Alhamisi, 27 Oktoba 2016

IT TAKES "A LITTLE EXTRA" TO MAKE A DREAM COME TRUE


Katika zawadi kadhaa nilizowahi kupata maishani mwangu ambazo zilibadilisha maisha yangu moja wapo ni kadi ya kunitakia mafanikio mema katika mitihani yangu ya kumaliza kidato cha sita.

Kadi hiyo niliipata kutoka kwa walezi wangu Mr & Mrs Senga Kabipi aka baba na mama Laurent Kabipi. Nikiwa nimepitia mabonde na milima hadi kufikia kipindi cha mimi pia kuikabili NECTA ya Form VI, kadi hiyo ilikuja  katika kipindi muafaka sana ambacho nilikuwa nikihitaji binadamu yeyote wa kunitia moyo na kuniambia nitafanikiwa. Ninakumbuka daima nilivyotiwa nguvu na kitendo tu cha kupewa ile kadi. It was so powerful!

Hata hivyo ni maneno yaliyoandikwa kwenye hiyo kadi ambayo yalinifanya niikumbuke zaidi ile kadi hadi leo. Yalisema hivi:

Dear Andrea,

It takes A LITTLE EXTRA..

A LITTLE EXTRA COURAGE

A LITTLE EXTRA HOPE

A LITTLE EXTRA BELIEF

A LITTLE EXTRA PUSH

A LITTLE EXTRA STEP

It takes A LITTLE EXTRA EFFORT...

....TO MAKE A DREAM COME TRUE.

Wishing you all the best in your exams,

Yours,

Mr & Mrs Kabipi.

That was it. So baada ya kufurahi nikaanza kujiuliza kuhusu ujumbe huo. Nikawaza kweli eti. Huu ujumbe mbona unanipa mawazo tena. Bado siku mbili kufanya NECTA. Nimeshasongoka miaka miwili mizima nimejiandaa nimeshajiamini kuingia kwenye NYAMBIZI la Makongo High School. Afu naambiwa #EXTRA tena? Lakini moyoni nikasema Mungu huenda ameniletea ujumbe muhimu mno kunisaidia si tu kwa mitihani yangu bali hata maishani. Nikaazimia kufanya hiyo extra. Walimu walisema usisome hadi siku ya pepa mi nikasema nitafanya EXTRA. Sitaenda kwenye mtihani wowote bila kufanya EXTRA. Nilifanikiwa kufanya vema mitihani yangu na nilishukuru kwa zile EXTRA nilizofanya kipindi chote cha wakati wa NECTA.

Ni miaka mingi imepita now na nimekuja kugundua kumbe ndoto nyingi hufia mlangoni. Maono mengi hufia karibu na kuzaliwa. Mafanikio ya watu wengi hushindwa kuwafikia kwa sababu tu ya kutofanya kitu EXTRA. Just some little extra stuff. Angalia watu wote waliofanikiwa duniani katika kila eneo. Iwe ni siasa, michezo, dini, biashara nk. Wote kuna kitu kidogo tu EXTRA wanafanya. Kuna wakati nilisikia kuwa Cristiano Ronaldo alikuwa wakimaliza mazoezi kocha akiwaruhusu kuondoka yeye anabaki anaanza kufanya mazoezi kidogo EXTRA. Huenda ikawa penalties au free kicks etc. Kidogo tu. Afu ndo anaondoka. A little EXTRA. Sets him apart.

Angalia wanamuziki waliofanikiwa. Siyo kipaji tu. Vipaji viko lukuki. Lakini nani yuko tayari kufanya that little EXTRA. Akae studio kwa muda extra kidogo. Akienda gym kwa ajili ya mazoezi ya pumzi basi azidishe muda kidogo tu EXTRA. Akifanya mazoezi ya vocals afanye kwa muda kidogo tu EXTRA. Nitajie ni nani na utakuta ni ambaye tayari ni jina kubwa kabisa!

Angalia watu wengi wanaopanda vyeo makazini kihalali. Wamefanya kitu kidogo EXTRA. Huwezi kufanya EXTRA halafu Mungu akakuacha. Never. Uwe mpagani uwe mnini kanuni za mafanikio si za dini ni tabia inayobidi kujengwa.

Angalia wafanya biashara waliofanikiwa lazima utakuta kuna hicho kitu EXTRA katika maisha yao. Anaamka mapema kidogo au kulala late kidogo. Siyo late akiwa anatuma katuni katuni WhatsApp no. Labda anasoma kitu fulani EXTRA. Au anasaidia wengine a little EXTRA. Kuna kitu EXTRA Dewji amefanya, siyo suala la kurithi. Wamerithi wangapi?

Angalia watu wanaokuwa wahubiri wa kimataifa. Utakuta kuna kitu anafanya EXTRA. One more EXTRA foreign language. Maombi kidogo EXTRA. Kufunga kidogo EXTRA. Kusoma NENO kidogo EXTRA. Nk. Hata Mtume Paulo ana nyaraka nyingi kuliko mitume wengine kwa sababu ya hiyo EXTRA.

So swali la kujiuliza kwa wewe unayetaka kufanikiwa maishani ni hili: NI KITU GANI EXTRA UNAFANYA AMBACHO WENGINE HAWAFANYI? Kama huna any little EXTRA basi utakuwa wa kawaida. Just ordinary. Just any Thom, Dick and Harry. Afu kila siku unajiambia  "MUNGU ALINIUMBA KUWA EXTRAORDINARY" Ni kweli kabisa. Lakini Mentor wangu mmoja alisema  tofauti kati ya ORDINARY na EXTRAORDINARY ni hiyo EXTRA tu. Ukiondoa EXTRA katika EXTRAORDINARY unabaki na ORDINARY. Sasa kama unakiri uliumbwa kuwa EXTRAORDINARY halafu huna kitu EXTRA unachofanya daily basi mtajuana na muumba wako ambaye bado amekupa uhai hadi sasa.

Azimia leo kufanya hizo EXTRA ndogo ndogo. You will definitely become EXTRAORDINARY.

Don't forget,

IT TAKES "A LITTLE EXTRA" TO MAKE A DREAM COME TRUE.

Barikiwa sana.

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
#o752366511
Tanzania,
East Africa.

Jumatano, 26 Oktoba 2016

USIENDELEZE TATIZO KUWA SEHEMU YA SULUHISHO.

Habari za wakati huu..

Watu #wengi mno wamekulia katika maisha duni ya #kimaskini.  Wamezaliwa familia duni, kusomeshwa kwa tabu au kushindwa kwenda shule au kuishia "njiani". Kukosa mavazi, kukosa malazi, kukosa chakula, kifupi kukosa basic needs. Bill Gates anasema kama wewe pia umezaliwa katika familia maskini hilo siyo kosa lako. Ila ukifa maskini hilo ni kosa lako. Unasikia maneno hayo? So shida siyo utokako rafiki. Shida ni uendako. Where are you going?

Shida ni maamuzi yako hapo ulipo. Je, umechukua uamuzi wa kuendeleza mlolongo wa umaskini ama umedhamiria kukata huo mzizi wa umaskini na uanzishe mkondo wa mafanikio kuanzia kwako kwenda kwenye uzao wako ujao mbele yako? That's the issue.

Tatizo haliko kwa wazazi wako diwani wako au mbunge wako au Naibu Spika au Meya wa Manispaa tatizo lipo kwenye fikra zako na maamuzi yako.  Umeamua nini? Kulalamika au kuchukua hatua. Kusoma message kama hizi za kukupa tumaini jipya na mawazo mbadala au kushabikia comments za watu wanaotukanana na kudhalilishana kila siku mitandaoni? Yote hayo ni maamuzi.

Umeamua kujiendeleza kwa kujisomea vitabu vya namna ya kufanikiwa kama kina #Shigongo walivyofanya au umeamua kusoma link za blog za umbea na vitu vinavyoua uwezo wako wa kuwaza vema? Umeamua kusikiliza clip za kina Jim Rohn au Darren Hardy huko YouTube au wewe ni nyimbo za Justin Bieber au za Ali Kiba na Diamond? Yote ni maamuzi.

Umeamua kuandika malengo yako ya mwaka huu na ya miaka mitano ijayo kwenye notebook yako ili uwe na ramani binafsi ya maisha yako au wewe unajiendea tu kulingana na matukio ya kila siku kwenye mitandao. Yaani ukiamka tu hata huna malengo unaanzia Facebook kuona kuna habari gani mpya, kisha uende WhatsApp kujua kuna video gani imetumwa ya kuchekesha. Bila kujua kidogo kidogo umri unaenda kidogo kidogo unaendelea kuulea na kuukomaza umaskini ulioukuta katika familia.

Magroup ya WhatsApp yamegeuka kuwa source ya taarifa kichwani mwako badala ya kupata taarifa kwenye vitabu vya kukusaidia kujikwamua katika maisha na hata kuikwamua familia yako au badala ya kuangalia videos za watu wanaokuonyesha njia ya kupitia wewe unataka video za watu wanaokata viuno tu au clip za bungeni basi. Halafu ukimaliza kupoteza muda wa masaa sita mtandaoni kesho unalaumu serikali kwa kutokukukwamua kiuchumi. Are you serious?? Muda unaoutumia kusoma vitu visivyokuwa na tija na kufatilia mijadala mireefu iliyokupeleka mbele kimafanikio muda huo ungeutumia kujifunza vitu muhimu ungeweza kupiga hatua haraka na kuwa msaada kwa wenzako wengi ambao hawana mwelekeo bado. Lakini kwa kuwa umeshailevya akili yako na vitu visivyokupeleka popote nayo inakukumbusha kila siku kuendelea kuilisha vitu hivyo hivyo.

Uko addicted na vitu vya kuchekesha chekesha tu eti unajifariji kuwa unacheka uongeze siku. Nani alikudanganya siku zinaongezwa kwa kucheka? Unazidi kujaza kichwa chako vitu ambavyo siyo serious wakati tatizo ulilonalo la kuuondoa umaskini ni tatizo serious.  Yaani adui yuko serious kajipanga kukumaliza afu  wewe unamwendea kwa kuchekacheka. Muda unayoyoma na wewe unazidi kuendeleza gurudumu la umaskini ulioukuta nyumbani kwenu.. Kutunza muda wako kwa WIVU ndiyo uamuzi wa kwanza mkubwa unaopaswa kuuchukua ili upige hatua kuelekea mafanikio.

Watu wengi ni #wabobezi wa kupoteza muda.  ðŸ•£ðŸ•£Mungu aliumba 24hours tu kwa kila mtu. Jinsi unavyopoteza muda wako ndivyo unavyopoteza fursa muhimu mno.  Mfano. Kuna wakati utafika hutakuwa na nguvu ulizonazo leo za kufanya kazi nk. Utajutia sana muda wako wa sasa. Usiambatane na mtu anayepoteza muda wake kwani kama wake anaupoteza hataona shida kupoteza wa kwako. Muda unaenda sana rafiki.

Hushangai mtu anafikia kupata mtoto halafu hana pampers.🚼🚼 Yaani utadhani mtoto kashtukiza kuja. Ama utadhani wamekuja wote mzazi na mtoto duniani siku moja. Huoni ajabu? Hiyo ni kwa sababu hakujua kuwa pampers zilitakiwa kuandaliwa zamani.  Wakati alipokuwa anaupoteza muda. Linda muda wako.  Utajitenga na umaskini taratibu taratibu. Umaskini hauna kawaida ya kuwapata watu wanaotumia muda wao vema kwa manufaa. Nzi hufuata uchafu si vinginevyo. Umaskini vile vile hufuata watu wasiojua thamani ya muda. Umaskini ni kama ugonjwa wa kipindupindu. Ili uwe maskini lazima kuna kanuni za mafanikio uzivunje. Kipindupindu pia ni kanuni za afya tu umevunja. Usikubali kuendeleza umaskini kuutoa kwa wazazi na kuwarithisha watoto wako huo ugonjwa.  Hebu chukia. Kama unavyochukia kipindupindu (kama unakichukia that is, maana watu wengine hata hawajielewi kabisa). Umaskini si kitu cha kukumbatia. Ni ugonjwa unaochangia kuharibu misingi mingi ya kiroho, kifamilia na taifa kwa ujumla. Amua kuutimua maishani mwako. Na ndo nasema njia ya kwanza ni kujifunza kutumia muda wako vizuri. Tembelea www.andreamuhozya.blogspot.com kujifunza zaidi.

Njia nyingine ni kujifunza kuangalia fursa mbali mbali zinazokuzunguka. Unajua linapokuja suala la fursa watu wengi wanahitaji kufundishwa jinsi ya kujua kitu fulani ni fursa na kitu fulani ni fursa ya sasa na kingine ni fursa ya miaka ijayo. Si kila mtu anajua. Usipoangalia fursa zilizopo na zijazo utalaumu serikali mpaka siku unakufa. Ili kuuzimisha moto wa umaskini unaotafuna jamii yako na familia yako inabidi ujifunze kutambua na kutumia fursa zilizopo mbele yako na uzifanyie kazi.

Umaskini hauna kawaida ya kuogopa mshahara wako. Utapata mishahara kila mwezi kwa miaka 20 - 40 hadi ustaafu na umaskini utakuwa bado ni sehemu ya maisha yako.  Why? Kwa sababu mshahara ni ujira kidogo tu wa kumwezesha mfanyakazi asije kazini uchi wala asije kwa miguu wala asije kazini akiwa na njaa. Basi.  Mshahara si njia ya kuuondoa umaskini. Ndiyo maana watu wengi walioajiriwa bado ni maskini. Umaskini hauogopi mshahara
. Ni ugonjwa mbaya na mgumu dozi ya mshahara haisaidii.  Ni sawa na kutaka kumaliza malaria sugu kwa panadol. Lazima utafute FURSA za kukusaidia kujikwamua hapo ulipo.  Fursa zipo nyingi mno. Ni lazima ujue pia fursa ipi inafaa katika mazingira yako. Usije ukawa kama mimi kabla sijajua vema mambo haya nilikuwa nauza vitu mahali ambapo hakuna wateja wa vitu vya aina ile. Usicheke.  Sikuwa na maarifa. Now ninayo ndo nakumegea na wewe. So ni hivi:

~ Tumia muda wako kutafuta fursa zilizopo.

~ Tumia muda wako kuzielewa hizo fursa vizuri.

~ Tumia muda wako vizuri kuzitofautisha hizo fursa.

~ Na tumia muda wako kufanyia kazi fursa uliyoamua kuituma kuutokomeza umaskini kutoka kwenye familia yako.

Kwa matumizi hayo ya muda sioni kama utahitaji Bunge liwe LIVE kwanza au sioni kama utakuwa na muda wa kulalamikia serikali kuhusu umaskini wako na familia yako. Ifike mahali ukubali kuwa jukumu la kujikwamua kutoka katika umaskini ni LA KWAKO mwenyewe.  Siku ukijivika hilo jukumu ndo siku utakayokuwa umeanza kuwa mtu mzima kiukweli ukweli. Mtu yeyote ambaye anataka au kutamani kukwamuliwa kutoka umaskini bado hajakuwa vizuri.  Simaanishi kuwa usiombe msaada.  La hasha. Kila mtu huhitaji msaada. ILA kuna watu wanataka mtu mwingine aje awasaidie kuishi maisha yao hapa duniani afu wajikute wamefanikiwa.  That's never going to happen. Wake up! Tumia muda tafuta fursa.  Ziko nyingi. Nenda semina mbali mbali ujifunze.

Kama unawaza kujikwamua kimaisha ila hujui wapi uanzie au unatatanishwa na fursa unazoziona au una hofu ya kujaribu basi wasiliana nasi kwa WhatsApp #o788366511 #o752366511 tushauriane.  Usikubali kurithi umaskini na kuwarithisha watoto wako.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.

Jumapili, 23 Oktoba 2016

AKILI YAKO ISIPOKAA SAWA MAFANIKIO HUTAYAONA


Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikichunguza maisha ya watu waliofanikiwa na wasiofanikiwa. Lengo langu hasa ni kufikia mafanikio makubwa na kuwasaidia wengine wanaotaka kufanikiwa pia.

Nimejifunza vitu vingi kutoka kwa watu waliofanikiwa ambao niliweza kuonana nao ana kwa ana. Na hata wale ambao bado sijaweza kupata fursa ya kuwaona nimekwisha jifunza tayari mambo muhimu kutoka kwao.

Leo nataka niongee kitu ambacho watu wengi wanaotaka kufanikiwa hawajakijua bado. Na hivyo wanakwama kupiga hatua kimafanikio na mwisho wanajikuta wanakata tamaa ya kutafuta mafanikio tena.

Hiki kitu kinaitwa MINDSET. Yaani MTAZAMO. Yani ni kweli sikatai kabisa kuwa kufanikiwa kunahitaji vitu kadhaa muhimu. Najua na wewe unavijua na hata nikisema tuvitaje kwa pamoja unajua.
Vitu kama:

~ kufanya kazi kwa bidii sana (kujituma),
~ kuishi kwa kuweka malengo,
~ kuwa na hamasa yani kitu kinachokuhamasisha  au kukusukuma kufanya kazi malengo yako (motivation),
~ pia kuwa na coach, na mentor na role model wako ni muhimu sana kwa ajili ya inspiration
~ na vitu vya aina hiyo

Lakini nimekuja kufahamu kuwa kuna jambo la msingi sana ambalo ndo nataka nikushirikishe hapa ambalo usipolijua utahangaika sana kufikia mafanikio. Jambo hilo ni kwamba ili vitu vyote tulivyotaja hapo juu ili vizae matunda sahihi na kukuletea mafanikio inabidi uwe na kitu kimoja kwanza: AKILI ILIYOKAA SAWA au unaweza kuita MTAZAMO SAHIHI (THE RIGHT MINDSET)

Mazingira ambayo tumezaliwa na kutokea au kukulia yana nafasi kubwa sana ya kutujenga kimtazamo. Yani MTAZAMO wako kuhusu mafanikio jinsi ulivyo unachangiwa sana na mahali ulipokulia, watu waliokulea (wazazi, shule, kabisa/msikiti etc) toka ukiwa mdogo. Pia jamii iliyokuwa inakuzunguka ukiwa mdogo.
Halafu na watu wanaokuzunguka sasa.
Hao woote wanachangia sana kukufanya kujenga MTAZAMO ulionao kuhusu maisha na kuhusu mafanikio.

Kuna watu kutokana na mazingira niliyoyaeleza hapo juu wamejenga mtazamo kuwa hawawezi kufanikiwa kimaisha mpaka uwe mjini au uwe na degree au utoke familia bora au uende Ulaya au Marekani hata akizama baharini.
Hata kama ni kwenda kuosha vyombo. Yani bora akaoshe vyombo Dubai kuliko kuuza mitumba au kuanzisha mradi mdogo Tanzania. Wengine wameshajiona kama wanyama vichwani mwao bila kujua. Mwingine anajiona mbwa. Yani wewe unaongea naye unamwona ni binadamu kumbe mwenzio MTAZAMO wake anajiona kama mbwa. Hujawahi sikia mtu anasema "bora ningezaliwa MBWA Marekani?" Huyo mtazamo wake ni kuwa mbwa walioko Marekani wana mafanikio kuliko yeye. Kama na wewe huo ni mtazamo wako unapaswa kutubu mbele za Mungu haraka mno yani usijisumbue kutafuta mafanikio wakati ushamfanya Mungu ni mjinga kwa kukuumba binadamu. Tubu kwanza. Unaweza ukawa na bidii na ndoto kubwa na malengo lakini mtazamo wa kwamba mpaka uende Marekani ndo ufanikiwe siyo mtazamo sahihi kukufikisha katika mafanikio.

Kuna ambao mtazamo wao ni kuwa akioa binti aliyesoma au kama ni binti ana mtazamo akiolewa na mtu mwenye uwezo mzuri kifedha hapo yeye pia atafanikiwa. Hawa wa hivi hata umfundishe biashara vipi. Hata umhamasishe vipi kuwa anaweza bado yeye ànawaza kupata mjamaa mwenye nazo. Na hawa baadhi yao wanajikuta wanachezewa tu na kushushwa thamani wakidhani wamepata mtu sahihi kumbe wamekosea mno sababu ya kuwa na mtazamo huo. Anaweza akawa na bidii ya kazi lakini mtazamo huo siyo mtazamo sahihi ili ufikie mafanikio.

Kuna wenye mtazamo kuwa kwa kuwa UKAWA haikuchukua dola hawawezi kufanikiwa. Na kuna wanaodhani kwa kuwa CCM imekamata dola ndo watafanikiwa. Sikia kufanikiwa ni suala binafsi. Kuna watu wamefanikiwa Tanzania na kuna watu Marekani ni hohe hahe. Kuna watu wanaipenda UKAWA/CCM ambao hata siyo wanasiasa kabisa wamefanikiwa na kuna wanaoiopenda UKAWA/CCM ambao ni hohehahe. Tofauti siyo chama kipi anapenda. Tofauti ni kichwani kwako kuna mtazamo UPI kuhusu mafanikio. Hufanikiwi kwa sababu ya chama unachoshabikiaunachoshabikia

Kuna watu wana mtazamo kuwa ili ufanikiwe labda uwe na sapoti ya watu wa karibu. Utasikia mtu anasema "Sisi wabongo hatupendani ndo maana hatufanikiwi" kashajenga hiyo. Kuwa hawezi kufanikiwa kwa kuwa hawapendani. Au "yani mi nina ndugu wana uwezo ila hata kukupa sapoti yani utadhani hawanijui". Anadhani ndugu wakimpa sapoti ndo atafanikiwa. Ni kweli wote waliofanikiwa wanapendwa, au walipewa sapoti na ndugu? Ukijua story za waliofanikiwa utashangaa mno. Huo siyo mtazamo sahihi.

Wengine wanafikiri kufanikiwa ni bahati. Hawa ndo wanawaza kuvaa pete za bahati. Au kuangalia nyota zinasemaje kwenye gazeti. Kuna watu wamesoma nyota toka darasa la saba mpaka sasa wana miaka 40 maisha yameshaanza rasmi na bado mafanikio hayasomeki. Huo siyo mtazamo sahihi. Watu hawafanikiwi kwa sababu birthday yako mvua imenyesha na jua likawaka. Huo ni ushirikina. Na hata ukifanikiwa mafanikio yako yatakutesa mpaka either uyakatae ufe maskini au uteseke na kuishi na majoka ndani ya nyumba sijui kulala na majini makaburini sijui kuua wazazi au watoto na kuishi kwa moyo ulio na majuto mno na uchungu usiosemeka maisha yako yote hata kama kwa nje unatoa tabasamu na kuwaambia vijana wasikate tamaa watatoka kumbe wewe una joka chumbani.
Huo siyo mtazamo sahihi.

Kuna mitazamo mingi mno ambayo si sahihi. Na nimeanza kusaidia kutoa elimu kidogo kidogo kwa vijana wenzangu kupitia kwenye blog yangu www.andreamuhozya.blogspot.com kuhusu mambo mbali mbali lakini pia kwa njia ya WhatsApp.

Kama wewe pia unataka kufanikiwa na umefanya vitu mbali mbali kwa bidii lakini bado hujaona mwelekeo njoo tuongee kuhusu mambo ya mtazamo. Ni muhimu kuliko unavyoweza kufikiria. Usije ukapoteza muda mwingi mno kufanya kitu ambacho ungeweza kuwa umeshafanikiwa ila kuna mahali una mindset isiyo sahihi. Au usijepoteza muda kufanya kitu kisicho na faida bila kujua kwa sababu ya kufata mkumbo tu. Afu mwisho unajikuta mtu mzima na majukumu makubwa mengi hela huna unaanza kupata pressure miaka 40 tu. Njoo tushauriane mambo muhimu.

Usiijaze mind yako na picha chafu za kwenye mitandao na vitu vya kuchekeshachekesha tu huko WhatsApp. Mafanikio yanahitaji akili iliyo SAFI. Lazima uwe na the RIGHT MIND. Ilishe akili yako vitu muhimu vya kuifanya itafakari siyo ilale tu na kukaa bila kukua. Mfano makundi mengi ya WhatsApp yamekuwa na vitu vya kitoto kitoto tu. Na watu ndo wanafurahi. Picha za ajabu ajabu na habari za umbea na entertainment tu haziifanyi akili yako ndo ikue. Unahitaji vitu tofauti. Unahitaji MTAZAMO mpya. Kama kweli upo serious na mafanikio yako. Muda haukusubiri. October inayoyoma. Mwaka unaisha.. Umefanikiwa malengo mangapi so far? Be yourself. Kuwa wewe. Angalia maisha yako!

Karibu tuzungumze WhatsApp #o788-366511 au #o752366511


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.

Jumamosi, 22 Oktoba 2016

WHAT KIND OF YOUNG PERSON ARE YOU?

WHAT KIND OF YOUNG PERSON ARE YOU?

There are things that are so easy to do in life and anybody can do these things. Especially young people.

It's easy to TALK
Yes it's easy to talk, talk, talk, talk and keep talking after keeping talking. Most young people are now involved in talking. Just talking. Talking about what they want in life. Talking about how they want it. Why they want it. When they want it. But that's all they do. TALK. They don't do anything about it.

It's easy to PROCRASTINATE.
I call procrastination the food of a lazy mind. It's most people mind's *default mode.*
And so most people do so, especially young people. (Especially here in Africa more than elsewhere.) Well, young people the world over generally somehow  think they still have all the time in the world to go about it LATER. They put it all off. It's not a convenient time, they think. They are looking for that perfect, perfect time. When they're grown up. The perfect, perfect moment to do it. When they have the money or a college degree. Now they're still having a little fun to lighten up their youthful selves a little, so they think. Their philosophy about life is founded on a lie that they not only believe but also protect: Have Fun While You're Still Young. Okay little brother, alright lil sister. Have fun. But remember TIME flies while you're having fun. So that's the generation of young people we have. Putting off everything. Or here in Africa they're waiting for a share of that AID MONEY promised by the government when it gets AID MONEY promised by the *donor!* If you're one of these wake up from that slumber! Learn from those who've woken up and done something.


It's easy to JUDGE.
So most people do that. Young people also do so. When they see someone successful their verdict is: inherited. Or: stolen. Or: swindled. Or: luck. And so on and so forth. They still want to be successful, yet most of them have no idea how to go about it.

It's easy to WATCH.
U-huh! Yes it is. And so most people do so. Young people love this the most. Yes they love watching TV series or watch their favourite athletes in action because it's easy to watch. Yes, it's easier to watch than to put in the work and sweat and discipline yourself until you become someone's favourite actor or athlete!
They love to put their headphones on and shut the whole world out and listen to their favourite songs and feel so good. Yes that's easier than putting in the work to nourish your talent and find a role model and get yourself a mentor and a coach who will subject you to a disciplined routine to ensure that you one day get paid for doing what you love doing. Look at how many people you'll find on a football pitch on early Monday morning drenched in sweat. Then look how many you'll find on Sunday afternoon - especially on a derby!

It's easy to do SMALL TALK.
So most people do so. And young people love it.
Talking nonsense and filling their minds with irrelevant and unhelpful things that intoxicate their minds and unknowingly impair their ability to have a sound judgement. Avoiding all serious subjects and deep, thought-provoking conversations. And then they expect to live a life that has a meaningful impact and to leave a meaningful legacy when they're gone.
To change this world!


We live in a world where the generation of young people we do have has lost its sense of purpose. Young people who don't know why on earth they're here for? A typical youngster of today thinks success is having a beautiful profile picture of Facebook and a 100k followers on Instagram or going out with the opposite number often. A typical youngster of today has half of their brain filled with filth, irrelevant information and negativity and thinks that you can actually MICROWAVE success!

So which young person are you?

Are you one that has spent this almost gone year just #talking and #procrastinating and #judging and #watching and indulding is #petty talk and #wishful thinking, or are you a young person that has spent this year taking steps to live with distinction and to make both your presence and your contribution felt and appreciated?

Will your family, or community or nation or continent or world at large ever get to benefit from the gifts and talents that God Almighty invested in you? Or did He create you to come here and just have all the fun you could have and then die, never having lived at all? Yes, never having lived at all, for I consider life as a service to others, and success as serving other people to the fullest and to the best of your ability - what the late Caribbean Pastor used to call DYING EMPTY!

What kind of young person are you? One that has spent 2016 striving to become well informed and knowledgeable of the things that you need to know in order to make a worthwhile contribution? Or one that has spent almost an entire year now going from music concert to another, downloading all the music songs you could download and watching them things: bad things, dirty things, and  thinking about #BAE 24/7? And yet having the audacity to say you want a good life? Who's going to give you that? You want to become successful? Good. But don't you know that what you've been doing is detrimental and amounts to sabotaging your own cause?

How many books have you read so far this year?
Books that added something to your knowledge bank account.
Or will you enter 2017 with the knowledge you acquired 5 years ago and expect to live to make a difference?  Coz I'm not talking about just existing! I'm talking about LIVING! And leaving a legacy. I'm talking about you becoming a leader and not a follower. Haven't you heard that "LEADERS ARE READERS"?

Listen to me, I once heard a story of one of the richest people of our time. He once visited this country's beautiful national parks and game reserves and spent all of his time there reading books and barely watching any of the elephants, gazelles, lions or flamingos! That man is Bill Gates!
"Why would he do that" you might ask. I will tell you why! It's because he knows the VALUE of spending time getting informed. Adding onto one's knowledge bank account. Lemme tell you something: Reading is one of the strongest and most valuable currencies in the KNOWLEDGE ECONOMY. You can quote me!
Will you emulate him?
Or would you rather die than read! Or write!
Don't you know your ideas can change our world?


What kind of young person are you? One that is the problem with this continent of Africa or one that's the solution to the many problems and challenges we do have including education, poverty, health related challenges and others? Are you one to ask other people to give you a job or one to give other people the job they need? What kind are you? I'm talking to you! Are you one to make your brothers and sisters step up and do something to change our continent or are you one who thinks that Africa's challenges will be resolved by some #muzungu with a briefcase of AID MONEY!  Surviving on life support!

What are you doing to mend the broken lives and alleviate the challenges due to poverty and backwardness of the people in your own nation?
Or are you still having a little more fun first? What difference has such entertainment and fun done into your life so far? And into the lives of those around you?
Are you hearing me?

What kind of young person are you?
One that Africa will be proud to have ever had or one that Africa's history won't consider to have ever walked this continent? Listen to me my friend. Your nation, your people, our people our continent is looking and yearning for serious young people. For young men and women that will be the envy of the world!
The problem with somevof you young people is you think you are a happenstance! You think you're an accident! Don't you know that you have a purpose? Haven't you heard that even while you were still in your mother's womb the creator knew you and had set you apart for a purpose? Find that purpose! It isn't about how or where or when you were born. It only matters that you were born.

So better get serious already, or our history will forget all about you like that ant you stepped on the first day you went to school so many years ago? Remember that #ant? Of course YOU DON'T. And that's how you'll be forgotten, if you don't take your life as seriously as you should.

What kind of young person are you?
And what kind should you have been?
What kind must you be to steer your nation and our continent to a better future. To our own African dream of progress, unity and excellence!
What's your contribution going to be?


Step up my brother! You're not here to get a degree on Six Packs Acquisition. Do something!
Step up my sister! You're not here to look sexy and flash a well-curved figure to lustful eyes and get LIKED but to contribute something to better our situation. Be one of those sisters of ours who've done that!
Step up and do your part.
Do everything you can do.
A noble human soul once said: ALL YOU CAN DO IS ALL YOU CAN DO, BUT ALL YOU CAN DO IS ENOUGH.
That man was Art Williams.
Don't you underestimate the power of All You Can Do!

So, are you going to do something?
Or are you going to just talk about doing something?
What kind of young person are you?

I dare you today!
I dare you to get yourself on active mode!
ACTIVATE THE CODES! Are you hearing what I'm telling you?
Put in the work!
Sweat if you will!
Give it your all!
Bring in the PASSION!
It's a noble thing you're doing.
And the sons and daughters of Africa will be proud you made a difference!
Coz that's the kind of young person you ought to be!
One whose life will make a difference!
Don't die with that greatness in you.
Don't deny us a chance to benefit from your contribution!
Step up and make a difference! Hold the pen and rewrite Africa's history with your name in it!
I promise you your story will be told to future generations and your name will live in their hearts forevermore.

Step up and make it happen!



Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa!

+255788366511(WhatsApp only)
www.andreamuhozya.blogspot.com

Ijumaa, 21 Oktoba 2016

JAMBO LA KUMI NA LA MWISHO (KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

JAMBO LA KUMI NA LA MWISHO
(KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

TUNAENDELEA:

Kwa neema ya Mungu naendelea ku-share mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia UHURU wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Na leo naendelea na sababu ya 10 na ya mwisho.

10. JAMBO LA 10: WAAJIRIWA WENGI HUISHIA KUWA WAOGA (MOST EMPLOYEES END UP BEING COWARDS)


SO WE ARRIVE.... Siku kumi za kujifunza pamoja.

Leo tutajifunza jambo la mwisho

Zamani nilikuwa nikijiuliza kwa nini wale watu ambao walikuwa na USHAWISHI (influence) sana shuleni ama vyuoni kwa nini wakiajiriwa ni vigumu sana kuwasikia tena. Mtu ambaye alikuwa akiitisha mgomo vijana wenzake Chuo kizima au shule nzima watu wanagoma mpaka wakati mwingine wanasababisha taifa zima kujadili hilo suala lakini akiingia kwenye ajira si rahisi kumsikia tena.
Wala kukuta akipewa cheo kikubwa labda.

Nikaja kugundua kuwa setup ya mfumo wa ajira ilivyo japokuwa inafanana na mfumo wa shule kwa maana ya ratiba lakini kuna tofauti kubwa ya PRINCIPAL au HEADMASTER na mtu anayeitwa BOSS aisee. Yani Principal wa chuo anaweza kuwa hata na elimu ndefu na umaarufu mkubwa nchi nzima lakini haogopwi kama mtu anayeitwa BOSS hata kama boss mwenyewe hata shule hakwenda ila ndo boss. Hapana chezea AJIRA.


Ni watu wachache sana... EXTREMELY FEW PEOPLE... ambao wako katika ajira na wana ujasiri katika mambo wanayoyaamini. Wengi wanapoajiriwa wanajifunza kuwa waoga. Bosi akiingia ofisini wengine hata mazungumzo yanakatayanakata
. Au mwajiriwa akiitwa ofisini kwa bosi yani automatically anajiset kuappear "vizuri" wakati alikuwa tu okay. Wengi hiyo inakuwa si kwa sababu eti heshima bali WOGA tu. Yani bosi akiingia ofisini ni shida...

~ wengine wanaweza kutetemeka hata kama kwa nje kajikaza. Anavibrate ndani kwa ndani. We jiulize kama wewe ni Mwalimu hivi Mama Ndalichako akitinga hapo shuleni bila taarifa hali itakuwaje. Woga. Kwani mmeua MTU nyie?

~ wengine hata anaweza kushindwa kuongea vizuri. Angalia Waziri akitembelea mahali hasa kwa idara zilizo chini yake.

~ wengine anaweza kutamani atoke katika mazingira hayo.

Confidence inaanza kuondoka taratibu.
Mwishowe wanahitimu katika UOGA.
Wanakuwa waoga wa vitu vingi.

~ Waoga wa kuomba kuongezewa maslahi.
~ Waoga wa kuondoka kazini kutafuta maslahi kwingine hata kama ni ajira nyingine
~ Waoga kabisa wa kujaribu kutafuta maisha katika mifumo mingine ya fedha nje ya mfumo wa ajira kama ujasiriamali au biashara. Yani aneshakuwa ADDICTED to kuishi kwa mfumo wa ajira tu.
~ Waoga wa kutoharibu kazi kwa sababu ya kuogopa itakuwaje akiambiwa kazi imeisha.


Mtu huyu anaanza kupoteza vitu muhimu:

1. Kwanza anapoteza UJASIRI.. Self confidence and hata self esteem.

2. Pili anapoteza HONESTY....hawezi kusema ukweli hadharani. Ila bosi akiondoka ndo unamsikia eti.."To be honest....." Hahaaaa

3. Mwisho anapoteza INDEPENDENCE OF THINKING.
Yaani hata angekuwa na mawazo au opinion tofauti vipi atasikilizia kwanza wenzake wanawazaje. Wanatakaje. Anaanza kuwa victim wa GROUP THINKING. Anasahau Mungu alituumba individually. Anasahau kuwa kuna vitu vya kukubaliana na wengine lakini when it comes to matters of PRINCIPLES zako unatakiwa usimame imara unshakable ukisimamia principles zako. Bosi akisema unaobey.


Kama wewe ni mwajiriwa jiulize hujawahi kucompromise principles zako kwa sababu ya kulinda "KIBARUA" chako? Kwamba unaamini hiki si sahihi hata aje nani na ukasimama imara kulinda msimamo wako! Come what may! Je ndivyo ulivyo katika ajira yako? Kwamba you can tell your boss to their face kuwa jambo fulani si sahihi hata kama itakuwaje ilimradi si sahihi?
Thubutu!

Ndo hii sasa kwamba kwa sababu kuna BOSS. MASTER. Hapo unajikuta unaCOMPROMISE kwa sababu mfumo huo umempa control yeye ya kudetermine mambo mengi juu yako. Unaogopa KUHARIBU kazi. Unaanza kujiuliza:

~ Watoto watakula nini?
~ Kodi ntalipaje?
~ Mkopo ntaumaliziaje?

Is that the mind of a free person?

Na wenzako "wanaokutakia mema" wanakuita kando wanakwambia "Aah, we huyu bosi mwache kama alivyo. We unadhani sisi hatuoni kuwa anakosea? We potezea tu atajiona mjinga"
Unapotezea.
Una compromise.

Hatimaye unakuwa miongoni mwao. Unakuwa muoga kabisa. Hata kama ulikuwa wewe ndo unaendesha migomo vyuoni.
End of your story.
Coz MAFAHALI WAWILI HAWAFANYI NINI.....?


And so..ndo hivyo...

Na kwa kuwa mada yangu katika hizi makala ilikuwa ni kuhusu uhuru wa kipato...then sababu hii ya mwajiriwa husika kuwa mwoga, na kuishi kwa hofu inamnyima uwezo wa kufikia FINANCIAL FREEDOM. Why? Kwa sababu uhuru wowote ule huwa mtu hapewi, huwa anautafuta na kuupata. Hata uhuru wa kisiasa w kifikra na hata huu wa kipato. No one will give it to you. Unapaswa kujifunza UKWELI kuhusu mfumo ambao wewe upo. Je mfumo uliopo wewe kuna mtu yeyote ambaye unaweza kuwa na access naye ambaye ametumia huo mfumo wa ajira akafikia uhuru wa kipato? Kwamba hahitaji tena kwenda kazini ili kuingiza pesa labda aende tu sababu working is a mark of NOBILITY? Je yupo unayemjua ambaye alimake FORTUNE kupitia ajira ili walau ukajifunze kwake? Jipe jibu.
Na kama yupo je wewe na yeye mpo katika footing sawa? Tafuta kujua ukweli.


TRUTH shall set you FREE.


And so I rest my case, for now. Nimezungumza mawazo yangu kwa siku 10 sasa. Naamini nimetimiza wajibu wa kutoishi na mawazo muhimu bila kuwashirikisha wengine ambao huenda yanaweza kuwasaidia.

Na kama ulisoma makala zangu hizi toka mwanzo utaanza kuona kuwa sababu zote nilizoelezea kuanzia ile ya kwanza hadi hii mwisho zinafanya kazi kinyume cha MWAJIRIWA linapokuja suala la kufikia uhuru wa kipato. Ziunganishe utaelewa vizuri. Again..Don't read them in isolation.

Na mpaka hapo nimefikia mwisho wa mfululizo wa makala hizi.

Asante sana kwa kuwa nami tangu mwanzo mpaka leo.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS, WhatsApp and Calls: +255752366511
WhatsApp Only: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com

Barikiwa Sana!


Semper Fi great people,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa

Alhamisi, 20 Oktoba 2016

JAMBO LA TISA (KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

JAMBO LA TISA
(KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

TUNAENDELEA:

Kwa neema ya Mungu naendelea ku-share mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia UHURU wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Na leo naendelea na sababu ya 9.

9. JAMBO LA TISA: KUPOTEZA UHURU WA MAMBO MENGI (LOSS OF FREEDOM)

Wakati nikiwa mdogo nilikuwa nikipenda sana maisha ya shuleni. Nilipenda sana kuanza  shule mpaka wakalazimika kunipeleka kabla ya wakati lakini shuleni nikarudishwa kwamba mkono sijui ukipita kichwani sijui hauvuki bega. Anyway. Nilianza mwaka uliofuata. Nilipenda vitu vingi. Nilipenda mazingira ya shule, nilipenda sare zangu za shule hasa zile za mara ya kwanza. Aisee! Nilipenda kuhesabu namba (hii nafikiri niliipenda kwa lazima hahaaa maana kulikuwa na stiki za hatari ukichelewa kengele), nilipenda kukimbia mchaka-mchaka na nyimbo zake za Makaburu na za Mandela na nyingine nyingi hasa ule wa "JUA LILE LITELEMKE MAMA!!!". Aisee. Nilipenda gwaride hadi nikawa kiongozi wa gwaride wa shule za msingi kata nzima. Mahaba ya dhati kumoyo. Nilipenda mazingira ya shule. Ramani za Tanzania, Africa, nk za mawe yaliyopakwa chokaa, nilipenda bustani na miti na viwanja vya shule. Nilipenda masomo hasa Kiingereza. Kwa ujumla nilipenda KWENDA shule.

Lakini nyakati za likizo nilizipenda zaidi na kutembelea ndugu, kucheza na rafiki zangu, kwenda kuwinda na kuvua samaki, kwenda kufanya mazoezi ya mambo ya kanisani, kwenda kuangalia mashindano ya mpira kwa watu wazima au jamaa wa Kisukuma wakicheza ngoma zao katika sherehe mbali mbali nk. Nyakati za likizo nilizipenda kwa kweli.

Na baadaye nikapemda kwenda sekondari. Nikaenda. Nikaishi maisha karibia sawa na yale ya shule ya msingi. In terms of ratiba na kanuni na taratibu nyingi. Na nyakati za likizo pia nilipata fursa ya kuishi hasa maisha binafsi yasiyo na kanuni zilizonifunga.

Taratibu taratibu nikaanza kuona kuna kitu fulani moyoni mwangu ambacho kimeanza kupungua kuhusu maisha ya shule. Mfano nikaanza kuona kama maisha ya shule yananiprogram kuanzia mbali ili ifike hatua nione hiyo ndiyo kawaida. Nikaanza kuwaza kuwa hivi siku moja nitaweza kuishi mwaka mzima nikivaa mavazi ninayoyapenda mimi asubuhi hadi jioni January hadi December, na nikienda kula muda ninaosikia hamu ya kula, nikienda kulala muda ninaojisikia kulala iwe SAA moja jioni au saa nane usiku. Niongee na watu kwa lugha ninayopenda na siyo lazima niSPIKI INGILISH! Niweze kwenda kokote ninakotaka kwenda wakati wowote kama nina sababu maalumu  bila kuambiwa NIMETOROKA na mtu yeyote wala bila kusubiri idhini ya mtu mwingine. Na nikaona kama kuanzia shule ya msingi nilitengenezwa kuipenda shule siyo kama mimi ndo niliipenda mwenyewe from nowhere. Wanafunzi walionekana bora kuliko watoto waliokuwa wapo tu nyumbani wanalialia na kuongea kikerewe tu mchana hadi usiku na kukaa bila kujua hata kusema neno "SHIKAMOO". Niko sekondari, Seminari, nikaanza kutamani ije siku ambayo nitaendelea na mosomo yangu pasipo kuvaa kitu kinachoitwa sare. Ndiyo ikawa sababu kubwa ya mimi kutaka kusoma Chuo Kikuu badala ya kuendelea na masomo ya Seminari. Sasa sijui ndo wanasema wito uliisha. Hahaaa. But naongelea kilichotokea.  Kilichotokea ni kwamba nyakati za likizo nilijihisi huru zaidi kufanya mambo yangu nilizipenda kuliko nyakati za shule ambazo zilikuwa na program ya kufuata kuanzia unapoamka hadi unaporejea kulala. Sisemi system hizo hazina faida. Zina faida nyingi mno. Ila kwa sababu ya series za Makala zangu hizi najaribu kukufanya kuona shida mojawapo ya mindset and mind control iliyotengenezwa na watu waliotengeneza mfumo wa aina ile wa elimu.

Mfumo ule (the Formal Education System) tumeurithi kwa wakoloni ambao waliuanzisha kwa ajili ya kupata watu wa kuwasaidia kazi zao za kiutawala na kazi zinginezo (white collar and a few blue collar jobs). Ni mfumo ambao waliopitishwa huko waliandaliwa kwa kusudi maalumu. Sisi tukaja kuurithi kama ulivyo na makusudi yake kama yalivyo. Na asilimia kubwa ya waajiriwa wamepita katika mfumo huo kwa namna moja ama nyingine.

Na ndiyo maana maisha ya mwajiriwa ni kama maisha ya mwanafunzi wa shule ya msingi au sekondari. Picha hii hapa chini nikikuuliza uniambie ikiwa ni ya WAAJIRIWA ama WANAFUNZI utasema ni kina nani?


I. Mwanafunzi anaishi kwa kengele mwajiriwa anaishi kwa kengele pia bila tu ameipa jina zurizuri. Anaiita ALARM CLOCK.


II. Mwanafunzi ana muda specific wa kwenda na kutoka shuleni. Mwajiriwa pia ana muda specific wa kwenda kazini. Hawezi kwenda  au kutoka muda wowote anaotaka yeye.


III. Mwanafunzi ana kazi specific za kufanya. Zinajulikana kabisa na zimeandikwa. Walimu wanajua maana ya SCHEME OF WORK na LESSON PLAN. Mwajiriwa pia ana kazi specific za kufanya zinajulikana na zimeandikwa kabisa. Waajiri na waajiriwa wanajua kitu kinachoitwa JOB DESCRIPTION


III. Mwanafunzi ana mavazi maalumu aendapo shule. Of course kuna shule zina safe. Na zingine hazina sare lakini zina dress code fulani. Na kuna sare za siku ya michezo. Mwajiriwa pia ana mavazi maalumu aendapo kazini. Na hivyo hivyo kuna ajira zina sare na kuna makampuni yana sare unapewa mpaka sare za kuvaa siku ya michezo. Hakuna shida katika hili is that what you're saying? Well, sawa. Inawezekana hakuna shida. Inawezekana nakompliketi maisha tu bila sababu za msingi, au siyo?


IV. Mwanafunzi ana muda maalumu aliopimiwa wa kula. Mwajiriwa pia ana muda uliopimwa wa kula. Hawezi kuamua kula masaa mawili eti alikuwa na mazungumzo na rafiki yake. Watazungumza WhatsApp. Kazi kwanza.


V. Mwanafunzi ana madaraja ya vyeo. Kuna mtu wa komonitor wengine. Class Monitor. Head Prefect. Nk. Hawa ndo CCTV za walimu. Mwajiriwa pia anayo hii. Kuna vyeo. Kuna officer, Manager, Excom, nk. CCTV ya MWAJIRI. Huwezi kuishi wala kuzalisha bila kuwa monitored.


VI. Kuna shule ukiongea kilugha unapewa pembe. Kiswahili ndo habari ya shuleni. Na ukienda sekondari Kiinglish ni lazima. Hata kama hukijui utafundishwa mpaka angalau ujue cha kumjibu mwalimu tu. Waajiriwa pia linapokuja suala la lugha kuna lugha maalumu ya kumhudumia mtu. Ukienda ofisi kadhaa unakuta maneno kwenye vibao tu yanaonyesha lugha gani hapa inaweza kutumika. Kikerewe acha kwenu. Kwanza kinamsaidia nani nchi hii. Hata kama mteja ni mkerewe.
Kuna waajiriwa wamekaririshwa mpaka jinsi ya kuongea na mteja physically kwenye simu. Ulishawahi kupiga simu ile namba 100!? Unasikia wanavyoongea. Piga tena baadaye wanaongea vile vile.
Ulishaenda airport au Railway stesheni usikie wale wanaotangaza matangazo. Ni monotone. Utasikia kale kamlio.. Tii-ntiiii... Afu unasikia sauti nzuriii... "Attention all passengers, the passenger train to Mwanza via Morogoro Dodoma and Shinyanga is on lane number one and will leave in 5 minutes time....! Njoo kesho utasikia hivyo hivyo. Utafikiri ni kitu kimerekodiwa.


Unaambiwa ni kuimprove quality ya service. Hivi ukimpigia Dewji simu na yeye anapokeaga hivyo kwani? Kwa hiyo yeye hana quality nzuri ya huduma kwa kuwa hajapokea kama wale wa namba 100?

Listen my friend. Life is a mind-control game. And employees play in that field very well. Wazungu walituletea dini hawakutuletea mindset education. Ili tubaki na dini tu bila matunda thabiti. Mind is better than religion. Coz Mungu alileta wokovu hakuleta dini. Wazungu walileta formal education wakatunyima SELF EDUCATION. Hii unapaswa kuitafuta mwenyewe. Na hii ndo itakukomboa kifikra.

Sasa kwa mifano niliyoitoa hapo juu hivi kama huna uhuru wa vitu vidogo kama:

~ muda wa kwenda na kutoka katika shughuli yako ya kiuchumi
~ mahali pa kuifanya hiyo shughuli everyday lazima uende hapo huwezi kuamua ukafanyie restaurant au beach hata kama unataka

~ muda wa hata kitu kidogo kama kula
~ mavazi gani uvae.
~ nini ufanye leo katika majukumu yako. Ushapangiwa cha kufanya
~ wakati gani usafiri kwenda utakako kwa sababu zako ni mpaka uruhusiwe
~ kupumzika kwa muda utakao hata kama ni masaa mawili ukakae hapo nje ya ofisini ukiwaza mpango fulani muhimu. Au ukipokea simu moja muhimu sana

Kama huna freedom na vitu vidogo kama hivyo. Unawezaje kupata FINANCIAL FREEDOM katika hiyo setup?
Kumbuka nilishasema kwenye makala zilizotangukia kuwa hata kipato chako hupangi wewe. Nk..

Nikukumbushe tu kwamba AJIRA ni mfumo ambao bado upo upo tu sana huku kwetu. Swali ni je mfumo huu upo kwa ajili YAKO wewe pia uajiriwe?

If YES, then good luck.
If NO, then DO take proper action.

Mi nimemaliza. Na kwa leo naishia hapa.

Na kama ulisoma makala zangu hizi toka mwanzo utaanza kuona kuwa sababu zote nilizoelezea kuanzia ile ya kwanza hadi hii ya 9 zinafanya kazi kinyume cha MWAJIRIWA linapokuja suala la kufikia uhuru wa kipato. Ziunganishe utaelewa vizuri. Again..Don't read them in isolation.

Bado 1 tu.
Endelea kuwa na mimi kidogo tu.

But kwa leo hicho ndiyo kikwazo cha 9 cha kumzuia mwajiriwa asifikie kamwe FINANCIAL FREEDOM. Kesho kwa neema ya Mungu nitaendelea na LIMITING FACTOR YA 10 na ya mwisho kwa mfululizo wa makala zangu hizi.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS, WhatsApp and Calls: +255752366511
WhatsApp Only: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com

Barikiwa Sana!

Semper Fidelis,

Yes,

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa

Jumatano, 19 Oktoba 2016

JAMBO LA NANE (KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

JAMBO LA NANE
(KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

TUNAENDELEA:

Kwa neema ya Mungu naendelea ku-share mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia UHURU wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Na leo naendelea na sababu ya 8.

8. JAMBO LA NANE: MAISHA YAKO YA KIJAMII UMETENGENEZEWA (YOU HAVE A SORT OF AN INBRED SOCIAL LIFE)

Leo nataka nianze kwa kusema kitu fulani.

Kuna siku nilisoma Biblia ikawa inaongelea habari za watu wanaitwa MATOASHI. Mathayo 19:12 pale. Rabbi (mwalimu) mmoja wa Kiyahudi aitwaye Yesu, ajulikanaye pia kama Kristo, akieleza hilo jambo pale. Kwamba duniani kuna #matoashi. Akafafanua kuwa kuna matoashi wa aina tatu:
i.) kuna wa KUZALIWA hivyo,
ii.) kuna matoashi WALIOFANYWA kuwa matoashi na watu wengine
na kuna matoashi WALIOAMUA kuwa matoashi kwa ajili ya Mungu.

Nikapata idea moja kuwa kuna mambo mengine yanakuwa yalivyo katika maisha yetu kwa sababu za our PAST. Historia. Asili yetu nk. Kuna ambayo yanakuwa kwa sababu ya watu wenye control na maisha yetu. Na kuna mambo yanakuwa yalivyo katika maisha yetu kwa sababu ya maamuzi yetu binafsi.

Kwa premise hiyo basi kuna watu wanaajiriwa kwa sababu ndiyo kitu kilicho asili yake. Ndiyo MINDSET yake ilivyojengwa toka utoto ikiwezekana toka akiwa tumbni kwa mama alikuwa akinenewa ajira akipiga teke mama anasema huyu atakuwa polisi huyu au wengine huyu atakuwa mwalimu atufundishie Jamii au huyu atakuwa hiki na kile. Katika formative years zake akiwa mtoto anaona maisha kwa jicho la ajira. Wazazi, ndugu, jamaa, marafiki, wengi wao au wote wakiwa wameajiriwa kwa namna fulani. Alipoenda shuleni walimu wanaongelea kusoma ili kupata kazi nzuri. Zingine wanamchagulia. Wewe utafaa kuwa meneja wa benki. Wewe mchafu mchafu utakuwa fundi "makenika". Akirudi likizo watu hata majirani wanamwambia "Soma mwanangu, someni mpate kazi mtusaidie sisi wazee wenu hatukusoma" wanampa mifano ya vijana ambao hawakusoma na wapo wapo tu hawana ajira jinsi walivyo hawana mwelekeo. Na wanamwambia kuhusu unaona mtoto wa fulani amesoma amewajengea wazazi wake nyumba nzuri. Soma usichezee elimu. Kama ni wakristo watampa na neno la Biblia "Mshike sana elimu usimwache aende zake" ambalo wengi hasa wanamaanisha FORMAL education.

Huyu mtu hata akija kufika Chuo Kikuu utakuta anachagua kozi ambazo zina AJIRA. Kweli anachagua mwenyewe. Hakuna anayemchagulia. Lakini mindset iliyoko nyuma ya hiyo choice ilijengwa siku nyingi bila yeye kujua. Anafikiri kuwa ana freedom kwa sababu kachagua mwenyewe kusoma LAW. Anachagua kozi ambazo zinaitwa "nzuri". Kozi ambazo "ZINALIPA" (mshahara mzuri). Kama unasoma hapa na ulisoma chuo hebu kuwa mkweli hukuchagua kozi unayoweza kupata AJIRA kirahisi? Kuna binti namfahamu toka akiwa mdogo sasa ni binti kashamaliza chuo ameajiriwa. Ninawajua wazazi wake. Ni wahandisi wabobezi na watoto wao wawili kati ya watatu waliwajengea mazingira ya kuupenda uhandisi na kuona ni kipimo cha kuwa KICHWA DARASANI. First born wao ambaye ndo huyo ninayemwongelea ameshamaliza UDSM COET now ameajiriwa serikalini kama Mhandishi huko Kanda ya Ziwa. Na toka akiwa binti wa shule ya msingi alikuwa akisema anataka kuwa mhandisi kama baba yake. Ukimuuliza kwa nini. Anasema my dad is very bright and we have a good life. Ni kweli walikuwa na maisha fair. Not bad. Middle class family. Chakula kipo. Ada hazichelewi tena English Medium. Toka utoto wanafundishwa hisabati na kiingereza na baba kila siku. Huyu binti alikuwa anasoma novel ngumu ngumu kama COSA NOSTRA akiwa darasa la tano. Fikiria hilo. Hesabu za darasa la saba ameshazikava akiwa STD V. In fact alirushwa kutoka darasa la sita kwenda la saba na mtihani wa taifa akiongoza shuleni kwako akiwa kasoma miaka 6 wenzake 7 yote. Yeye na wadogo zake darasani walikuwa wa kwanza katika madarasa yao wote watatu. Walikuwa level za madarasa tofauti. Na sasa ndoto imetimia kwa huyu wa kwanza. Amekuwa mhandisi ameajiriwa serikalini. Kama baba na mama. Mindset yake toka utoto iko hivyo. Hili ni kundi la kwanza. Yani ndo asili yake. Ndo hapa wanasema mtu anaweza kusoma sana lakini MINDSET yake ikiwa imeshikilia jambo fulani hata ungesema nini. It's a RIGID mind. Imeshakaa hivyo miaka mingi. Hicho ndo anachokiona yeye. Imeshakuwa ASILI yake bila yeye kujua. Haoni option yoyote nyingine. Baba na mama wamekaa serikalini na hawajawa na changamoto ndogo ndogo hizi. So why mtoto aone shida.
Waajiriwa wengi kuajiriwa kwao ni issue ya MINDSET tu. Ni kundi la watu ambao bila kujua wametengenezewa mazingira ya kuwa na vision fulani specific. Toka siku nyingi.

Kundi la pili la waajiriwa ni la wale ambao kuajiriwa ilikuwa siyo saana kwamba aliandaliwa hivyo kifikra ila huyu aliwekewa ulazima fulani wa kuajiriwa. Ametoka familia ya wazazi wanaoitwa HELICOPTER PARENTS.
Mfano kutafutiwa kazi anakuta ipo tayari tayari. "Tushakutafutia kazi mwanetu, keshokutwa unaenda kuanza, usije ukatuangusha huko". Ukitaka kuwaambia kuwa ungependa ufanye mambo binafsi unaulizwa wewe ndo unalipa kodi hapa? Unajua tumegharimika kiasi gani kukusomesha huko Malaysia na kwingineko? Ukitaka kuongea utasikia:  Nyie watoto wa siku hizi hamna ADABU? Mzazi anaongea na wewe unaongea. Sasa aina hii ya mazingira huchomoi. Lazima uende kuajiriwa na usiwaangushe wazazi. Unataka kuachiwa LAANA? Washakwambia wanategemea wewe ndo uje uwe meneja au Mkurugenzi siku moja so usiharibu kazi. Kundi hili la waajiriwa ni kundi la watu ambao wanaishi kwa VISION za wazazi wao. Yule binti mhandisi ana mdogo wake wa kiume anakaribia kumaliza elimu ya juu. Wazazi washaanza kumtafutia kazi. Asije kuhangaika. Internship wanatafuta wazazi. Ajira wanaandaa wazazi.
Wasomi wengi wangetamani maisha yawe hivyo. Straight line life. What a life!

Kundi la tatu ni wale ambao WAMEAMUA wenyewe kuajiriwa. Siyo mindset wala siyo suala la wazazi kutaka na kufunga na kuomba aajiriwe bali yeye kapenda. Mara nyingi hawa wanaajiriwa kwa muda au just for the sake of it. Siku akiona vipi anaondoka kwenye ajira kufanya vitu vingine. Hawa ni wenye vision binafsi. Na anaweza kubakia kwenye ajira maisha yote bila influence ya mtu kwa sababu ndivyo alivyoamua. Ndo vision yake. Kama wale matoashi walioamua wenyewe kuwa mimi nataka niwe TASA nisizae wala kuoa kwa ajili ya Mungu. Vision binafsi. Siyo influence ya mtu wala ya wazazi.

Sasa kama wewe ni mwajiriwa ni muhimu ukajitathmini. Uko kundi gani katika makundi hayo matatu. Mada ninayozungumzia mimi katika Makala zangu hizi ni JINSI ILIVYO NGUMU KWA MWAJIRIWA YEYOTE KUPATA UHURU WA KIPATO. Kwa maana nyingine likija suala la kuingiza kipato mwajiriwa anazaa. Hakuna shida kabisa  Lakini likija suala la uhuru wa kipato mwajiriwa ni TOASHI. Hawezi kuzaa.
Castrated.

Ndo nasema jiulize wewe ni aina gani katika hao watatu.
Umefanywa hivyo toka umezaliwa (uliumbwa na kukua ili uajiriwe)?
Au ulilazimika kuajiriwa kwa sababu ya watu kwenye control na maisha yako?
Au umeamua tu kuwa hutaki kuhangaikia uhuru wa kipato kwa sababu tu "siyo ishu". Au unazopata zinatosha umejenga una magari unaishi vizuri nk watoto wanasoma Intaneshno Skul so inatosha huhitaji kuwa na "tamaa" ya mahela mengi!
Comfort zone.
Which one are you?

Au wewe hujui wewe ni aina gani ya mwajiriwa katika hao. Unatiririka tu. Uko bize from Monday to "THANK GOD IT'S FRIDAAAAAY!!!"


Nimeona niweke hizo categories ili kama umeajiriwa au unataka kuajiriwa ujue WHY? Labda itakusaidia. Na utaelewa zaidi mambo ninayofundisha hapa. Usije kujikuta unakubaliana tu na mimi hata hujui why au unatofautiana na mimi bila kujua why.

Sasa naendelea na sababu ya nane inayozuia mwajiriwa kufikia UHURU WA KIPATO.

Ukiacha sababu saba ambazo nimekwishazisema toka mwanzo.. Maisha ya mwajiriwa yana mambo mengi ambayo si maamuzi yake na mengine ambayo si maamuzi yake.

Mojawapo ya jambo ambalo hana maamuzi nalo ni social life yake. Maisha yake ya kijamii. Asilimia kubwa ya muda wa wajiriwa wengi hutumika katika ESSENTIALLY mazingira yale yale, na watu wale wale, katika working field ile ile, wakizungumzia zaidi mambo yale yale. Kama uliwahi kwenda kutembea gerezani utaelewa kuwa kuna ukuta. Na watu ni wale wale zaidi. Ukiacha wachache wanaokuja kutembelea gereza kusalimia wafungwa, kufundisha dini, kuwatia moyo wafungwa nk.

Ni vizuri ukakumbuka kuwa katika viumbe vyote duniani ni binadamu peke yake ambaye aliumbwa ku-socialize. Maana yake ni kwamba your social life as a human being ina maana kubwa sana katika maisha yako kuliko hata your financial life ambayo ndo ninaiongelea hapa. In a point of fact ni kwamba your financial life inabebwa kwa kwa kiasi kikubwa na your SOCIAL LIFE. Wanasema "YOUR NETWORTH IS EQUAL TO YOUR NETWORK". And vice-versa. Sasa katika setup ya ajira ndo nasema UMESHATENGENEZEWA SOCIETY ya kuishi nayo kila siku bila kupenda kwako.
Unalazimika kukubaliana na hiyo social life. Uwe unawapenda huwapendi ndo hao hao. Wawe ni watu wenye mawazo mazuri kichwani au wawe ni wanaowaza vitu vidogo vidogo ndo hao jamii yako.

Na waajiriwa wengi network yake ni hasa hasa watu wa pale kazini kwake. Watu wa kazini kwake ndo wanajua birthday yake ni lini siyo majirani. Kama umeajiriwa jiulize kati ya labda majirani zako na waajiriwa wenzako nani wanajua zaidi ishu zako? See? Network yako imekuwa ile unayoishi nayo siku nzima. Kuishi kwa kutegemea network ya kazini kwako tu ni sawa na kuishi kwa kudhani kwamba kupata marafiki 5000 Facebook inaonyesha una impact kubwa. Nilisema mwaka jana kuwa Ukurasa Facebook wa Mhe. January Makamba ulikuwa na Likes nyingi kuliko wa Mhe Magufuli. Lakini aliyepitishwa akawa JPM. Impact. Hata sasa Diamond Plutnumz ana watu wengi Fb kuliko Mohamed Dewji. Ni kweli kuwa ana impact zaidi ya MO? Au network ya diamond in life na ya MO vinafanana? Likes za Facebook siyo Network Yako halisi. Hao ni FANS tu. Wanaokubaliana na wewe kwa baadhi ya mambo tu kwa sababu zao. Network yako halisi ni nje ya mitandao hii. Watu wanajua ndoto zako na wanaweza kukupa mawazo yao wakati wowote. Unaoweza kuwauliza siri za mambo yao mfano mafanikio na wakakupa bila kukuficha.

So network yako ya kazini inaweza kuwa ya watu maarufu mno. Lakini kwa kuwa ni ya kutengenezwa huwezi kufikia Uhuru wa Kipato. Lazima utengeneze MWENYEWE network mpya!

Kuna watu network yake kwa sababu ni ya wafanyakazi wenzake wa BOT anadhani kwa kuwa ni BOT basi atafanikiwa kiuchumi based on that network only. Unapaswa kujenga uwezo wa kufahamiana na kukutana na watu wengi tofauti ujifunze vitu tofauti ambavyo ndo vitakusaidia kufikia malengo ya kuwa huru kifedha. Kuna watu hapa watasema "aaah kwani si hata hapa nakutana na wateja tofauti tofauti". Siongelei wateja. Nimesema hata gerezani kuna wageni wanaenda kila siku. Mi naongelea uwezo wa wewe kwa kuamua kwako kukutana na watu katika mazingira ya nje ya ofisi yako na kushare vitu kuhusu maisha nk wakati ambao unataka kukutana nao ili kujifunza vitu tofauti. Ni vigumu mwajiriwa labda wa Wizarani kunetwork na Waziri. Lakini ni rahisi kwa mtu asiye katika setup ya ajira kunetwork na waziri bila hata woga.

Waajiriwa wengi kwa kuwa ameshasocialize kazini kwake kwa masaa 9 au 10  akili imejaa mafaili na mawazo ya kazi za kesho hana muda wa kusocialize na watu wengine tena anahisi imetosha. Kumbe hajui Uhuru wa kiuchumi unakuja kwa mkusanyiko wa mambo mengi ikiwemo kuwa na watu kwenye network yako ambao either wako level hiyo au wamekaribia au angalau wanaelekea huko.

Wakati nimeajiriwa miaka 7 hivi iliyopita kulikuwa na program niliyokuwa nahudhuria kila Jumatano jioni saa 11 hadi saa mbili usiku yenye lengo la kukutana na watu wengine waajiriwa na wasio waajiriwa kubadilishana mawazo. Bwana Anthony Luvanda anaweza kuikumbuka pale HOLIDAY INN (sasa panaitwa SOUTHERN SUN). Kuna watu waliandaa hiyo program. Tulijengewa mazingira ya kufahamiana na watu wengi tofauti na kujifunza vitu tofauti. Lakini wenzetu wengi walikuwa hawaji kwa sababu "wamechoka" japo ilikuwa bure na chai/maziwa/kahawa/bites za bure kabisa. Siku moja bwana mmoja kutoka Uingereza akasema nchi za Asia watu wanatafuta sehemu kama hizo na wanalipa kiingilio kujifunza na kusocialize. Lakini akasema anashangaa huku ukiweka kiingilio watu waje kusocialize na kujifunza hawatakuja. Na hata ukiweka bure pia hawaji. Hasa waajiriwa.

Hili suala liliniingia sana kichwani. Na naweza kushuhudia kuwa idadi ya watu niliokutana nao kusocialize katika miaka yangu miwili ya ajira ni ndogo kuliko watu niliosocialize nao ndani ya miezi sita tu ya kwanza baada ya kutoka katika ajira. Nikitazama leo mambo ambayo nineshajifunza kwa watu mbali mbali waliofanikiwa maishani tayari ni mengi na makubwa na kuna wakati nawaza nisingekutana au kuwatafuta baadhi yao ningekuwa sijui vitu vingapi.

Siku hizi watu walioajiriwa pamoja wana magroup ya WhatsApp. Wanajadili essentially ishu zile zile. Social life ile ile inaendelea online. Network extension. Not expansion. Don't extend your network.
EXPAND it!

Kama umeajiriwa na ndoto yako siku moja uwe na Uhuru wa Kipato. Usiwe mtumwa wa kipato basi jitathmini kwanza wewe ni aina gani katika yale makundi matatu. Kisha acha kutegemea network ya waajiriwa wenzio. Be bold enough to expand your network. Ujifunze kwa wengine. Mazingira ya kuajiriwa yanakupa uwezo wa kuextend network yako tu. Kama tu simu zenye extension.. Network ni ile ile. To attain financial freedom you must FIRST expand your network.

This is a business school nakupa. Unaweza kuchagua kutilia maanani au kuignore.
It's your choice.

Leo niishie hapa.

Na kama ulisoma makala zangu hizi toka mwanzo utaanza kuona kuwa sababu zote nilizoandika kuanzia ile ya kwanza hadi hii ya 8 zinafanya kazi kinyume cha MWAJIRIWA. Ziunganishe utaelewa vizuri. Again..Don't read them in isolation.

Bado zingine 2 tu.
Endelea kuwa na mimi.

But kwa leo hicho ndiyo kikwazo cha 8 cha kumzuia mwajiriwa asifikie kamwe FINANCIAL FREEDOM. Kesho kwa neema ya Mungu nitaendelea na LIMITING FACTOR YA 9.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS, WhatsApp and Calls: +255752366511
WhatsApp Only: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com

Barikiwa Sana!

Semper Fidelis People,

Yes,

Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa