jambo moja muhimu ambalo zamani sikuwa nalijua kuhusu mafanikio. Nalo ni hili: UKIWA MWANAFUNZI MZURI WA ASILI (NATURE) UTAYAFIKIA MAFANIKIO YAKO KWA WAKATI MUAFAKA ZAIDI.

Iwe unaamini katika Mungu au la hiyo haiondoi ukweli kwamba ASILI (nature) ipo na inaendeshwa na taratibu fulani ambazo hazibadiliki toka enzi na enzi. Na kwamba taratibu hizo uwe unazijua au huzijui zinaathiri namna utakavyoishi hapa duniani na yale utakayopata au yatakayokupata ungali hapa ulimwenguni. Taratibu ama kanuni hizo zimekuweko toka zamani zilizopita zip oleo na zitakuwepo zamani zijazo. Mfano kanuni isemayo: unachopanda NDICHO utakachovuna.


Kwa kutazama kwangu maisha yangu binafsi na ya vijana wenzangu na hata watu wazima katika eno hili la kupata mafanikio nikajifunza kuwa pamoja na kuwa wengi wetu tunajifunza kwa watu mbali mbali kama nifanyavyo mimi lakini tumesahau kuzingatia kanuni muhimu wanazofundisha hasa zile zinazoendesha asili (nature).

Kujaribu kutafuta mafanikio pasipo kuzitii hizi taratibu ama kanuni muhimu ni kujaribu kuidanganya ASILI kitu ambacho huwa hakina manufaa kwani hakiwezekani. You can’t cheat nature. Huwezi kuidanganya asili. Nakualika uendelee kuwa nami hapa chini ninapojaribu kuzielezea baadhi ya hizo kanuni ili uone kama zinaweza kukusaidia pia katika mchakato wako wa kuyaendea mafanikio uyatakayo.


1.       KANUNI YA MJUMUIKO (THE LAW OF ASSOCIATION)
Ulishawahi kuona video iitwayo THE CHICKEN AND THE EAGLE? Unaweza kuitazama hapa https://www.youtube.com/watch?v=dHAfVl-t1Hg na itakusaidia kuelewa hili nitakaloeleza hapa chini..
Kwa asili ni kwama vitu vinavyofanana vina kawaida ya kujumuika pamoja, kuenenda pamoja na kufanya mambo yao kwa namna inayofanana. Watu wa kale waliliona hili wakasema vitu kama: Ndege wafananao huruka pamoja.. kama ndege hawa wawili waitwao Steve Jobs na Bill Gates katika picha yao hii mwaka 1985 

Ni muhimu sana kama candidate wa Mafanikio ukalijua hili na kulizingatia sana. Wengine wakaitazama hii na kuiweka hivi: Kwa kawaida wewe utakuwa ni wastani wa watu watano wa karibu unaojumuika nao kila mara. Kwa maana nyingine ni kwamba ukitaka kujua mafanikio yako yatakuwa kwa kiwango gani angalia mafanikio ya watu wako wa karibu watano. Mwingine aliyeiona kanuni hii ya asili akasema ukikaa sana na watu wanne wasio na kipato unajua nini kitatokea? Halafu akajibu hilo swali kwa kusema: WEWE UTAKUWA WA TANO.

Jambo hili ndo linasabisha uone jinsi inavyokuwa ngumu kwako kuwa mtu wa karibu wa Dewji “from nowhere” tu. Si kwamba hapendi binadamu wengine ila anaheshimu kanuni hii. Anatii ASILI inachotaka. Asili inamtaka awe na watu wa aina fulani karibu ili weweze kumpasha habari sahihi na kumpeleka mahali sahihi kwa nyakati sahihi ili aweze kuyafikia yale anayoyataka. Kama hujawa aina hiyo ya mtu ASILI itakataa ukaribu wako na Dewji. Hata ukiwa jirani yake au mnasali msikiti mmoja au mko gym moja na treadmill anayotumia ndo na wewe unatumia. Utaishia kusema tu Dewji tuko naye gym moja yule. 

Unapoanza kutii kanuni hizi hazitofautishi mpagani au mtu wa dini au mtu anayeamini kuwa kanuni zenyewe zipo au ni uzushi tu. Ukizifata utapata matokeo. Ukijumuika sana na wavivu utakuwa kama wao, ukijumuika sana na wasomaji vitabu utaanza tu kuongea na kuwa kama wao, ukikaa sana na watu wanosemekana kuwa wako kwenye “system” si muda mrefu utaanza kuwa na tabia na lugha na haiba ya aina hiyo. Ukijumuika sana na walalamishi utaanza kulalamika na kulaumu laumu tu kila kitu. Ukijumuika sana na wakosoaji  kila kitu utaanza kuwa mkosoaji pia na hata hutaona kuwa umebadilika. 

Kama wewe ni mwanafunzi ukijumuika sana na wanafunzi wanaonyoa viduku na kuvuta ile kitu kwa siri basi utajikuta umekuwa mmoja wao. Kama wewe ni mchungaji au mfanyabiashara ukijumuika sana na watu wanaovaa mapetepete sijui ya bahati na kupiga ramli na kuvuta watu utajikuta na wewe una mapetepete na vitu vya aina hiyo. Ndege wafananao..... 

Ukijumuika na walevi au watumia mihadarati vivyo hivyo kuna aina fulani ya tabia utaanza kufanana nao. Wewe ni tai lakini utajikuta unaishi na kuenenda kama kuku. Na hata ukiambiwa kuwa unatakiwa kutoka miongoni mwa kuku unaweza kuona wanaokwambia ndo hawajui kitu kuhusu wewe. Kumbe shida ni kanunu hii unaiishi ndivyo sivyo. Ukifollow page za umbea utakuwa mbea ukifollow za wanaotoa taarifa sahihi kuhusu maisha, mahusiano, biashara, nk utaanza kuwaza kama wao.

Sasa ukidhani kuwa kufanikiwa ni kuwa na ndoto tu na kuweka malengo hapo na kufanya kazi kwa bidii ukaignore kanuni hii ukajiendea tu na kujijumuisha tu na any THOM, DICK AND HARY unaweza kuwa frustrated kwa nini huoni mafanikio mapema. Angalia basi kila unayeona amefanikiwa kwa definition yako mwenyewe halafu uone kama katika marafiki zake watano wa KARIBU kuna mtu asiye na tabia za kimafanikio. Chunguza mwenyewe. Utapata majibu sahihi. Mimi nililitazama hilo  nikajifunza kumbe nahitaji kuiitii kanuni hii pia KWANZA!


2.       KANUNI YA KUPANDA NA KUVUNA (THE LAW OF SOWING AND REAPING)
Unaonaje kama ingekuwa ukipanda mahindi unakuwa hujui kitakachoota ni mchele au minazi au mipapai! Unadhani hiyo level ya uncertainty ingeathiri vipi maisha yetu? 

Lakini kanuni hii ya asili ikawekwa. Na hii inapatikana hasa ndani ya kanuni nyingine kubwa inayojulikana kama KANUNI YA KISABABISHI NA MATOKEO (ama the LAW OF CAUSE AND EFFECT) ambayo inasema kuwa hakuna kitu kinachotokea kwa bahati mbaya tu yani from nowhere ila huwa kuna kisababishi kwa kila jambo unaloona linatokea. Yaani ukiona ardhi imechipusha mahindi ujue kuna kilichosababisha. Na hapa ndo kanuni ya kupanda na kuvuna inapoingia. 

Anhaa! Kumbe kilichosababisha ni kuwa kuna kilichopandwa. 

Katika vitabu ninavyokusihi upitie kujiffunza bila kujali imani yako ni Biblia. Mfano ndani ya kitabu hiki tunapata reference ya kanuni hii. Kitabu cha Wagalatia 6:7 na kitabu cah Ayubu 4:8. Wagalatia wakaambiwa kuwa Mungu hadhihakiwi bali apandacho mtu ndicho atakachovuna! Hii ni kauli kali sana. Kali kwa sababu inalinganisha kutegemea kuvuna usichopanda kumbe ni sawa na KUMDHIHAKI MUNGU. Unataka kucheat kanuni zake za uumbaji wa mambo. Unataka kumfanya Mungu kama asiyejua alichoweka in place. 

Watu wote waliofanikiwa wanaitumia hii kanuni vlivyo. Kama ilivyo ukipanda mahindi unavuna mahindi ndivyo ilivyo pia ukipanda mahindi MENGI utavuna mengi. Kama wewe ni mwanamichezo ukifanya mazoezi mengi utapata matokeo bora zaidi ya asiyefanya mazoezi kabisa. Michael Phelps ni muogeleaji wa Marekani anayeongoza kwa medali za dhahabu za Olympic duniani kwa michezo yote inayochezwa kwenye Olympics

Mojawapo ya kitu alichowahi kufanya ni kufanya mazoezi makali kila siku mwaka mzima kwa miaka mitano mfululizo bila kukatisha. Kuna kukimbia, kunyanyua vuma, na kuogelea. na kwa juma moja anaogelea takribani kilometa 80. Umbali huo ni kama kutoka Dar es Salaam hadi Zanzibar kwa mtari mnyoofu (https://www.distancecalculator.net/from-dar-es-salaam-to-zanzibar

Sasa mtu anayepanda hilo unahisi anapaswa avune nini? Akivuna medali nyingi za dhahabu kwenye Olympics kuliko binadamu yeyote unashangaa? Tuna waogeleaji ambao wana huo uthubutu? Na je wewe na mimi katika maeneo yetu ya kuogelea (ndoto zetu) tunapanda bidii kiasi hicho?

Nasema tena ukidhani kufanikiwa ni kuandika malengo tu na kuyafanyia kazi ukashindwa kujua kumbe kwenye kufanya kazi ukipanda sana mgongo ukauma jua likakutandika sawasawa na ukachoka kweli kweli ndipo utavuna kwa kiwango cha “kutisha” basi utatamani mafanikio makubwa ya wengine bure bila kujua unatakiwa uogelee Dar hadi Zanzibar kwa wiki moja pia. Nilikuwa najiona ni mwenye bidii katika mambo yangu hadi nilipoanza kujua ratiba za watu waliofanikiwa katika maeneo ya ndoto zao ndipo nikaona nina kazi kubwa ya kufanya pia. Nimeona nishee na wewe huenda nawe ukaona unahitaji kukaza kamba za viatu zaidi.


3.       KANUNI YA NGUVU YA UVUTANO (LAW OF GRAVITATIONAL PULL)
Hivi Isaac Newton alipokuwa anafikiria kuhusu lile apple sijui kama alijua ilikuwa ni observation muhimu sana siku ile. Mojawapo ya nguvu kubwa mno za asili ni nguvu ya uvutano. Dunia hii inategemea mno nguvu hiyo na kumbe hata kutembea kwako juu ya ardhi ni kwa sababu ya nguvu hiyo. Yani wewe haujasimama wala kukaa wala kulala ardhini hivi hivi (CAUSE AND EFFECT) ila kuna nguvu inakuvuta. Ikikata hiyo tutaelea huko angani na kila kitu kinachojongea juu ya uso wa dunia kitaelea huko angani kuanzia hapo! Ajabu iliyoje! 

Ndipo nikajifunza kuwa ASILI iliweka hilo nalo litufundishe kitu. Yeyote anayetaka kufanikiwa hana budi kutii kanuni hii ya gravitation. Siku zote utavutwa pale ambapo nguvu ya kukuvuta ilipo.
Hivi nguvu yako iko wapi? Katika mambo ya mafanikio ama katika mambo yasiyo ya mafanikio?

Huenda hujanielewa. Labda nitoe mfano. Ukapita Kariakoo ukakuta kuna TV nje ya duka zinauzwa ila zinaonyesha matukio mbali mbali. Moja inaonyesha Eric Shigongo anazungumzia jinsi ya kujikwamua kutoka katika hali ngumu, nyingine inaonyesha Askofu Gwajima yuko LIVE anasema ana siri nzito anataka kuitoa. Wewe binafsi kiukweli kutoka moyoni wapi utaangalia sana. Anhaa. Mi sijui. Ila popote utakapoangalia naturally umevutwa kwa sababu huku ndo kuna nguvu kama sumaku inayoweza kukuvuta zaidi.

Kijana ukiingia mitandaoni ukaanza na page ambayo inakupa nyepesi nyepesi kwanza mpaka ukasuuzika roho yako hapo ndo ukaanza sasa kuscroll uone kama kuna kingine cha kukusaidia kupeleka bando ukingoni kabla haijachacha.. hahaaaaa. Ok. Like seriously, kule ulikoanzia ndo kuna gravitational pull huko. 

Kimsingi basi ni kwamba nguvu inayokuvuta inatosha sana kukupa majibu ya wapi unaelekea katika safari yako ya mafanaikio au la.
Kumbe siyo tu kuandika malengo na kuyafanyia kazi. Unapaswa kuwa na watu sahihi wanaokuzunguka na pia kujua upande nini ili uvune nini na pia kujua nguvu gani iliyo ndani yako na inavutiwa zaidi na vitu gani vilivyo nje yako. Usipoangalia utapoteza muda mwingi wa maisha yako mafupi ya hapa duniani kuvutwa na nguvu ya vitu visivyokuwa muhimu. 

Mwaka 2010 nilisoma kitabu cha Robin Sharma niliyemtaja pale juu kiitwacho THE MONK WHO SOLD HIS FERRARI ambamo ndani yake anasema ukitaka kufanikiwa lazima ufanye mambo kama roketi zinavyofanya. Kwambo roketi hutumia nguvu ya ziada na mafuta mengi sana ku-launch maana zinatakiwa zishindane na nguvu kubwa ya uvutano na ziishinde ndo ziweze kwenda huko  outer space. Akasema na wewe inabidi upingane na nguvu zinazokuvuta kukurudisha chini ili uweze kufika kwenye outer space yako. Kwenye mafanikio yako. Sijawahi kusahau.

Kwa hiyo unapaswa kuangalia pia hilo. Pingana na nguvu zinazokuvuta kukurudisha chini. Una malengo makubwa na ndoto nzuri lakini kuna nguvu ya marafiki wabaya inakuvuta kukurudisha chini.  Usipoishinda utarudi chini tu. Si unaona ukisimama halafu ukaruka juu. Huwa huendelei kwenda juu huwa unarudi chini tu. Hata wale rafiki zetu wamasai wanaruka wima wima wale lakini huwa wanarudi chini. Wanavutwa na nguvu wasiyoweza kuishinda. Kuna watu wanavutwa na mahusiano yasiyofaa, kuna watu wanavutwa nyuma na kupenda usingizi sana, kuna watu ni kuchati. Yani hawezi kushinda nguvu ya kuchatichati. Kuna watu ni habari za siasa na mpira na shilawadu. Yani zisipokuwepo anaweza kuumwa. Lakini na yeye anataka kufanikiwa kutimiza ndoto zake. Kweli?

Hilo pia nililiona na nikaona kuna vitu vinanivuta kwa nguvu kweli, lakini ili niwe yule Mungu alliyenikusudia kuwa yanipasa niondoke kwa nguvu ya roketi pia. Nimeona nishee hili pia kama litakusaidia. 


4.       KANUNI YA MVUTO (LAW OF ATTRACTION)
Miaka mingi iliyopita nikiwa mtoto wa shule ya msingi huko kijijini nilikuwa napenda kuimba nyimbo za bendi nk. Kuna siku mama akanisikia naimba wimbo wenye maneno yafuatayo: “SINA RAHA MASIKINI MIMI, SINA RAHA HATA KIDOGOO EEE.. KULALA KWANGU GHETO, MAISHA YANGU GHETTO....” wale wanaoufahamu nadhani wanaelewa. Mama alisikitika sana akaniomba nisiumbe tena maishani kwa sababu siyo wimbo mzuri. Lakini nikawa naimba kwa siri. Hahahaaa.. Miaka mingi imepita sasa na nikitazama mambo ya aina hiyo najifunza kuwa kumbe kweli nguvu ya maneno ni kubwa sana maana kuna kipindi kweli nilikuja kuishi ghetto na ‘masela’ maisha magumu kweli.  Na wakati naishi ghetto hivyo sikuwahi kuwaza kuwa kuna connection yoyote ya maneno yangu ya zamani na uhalisia huo.

Kimsingi kanuni hii haina tofauti na kanuni ya kupanda na kuvuna ambayo kama nilivyosema ni mzaliwa wa kwanza wa kanuni ya CAUSE AND EFFECT. 

Yaani sikuishi tu ghetto hivi hivi. Kwa maneno yangu na kuimba kwangu na hisia nilizokuwa naziweka nikiwa naimba nilikuwa naanzisha KISABABISHI cha hali ninayoiimba toka utoto. Nilikuwa na-ATTRACT hali hiyo maishani mwangu. Bila kujua. Nilikuwa najenga negative faith bila kujua.

Vile ulivyo, mambo unayoyamini, mambo unayoyasema ni mbegu. Inaenda kuATTRACT vitu unavyotamka bila wewe kutaka. Kuna mtu anasema hivi: YANI MIMI NIKIWA NAENDA KITUO CHA DALADALA HUWA NAKUTA DALADALA INAONDOKA YANI LAZIMA NIKUTE HIVYO. Huyu anasema kitu anachohisi hakina madhara yoyote. Mwingine anasema MSHAHARA UKITOKA BANA MI NAJILIA ZANGU RAHA BANA KUJIBANABANA YA NINI KAMA IPO IPO TU... Haya hizo kauli nyepesi nyepesi zisizotii kanuni za asili. Unapanda mbegu. Inaenda kuaATTRACT maisha yasiyoleta matunda mazuri maana hutaki kutii kanuni husika.

Mafanikio si kitu cha ku-PURSUE mafanikio ni kitu unacho ATTRACT kwa vile unavyozidi kuwa. Mfano kama hujawa mtu ambaye unastahili kumiliki pesa nyingi huwezi kuziattract. Utakuta unalazimisha tu zije wakati hujaweza kuwa na urafiki nazo. Haziwezi kujiASSOCIATE na wewe. Ukilazimisha utaleta matatizo.

Nilimpa mfano kijna mmoja anaishi maeneo ya Kimara hapa Dar es Salaam hivi karibuni nikamuuliza kwamba itatokea nini maji ya mto Ruvu yakiamuriwa na nature yatoke huko yaliko yaje nyumbani kwenu. Akasema yatabomoa nyumba. Nikamuuliza kwa nini? Akasema sababu hakuna kitu cha kuya-contain yaingie na kutulia. And yes. Maji yakienda nje ya utaratibu wake ulioamriwa bila kuwa na nguvu ya kuyazuia huleta uharibifu usiopimika. Nikamwambia ndivyo na pesa zilivyo. Ukilazimisha milioni 100 zipite mikononi mwako kabla hujawa tayari zitafurikisha maisha yako nay a wengine pia.

Kwa hiyo badala ya kuweka lengo tu la kupata mahela mengi weka lengo la kuwa mtu sahihi. Pesa sahihi itakuja. Kama pesa sahihi kwa jinsi ulivyo sasa ni laki 5 kwa mwezi itakuwa hiyo. Hata ukipata milioni mbili hutaiweza. Kama pesa sahihi kwako ni milioni 100 kwa mwezi utaipata na wala hutanyanyua mabega wala kutukana trafiki njiani tena inawezekana hakuna atakayejua. Benki tu ndo zitajua na watu wachache wa karibu na TRA labda. Lol.

Nikazingatia pia hili. Na lilileta kwangu matokeo mazuri mno na linazidi kunipatia matokeo mazuri kila siku. Badala ya kukimbizana na kufanikiwa inabidi mafanikio yanikimbize mimi. Sasa hapa kwenye mafanikio kukukimbiza siongelei habari za uganga hapa. Maana kuna watu ni mwendo kasi sana. Huko kwetu zamani kuna jamaa alimpenda binti. Akaenda kwa mganga. Apate dawa ya kupendwa na yule binti. Sasa mganga akamwambia jama njoo keshokutwa na yule ndege mwenye rangi rangi nyingi yule. Kule kijijini tulikuwa tukimwita “engolobhya” na pia uje na jogoo mweupe. Jamaa akamsaka akampata. Mganga akachukua zake jogoo kama kawaida halafu akamchinja yule ndege akatoa firigisi halafu akaipakazapakaza ile firigisi kwenye fimbo mbichi. Akaianika ile fimbo eti ikauke. Kisha akampa yule jamaa akamwambia sasa nenda ukimwona yule binti mpige na hii fimbo atakufata mpaka utakapoenda. Jamaa akaenda kisimani akategeshea yule binti alipofika tu kisimani jamaa akaenda taratibu akamtandika binti wa watu bonge moja la stiki binti akahamaki. Akaanza kumkimbiza yule jamaa hee jamaa ikabidi aanze kukimbia binti akamkimbiza mpaka kwao. Ikawa kesi kubwa sana sasa jamaa kujieleza hawezi lakini kumdai mganga hawezi maana mganga alisema atakufata popote utakapokwenda! Waganga hawana kitu ni akaili tu kidogo.

Sasa kwenye mafanikio usiishi kwa akili za kishirikina kama hizo. Mi naongelea kanuni. Jiweke katika hali ambayo mafanikio yatakata kona zoote mpaka yatakuja kwako! 

Kwa hiyo malengo ni sawa, bidii ni sawa, kujumuika na watu sahihi tumesema, kupanda mbegu sahihi ni muhimu, kuvutwa na mambo ya maana ni muhimu ili usije kuvutwa na yasiyo ya maana na hapa nimesema kujiweka katika hali amabayo unavuta vitu sahihi kwako. Wewe ndo unavivuta. Ukiwa kiongozi uongozi utakufata. Ukiwa si kiongozi utagombea kila kitu mpaka siku ya mwisho hupati. Na ukipata nature itakataa itakutema tu. Utalaumu watu lakini kuna kanuni haiko sawa. Kuna mtu anagombea ubunge jimbo gumu anapata. Kuna mwingine udiwani kata nyepesi tu hapati. Huyu hajaattract hiyo position. Kuattract siyo suala la kutembea unatamka kuwa ntakuwa raisi ntakuwa mbunge. No. Unapaswa kuwa raisi NDANI YAKO kwanza. Yesu alisemaje OSHA KIKOMBE NDANI KWANZA.....nje patakuwa safi tu penyewe. 

Kuattract mafanikio inabidi uoshe kikombe ndani. Character sahihi. Hapa nilijifunza the hard way. Na nimekuwa mwanafunzi mwenye kujifunza mno enoe hili kwa sababu ya unyeti wake. Kuna level fulani ya success huwezi kuifikia kama kikombe ndani ni kichafu. Hata kama nje ni pasafi kivipi. Mafanikio yanataka yaingie kwenye kikombe chako. Na huwa yana kawaida ya kunusa kwanza kikombe chenyewe. Yesu akasema, Safisha kikombe ndani kwanza...

Alijua asili inafanyaje kazi. Uko tayari kujifunza pia? Fanyia kazi. 


KANUNI YA TAFSIRI YA MPANGILIO WA MAMBO (LAW INTEPRETING THE ALIGNMENT OF THINGS)
Katika biblia kuna mambo kadhaa yaliyowahi kutokea yanayoweza kutusaidia kuelewa hii kanuni. Mfano kwa habari za kuzaliwa kwa Yesu kuna mambo kadhaa yaliyotokea na kujipanga sawia ku-indicate kitu kisicho cha kawaida. Mfano mamajusi na habari ya nyota. Malaika na wachungaji wa mifugo usiku. Nk.

Kwa habari za kifo cha Yesu kuna habari za pazia la helaku kuchanika katikati toka juu hadi chini, Kuna jua kuwa giza kwa masaa matatu, kuna tetemeko kubwa la ardhi. Na kuna AKIDA wa utawala wa RUMI (Roman Centurion) ambaye alikuwa amesimamia zoezi zima la kuhakikisha mtu anayeitwa Yesu Mnazareti anakufa kama hukumu ilivyokuwa imetolewa na mamlaka. Tunaambiwa huyu mtu ALIPOONA hayo yaliyotokea (kwa yale aliyoona mwenyewe) ile alignment ya mambo ikampa jibu moja tu: “HAKIKA HUYU ALIKUWA MWANA WA MUNGU”.

Interpretation ya NATURAL ALIGNMENT OF THINGS. Mungu alituwekea alama nyingi mno kuthibitisha kuwa yupo. Na akaweka kanuni nyingi za kutusaida kutambua mambo yaliyopo na yajayo. Ukiwa mwanafunzi mzuri wa nature pia utajifunza vitu vikubwa mno katika mambo yanayoonekana ya kawaida. Confucius aliwahi kusema ukiwa na utayari wa kujifunza unaweza kujifunza hata kwenye MWAMBA. 

Nikiwa mdogo nilikuwa naambiwa ukiona sisimizi wanatoka nje ya nyumba wanaingia ndani na wamebeba mayai yao ujue siku hiyo ama siku chache sana mvua itanyesha. Sasa sisimizi wanajuaje ni kitu kingine lakini hapa naongelea kujifunza kwenye asili. Na kweli mvua ilikuwa inanyesha katika timeframe hiyo.

Tukiwa tunawinda kuna milio ukisikia ndege wanalia wengi kwa wakati mmoja unaweza kukuta kuna nyoka mahali hapo. Na ikawa tunaona kweli kuna nyoka. Mvua ikinyesha ng'ombe wakalia sana usiku ujue mafuriko yanaweza kutokea na kweli mafuriko yanatokea.
Yapo mengi. 

Point yangu hapa ni kuwa kuna haja ya kutazama ASILI na kujua namna ya kuitafsiri kulingana na hali ilivyo. Kuna mambo Mungu alitaka tujifunze kwenye ASILI. Kamtazame chungu ewe mvivu! Hiyo ni Mungu anasema mtu mvivu anatakiwa akajifunze bidii kwa ANTS!! 

Kumbuka kufanikiwa nje ya season yako siyo mafanikio. Kama kuna mzee sasa hivi aliyekuwa na ndoto ya kuandika kitabu kuhusu jinsi ya kuimarisha chama labda cha AFRO SHIRAZI PARTY halafu anataka akiandike sasa hivi, dah, ni kweli amefanya lakini ni out of season. Enzi hizi na Afro Shiraz tofauti. 

Njia mojawapo ya kufanikiwa inside of your season yako ni kujifunza sana kwenye ASILI. Nature has so many answers kuhusu mafanikio yako. Kila mtu unayekutana naye, kila unachosoma kuna namna ambavyo vinaathiri destiny yako.
Nature haiwezi kudanganya. Yule akida alikuwa anajua kutasfiri nature’s alignemnet of things. Kuna watu lukuki walikuwa pale lakini ni yeye tu aliyeona kuwa tafrisi sahihi ya mambo yaliyotokea pale Fuvu la Kichwa ilikuwa ni ujumbe kuwa huyu mtu alikuwa ni MWANA WA MUNGU.

Kuna wakati ASILI itakuletea mke au mume usijue. Mvua imenyesha daraja limevunjika mko stranded upande wa pili wa barabara nature imeleta tukio ili kukukutanisha na mke/mume au business partner mtarajiwa wewe uko busy unachati na kutuma picha za daraja WhatsApp. 

Kwa kuwa tunaishi kipindi cha kutokuwa sensitive na Mungu na ASILI itokanayo na  yeye ndo vitu kama hivyo tunaishia kulaani mvua kwa nini inanyesha mjini. Internal antennas zetu zimeota kutu siku nyingi. We can't tell a B from a Bull. Unaota ndoto unapotezea tu unasema kwa kuwa usiku nilikula ugali ndo maana nikaota niko DUBAI. Tena unajiambia eti DUBAI NA MIMI WAPI NA WAPI? Hahaaaaa. Antena iko na kutu. 

Jua limewaka sana likakupiga ile mbaya kumbe huenda Mungu anataka ukumbuke ile idea yako ya kuuza jusi za baridi wewe unakazana tu kulalamika jamani jua litatuua. Na litakuua kweli hata kama siyo leo. Maneno yana nguvu. Usishangae likakuchagua wewe ndo likupe kansa ya ngozi of all people. UZIMA NA MAUTI VIKO WAPI.........?  Biblia inasema viko kwenye uwezo wa ulimi wako. See?

Unasafiri kwenda South Africa mmetua tu mkaambiwa kuna fujo mtaani subirini kidogo. Au mtu wa kukupokea atafika baada ya nusu saa alichelewa kidogo. Usilaani. Unatakiwa kuwasha antenna. Fast. Nini ASILI inamaanisha. Nini MUNGU anataka kufanya na wewe. Usikute kuna kitu muhimu cha kufanya au mtu muhimu wa kuonana naye kabla hujatoka airport. 

Mafanikio yamewapita wengi kwa sababu ya kutokuwa sensitive na mahali walipo. Kuna watu walikaa na John Pombe Magufuli au mama Samia na pengine hawakuona umuhimu wa kuwa na ukaribu na Magufuli au Samia kwa miaka mingi tu. Leo hii anatamani angejua enzi hizo. Too late. Out of season.


Unajua kusudi na mambo yalivyojipanga maishani mwako? Umekosa ajira, unadhalilishwa kwenu, boyfriend kakuacha. Unaweza kuinterpret hayo mambo tofauti. OPRAH aliyainterpret  mambo ya aina hii tofauti. Ndo maana akawa OPRAH. JK ROWLINGS alitaka kujiua kwa sababu ya kumisintepret mambo lakini alipoaacha kujiua leo hii ni bilionea ili wewe ujifunze.
Una bidhaa yako unauza hakuna anayekubali kununua....

Colonel Sanders mwanzilishi wa KFC alipopokea pensheni yake akakata tama ya maisha akainterpret vibaya hiyo hali pia akataka kujiua. Lakini kabla ya kujiua akasema hebu ngoja nikaandike vitu amabavyo sijawahi kufanya. Kaandika. Ukawa mwanzo mpya na mawazo ya kujiua yakaishia hapo.Kama unasoma hii article na ulishawaza kukatisha uhao wako, au wa mtu, hujatafsiri ASILI kwa usahihi. Asili ikitaka ufe haihitaji uisaidie. Mungu akitaka ufe hahitaji umsaidie hiyo kazi. ASILI bado inakuhitaji uwepo.

Hilo nalo nikajifunza na kulitazama kwa makini. Nalo nialifanyia kazi kila mara. Na nina shuhuda za jinsi kuwasha antenna zangu za ndani kulivyonisaidia sana katika safari yangu ya mafanikio. Ujifunze pia kama utaona yafaa. ASILI ni mwalimu mzui ukijifunza vema kutafsiri mafunzo yake kwa usahihi. Kwa hiyo ukijua kwa nini mambo yamejipanga jinsi yalivyojipanga maishani mwako sasa. Kwa nini umefiwa. Kwa nini umeachwa. Kwa nini umefilisika. UKIJUA USAHIHI WAKE utapiga hatua haraka sana.


Ninatumaini makala hii imekuwa muhimu kwako. Kama ndivyo nitafurahi kupata maoni yako. 

Mungu akubariki na kukufanikisha katika safari yako ya mafanikio.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.
WhatsApp +255788366511


   

Jumapili, 12 Machi 2017

WHAT MARK WILL YOU LEAVE? LEARN FROM AN OLD CHIEF OF UKEREWE

WHAT MARK WILL YOU LEAVE?
WHAT WILL YOUR LEGACY BE?


This building was erected in 1927/28 by the 16th Chief of UKEREWE, Omukama Mwinamila GABRIEL RUHUMBIKA. He was a very wealthy chief not because his subjects brought virtually everything to him but because he had a business man's mind. He traded in cotton, sugarcane and sugar (he had a factory for sugar production close to this residence). His businesses grew beyond the shores of this island to Kagera and Uganda. It's in Uganda where he got an Italian architect who designed this building and all the materials for this building came from there! That's the late 1920s we're talking about. Man.!

He is the most revered chief of Ukerewe and this is mostly because HE LEFT THIS MARK. Neither his son and heir, chief Omukama Mwinamila MICHAEL LUKUMBUZYA (17th chief) who ruled after him and who was well educated and was later appointment as Tanzania's ambassador to Canada, nor his grandson the current chief VIANNE KASEZYA (18th chief) who resides in Austria are as revered as chief RUHUMBIKA because of the mark he left. My grandfather worked as his secretary and was rewarded a plot of land close to this place - our home place till today. So the chief had an impact even in my family and my life. He left a mark to our family too...

And so I thought of this thing called LEGACY. Leaving a MARK. This story may not concern you one bit as it does me but I believe you will agree that we all can learn something from it. We live in a world where people are increasingly encourage to love themselves more than loving anyone else where people are shown how to spend their money or time on and for themselves more than on or for anyone else. We forget that GREATNESS is the outcome of, even a reward for SERVICE TO OTHER PEOPLE. The legacy of the aforementioned chief may not be of importance to you but the nail I'm trying to hit into your wall here is: WHAT MARK ARE YOU LEAVING BEHIND? What will your family, street, community, country or the world at large remember you for? What will people show future generations that will demonstrate that YOUR LIFE WAS NOT IN VAIN...?

What will the universe look back at and hold in its incredible infinite hands and declare that there once lived a human being IN YOUR NAME?
If someone can erect a building that can stand the test of time you can do something too. You can build a school, plant a tree, clean a riverbank, feed the poor or cut their hair for free. You can compose or sing a song, write a book, protect elephants, build an incredible sports team, take man to the moon or Mars or develop a life-changing App.

There's more than enough room for all of us to build our legacy. There's no shortage of raw materials to build your legacy with.
There's no shortage of time for those who want to leave a mark.

Just find your WHY? Why you were created, why you're here. Why anyone needs to remember your name when you're long gone. Hold the pen and write your own history.

Leave a mark.

Semper Fi,

Andrea G Muhozya
Bukindo, Ukerewe, Mwanza, Tanzania.
East Africa.
www.andreamuhozya.blogspot.com

WANNA START A BUSINESS? THEN THINK LIKE YOU'RE IN FAST-FORWARD MODE

So we meet again.
Yep. And this is what I have for you today.

If you want to start a business just start. Fast! Don't sit on it waiting to ask for people's opinions.

Listen to me my friend. HENRY FORD. You know that name? Hope you do. Now let's talk a bit about him.
This guy once said if he had gone around asking people what they wanted before making his car they probably would have told him they wanted "FASTER HORSES". Okay, from the horse's mouth..
 But he came with the idea of a car. And then told people why they needed one. Brilliant! Don't you think?

ZUCKERBERG! You know him right? He's the reason you're guaranteed to read a book every day. I mean, Facebook. So, this guy didn't ask anyone what they needed before he created Facebook. He showed us mortals what we needed.

JOBS. I'm not offering any jobs. I'm talking of STEVE JOBS. He didn't ask people if they wanted shiny sexy gadgets for a computer or phone. He just went "LOOK-A-HERE GUYS, SEE WHAT I'VE GOT" and today when you say the world APPLE it's no longer unambiguous.

So....
If you think you have to ask people first what they need before you start your business you're going to spend the rest of your time as a living creature trying to make "faster horses".

ELON MUSK didn't go around asking "what kinda car d'yall need buddies?" He said instead "HEY EVERYONE LOOK WHAT WE'VE GOT... AN ELECTRIC CAR" and he together with his lot are really dooming the oil business to obscurity, albeit slowly. But a thing in slow motion IS only an illusion of delay. I mean, think about it.

What about ARTIFICIAL INTELLIGENCE (A.I.)? No one ever asked you if you're okay being operated by a robot or a human doctor or if you are okay being served by a robot in a restaurant or if you want to go with human beings carrying trays for ever? No one asked you these questions. People just made robots. And that's the FUTURE my friend. The PRESENT in some places of course.

If you are going to have a flourishing business my advice is be creative and get going faster than horses. Don't wait for anyone to validate your idea. I tried a few creative things without asking customers and they are actually working. They will work for you too.

Bill Gates talks of BUSINESS AT THE SPEED OF THOUGHT. It's no longer the stronger eating the weak. No, no, no. Now it's the era of the FASTER eating the SLOWER. So think FASTER.

Think like you're in Fast-forward mode!

Let me know your thoughts on this article or blog.


Semper Fi,


Andrea G Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa
www.andreamuhozya.blogspot.com

Jumatano, 15 Februari 2017

KIPI HUNA KATI YA HIVI: NDOTO, MALENGO, MIPANGO, NA NIA YA DHATI? AU HUNA VYOTE?

*KIPI HUNA KATI YA HIVI: NDOTO, MALENGO,  MIPANGO, NA NIA YA DHATI?
AU HUNA VYOTE?*

Karibu kupitia haya pia..

Kila siku iitwapo leo nakutana na kuwasiliana na vijana wenzangu kutoka kila pembe ya nchi hii na wananiambia wanataka kufanikiwa. Katika kuzungumza na kila mtu ninazidi kujifunza vitu vingi. Nimeona nikushirikishe wewe pia huenda vikakusaidia.

So, nimejifunza kuwa kuna vijana wa aina 4.

*KUNDI LA KWANZA*

Hawa hawana ndoto (dreams)❌, wala malengo (goals)❌, wala mipango (plans)❌ za kuwafikisha wanakotaka.

Yes. Wapo wengi tu.
Kwa kifupi hawajui kwa nini hawajafa bado. Seriously ukimuuliza kwa nini bado uko hai atakwambia "ni mipango ya Mungu".  Unaweza kusema hawajajitambua bado. Unaweza kusema hawajielewi. Unaweza kusema hawajui hata kwa nini waliumbwa. Hawa ndo hawajui hata tafsiri ya mafanikio. Wengi wao wanaishi kwa kufuata kinachoitwa "societal norms". Mkumbo tu. Hawa ndo wana muda wa kutosha kujadili kuhusu skendo za wasanii, nchi ina njaa au haina, tuhuma za madawa, Makonda anafaa au hafai. Wewe uko Ukerewe huko tena Ukara, Makonda anakuhusu nini truly?😞😞
Kundi hili lina watu wengi wa kada zote waliosoma na wasiosoma wenye ajira na wasio na ajira na waliojiajiri. Ni kundi kubwa na lina kelele nyingi kwenye social medias. Huyu anaweza kuingia Facebook ku-scroll tu. Kisha mlio wa WhatsApp ukilia huyo. Anaingia kuchek kwenye group kuna nini. Kisha Insta kuangalia nani kapost nini!
Hawa wanaongoza kulaumu serikali na wazazi na kulalamika kukosa sapoti au kukosa mitaji pasi na kujua kuwa tatizo kubwa liko kuanzia shingoni kwake kwenda juu!

Kama upo kundi hili ni dhahiri umaskini ni fungu lako. Hawa hata Mungu wanamfanya mganga wa kienyeji. Wanataka waombewe eti wafanikiwe. Kwa dreams zipi sasa? Kwa goals zipi na plans zipi?
SMH

*KUNDI LA PILI*

Wapo ambao wana ndoto tu peke yake (dreams)✔ ila hawana malengo (goals)❌ wala mipango❌

Hawa angalau wanajua kuna kitu wanapaswa wafanye. Shida unakuta hana malengo. Mfano ana ndoto ya kuwa mwanamuziki wa kimataifa. Ok sawa. Sasa umejiwekea malengo yapi? Hola. NIL. Nada!!
See? Anaongelea ndoto zake kweli kweli. But hajui aanzie wapi. Mwisho anakata tamaa. Anaanza naye kuongelea madawa ya kulevya mpaka akili yake inaanza kulewa nayo. Afu anaishia hapo.
Hawa huwa nawaambia wakae chini watulie wajiulize kama kweli ndoto wanazosema wanazo ni ndoto kweli au just wishful thinking? Maana ukiwa na ndoto kweli hutatulia. Utakuwa kama mjamzito. Hali yako itakuwa inabadilika tu as time goes on. Nikiona una ndoto halafu maisha yako hayana kuhangaika fulani hivi kusaka njia ya kuitimiza najua hiyo ndoto si yako.
Lazima ukae chini kubuni Goals na Plans za kufikia ndoto yako.
Mfano nina ndoto ya kuwa mtu mwenye maarifa ya mambo mengi. Hiyo ni dream. Goal gani nimeweka? Ok mwaka huu nimeweka lengo (goal)  kusoma vitabu 50 kwa mwaka ili kuongeza maarifa. Kitabu kimoja kila juma. Tunavyoongea tuko juma la saba la mwaka na niko kitabu changu cha saba pia.
Kama upo kundi hili tafuta mtu anaitwa JOEL NANAUKA hapa Facebook. Search hilo jina. Ameandika kitabu kizuri kinaitwa TIMIZA MALENGO YAKO. Kitakusaidia.

*KUNDI LA TATU*

Wapo ambao wana ndoto ✔ na wana malengo✔ ila hawana plans (mipango)❌ ya jinsi ya kutimiza malengo yao.

Hawa wanahitaji usaidizi kidogo.
Nimekupa mfano wa dream yangu na goal ya 50 books. Plan yake je? Hapa iko hivi nimeweka PLAN rahisi tu kuniwezesha kutimiza hiyo goal. Mojawapo ni kuwa kila kitabu nachukua idadi ya kurasa nagawanya kwa (siku) saba. Mfano kitabu nilichomaliza juma lililopita kilikuwa na kurasa kama 420. So nilisoma kurasa 60 kwa siku. Everyday. Cha wiki hii kina kurasa 200. Vingine unakuta kurasa 150. Hivyo hivyo. Nadhani umepata picha.

So ninakutana na vijana wengi wana mpaka malengo. But plans hana. Anataka kuingiza sh milioni 50 mwaka huu ili mwakani afanye kitu kinachompeleka kwenye ndoto zake. Goal nzuri kabisa. Lakini hana plan. Hawa ndo unakuta wanacomment AMEN akikuta Facebook mtu amepost picha ya maburungutu ya pesa. Anaishi kwa superstition.

Lazima uweke plan. Na uifate. Je plan yako ni nini unajiajiri? Au unaajiriwa part time?
Plan.
Plan.

Ukiwaza hivi vitu utapata muda wa kufatilia mambo yasiyoisha ya siasa na wasanii kweli? Unaishi na akili imejaa sura ya Gwajima na Makonda siku nzima. Unajitambua?

Sumbua akili yako. Be serious. Mentor wangu aliniambia "Your mind has to be on a leash at all times! Like a dog on a leash. You must control your mind". #IloveMyMentor.

Kataa kupoteza muda.
Bila hivyo utasema dream zako hadi unaingia kaburini. Ishu ni DISCIPLINE. Nidhamu. Bora ukose kula kuliko kukosa kufata plan yako.

*KUNDI LA NNE*

Wapo ambao wana ndoto✔ wana malengo✔ na mipango mingi✔ tu ila kuyafanyia kazi  wanashindwa❌

Yes. Unaweza kugawanya kurasa za kitabu na usisome vile vile.
Hapo ni ishu ya UDHATI. Napoleon Hill anaiita hii DESIRE na kusema ndiyo chanzo cha mafanikio yoyote. Jim Rohn anaiita hii AMBITION. Kutaka kwa dhati. Nenda You Tube andika Jim Rohn: Power of Ambition usikilize. Kipi bora: bando yako iishe kwa kusikiliza Wema Sepetu sijui anaeleza nini kuhusu Masogange au iishe ukisikiliza na kujifunza vitu vya kukusaidia kufanya lililokuleta hapa duniani. Unakuta mtu yuko Chuoni anasoma lakini mind imejaa ramani ya Central Police Dar. Yani wewe uko UDoM central ya Dar inakuhusu nini lakini? Notes hujamaliza kuandika uko WhatsApp!

It's your choice though.

But hii "EAGER DESIRE", hii ambition ndo Dangote alisema kama huna basi hupaswi kuwa hai. Unasikia maneno hayo?

So kundi hili la watu wasiofanyia kazi mipango yao shida ni HAWANA DHAMIRA YA DHATI kutimiza ndoto zao japo kwa nje wanaonekana kama vile wanaenda kwenye ndoto.

Sasa sijui wewe unajiweka kundi lipi. Najua huwezi kujidanganya mwenyewe. Unajijua ulipo.
Asubuhi ya leo nilikuwa na vijana wanne  mmoja kamaliza kidato cha nne watatu wamemaliza chuo wote wana DREAMS. Hawana goals wala plans! Nimewaelekeza na kuwaomba tuonane kesho Asubuhi tena kila mmoja wao akiwa keshaandika hayo. Watu unaowajadili wana maisha yao. Jaribu kujadili ya kwako.

My friend,

Tafuta kuunganika na watu wanaokupeleka kwenye mafanikio yako. Watu wasiopoteza muda na clip za bungeni kila siku. Mi nataka clip za mambo yanayonipeleka kwenye ndoto zangu. Siyo za madawa ya kulevya. And that's me. Wewe kama unataka za Bunge fine. But if unataka kubadilika utimize na kuishi ndoto zako basi karibu tuzungumze zaidi. I hope nitajifunza kwako na pia utajifunza mawili matatu kwangu.

But truly, UTAWAAMBIA NINI WATOTO WAKO KUHUSU KWA NINI HUKUFANIKIWA MAISHANI with all the time you have?

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa

www.andreamuhozya.blogspot.com

+255788366511