Ijumaa, 11 Septemba 2015

NGUVU NA MUDA VIKIISHA MWENYE MAONO ATAFANYA NINI?

NGUVU NA MUDA VIKIISHA MWENYE NDOTO ATAFANYA NINI?

WHAT WOULD A DREAMER DO WHEN THEIR ENERGY IS GONE OR THEIR TIME IS OVER?

Hapa Sinza kuna mahali panaitwa Sinza Makaburini. (Nadhani unaelewa kwa nini panaitwa hivyo). Kuna siku nilikuwa narejea nyumbani kutoka kwenye "mishe mishe" zangu. Late night. Saa nne hivi usiku. Nikapita eneo hilo upande zinakopaki taxi kwa wanaopafahamu. Niko natembea kwa mguu. Nimechoka. Ninawaza mambo yangu yalivyoenda siku hiyo. Ghafla nikasikia sauti ndani mwangu from nowhere inanambia: "Angalia hilo kaburi palee". Of course nikaangalia. Ile sauti ikaniambia hivi: " Huyo mtu alikuwa na ndoto kubwa kuliko za kwako, lakini nilishamchukua. Hayupo tena duniani" Halafu basi sauti ikapotea. Can you imagine? Kwanza moyo ukadunda balaa.. Si unajua..? Teh. Halafu akili ndo ikarejea japo hayo yote yalikuwa kama ndani ya sekunde 10 tu hivi!! Nikajua Mungu alikuwa anasema na mimi kitu kuhusu ndoto zangu. Maana yake yule mtu kwenye lile kaburi MUDA wake uliisha kabla ndoto zake kubwa (kuliko za kwangu) kutimia. Na ndivyo inavyokuwa kwa watu wengi. Nilifikiria usiku wote siku ile. Ni true story hii. Niliwaza sana kuhusu maisha yangu that night.

Hii inanirudisha miaka kadhaa iliyopita. Nilipokuwa nimeajiriwa.  Nilipenda sana kuwahi kazini alfajiri ili kupata muda wa kuomba, kusoma vitabu na kuota ndoto zangu za maisha.  Stanbic Bank HQs...Sehemu ambayo sitaisahau kwa sababu ya mambo meengi sana ikiwemo jambo hili. I will always love that place. Mara nyingi nilifika kazini saa 12 kasoro na hivyo nilikuwa na muda mwingi wa kukaa parking kusoma kuomba na kuota ndoto zangu mpaka saa moja na nusu yaani nusu saa kabla ya muda wa kazi. Huo ulikuwa ulimwengu mwingine. Ulimwengu niliokutana na Mungu kila asubuhi halafu baada ya hapo nikawa na kina Robin Sharma (The Monk Who Sold His Ferrari, Who Will Cry When You Die, Family Wisdom, Leadership Wisdom, The Leader Who Had No Title), kina Ryuho Okawa (An Unshakable Mind), Napoleon Hill (Think and Grow Rich), kina Robert Kiyosaki (Rich Dad Poor Dad na Cash Flow Quadrant) Zig Ziglar (How to Raise Positive Kids in a Negative World) Sergio Bambaren (The Dolphin - Story of a Dreamer) na vingine kadha wa kadha..

Kama umewahi kusoma kitabu ukahisi mwandishi alitumwa akuandikie wewe basi ndo ilivyokuwa kwangu. Nilipata mawazo mapya chanya na vitabu vilinipa pia nguvu na mwamko mpya wa kuota ndoto upya. Ndoto nzuri. Ndoto kubwa. Vitabu vilinifanya nione maisha yangu kwa mtazamo mpya na mpana. Ndoto zangu ziliongezeka ukubwa kila kitabu kipya kilipoingia ufahamuni mwangu. Mwishowe nikaona niache kazi (ku-resign) ili kuzifuata ndoto zangu mpya.

Halafu nikaanza safari ya kuzifuata ndoto zangu. Sasa hapa ndo nataka kuongelea zaidi leo.

Kuna mambo kadhaa niliyoyaobserve wakati naanza kuzifuata ndoto zangu.

MTAZAMO WA VIJANA
Vijana wengi wa rika langu au chini yangu walihisi nimepata dili jipya au nimepata kazi nyingine ya maana nk. Na wengine waliojua nataka kuanza maisha ya biashara hawakujali sana (kuhofia) kuhusu maisha yangu yatakuwaje maana walijua bado ni kijana na nikishindwa huko niendako labda ntarudi kazini hata kama siyo pale. Kwa kifupi mtazamo wa vijana walio wengi ulikuwa "GO GET IT MAN" au "SEE YOU MAN". Whatever it was. Walichukulia "poa" tu ngoja kijana akaangalie ustaarabu mwingine mwenyewe. Lakini wengi wao hawakuwa tayari kufanya maamuzi binafsi ya aina hiyo.

MTAZAMO WA WATU WAZIMA
Kwa heshima kubwa ya watu wazima wengi nilijifunza kitu kikubwa sana kwao katika kipindi hiki. Asilimia 99% ya watu wazima wote niliokutana nao kipindi hicho walinishauri nirudi kazini kwanza, na wengine walinioffer ajira kwa kuona potential waliyoifahamu ndani yangu, na wengine kunihofia sana kuhusu future yangu ingekuwaje bila ajira ya kueleweka iikizingatiwa kuwa niliacha kazi katika ofisi yenye jina kubwa mjini ambapo vijana wengi wangependa kufanya kazi. Tena ajira ya kwanza maishani halafu baada ya miaka miwili tu ya kuajiriwa.
Kitu walichofanya wote hawa ilikuwa kunishauri kama watu wanaonijali kabisa na nitawashukuru kila siku kwa kunijali hivyo. Lakini sikufuata ushauri wao licha ya kuwaheshimu sana. Sikufuata ushauri wao  sababu tu ya nguvu ya ndoto na maono yangu ambayo wengine sikuwa na uwezo wa kuwafafanulia katika lugha ambayo wangeielewa. Kiukweli wapo walioniona "much know" na wengine waliodhani "nimetupiwa" kitu. Wengine waliona nina haraka na maisha. Na kiukweli wote niliwaelewa tu.
Lakini niliona jambo fulani pia kwa kundi hili la watu wazima. Tulikuwa tukitazama suala la ku-RISK kwa macho tofauti kabisa. Au lensi tofauti. Lensi mbinuko na lensi mbonyeo.
Kilikuwa kipindi muhimu sana kwangu.

MTAZAMO WANGU BINAFSI
Kitu kikubwa nilichokiangalia zaidi ya vyote ni mtazamo wangu binafsi. Nilikuwa nikiwaza zaidi kuhusu uhusiano wa NDOTO ZANGU na NGUVU ZANGU. Nilijua nguvu zangu zilikuwa zikiongezeka kama kijana zinaongezeka lakini sikujua lini zitaanza kupungua. Na hilo lilinifikirisha sana. Nilizingatia sana hilo na kuona ni vema nianze kutumikia ndoto zangu ningali na nguvu zangu mifupani mwangu.....

~ Nianzishe vitu na kushindwa ningali kijana ili nijue mapema nini hakifanyi kazi.
~ Nianguke mara nyingi na kuinuka mara nyingi zaidi ningali na nguvu za kunyanyuka mara nyingi zaidi.
~ Nijue mimi ni mtu wa aina gani mapema na kurekebisha yanayonipasa kurekebisha kila inipasapo..ningali kijana.
~ Nisafiri huko na kule kujenga msingi wa kutimiza ndoto zangu ningali na nguvu na muda wa kufanya hivyo...ningali kijana.
~ Nithubutu kujaribu mambo magumu mapema ningali na nguvu za kupambana.. Ningali kijana.
~ Nichekwe na kusemwa mapema ningali na moyo wa kutosononeka nikichekwa.. ningali kijana.
~ Niutest uwezo wangu wa kufikiri na kuijaribu akili yangu pasipo vyeti vya shule wala CV
~ Niwaandikie watoto na wajukuu Mungu atakaoikirimia familia yangu historia ya wao kuiga na kujifunza mapema. Ningali kijana.
~ Nijifunze namna ya kuandaa watu wa kwenda nao kwenye kutimiza ndoto na maono yangu na watu wa kuyaendeleza nitakayoanzisha..ningali kijana.
~ Nijifunze wapi pa kupata msaada nitakapokuwa peke yangu bila mtu yeyote wa kunisaidia bila godfather, bila mjomba, bila pesa benki, bila mali, bila cheo, bila kutumia jina kubwa la kampuni, bila cheti chochote.

NILICHOJIFUNZA SO FAR..
Pamoja na kwamba ndo kwanza safari yangu imeanza lakini ninamshukuru Mungu kwa maamuzi niliyoyafanya. Ni karibu miaka mitano sasa na nimejifunza mambo mengi na ya msingi sana sana katika kipindi hicho kifupi. Najua safari ya kutimiza ndoto zangu ndo imeanza. Yaani nikiangalia ndoto zangu na nilipo sasa hivi ndo kwanza "majogoo". Ndo nafungasha mabegi kuanza safari. Ila sasa ramani ninayo. Siyo kama nilipoanza miaka minne iliyopita. Namshukuru Mungu kuna mambo muhimu ya msingi kuhusu hiyo safari nimeshayapata. Nimefanya makosa mengi sana, sana, na siwezi kusema sasa nimeshamaliza kufanya makosa. La hasha. Makosa mpaka kina Jack Ma, Richard Branson, waliobobea kwenye ujasiriamali bado wanafanya makosa mpaka leo. Ila ninamaanisha tu makosa ya mtu anayeanza biashara mengi nimeshajifunza. Lengo langu ni kukutia moyo kuanza kufuata ndoto zako mapema. Maana kuna kukosea kwingi na inahitaji muda wa kuweza kujifunza kutokana na makosa.. Kuna kupotea kwingi pia na kurudi tena pale ulipopotelea kuanza moja. Kama ukipotea ukiwa na miaka 60 unaweza kusema dah basi tena. Lakini ukipotea  ukiwa na miaka 25 je, si ni rahisi kurejea na kuanza moja tena maana umri na nguvu vinaruhusu. Ukiwa na miaka 60 ukigombea Ubunge unataka upate tu iwe isiwe maana miaka imeenda. Ukiwa na miaka 24 je? Kupata au kukosa inakuwa kama siyo ishu kivile. Ndo nachomaanisha hapa.

Watu wengi huwa na ndoto kubwa. Kuliko za kwangu. Kama yule mtu kwenye kaburi. (Usisahau)
Lakini hawana uthubutu wa kuzifuata ndoto hizo MAPEMA kwa gharama iwapasayo. Kwa hiyo wanabaki na frame nzuri ya vioo ukutani ambayo haina picha yoyote ndani yake. Hawajui thamani ya fremu ni picha iliyopo ndani yake.
Watu wengi wanakaa na kufurahia kichwani ndoto zao na kuona namna zitakavyokuwa nzuri SIKU ZIKITIMIA. Halafu wanafuta vumbi kwenye fremu tupu ya vioo. Ili iwe safi. Bila kujua nguvu za kutimiza maono ni nyingi zinahitajika. Na muda huenda ukawa mchache sana. Wana fremu na picha imebaki kichwani. Hawataki kujifunza kuchora picha zao wenyewe.  Wanatumia muda wao mwingi na nguvu zao nyingi kuchora picha za watu wengine. Wao wako na fremu tupu. Na picha zao zingechorwa ni nzuri mno kuliko za huyo wanayemchorea. Wanafurahia asante kutoka kwa mwenye picha inayochorwa. Wanadhani ndiyo mwisho.
Muda unakwenda nguvu zinapungua.

Halafu wanastuka muda ukiwa umeenda. Moyo wa kurisk ukiwa umeanza kupotea. Hamu ya kuchora picha zao ikiwa imeshaanza kupotea, nguvu za kukimbizana na makopo ya rangi zikiwa zimeanza kupungua au hata kwisha. Nadhani unanielewa. Utayari wa kujichafua kwa rangi na kuchekwa ukiwa umeshapotea. Reality inawakumbusha kuwa inabidi wachore picha zao mwenyewe (kutimiza ndoto/maono) kama kumbukumbu kuwa waliwahi kuwepo duniani pia. Wanakuta moyo wa kuchora haupo tena. Fremu pia zilishapata kutu. Hazina mvuto tena. Halafu picha waliyokuwa nayo kichwani wakiwa vijana wanahisi huenda waliona vibaya. Labda ulikuwa ujana. Kuota ndoto kubwa kubwa. Mbona wengine wamezeeka bila kuchora. Labda ni sawa tu kutochora. Akiwaza waliochora picha zao wenyewe anajisemea hao wana bahati sana. Anakufa na ndoto kichwani. Kama yule mtu kwenye lile kaburi.

Angalia sana jambo hili. Huenda pia una ndoto kubwa kuliko za kwangu. Angalia Mungu asije kukutolea mfano kwa wenye ndoto wengine. Kuwa ulikuwa na ndoto kubwa weeee kichwani mpaka muda wako ukaisha.

Huenda huu ni ujumbe muhimu kwako. Kama ndivyo fanyia kazi. Watu wengi huua ndoto zao wakiwa na miaka 20 hadi 30. Baada ya hapo wanaishi ndoto za wengine.
Usiwe miongoni mwao Mungu hawezi kukutolea mfano halafu asikudai. HAKIKA atakudai.
"Ulifanya nini na ndoto niliyokupa kichwani mwako?"
"Ulifanya nini na maono niliyokuwekea moyoni mwako?"
Mungu atakuuliza.
Sasa sijui utamwambia "Ulinipa (ndoto/uwezo/kipaji) kidogo nikaamua kukitunza ili nisije nikakiharibu angalau nikirudishe kwako kikiwa intact" Unajua atakujibuje? Kasome Mathayo 25:28-30 kuna mfano unaohusu hili jambo squarely.
Au utamwambia Mungu nirudishe tena tafadhali nimejifunza. Wazungu wanasema WHEN THE CURTAIN IS DOWN THE SHOW IS OVER hata kama uliipenda vipi show ikiisha imeisha. Pazia likishushwa show imeisha.
Kama yule mtu kwenye kaburi.

Kumbuka tu tena nguvu na muda wako vikiisha utafanya nini na ndoto zako kubwa kichwani? Kama nilivyouliza kwenye title ya ujumbe huu: NGUVU NA MUDA VIKIISHA MWENYE NDOTO ATAFANYA NINI?
Do something before it's curtain time for you!

Yes better do something now. And good luck. Walimu wa kukufundisha wapo wengi tu.
Wewe tu.

Na kama unatamani kujifunza chochote kwangu binafsi nitafute tu kwa WatsApp #o752366511.

When my curtain is down I want to be done with my race.
What about YOU?


Semper Fi,

ANDREA G. MUHOZYA
DAR ES SALAAM, TANZANIA,
EAST AFRICA.

WITO KWA NDUGU ZANGU WA MIKOANI

.
🚴 WITO KWA NDUGU ZANGU WA MIKOANI 📚📖

Ni siku #nyingine tena. Na leo niongee kitu kingine tena. Huenda umeshasoma message zangu nyingi hasa LIFE BEGINS AT 40  (uhalisia wa maisha huanza ukifika umri wa miaka 40) ya kwanza na ya pili ambazo zimesomwa na watu weengi zaidi toka nianze kuandika. Usisome tu ukaishia kuwaforwadia wengine  halafu ukaachia hapo. Fanyia kazi.

Okay.. Nimekuwa nikisafiri nchi hii huku na kule kwa shughuli binafsi na pia biashara. Okay safari za ndani ya nchi zinakufanya ujue nchi yetu hii ikoje kama vile safari za nje zinavyofanya ujue nchi zingine maisha yakoje.

Safari nyingi huwa nasafiri kwa njia ya mabasi. Nimekuwa nikijifunza mengi sana kutoka kwa watanzania wasafiri wenzangu. Na mojawapo ya vitu nilivyojifunza ni kuwa UKITAKA KUJUA MTU ANAWAZA NINI ANGALIA VITU ANAVYONUNUA.

Ukiwa stendi ya Ubungo kuna wachuuzi  wa vitu mbalimbali mle ndani wanapita yalipopaki mabasi madirishani na wengine huingia ndani ya mabasi. Wengi wanauza maji, mikate, juisi, matunda, magazeti, vitabu, leso, simu, flash, power bank, miwani, nk. Sasa ukiwa pale unaweza kuona mtu ananunua kila kitu kwenda nacho huko mkoani lakini siyo KITABU.

Sasa huwa najiuliza. Hivi nyie ndugu zetu kutoka huko kwetu mikoani mkija Dar huwa mnaona tu nguo na juisi na mikate vitabu hamuoniiiiii au????? Mtasema labda vya kidhungu.. Mbona vya kiswahili vipo viiingi tu..!!
Mbinu za Kupata Kazi
Mbinu za Kufanikiwa katika Maisha
Mbinu za Kufanikiwa Katika Biashara.
Mbinu za Kuanzisha Biashara.
Siri za Kutoka Umaskini Hadi Mafanikio
Mbinu za Kupata Mtaji
Mbinu za Kupata Masoko..
Nk nk

Hivi hamjaona tu..? Yaani kila siku mnanunua tu magazeti kuona nini kipya leo toka enzi na enziiii na enzi.. Vichwa vya habari vya magazeti havitabadili maisha yako. Ulishasoma habari ngapi:

MKAPA ANG'AKA..
KIGOGO TANESCO AFUMANIWA..
MWINYI APIGWA KIBAO..
ULIMBOKA SIRI NZITO..
DR BILALI AIBUKA..
JK NJE TENA..
BUNGENI HAPATOSHI..
TAIFA STARS HOI..
KIKWETE ABADILI MAWAZIRI..
MADAKTARI WASALIMU AMRI..
PINDA AMWAGA MACHOZI BUNGENI..
MANGU IGP MPYA..
GWAJIMA HALI MBAYA..
LOWASSA TISHIO CCM..
SELELI AHAMIA CHADEMA..
nk nk!

Nunueni vitabu aisee. Mna uwezo wa kuibadili nchi hii na kubadilisha taswira ya maisha huko bila kuhitaji watoto waje wajenge huko. Mtajenga wenyewe na hawa wanaokatalia mjini mtaona wanakuja  tu. Vitabu vina maarifa mengi sana na huenda ukawa hujajua hilo bado.
~ Vitabu ni vitamu kuliko juisi ya Azam.
~ Vitabu vinakata kiu kuliko maji ya Uhai
~ Vitabu vinatoa habari muhimu sana kuliko ITV
~ Vitabu vinaleta matokeo mazuri sana kuliko Simba 5 Yanga 0
~ Vitabu vinajenga msingi imara zaidi kuliko Twiga Cement
~ Vitabu vitakufikisha mbali zaidi ya basi la Shabiby

Sijui niseme nini zaidi ili twende sawa?
Utajiri mkubwa uko huko mikoani lakini sababu ya kukosa maarifa utajiri huo utafaidiwa na watu wa Kinondoni na siyo Simiyu au Njombe. Someni vitabu. Vitabu vitawafanya mpate maarifa ya kumiliki uchumi na utajiri ambao Mungu aliuweka kwenye mipaka yenu. Sasa nyie mpo mpo tu halafu mmekaa na ardhi ipo tu mnalishia ng'ombe miaka nenda rudi mpaka inamomonyoka mnahamia ardhi nyingine ugomvi kila siku na wakulima.  Ufugaji wa kisasa upo hamjui kwa sababu upo kwenye vitabu. Mna uwezo wa kumilikishwa ardhi mkaitumia kufanikiwa ila maarifa hayo hayapatikani kwenye front page ya Nipashe. Someni vitabu. Mtaishia kuchoma moto mashamba ya wawekezaji au kuvamia migodi na bado maisha yenu hayatabadilika. Mtaishia kuchagua viongozi wakawawakilishe bungeni halafu nyie mkae mnywe viroba na kusikiliza bunge redioni na kusubiri maisha bora. Ndo maana na wao wamelifanya bunge kama sehemu ya kubadilishia maisha yao. Mtabadili wabunge, mtabadili vyama, mtabadili mpaka nguo badala ya kuvaa kijani mvae nyekundu na blue lakini nasema hivi kama hamna maarifa nyinyi wenyewe mtakaa kweli kweli.

Sikia, kipato chako hakiongezwi na mwajiri wako au serikali. Ni wewe mwenyewe. Lakini kama unachonunua wewe ni vocha, juisi na magazeti aisee daah utakaa sana. Mwanamama mmoja maarufu wa Ujerumani Helen Keller ambaye alizaliwa kipofu aliwahi kusema: KITU KIBAYA ZAIDI YA KUZALIWA KIPOFU NI KUZALIWA NA MACHO YANAYOONA HALAFU UKAKOSA UWEZO WA KUONA MBELENI (SIGHT without VISION). Sasa uwezo wa kuona mbeleni unakuja kwa maarifa.
Hata Biblia inasema WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA. Unaona mambo hayo? Ukombozi wako uko mikononi mwako mwenyewe. Ukombozi wa familia yako si kazi ya bosi wako.
Mafanikio ya kizazi chako si kazi ya Serikali. Kama hutaki kukubali endelea kumsubiri Magufuli aje akufanye wewe uanze kutumia jiko la umeme au gesi badala ya mkaa. Utashangaa nyumba yako iko karibu na bomba la gesi lakini unapikia kuni. Halafu unalaumu serikali. Soma vitabu upate maarifa. Utashangaa namna utakavyopata MTAZAMO tofauti sana kuhusu maisha. Kila kitu chako kitabadilika. Hutolaumu mtu wala serikali.
Sasa nyie kujisomea bado..haya basi hata kuwasikiliza watu waliojisomea hamtaki. Au uongo? Nyie mnataka kusikikiza politiki tu. Akija #Slaa, au #Magufuli au #Zito Kabwe haooo mnajaa. Akija #EricShigongo au James Mwang'amba hata hamwendi. Sijui hata kama mnawajua.

Halafu na nyinyi wasomi mlioko mikoani hivi mmeenda kugonga mihuri tu na kusaini mafaili jamani. Hebu watu waone mkiiathiri jamii kwa kuambukiza watu hamu ya kutafuta maarifa. Sasa wewe mwalimu wa Sekondari au afisa wa serikali au meneja wa benki mtu akija kwako kumejaa CD za bongo movie na magazeti ya Udaku. Umenunua bodaboda kuna kijana anaendesha anakuletea posho jioni unaona maisha yameishia hapo. Hebu waonyesheni mfano watanzania huko mliko. Someni vitabu. Na wataanza kuiga mfano na wengi mtajikuta mnapata maarifa sahihi. Huko huko Simiyu, Namanga, Mtera, Kasulu, Dumila, Shirati, Bihalamuro, nk mtafanikiwa kweli na kuwafanya watu wakutafute wewe kujifunza mafanikio. Haijalishi elimu yako. Amua tu kuanza kusoma vitabu. Sasa nyie stendi za huko kwenu mnauza vitunguu tu na nyanya na vikapu na mahindi ya kuchemsha hakuna mwenye wazo la kuuza vitabu? Haya Sasa hata mkija huku mnataka bado mnunue mahindi na juisi na karanga halafu basi. Hebu badilisheni hilo mtaona mabadiliko makubwa sana. Kumbuka tu wapo watakaokucheka lakini ipo siku watakuita uwafundishe kuhusu mafanikio!
Tena utaitwa mpaka huko mjini. Mnaweza kufanikiwa huko huko mkajenga hoteli zenye hadhi kubwa na utalii ukafika huko mkaingiza kipato zaidi. Huko huko mkajenga Shule zenye hadhi.. Huko huko maendeleo yakawafata. Makampuni yatawafata. Watalii watawafata. Siyo kila siku watalii wanaishia Arusha tu Ruaha na sehemu kama hizo. Maarifa ni muhimu sana. Soma vitabu. Anza leo. Hakika mtakubali haya maneno siku moja.

Kama unataka kujua zaidi kuhusu vitabu vya kukusaidia, ama kuhusu wazo la biashara, ama mambo ya elimu ya mafanikio kwa ujumla WatsApp #o752366511.

Semper Fi

Andrea G Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.

Nimerejea...

Kwa muda mrefu nimekuwa kimya kidogo lakini sasa nimerejea.

Mungu awabariki.

Andrea Garsper Muhozya

Alhamisi, 7 Novemba 2013

What Is Network Marketing?

What Is Network Marketing?


The simplest explanation of network marketing is that it is a method of marketing that utilizes independent representatives to reach potential customers that a company otherwise would not reach with traditional online or offline marketing methods.

Still difficult somehow, okay...

In short Network Marketing is a business model which is the opposite of traditional (normal way) of business/distribution. In the traditional model, for the consumer to get a product, it has to move from the MANUFACTURER down to the NATIONAL AGENT down to the WHOLESALER then to the RETAILER and finally to the CONSUMER. In so doing the price will have escalated from say, 300/= shs for a bottle of soda at the MANUFACTURER'S to 600 by the time it reaches the RETAILER due to costs incurred by each of the players.

In Network Marketing the MANUFACTURER finds a partner eg. ME, and asks the PARTNER to distribute the products which this PARTNER gets from the MANUFACTURER at 300/= for example and sells at 600/= so the PARTNER gets all that profit which would have gone to the AGENT, WHOLESALER and RETAILER. See? But it doesn't end there.

The MANUFACTURER then asks this PARTNER to bring in any other person who would like to become a partner too and when this new person comes in and joins, then  the 1st PARTNER is paid a "commission" and if the second partner brings other partners the both the 1st and 2nd partners both get paid due to the compound effect of the new partners who due to the power of the word of mouth have helped the company/manufacturer to make more sales than if it had relied on adverts or the traditional way of business. And this is where the "network" applies.

So briefly it's something like that.. Watch this video.

HOW MANY PEOPLE ARE DOING NETWORK MARKETING TODAY?
Millions of people are doing this, highly probably YOU also are. Let's see if you are doing it or not. Okay, do you have a PC, mobile phone, or car? If yes, did anyone tell you about the particular brand before you decided to go for it or did you just buy everything you have out of the blue without anyone's reference?

Or where do you go to eat your food, where do you buy your groceries, which supermarket do you visit often, what brand is your kind when it comes to bottled water for instance, and did you just start using the brand or did someone else tell you about it. Did someone else tell you where to buy your groceries, or where to go wash your car or which school to take your kids to? And what do you think, did that person get paid by the business owner for recommendung those things to you? Of course not!! Did you get paid anyone when you recommended certain brands to your friends or relatives? Yes? No? Yes? NOOOO!

See? So many people are involved in the Network Marketing Business everyday for free and they are happy to do so! Imagine if a friend comes to you and they want to go buy a new cellphone, which brand would you recommend? And suppose that friend of yours follows your advice and buys that brand how much will you get paid for that? Nothing. Why? Because you are doing network marketing (or recommendation) business with the wrong company.

BUT THERE ARE now Companies which are ready to pay you for doing exactly that! Recommending their products to other people. That is what is in the book titled: The Business of the 21st Century by Robert Kiyosaki! One such company is called FOREVER LIVING PRODUCTS... Refer the short presentation on the video.

INFORMATION IS POWER! It is important that you are informed so that the choices you make about your present or future financial status are not made out of ignorance. Network Marketing is a great OPPORTUNITY.

There are several business meetings and presentations taking place where you are everyday! Probably you are not aware, and probably it's because you were never informed.
NOW THAT YOU ARE... Take the next step...Seek for more information.
Thank you for reading through..
Andrea Muhozya.

Call or Watsapp via +255-752-366511 for more info.
Or let's hook up in the comment section below.

Cheers!






Jumanne, 21 Mei 2013

Lead A Life Of No Regrets

Don't Have Any Regrets in Life

By Mike Michalowicz
 
I have regrets.
It seems like yesterday that I was in college (Go Hokies!). I remember high school so vividly that I still think (and act) like I am in it. It feels that moments ago, I was swinging from the jungle gym and enjoying nap time during my kindergarten class. But that stuff is far gone now.
Looking back, I have clearly made mistakes. That doesn’t bother me so much. I have learned from most of them. What does bother me is the missed opportunities. What bothers me are the times I ran toward comfort instead of trying something new. What bothers me are not the risks that I took, but the risks that I avoided.
My past is as dead. So is yours. Don’t waste your time worrying. The only thing you can, and should, do is change your behaviors now. Push away from the comforts of repeating your past, because until you do, you too will regret what you missed.

The No Regrets Formula

Here is my little formula for living without regret (or at least with a whole lot less regrets):
If you heart says “Yes!” and your head says “No!”, go for it! – This is the clearest sign you will get from your soul, trying to guide you. Your head is just going into the protection mode of keeping you in the “tried and true” past. Lead with your heart, and be clear about the fear of danger and the fear of inexperience!
If it won’t go away, go for it! – Sometimes life will present the same opportunity over and over. That can be a clear signal you should be giving it a shot.
Follow your heart, not your urge! – I love jelly beans. When they are put in front of me, I go through a whole bag in seconds. Then I get sick as a dog. I followed my urge to devour the jelly beans, and not my heart that was telling me to enjoy just a few. When temptation presents itself, make sure you are listening to your heart and not an urge.
Fear the pressure of peer pressure – Just because everyone else is doing it, doesn’t mean it is right for you. You gut knows what’s right, go with that.
If you regretted it once, don’t regret it again – If you have regrets, it is a clear signal not to make that mistake again. If you are lucky enough for the opportunity to present itself again… Go for it! Go for it! Go for it!

You Can Say You Lived

Do you have any regrets? Do you regret something in your entrepreneurial life? Personal life? It’s time to start living without regrets. It is time to push the limit today, so when you reflect back tomorrow, you can say you lived.
###
Twenty years from now you will be more disappointed by the things that you didn’t do than by the ones you did do. So throw off the bowlines. Sail away from the safe harbor. Catch the trade winds in your sails. Explore. Dream. Discover.
- Mark Twain

Jumamosi, 4 Mei 2013

Success is Simple...Don't Complicate it... lol..!


    

If You Want to Succeed Don’t Complicate Things – Just Succeed..!
 
The first step in attaining the success you desire is to be prepared to know yourself better. A serious appraisal of your life is essential to truly living the life you desire.
If you need to get to Pittsburgh by Friday, you’ve got to know
where you’re starting from. A serious self-appraisal may take some time to complete.
How well educated are you in the things you would like to know,
do or have? How much effort do you put into each aspect of your life? What are your best and worst points? How do you choose your friends? Your home? Your hobbies?
How do you treat your friends? Your family? Strangers? How deep is your personal spirituality? Are you one of those who “go to church”? Those who think a church is a place?
You have hundreds and hundreds of special traits, but how well
developed are each of them? Which of your traits are the worst?
What have you accomplished over the past twenty years? Ten years? Five years? Two years? One year? In the past month? The past week? Today?
Who have you hurt? Who deserves better than you’ve given them?
And most important, how close are you now to where you hoped
you’d be when you looked ahead a year ago, five years ago,
or even as a child?
Be prepared to cry a little as you make this appraisal of your
life. Humans are far from perfect, and even the minor goals we
set for ourselves are not achieved, and it can hurt to see
exactly where you are.
Draw upon every bit of serenity and peace you have when making
this appraisal and always keep in mind you are on a fact-finding,
not a fault-finding mission.
Whether your strengths match evenly with your weaknesses on paper is not important. What you want is a written record of who and what you are in as great a depth as possible, a blueprint of your house which you can use as a base for improvement.
Great people in every field start with such a deep analysis and
revise it yearly to chart their progress, and the time and
emotion spent in such an appraisal will be chicken feed compared
to the value you will receive from it.
Next, write out a report based on your self-appraisal and
include in the report everything you ever did which you didn’t
think you could do.
THIS STEP IS ABSOLUTELY VITAL!
It will provide you with enormous inspiration when faced with a
problem you don’t think you can overcome. These are not only real-
life success stories, they are YOUR success stories, positive
proof that there’s more in you than you might think.
These experiences are the fuel you’ll use to power the bulldozers
which will move mountains in the future. Remember, even an almost-
dead battery will start a car. Have this report in writing and
keep it with your personal analysis, and make a copy in case you
lose it. This will be a vital document in times to come.
Next, decide where you want to go. Most people fail because they
don’t set goals worthy of themselves. If they do, they do not live
each day in pursuit these goals. This, along with every other step
outlined here, is absolutely vital to a truly successful life.
When you set your goals, make them better than you’ve done before,
but make them achievable. In other words, if it is at all possible
that you or someone like you could achieve the goal, it is worthy.
But don’t set them too low either, or you’ll be breezing through
life bored and unchallenged. Set goals for each day, for the next
week, month, year, two years, five years, twenty years, fifty
years (regardless of your age).
Be definite about what you want. Write your goals down and use as
much detail as possible. Make them firm… for the moment. You will
find as you achieve certain things that some goals must change, and
that’s fine. Just don’t go around changing your mind every time the
wind changes or you won’t know which way is up.
Set as many goals as you like, and include among them – what you’d
like to be doing, where you’d like to go, what you want for your
family, what kind of person you’d like to be, how much you’d like
to be earning, your net worth, your health, personality, education
and spiritual growth.
Keep your daily goals confined to activities which will lead to
accomplishment of your long-term goals. Don’t be afraid to set
goals. Don’t be afraid to make mistakes because mistakes can be
corrected. Doing nothing cannot be corrected.
The next step takes no real effort, and strangely enough, it is
the most difficult step for the average person to take and that
is to
COMMIT!
Make the decision to achieve those goals, to
strive for the things you want which will make your life and
yourself all that much better. Make that commitment from the
heart, not at the lips!
It will take time to really feel that commitment, and regularly reviewing the goals you’ve written down will make it possible to truly feel that commitment. You’ll go through agonies at first and wonder if any of this is really worth it, and that’s the point most people give up.
Remember this and you’ll look forward to that agony. Every change comes with pain. It hurts to be born, to fall in love, to pass an exam, run a marathon.
Once you start feeling that pain, know it for what it is – your old self screaming for life. Let your old self win and you lose!
Once you pass through that barrier of pain between what you are and what you want, you will know what it is worth every bit of discomfort.
You’ve been through it before, and you’ll need the memory of past incidents where you’ve made it to help you get through it.
You’ll need the support of others too so you’ll have to consider the people with whom you spend most of your time.
If they are not as interested in improving themselves as you are, it’s time to expand your circle of friends to include those people and make them the best you could want. Make your friends inspirations and examples to you in your quest for a better life.
The final step is so simple and so tough it literally separates success from failure. You must be willing to sacrifice immediate pleasure for real satisfaction down the road. If you’re not ready to make the trade, you must settle for the life you have today.If you are ready to make the trade, spend every moment of your life in the most effective, efficient way possible in the pursuit of your goals.
You’ll never be able to do this as well as you will want to, but
that’s fine. Nobody spends all their time as effectively as humanly
possible.
The degree to which you can tune your desire to the things you
want and discipline yourself to do the things that lead to getting
them – will determine how successful you will be.
Regardless of how weak you are now, you can and will increase
the value your time and activities and garner more happiness
than you might think fair only if you’ll keep your failures in
perspective.
Think of them as lessons and gain something from them. Use your
successes as a well of strength on which you can draw when you’re
ready to quit.
These simple steps are the true secret to getting what you want
out of life.
It has been proven time and time again by great men and women
down trough history and will continue to do so centuries from
now. The words may change, but the ideas will be the same.
For centuries people have tried to find ways of making this
simple set of guidelines more complicated and more difficult
to understand and follow.
Many who do so have attained “success.”
Or have they?
What they really attained was less than they set out to achieve.
All because they made it harder than it actually was.
Getting what you truly want is so difficult precisely because
it is so simple.
Humans are very complex beings and thrive on making things even
more complicated.
As Jim Rohn said, “Don’t take that class.”
Keep it simple.
Follow the guidelines shared here and you will truly live the
life of your dreams.
See?? Success is AS SIMPLE AS THAT. Don’t complicate it by sitting down goalless, visionless and powerless.  
Thank you for giving me this opportunity to serve you.

****[This article, or rather, most of the ideas herein, belong to Ron – an  example. A model. I have just shared. Hope it helps you!!]
Thank you for reading,. Remember to leave your comment!
Andrea