Ijumaa, 29 Septemba 2017

MAHALI SAHIHI PA KUANZIA BIASHARA

*MAHALI SAHIHI PA KUANZIA BIASHARA*

Katika maisha mafanikio huwa ni kitu cha watu wachache tu. Iwe kwenye: masomo, michezo, muziki, siasa, biashara, mahusiano nk. Ni wachache tu hufanikiwa. Hii ni kwa sababu mafanikio ni mchakato ambao watu wengi mno hawako tayari kuufata maana inahitaji NIDHAMU ya hali ya juu na BIDII ya kiwango cha juu pia. Na haya si maneno yangu tu bali hata watu waliofika mbali zaidi kama Mohamed Dewji wanasema hivyo.



Kama unasoma makala hii ikiwa tayari nilikutumia audio ya kukukaribisha katika mafunzo haya tulipoanza mazungumzo basi ndani ya ile audio nilieleza kuhusu aina za biashara zinazoweza kukusaidia kufika mbali. Mfano Real Estate, Platform Business, Service Oriented, Minerals Oil and Gas nk. Ya mwisho katika mlolongo wa kuzitaja nikasema ni INTELLECTUAL DISTRIBUTION. Na nikasema ndo biashara ambayo nimewashauri watu wengi sana hasa wanaolalamika kuhusu shida ya mitaji kuwa mikubwa kwamba nawashauri kuanza na hii kabla ya kwenda biashara zingine kama Real Estate na zingine nilizotaja. Tatizo watu wengi hawataki process. Wanataka wafanikiwe kufumba na kufumbua. Lakini naamini wewe unaamini katika process. Lakini hata kama sikukukaribisha kwa audio kilichomo kwenye hiyo audio fupi kilikuwa ndicho hicho yaani aina za biashara na story yangu mimi katika safari ya mafanikio.

Katika dunia ya leo wanaofanikiwa ni watu wanaojifunza njia MPYA za kufanya vitu.



So ngoja nitoe ufafanuzi kidogo wa hii biashara kisha utaamua mwenyewe kama unaona inakufaa pia au la. Mimi kazi yangu ni kukufundisha kwa kina (in details). Lakini maamuzi ya kusema uendelee kujifunza zaidi kwangu ni maamuzi yako. Japo najua ukiamua kuendelea tu kujifunza bila kuchoka utakuja kuelewa vitu vingi sana ambavyo wengi hawaelewi. So sasa ngoja nifafanue zaidi.


I. *INTELLECTUAL DISTRIBUTION NI NINI?*

Hii ni biashara ngeni kwenye masikio ya watu wengi. Hivyo ni biashara ambayo wengi inawapita. Na wengi wakisikia kuhusu hii biashara wanapata "ALLERGY" hasa kwa sababu jina maarufu linalotumika kuitambulisha hii biashara ni NETWORK MARKETING. Kutokana na kuwa ngeni hii biashara imeshindwa kueleweka vizuri kwa wengi na wengi kutoichukulia serious na kukosa fursa nzuri kweli kweli. Naamini wewe utapenda kujifunza vizuri.

Lakini niseme tu kuwa kama ilivyo katika biashara nyingine zote hii nayo SIYO RAHISI RAHISI tu. Hakuna jambo lenye faida ambalo huwa rahisi rahisi tu. Ila tu hii biashara haina complications kama biashara zingine.

*Sasa Intellectual Distribution (ama Network Marketing) ni nini?*

Huu ni mfumo au utaratibu wa kufikisha taarifa kuhusu jambo fulani ama huduma ama bidhaa kwa KUAMBIANA AMBIANA. Yani mimi nikwambie wewe kitu kisha nikwambie na wewe kawaambie wawili. Na ukiwaambia  unawapa maelekezo pia hivyo hivyo wao kila mmoja aambie watu wawili. Sasa kwa mtindo huu ujumbe ule utafika kwa watu wengi mno. Kama ambavyo tumeambizana kuhusu wapi wanauza simu nzuri au mabegi mazuri au wapi wanapika chakula kitamu sana.


Changamoto kubwa hapa ni kuwa ujumbe unaweza kufika mbali lakini ukawa umeshaongezwa chumvi au umeongezwa maji.


Lakini kama kutakuwa na utaratibu labda ujumbe uwe unapewa ukiwa umeandikwa na pia uwape wengine ukiwa umeandikwa kama ulivyoupokea basi hilo tatizo la kuongezwa chumvi au maji litakuwa halipo. Right?

Kwa sababu ya NGUVU ya habari kutembea kwa njia ya mdomo zaidi basi kuna makampuni yaliamua kuutumia utaratibu huu kwa MAJARIBIO kama njia ya kutangaza bidhaa zao. Yani mfano kampuni FULANI inakupa maelezo kuhusu bidhaa yao. Labda simu. Halafu wanakwambia ilivyo nzuri. Kisha wanakwambia nenda kawaambie watu wawili tu unaowajua. (Hii ndo inaitwa INTELLECTUAL DISTRIBUTION yaani unadistribute intellect). Na wao uwaambie hivyo hivyo. Kampuni zile zikaja kugundua kuwa zile habari zilifika mbali mno. Ambako hata watu hawana TV au hawasikilizi sana redio au kusoma magazeti.


Kampuni hizo zikaamua kuurasimisha mfumo huo. Ila sasa zikasema ukipeleka habari UNALIPWA kama uliyempa habari atakuja kwenye kampuni kununua ile bidhaa uliyomwambia. Kwa hiyo unachosambaza siyo kitu bali TAARIFA. Information. Sasa jiulize hivi huwezi kusambaza taarifa? Hujawahi kumwambia mtu kuhusu jambo fulani linapatikana wapi? I bet ulishawahi. So hapo hukuwa unauza hicho kitu bali ulikuwa unasambaza tu taarifa. Kama ulimwambia mtu kuwa simu nzuri zinapatikawa wapi hukuwa unasambaza simu ya mtu au hakuna aliyekuuliza kama siku hizi unauza simu. Wewe ulikuwa unasambaza tu TAARIFA.

Sasa unayemwambia pia anaweza naye kuwaambia wengine ambao wewe hata hawajui.  Ina maana anatumia muda WAKE kusambaza taarifa. Kwa hiyo sasa mmeanza kuwa wengi mnaosambaza hiyo taarifa. Hicho kitu ndo kinaitwa Intellectual Distribution. Au Network Marketing. Yaani MMEFANYA MARKETING ya kitu kwa network ya watu mnaowafahamu au kukutana nao. Ndipo neno NETWORK MARKETING lilipotokea. Naamini tupo pamoja. 

Dunia ya leo haipo tena kwenye MAPINDUZI YA VIWANDA (Industrial Revolution) yaani namna bidhaa zinavyozalishwa kwa wingi (in bulk) na haraka kwa sababu ya uwepo wa mashine na mitambo ya kisasa. Hapana. Huko dunia imeshatoka. Yaani kuzalisha vitu haraka na kwa wingi hilo siyo tatizo tena. Dunia sasa hivi ipo kwenye MAPINDUZI YA USAMBAZAJI (Distribution Revolution) yaani bidhaa zako zikishazalishwa ZITATUMIA njia gani KUSAMBAA kufikia watu wengi zaidi. Yaani TAARIFA kuhusu hivyo vitu vyako zitasambaa haraka au polepole. Hilo ndo litasababisha ufanikiwe kibiashara au la. Ukiwa na duka una vitu hapo dukani labda Sinza halafu taarifa za unachouza zinaishia Sinza tena mtaa ambako duka lako lipo ujue kufanikiwa kwako ni ngumu maana taarifa zimewafikia watu wachache. Maana saivi hatupo kwenye era ya kuzalisha vitu na kurundika ghalani au dukani bali KUSAMBAZA TAARIFA kwenda mbali na wewe ulipo ndo kinaleta mafanikio. Hii ndo elimu mpya lakini wengine wameshaitumia tayari.

Kufanya mambo kwa namna tofauti.



So ndo maana unaona Facebook imeanza miaka michache tu iliyopita lakini mmiliki wake leo ni tajiri mkubwa kabisa duniani.

Fikiria huyu ameanzisha Facebook mwaka 2014 tu wakati huo watu tayari wakiwa ni matajiri leo keshawapita. Hapa ndipo ilipo ELIMU. 

Ni kwamba yeye hahangaiki kuzalisha chochote. Hazalishi habari yoyote tunazalisha sisi wenyewe. Tuna edit wenyewe. Tunapost wenyewe bure.  Yeye amekaa katikati kutusaidia KUSAMBAZA taarifa tu. So taarifa zinasambaa kutoka Mbagala au Upanga au Mbezi Beach kwenye simu yako au yangu na kufika SONGEA au KENYA au CHINA au RUSSIA dakika hiyo hiyo. Usambazaji wa taarifa kwa sasa ndiyo kipindi chake. 
Ndo tunaita DISTRIBUTION REVOLUTION.

So kwa sasa si lazima sana wewe kuwaza uzalishe nini. Acha wengine wazalishe. Wewe angalia je walichozalisha ninaweza kusaidia kusambaza taarifa za hicho kitu na nikatengeneza pesa? Hiyo ndo tunaita INTELLECTUAL DISTRIBUTION ama wengine wanaita RECOMMENDATION BUSINESS. Ama NETWORK MARKETING BUSINESS.

Lakini ukilazimisha tu uwe na duka utakuwa hujaelewa vizuri kipindi gani tupo. Angalia kuna maduka yapo mtaani toka mwaka 1998 hadi sasa lipo mtaa huo huo halijapanuka likawa Supermarket. Aliyeliyelianzisha anakufa wanarithi watoto (kuzazi cha pili) lakini bado halijapanuka kuwa na matawi sehemu tofauti. Why? Kwa sababu tu duka hilo taarifa zake hazifiki mbali ambako ndo kuna wateja wengi zaidi kuliko watu wanaoishi mtaa ule. Na bado Tanroads hawajapita kuvunja ili kupanua barabara. 

Lakini Facebook utamvunjia nini na wakati hana duka? Utamkatia umeme upi. Utamlipisha kodi ipi? See?

Tuendelee. Usichoke. Jifunze tu. Mara nyingi elimu kubwa utaipata kwa kujifunza kusoma vitu virefu. 



II. *FAIDA ZA INTELLECTUAL DISTRIBUTION*


Kwa kawaida watu wengi wanatamani kumiliki biashara lakini hawajui basics yani vitu vya muhimu katika biashara ambavyo ni hivi vifuatavyo:


1. UBORA WA BIDHAA. 
Yaani bidhaa yako tukiiweka pamoja na bidhaa ya GSM zinaweza kushindana kwa ubora?

Usitake kuwa kama Dewji au GSM anyhow tu. Lazima ujifunze ukweli wa mambo.


2. MARKETING STRATEGY
Namna gani watu wengi watapata habari kuhusu hizo bidhaa zako. Utatangaza kwenye TV au utatenga bajeti ya kuweka mabango barabarani na mitaani nchi nzima mitaa yote. Au utatumia njia kama waliyotumia Facebook tu hawana Bango wala tangazo na bado Facebook inajulikana zaidi kuliko brand kama VODAFONE.

Tarehe 27 June 2017 Facebook walitangaza kuwa walikuwa na members (users) bilioni 2 wanaopost na kucomment nk kwa mwezi. Imagine. Lakini ulishawahi kuona tangazo la Facebook kwenye TV eti ili ijulikane kwa watu waje kujiunga?  No. Njia gani inatumika ili watu waijue Facebook?

Simple: *WATU NDO WANAANBIANA*. Hata wewe uliambiwa na mtu. Instagram vile vile. Na sasa THREADS. Hiyo ndo inaitwa *RECOMMENDATION BUSINESS* na hii ni rahisi hata wewe unaweza.

Unaweza kufanya ana kwa ana



Ama unaweza kufikisha hizo recommendations zako kupitia njia ya kisasa zaidi ambayo wengi wanaita SOCIAL MEDIA kama mimi nilivyofanya kukupa taarifa kupitia Social Media. Unaweza kuzitumia kufanya hii recommendation business au Intellectual Distribution.


3. DISTRIBUTION MODEL
Mfumo gani mwepesi wa kuutumia kuwafikishia bidhaa mahali walipo siyo mpaka waje ulipo. Yaani wanunuzi wako watatoka mahali unapoishi wewe au waweza hata kutoka mabara mengine? Unafanyaje ili kitu chako wateja wengi wawe si majirani zako. Hili watu wengi hawajui wafanyeje. Ulishawahi kujiuliza kwa nini hakuna tajiri mwenye kutumia duka mtaani kwake kuuza vitu vyake. Maana duka mtaani ni biashara inayohudumia watu wachache tu wanaoweza kufika duka lilipo. Hakuna tajiri mwenye duka eti anauza unga na sukari vya kupima na viberiti na dawa ya mbu na OMO na wembe. Ingawa akiamua kufungua hayo maduja anaweza kuyaweka kila mtaa. Swali ni kwa nini hawafanyi hivyo eti? Kuna sababu. Na sababu ni kuwa ni watu wachache wataweza kufika duka lilipo hivyo huyo tajiri atalazimika labda afungue duka kila mtaa. Kibiashara inakuwa kipoteza pesa kwani kuset up biashara ya duka inahitaji mtaji mkubwa.

Watu wengi wameanza biashara huko mtaani bila kuangalia hayo mambo matatu na wameishia njiani. Nadhani unaelewa ilivyo muhimu kuyachukulia serious hayo mambo matatu. Hii ni elimu ya biashara ambayo huwezi kuipata kwenye Degree au Masters ya Biashara. Inatokana na practical experience yangu.


Sasa sisi tunafundisha biashara siyo kwa nadharia. Bali practical. Maana hizo za maduka tumefanya pia tena kwa mitaji mikubwa. Tukajifunza na kujua kumbe kuna njia nyingine. Na tunakuonyesha biashara ambayo inatumia system inayoweza kumfanya mtu wa kawaida kabisa akaweza kuwa mfanyabiashara mkubwa mno au hata kuwa mwekezaji na hayo mambo matatu yote akawa ameya-cover bila shida. Yaani akawa anajihusisha na biashara ambayo:


1. Ina bidhaa bora sana tayari. Kwa hiyo anaposambaza taarifa hana wasiwasi na ubora wa kitu anachosema. Kumbuka nimesema dunia ya leo siyo lazima wewe uzalishe kitu. Acha wazalishe wengine wewe angalia ufanyeje ufaidike na uzalishaji wa wengine. Mpaka hapo unakuwa umepunguza ukubwa wa mtaji wa kuanzia.


2. Mfumo mwepesi wa kufikisha taarifa  (njia ya watu kuambiana tu.)


3. Njia nyepesi ya watu kupata hizo bidhaa endapo wako mbali na wewe ulipo. Yani kama ambavyo Azam Cola inauzwa mbali kabisa na hapa Dar es Salaam ambapo ndo Bakhresa anaishi.


Na uzuri ni kuwa mtaji wa kuanzia biashara aina hii yaani hii INTELLECTUAL DISTRIBUTION ni mdogo sana sana ukilinganisha na biashara zingine. Pia hapa mtu atapata mafunzo mengi mno. Hebu fikiria tu ni mambo mangapi umejifunza toka umenifahamu kwa muda huu mfupi. Na hii haijalishi kama utaamua kufanya biashara na sisi au la. Hii elimu itabaki kuwa ya kwako vile vile.

But nataka ni mambo mangapi utajifunza kama ukiwa katika mikono ya watu aina yangu kila siku kwa miezi sita tu? 

Sasa naomba utazame video links nilizokuwekea hapo chini zinaelezea biashara hiyo ninayokwambia ambayo binafsi nimewashauri vijana wengi kuifanya na nimeona wakianza kupiga hatua kuelekea katika mafanikio yao. Of course mimi mwenyewe nafanya na imebadilisha maisha yangu sana! 

Kumbuka jambo hili. Kuna makundi manne ya watu duniani:

1. Wenye muda mwingi ila hawana hela.

2. Wenye hela nyingi ila hawana muda kabisa hawana hata muda na familia ni kazi tu hata makochi yake nyumbani yanakaliwa na housegirl tu.

3. Wasio na muda wala pesa (hawa wanaitwa busy for "nothing". Anahangaika kila siku na kazi ambazo haziwezi kumfanikisha kwa kujidanganya kuwa one day yes. Kumbe hajui ili ufanikiwe kuna vitu inabidi uache. Ikiwezekana hata aina ya vitu unavyofanya inabidi uache uwe tayari kufundishika na kuanza moja toka zero. Wengi hawako tayari. Maskini ni mtu ambaye anafanya kitu hata miaka 10 hapigi hatua ya maana analalamika tu ila hayuko tayari kujifunza vitu vipya au kusikiliza mawazo ya waliokuwa kama yeye zamani ila sasa wamepiga hatua.

4. Na kundi la mwisho ni wale wenye muda mwingi na pesa nyingi ambao hawa ndo watu waliofanikiwa wanaweza nunua chochote popote wakati wowote na wanaweza kwenda popote wakati wowote siyo lazima wasubiri likizo.

 SIJUI WEWE UPO KUNDI LIPI KATIKA HAYO MANNE?

Ji challenge ujijibu kwa DHATI wewe upo kundi lipi katika hayo.

And one more important thing ni kuwa *Intellectual Distribution* ni biashara ambayo inakupa kitu kinachoitwa *LEVERAGE* yaani uwezo wa kujigawa wewe ukawa kama vile uko kila mahali. Kwa hiyo unaweza kukuta unapata pesa na muda unao pia. Watu wengi wamekuwa wakii-miss hii concept na hivyo kutoelewa vizuri namna hii biashara ilivyo na manufaa makubwa sana kupitia hiyo LEVERAGE hasa kwa mtu wa kawaida. 

Yaani uwezo wa wewe kunufaika kupitia muda wa uzalishaji wa watu wengine. Na mfumo unakufavour sababu ni *Recommendation Business*. 

Again usichoke kujifunza vitu vipya. Mshauri wa Uchumi wa maraisi wawili wa Marekani Profesa Paul Zane Pilzer anasema mafanikio au utajiri upo mikononi mwa wale wanaojifunza vitu vipya HARAKA.


Lakini pia tunawafundisha vijana kuwa itakusaidia kuongeza mkondo mwingine wa kipato tofauti na kipato ulichonacho kwa sasa kama unacho kipato tayari ila tu hakitoshi.

Hii ni muhimu kwa sababu matajiri wote wana njia nyingi za vipato. Forbes wanasema Average Millionaire ana njia saba tofauti za kuingiza pesa. Maskini wana njia hasa moja tu, utakuta hasa mshahara au ana duka halafu basi.


Angalia mtu kama Bakhressa ana vyanzo vingapi vya mapato. Hayati mzee Mengi, alikuwa na  mahoteli nje ya nchi, mashamba, biashara za madini, media house (TV channels, redio stations na magazeti), na HISA kwenye viwanda vya CocaCola hapa Dar (Coca-Cola Kwanza) na Moshi (Bonite Bottlers), alikuwa na viwanda vya kuzalisha bidhaa kama sabuni nk, na vitu vingine vingi. Huko kote alikuwa anapata mapato. Ndivyo walivyo matajiri wengi.

Mtu kama huyu mwenye vyanzo vingi vya mapato huwezi kumlinganisha na mwajiriwa anayesubiri mshahara eti au mtu aliyejiajiri tu ana duka lake mahali fulani pesa zinatoka hapo tu. Kuna tofauti kubwa sana. Nayasema haya kwa nia njema kabisa. Na si kuwazodoa watu. Ni kukumbushana tu. 

Sasa hiyo video link  ninayokutumia inaelezea biashara ambayo unaweza kuifanya popote na biashara hiyo inaweza kukupa VYANZO VINGI VYA MAPATO PIA kwa kutumia huu mfumo wa intellectual distribution yaani recommendation. Nimesema Facebook inatumia recommendation lakini hakuna anayelipwa kwa kurecommend kwa mwenzake. 

Lakini sisi katika biashara hii utalipwa kwa kurecommend kwa mwingine. Naamini unaweza kufanya hayo yote ukiwa nyumbani kwako. Ndiyo dunia mpya ya leo hii si lazima ukakodi duka mahali ulipe kodi wakati unaweza kufanyia kazi nyumbani kwako.



Naamini mpaka hapo tuko pamoja.


So kama ulinifatilia kwa umakini toka mwanzo mpaka sasa basi utaelewa mara dufu hizi video. Nimeweka link kwa lugha ya KISWAHILI na nyingine kwa LUGHA ya kiingereza. Utachagua. Ukipenda kufanya nasi karibu sana kuwasiliana nami kwa WhatsApp number +255 788 366 511.

Karibu kutazama video. Video hizi ni za zamani kidogo hivyo mafanikio kwa sasa ni makubwa mno. Nilipost hizi video hapa nilipoolipost makala hii kwa mara ya kwanza mwaka 2017. 

Nachokifanya ni kuedit tu kidogo. Mfano wakati napost mzee Mengi alikuwa hai bado. Lakini hapo juu utsona nimemwita "hayati" maana yake nimesha edit. 

Karibu kutazama video hizi..


1. SWAHILI (testimony)...

Play Video




2. ENGLISH (Official Presentation)...

Play Video



Karibu sana ukishaziangalia hizo video niambie kama upo interested kuanza ili nikueleleze unaanzaje.


Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
WhatsApp +255 788 366 511

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni