Alhamisi, 24 Novemba 2016

TAKING ACTION: THE BIGGEST SIGN THAT YOU WILL BECOME SUCCESSFUL KUCHUKUA HATUA: DALILI KUU YA KUWA UTAKUWA MTU WA MAFANIKIO


Wakati wa mwanzo kabisa wa huduma (ministry) ya Yesu Kristo hapa duniani kuna watu walikuwa wa kwanza kwanza kufanikiwa kujua (ku-taste) ukuu wake kwa namna ya pekee sana. 

Lakini wote hao mpaka kufikia kuexperience jambo hilo walichukua HATUA fulani ya mwanzo ya kumfata. Ambayo huenda ingeonekana ndogo mno wakati wanaichukua KUMBE ndo ikawa hatua muhimu kupita kiasi!

Kila mmoja kati yao alienda kwa Yesu kwa style tofauti. Kuna aliowaita mwenyewe. Na kuna waliomfata wenyewe. Na katika hao wote kuna waliomfuata au kumjia wakiwa bado hawajui vizuri wanachotaka kwake. 
Kuna waliomfata kwa sababu wamealikwa tu na watu waliowaamini. 
Na kuna waliomfata wakiwa na mashaka wanataka labda tu wakathibitishe mashaka yao.

Lakini point yangu hapa ni kwamba WALICHUKUA HATUA!

Ngoja nitoe mifano kidogo:


Mfano wa Kwanza:

Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji.

Kuna wanafunzi wa Yohana Mbatizaji walikuwa na mwalimu wao one day yani huyo Mbatizaji. Wakasikia anamwongelea Yesu kuwa ndo "dili lenyewe yani". Yani kwamba ndo kitu TRENDING. Maana alianza kusema siku moja: "TAZAMA MWANA-KONDOO WA MUNGU, AICHUKUAYE DHAMBI YA ULIMWENGU...." Wanafunzi wake waka-note. Lakini hawakuchukua hatua yoyote. Ndivyo ilivyo sometimes. 
Kesho yake tena akiwa yuko na wawili kati ya wanafunzi wake Yesu akapita zake Yohana alipomwona akarudia tena "TAZAMA, MWANA-KONDOO WA MUNGU!" So hao wawili wakam-UNFOLLOW Yohana Mbatizaji rasmi wakamfata Yesu. Na Yesu akawaona akawauliza wanataka nini kwake jamaa nao wakamuuliza tu "UNAKAA WAPI?". Hahaaaa...Kama bongo hapa ukiuliza swali unajibiwa na swali. Hii kumbe imeanza zamani. Akawaambia tu "COME AND SEE". Note this... Hao wawili walienda na kukaa na Yesu kwa masaa machache tu and it changed their lives completely.
Lakini yote ilianzia na wao kuchukua hatua.
Kumbuka kuna wanafunzi walibaki kwa Yohana maisha yao yote mpaka anakatwa kichwa!
They never took action kumfata Yesu kamwe.
Only TWO did.

Sikia ndugu yangu, mafanikio siyo suala la 'wenzako' wanasemaje bali WEWE unaonaje. Usipoangalia utabaki na watu ambao wanakoenda ni dead-end. Yes dead-end kwa sababu mission ya Yohana Mbatizaji iliisha Yesu alipoanza kazi but hata Yohana Mbatizaji hakutambua bado aliendelea na kazi akiwa na matarajio mengine. Maana kuna siku akawatuma tena hao wanafunzi wake. Hebu kamuulizeni hivi ndo yeye mwanakondoo kweli au tusubiri mwingine? Funny. Wakapewa nao majibu mazuri na Yesu wakayaleta kwa Yohana Mbatizaji. Na ajabu wanafunzi wale wale waliendelea kumfata Yohana huyo huyo badala ya kumfata Yesu. Licha ya kuona mambo amazing aliyofanya Yesu na licha ya kuwa Yesu alishatambulishwa kwao na Yohana Mbatizaji siku nyingi!

Nazidi kukuonyesha kuwa usifate watu tu kwa kuwa ni wengi. No. Think for yourself. Ni wanafunzi wawili tu kati ya wanafunzi wa Yohana ambao walimfata Yesu!
Only two.
Tena hawakuwa na hakika kivile. Lakini walipomfata Yesu. Kwa maana ya kuwa "FOLLOWERS" kabisa basi masaa machache tu ya kukaa naye yalitosha sana kuthibitisha kuwa walifanya the decision of their lifetime!

Mafanikio ni ya wachache.
Na ni personal issue. 
Avoid group thinking. 


Mfano wa Pili: 

Hapa tunauona kwa  SIMONI (PETRO). 
Sasa kati ya wanafunzi wale wawili wa Yohana waliomfata Yesu mmoja alikuwa ni ndugu ya Simoni. Anaitwa Andrea. Alipotoka tu kwa Yesu stop ya kwanza ilikuwa kwa ndugu yake. Akamwambia Broooo! "TUMEMWONA MASIHI (KRISTO)". So kitendo bila kuchelewa akampeleka Simoni kwa Yesu. Kumbe Simoni kuchukua ile action ya kwenda kwa Yesu ilikuwa very muhimu. Maana ile kafika tu kwa Yesu akakutana na surprise ya kupewa jina jipya linaloendana na destiny yake. Bonge la surprise. Well, surprise hasa siyo kupewa jina jipya per se. Surprise ni kuwa Simoni alikuwa ameishi miaka yote duniani bila mafanikio kumbe moja ya limiting factor kwake kufikia mafanikio ilikuwa JINA. Yesu akamwambia from now utaitwa KEFA (au tafsiri yake tuliyozoea sisi, PETRO, yani Jiwe)!! Duh. 
Mafanikio makubwa ya Petro yalianzia kwenye kubadilishwa jina.
Lakini KWANZA alichukua hatua kwenda kwa huyo Yesu mwenyewe!
Action.
Ni neno dogo sana. Lakini limefanya wengi kubaki duni na kutoishi destiny zao sababu kuna mahali hawakuchukua hatua stahiki.

Unaweza kuwa unatafuta mafanikio and your purpose in life bila kujua kipi kinakulimit, mpaka siku uchukue hatua fulani ndogo tu. 
Labda kwenda mahali. 
Labda kusoma kitabu fulani. 
Labda kuhudhuria semina au mafunzo fulani. 
Labda kukutana na mtu fulani. 
Labda kwenda mji fulani, etc. na huo ukawa mwanzo wa safari yako ya mafanikio.

Petro angekataa kwenda kwa huyo Yesu ingekuwaje? Huenda angevua samaki mpaka siku anakufa na asingefikia mafanikio. Maana destiny yake ilikuwa imefichwa katika kazi ya kuhubiri na kusimama imara katika kanisa la kwanza nk. Siyo kuanzisha soko kubwa la samaki wakavu na dagaa mchele.

A very small, even sometimes seemingly insignificant action, inaweza kubadili maisha yako completely.
Muulize Petro.


Mfano wa Tatu:

Mwingine ni NATHANAELI. 
Huyu jamaa alikuwa mtu mmoja mwenye roho nzuri mno. Ana pure intentions katika mambo yake yote. Mtu safi. Siku moja akakutana na mtu fulani wanafahamiana. Anaitwa Filipo! Ebana Nathanaeli mambo vipi? Poa. Afu huyu Filipo anamwambia Nathanaeli... Ebanaee sikia "TUMEMWONA YEYE ALIYEANDIKIWA NA MUSA KATIKA TORATI, NA (aliyeandikiwa pia na) MANABII, YESU, MWANA WA YUSUFU, MTU WA NAZARETI". Nathanaeli akasema We Filipo, acha hizo, toka lini Nazareti kukatoka jambo jema lolote. Let alone unaongelea jambo kubwa kama hili?

Ndo maisha yalivyo. Ukimpa mtu habari yoyote unayoona nzuri kwake usishangae akawa wa kwanza kukujaza wewe tena DOUBTS. Unaweza kuta unadeal na mtu ambaye ndivyo mindset yake ilivyo. Labda umetoka Sumbawanga juzi juzi na umeona huko fursa moja muhimu mno na umeamua kumshirikisha pia. Usishangae akaanza kukuhubiri wewe na kukuuliza: "Toka lini Sumbawanga kukatoka......? We unapajua Sumbawanga vizuri? Usikute hicho ulichoona kiini macho tu? Sumbawanga si mchezo?" See? Usipokuwa makini wewe mwenyewe unapotezea kabisa. Hahaaa poor you. Umesahau ndivyo watu walivyo. So usitetereke. Filipo hakutetereka. Watu wako hivyo always. Umemshirikisha kuna jambo zuri Tanga atakwambia: Toka lini Tanga kukawa na..... Hayo ndo maswali ya wanadamu: Toka lini wazaramo wakapata.....? Toka lini? Chaweza kitu chema kutokea Mkuranga??
Zoea tu hayo maswali.

Ni kawaida ya watu kuuliza. Hata kama wana moyo mzuri ama nia njema kama Nathanaeli. Mashaka ni sehemu ya ubinadamu. Na nilichojifunza mpaka sasa ni kuwa mashaka ni sehemu ya fursa ya kumfunza mtu. So usikasirike mtu akikuonea shaka. Ni opportunity tu ya wewe kumwondoa shaka. Ndicho Yesu alichofanya.

So Nathanaeli akawa na shaka na ujumbe wa Filipo. "LAWEZA NENO JEMA KUTOKA NAZARETI?" Filipo akamwambia Nathanaeli "NJOO UONE". Powerful.

Nathanaeli alipokuja akakutana pia na surprise.

Kwamba kumbe Yesu alikuwa anajua everything kuhusu maisha yake. Maana alipokaribia tu Jesus was like, waooh, now huyu ndo muisraeli pure asiye na ila ndani yake. Which was true. But kumbe mafanikio ya Nathanaeli pia yalitegemea mno yeye aanze kuishi BILA MASHAKA MASHAKA. And moja wapo ya vitu muhimu nilivyojifunza kwa Yesu ni His INCREDIBLE ABILITY TO ELIMINATE DOUBT! Coz Nathanaeli akashangaa. Huyu mtu ndo tunaonana kwa mara ya kwanza amenijuaje? So ikabidi aulize. Aisee " UMEPATAJE KUNITAMBUA (kwamba ninaishi bila ila in my life?". Yesu akatoa jibu lililozidisha BELIEF ya Nathanaeli. Akasema like, usishangae nimejuaje kuwa unaishi bila ila, najua vingi tu, mfano mimi nilikuona kabla hata hujakutana na Filipo kuna wakati ulikuwa umekaa chini ya mti fulani hivi (Yesu aliutaja jina kabisa mti wenyewe: fig tree. Mtini). Daaah! Nathanaeli alikuja na doubts lakini mwisho akaondokewa na mindset iliyojaa doubts. Na ukawa mwanzo mpya kuelekea destiny yake.


But what if angekataa kutake action kwenda na Filipo? You see my point? Angeweza kuishi vizuri bila ila, bila kusema uongo wala kumfanyia mtu jambo baya na mwisho asingefanikiwa kuishi destiny yake kwa kuwa mafanikio kufikia destiny yake yalikuwa yamefichwa kwenye yeye kuishi pasipo mashaka mashaka maishani mwake. Alikuwa vizuri kimaadili nk lakini mind yake imejaa doubts. It means hakuna na imani. Biblia inasema bila ya imani HAIWEZEKANI kumpendeza Mungu. Can you imagine. Kuishi na mashaka mashaka ni binge moja la limiting factor kwa wengi. That's why ni muhimu kufind out the truth. Kweli tu ndo itakuweka HURU. Kumbe kuishi na mashaka kuhusu vitu ni UTUMWA.

Nathanaeli alipotake action tu kila kitu kikabadilika!

Action..
Unamkumbuka yule kijana tajiri? Yesu alimwambia KAUZE KILA KITU KISHA UJE.

Action ikawa ngumu.
Action.

Siyo rahisi. But ndo kila kitu. 

Ndiyo maana watu wanatangaza semina za dini, makongamano, mikesha, mikutano ya biashara na ujasiriamali, umuhimu wa kujisomea vitabu. Everyday! 



Lakini wewe unaignore tu. You don't take ANY action. Unascroll tu. Na kwa kuwa msiochukua hatua mko wengi unajifariji. Unadhani ili kitu kiwe dili lazima kila mtu akifate. Unasahau wanafunzi wengi zaidi wa Yohana walishindwa kutake action mpaka wakafika DEAD-END!
Be careful my friend. 
Be careful.

Sisi tutaendelea kusema tu maana tunajua kwa nini tunasema soma vitabu. Tumesoma na tumeona namna vimetusaidia. Tunajua why tunakwambia hudhuria seminars. Kajifunze ujasiriamali using'ang'ane na ajira. But you're not taking ANY action. Wewe endelea kujifariji kwa kuwa mko wengi. Ukifika DEAD-END utakumbuka. Sisi hatutaacha hata kama hakuna anayeamini tusemacho. Yesu mwenywe yaliwahi kumkuta na akamwambia Nikodemo: SISI TUNASEMA TUNALOLIJUA NA TUNASHUHUDIA TULILOLIONA LAKINI NYINYI HAMKUBALI..!! (Yohana 3:11)

Na hata Isaya, nabii yule wa kale, aliwahi kuuliza: UNADHANI KUNA MTU AMESADIKI HABARI TULIYOILETA? 
(Isaya 53:1)

So my friend habari niliyoileta Leo ndo hii:

LEARN TO TAKE ACTION.


Usiangalie wenzako.  Usiangalie bosi wako.
Sometimes hata mzazi huangalii kama atakuwa kikwazo kufikia destiny yako. Aliumbwa kukuongoza siyo kuzuia destiny yako na kukupangia ya kwake yeye. 

Usije ukashindwa kufikia mafanikio ukakosa mafanikio kumbe kisa kuna kitabu kimoja tu hukusoma ndani yake kulikuwa na chapter ina ujumbe wako!
Au kwa sababu kuna mtu mmoja tu hukukutana naye angeongea na wewe dakika 10 na maisha yako yangebadilika!
Au kuna clip fupi au audio au message kama hii uliona NDEFU wakati ingekuwa inaongelea Wema Sepetu ungeona mbona story umekuwa fupi?? Hahaaaa. Poor you. 
Be careful.

Learn the science and art of TAKING ACTION.
Waliofanikiwa wote walijifunza kwanza umuhimu wa KUTAKE ACTION.


Have a great day.

Kwa mawasiliano zaidi
WhatsApp Only: #o788366511
Sms+Calls        : #o752366511
Instagram         :@andremuhozya

Kujifunza zaidi nenda:
www.andreamuhozya.blogspot.com


Love you lots!


Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam Tanzania
East Africa.

Alhamisi, 17 Novemba 2016

DO YOU BELONG TO THE "SOFT GENERATION"? THEN FORGET ABOUT SUCCESS. (KAMA U KATI YA WATU WA KIZAZI LAINI-LAINI BASI SAHAU KUHUSU MAFANIKIO)


Toka kuumbwa kwa dunia kumekuweko watu waliofanikiwa na watu wasiofanikiwa. Kumekuweko kizazi cha watu wachache jasiri na wenye uthubutu wa kweli na kizazi cha watu wengi laini-laini ambao kwao mambo yanapaswa yatokee tu kama wanavyotaka bila wao kuyaleta. Kumekuwako kizazi cha watu wachache waliotaka kujua ukweli hasa wa mambo upoje licha ya "uhalisia" unaohubiriwa, na kumekuweko kizazi cha watu wanaosema "hali iko hivi" (yani uhalisia uko hivi) na hauwezi kubadilika mpaka mtu au watu fulani waibadili. Kumekuwako watu wanaosema "Wazazi wangu wange....basi ningefanikiwa. Au Serikali iki...... nitafanikiwa. Bosi wangu akiniongeza mshahara....nitafanikiwa. Nikipata mkopo nitafanikiwa kufanya hivi na vile. Nikilipwa na wateja wangu mapema nitafanikisha hili. Au anasema: Mimi  ningeshaanzisha saluni yangu lakini... Ama: Aisee ninataka kuwa mwanamuziki mkubwa lakini....

See? Kizazi chenye "ifs-and-buts". Kizazi chenye litania ya sababu kwa nini mafanikio ni magumu kwao. Hii ndo soft generation ninayoiongelea.

Kama umebahatika kusikia ndoto za watu wengi hapa duniani unaweza kushangaa jinsi watu walivyo na ndoto kubwa ambazo zinaweza kumaliza matatizo mengi tuliyonayo. Na yumkini wewe pia una "mandoto" ya kufa mtu. Yani ukiangalia ndoto zako daah unajisemea aisee "one day ntakuwa balaa". But jiulize swali moja tu: DO YOU BELONG TO THE SOFT GENERATION?
Kama ndivyo then sahau kufanikiwa!

Success is not for soft people. Are you hearing me?
Mafanikio hayakuumbiwa watu soft-soft. Mafanikio siyo kitu kinachokuja kama upepo tu from nowhere. Mafanikio ni kitu unachopaswa #kukitafuta na kukiendea na mpaka ukipate you've got to be #TOUGH first.

Usifikiri ni swala la kuomba Mungu tu. Unaweza kupiga magoti kuomba mpaka magoti yapate "sigda" na usifanikiwe kama wewe upo katika kundi la soft generation. Nimestudy watu waliofanikiwa na bado naendelea kuwastudy wengi zaidi and naweza kukwambia wote niliowastudy hadi sasa ni watu TOUGH. Imara. Wasiolialia wala kulalamikia hali ya maisha wala kuongelea "uhalisia". Watu kama Jack Ma, watu kama Nelson Mandela, watu kama Mohamed Dewji watu kama Jim Rohn watu kama Margareth Thatcher watu kama Abraham Lincoln watu kama Aliko Dangote. Hawa ni watu tough! Angalia toka enzi na enzi, hivi baba yetu wa imani mzee Abraham alikuwa soft soft? Musa je? Mtu anaweza kufunga siku 40 usiku na mchana na akarudia tena hilo zoezi mara ya pili akiwa ni mtu soft soft? Wewe ukifunga siku mbili unaanza kusikilizia tumbo na kichwa. Coz you're soft. Hivi Christopher Columbus alikuwa soft soft? Hivi kweli mwalimu Nyerere alikuwa soft soft? TOUGH people.
Watu wanaofanikiwa huwa hawana kawaida ya kuishi kwenye eti uhalisia. And let me tell you my friend. "Uhalisia" ni kitu BINAFSI. Unaweza kuwa katika watu wanaosema maisha ni magumu but kwako uhalisia ukawa tofauti. Unaweza kuwa kati ya watu wenye furaha na amani na ukawa anxious and perplexed. Na unaweza kuwa kati ya watu wasio na furaha na wanaolalamika na ukawa positive and happy. But you've got to be a tough person first. Lazima uachane na tabia za kitotototo za kulialia. Usifikiri Mungu anabadilisha formula zake kwa sababu ya kulalamika kwako wiki nzima afu weekend unaenda kumwimbia nyimbo za slow motion. In fact ukizidi kulalamika Mungu anafika mahali anachukia na anaweza kukufuta kabisa. Maana your mind inakuwa imeanza kupoteza uwezo iliyoumbiwa wa kuwa creative na kuwa positive. Kumbuka kuna KIZAZI cha taifa fulani Mungu aliwahi kuzuia kisifikie kilele cha mafanikio kabisa sababu ya kulalamika. Kawatoa utumwani wanalalamika. Kawavusha bahari ile kuwa test kidogo tu wanalalamika. Kawajaribu tena kuona kama wanamwamini zaidi wanazidi kulalamika tu. Kakaa kimya na kiongozi wao mwezi mmoja na siku 10 tu wakaanza mchakato wa kupata "mungu" mpya! Khaa. Kwa kuwa Mungu  HANAGA kawaida ya kushindana na wanadamu akazuia tu hawa hawaingii Canaan aisee never bora waingie watoto wao kuliko hawa. Kulalamika. Hiyo ndo effect ya complaining and whining. Na kukasirikakasirika tu usipopata unachotaka - Being crybabies!
Yani usipopata unachotaka badala ya kuwa creative unatafuta wa kulaumu huku umekasirika. Mungu ataku-mind sana yani.

Tuna wimbi kubwa la soft generation people siku za leo.  #Whiners and #crybabies! Watu wanaolialia tu. Ooh nimeomba nauli sijapewa sasa mi ntaendaje shule. Oh nilitaka kuja ila mvua ikanyesha sasa ningefanyaje? Khaaa!
You are such a soft person my friend! Oh  "Nimeapply kazi sijaitwa yani serikali hii imezuia ajira sijui tutaishije nchi hii mi nachukia sana".
You're a Crybaby! Mtaishije wewe na nani kwanza?

Ooh, "Tumemaliza JKT hakuna ajira mtupe ajira tusije kuwa majambazi kwa nini hamtupi ajira".

Crybabies! Huko JKT mlienda kujifunza kuandika CV za kazi kwani?

Ooh ninataka kujiajiri lakini sina mtaji serikali yenyewe haijaleta viwanda walitudanganya tu!
Crybaby wewe!

Juzi niliongelea hilo la mtaji kwa mfano. Kwamba ukihitaji mtaji inabidi uwe na a very consuming idea kwanza kichwani. Naamini uliisoma hiyo makala. If not utapoteza muda kutafuta mtaji na hutaupata. Kuna formula za kufanikiwa. Usijiendee tu. Unakuwa tu mtu wa kulialia tu.
Halafu unasubiri pia uje ufanikiwe! Kweli?

Oh mi natamani kuwa mbunge lakini huko mpaka umjue MTU.
Are you serious? You simply don't really know what you want.
Soft generation!

Oh mi ninataka sana kusaidia yatima lakini sina uwezo! Usitudanganye unataka kusaidia yatima wewe. Kwa nini usiende kuwasaidia kupiga deki? Who told you kuwa msaada ni hela tu? Why usijitolee kwenda kuwafundisha tuition au kuwafundisha muziki au kucheza nao tu, kwani huo si ni msaada wa kisaikolojia mzuri zaidi kuliko kwenda kuwapelekea biskuti na peremende na kupiga nao picha ili ukapost Instagram!?

Kawaombe kupiga deki weekend uone kama watakataa. Hapo unaanza kujihurumia na kuhesabu gharama. Coz you are so sooooft. Yani kila kitu ooh mimi, unajua, yani hii hali, yani uchumi.. Soft generation.

Wengine huwa wananambia unajua kaka wewe hujui tu. Listen, najua sana. What I'm trying to tell you here is usipoacha kuwa "a whiner na crybaby" basi utafika mwisho wa maisha yako unalalamika tu na kukasirika huna kitu cha maana umefanya duniani hapa. Ukiambiwa jisomee vitabu ooh unajua mimi, muda, nachoka sana, narudi usiku sana.
Soooft generation!
Unajihurumia.
You don't want to sacrifice.
Mentor wangu alisema juzi kuwa kama huwezi kusacrifice #USINGIZI au #CHAKULA hivyo vitu viwili basi mafanikio kwako ni ndoto hata mafanikio ya kiroho. Smart man. #ILoveMyMentor.

Na ndo maana kuna vitabu lukuki vimeandikwa kukwambia cha kufanya ili ufanikiwe katika nyakati zinazoitwa ngumu. Lakini wewe unaweza kukesha kusubiri matokeo ya TRUMP na HRC kuliko kusoma kitabu cha namna gani ufanikiwe kutimiza ndoto zako. Eti ooh siyo hobby yangu. Kwa hiyo kukesha unakodolea macho CNN ndo hobby yako? Hobby? Na mafanikio yatakujibu hivyohivyo wewe siyo hobby ya yenyewe! Hivi unawezaje kukesha ukisubiri pambano la MAYWEATHER afu ukashindwa kukesha ukiandaa mipango yako halafu ukataka ufanikiwe?
God is not a fool my friend.
Afu unatoka unaenda kulaumu mbunge wako!  Wakati hutaki kujifunza unataka vitu vinavyofurahisha akili tu. Ndo maana magroup mengi ya WhatsApp hayakujengi lakini unapenda kukaa humo. Vitu unavyofeed mind yako kutoka kwenye hayo magroup vinaua safari yako ya mafanikio but hutaki kuviacha. Ajabu ukiambiwa kuna group la kusaka mafanikio unasema "na mimi jamani niungeni". Coz ni kweli unatamani kufanikiwa. Lakini ukiwekwa kwenye hilo group afu ukaambiwa jamani eeh humu kwenye group kila siku jioni lazima kila mtu aseme amejifunza nini kwenye kitabu anachosoma kwa sasa, heee group linageuka kuwa chungu. Halafu unataka mafanikio! No my brother, no my sister, mafanikio hayatakuja kwako kamwe!
Coz you are too soooft. Ukiambiwa kuna semina ya bure kujifunza ujasiriamali unasema ooh muda sina, ooh muda mbaya muda huo ndo nakuwa natoka kazini. Lakini ukiambiwa kuna Fiesta usiku wa manane na kuna kiingilio elfu 20 siku hiyo hata kazini unatoroka mapema ili uwahi kukaa (I MEAN KUSIMAMA) mbele karibu na jukwaa na kupigwa na umande mpaka asubuhi huku ukichekacheka watu wanaokata viuno na kuitikia imoooooooooo!! Afu unashangaa hela huna. Huo muda ungekuwa umekaa unajifunza mambo muhimu ungefika mbali. Wengine nyie ni mabilionea wakubwa wa baadaye lakini you are too soft! Unataka vitu vya kudumaza mind yako tu. Mungu atakupaje mafanikio?
You are not ready!
You're too soooft! Watu niliokutajia pale juu ni tough people. Check baadhi yao hapa wanasemaje.


Quit being soft.
Kama unataka kufanikiwa lazima uwe TOUGH kwanza kabla hujaanza safari ya mafanikio. Why? Sababu utakumbana na challenges njiani, utakutana na watu wa kukukatisha tamaa wengi mno. Utafika mahali inahitaji upersist lakini kwa sababu you belong to this SOFT GENERATION utaachia njiani..
Coz you're too soft.
Success is not for soft people or crybabies! Unalialia tu. Utafika uzeeni una Ph.D ya kulialia. Crybaby! Utapoteza nafasi ya kuwasaidia wengine kufanikiwa kwa sababu ulichagua kuwa MLALAMISHI na CRYBABY. Ukasahau you have to toughen up in order to get the things you want in life. Unaishi kwa "group thinking". Kwa kuwa wengine wanalalamika basi unadhani na wewe uliumbwa kulalamika kama wao! Unaanza kuwa mbobezi wa kujihurumia na kuomba huruma za wengine. Ndo maana unashangaa mtu anakuja Facebook kila siku status zake mara "This flu is killing me". Mvua ikinyesha tu ooh "jamani hii mvua si ikanyeshe Mtera?" Khaa! Mungu anakuangaliaaa..anakuacha tu. Jua likiwaka sawasawa unaona status eti "Arrrgh hili joto litatuua". Khaa. Si uweke mabarafu kwenye kwapa!? Crybaby!

Haya mara kaandika: Jamani "Baba Jesca" punguza kidogo hali imekuwa ngumu mno! Huoni mazuri coz your mind imekuwa tuned kulalamika.
Ndo hapo unashangaa mzee ndo anaongeza kaspidi gavana kidogo anabinya kidogo zaidi anakaza zaidi. Hahaaaaaa. Hapo ndo utajua kama ile mikia ya pweza hivi ni mikia au miguu, au mikono?

Sasa wewe endelea kusubiri raisi mwingine. 2020. Au 2025 ndo uanze kufanikiwa. Utashangaa anakuja wa type hii hii yani. Hapo unashangaa na kujiuliza hawa wenzangu waliofanikiwa wamefanyaje?

Wamefanyaje?

I'll tell you wamefanyaje:
Walichagua kutokulalamika na kuwa creative...
Walichagua kutotegemea serikali na kujitegemea wenyewe...
Walichagua kujifunza mapema...
Walichagua semina za mafanikio badala ya fiesta...
Walichagua kuahirisha "entertainment" kwanza...
Walichagua kusacrifice muda wao wa kuenjoy na kupumzika wakaamua kupigana kufa na kupona no matter what wakati wewe ulipokuwa unatukana serikali kwenye mitandao...
Walichagua kujitafutia njia za kutengeneza kipato wakiwa chuo wakati wewe ukichagua kutegemea siasa na kusubiri mkopo na ajira...
Walichagua kuonekana wajinga wakati wewe ukila bata...
Walichagua kuomba Mungu kila wakati mpaka usiku wa manane wakati wewe ukisubiri kuombewa na kuonewa huruma na kuwekewa mikono na nabii naniliu...

Walichagua kuanza kidogo chini wakati wewe ukisubiri ukafanye Masters kwanza...
Walichagua kuamini katika kujibidiisha na kujituma ili kubadilisha maisha yao na vizazi vyao wakati wewe ukiridhika na comfort zone...

Hapo ndo utajua kama utakula mijadala uliyokuwa unapoteza nayo muda sijui Wema Sepetu sijui Boss Lady. Hapo ndo unabaki unakasirikia waliokupita kimafanikio. Unawachukia bila sababu. Unabaki kushabikia siasa na Simba na Yanga. Ikikodishwa unalalamika, coz ndo unachoweza zaidi, hahaa hapo muda umeisha uzee umekukuta.
Hapo ndo utajua Fiesta imoo au haimo!

So achana na group thinking.
Itakupoteza. And by the way kama kweli hali imekuwa ngumu kwako like you say basi nikushauri tafuta kakitabu kanaitwa TOUGH TIMES NEVER LAST BUT TOUGH PEOPLE DO.
Utaelewa nachosema. You've got to be TOUGHER than your situation.

Muda unaotumia Facebook, Instagram na Snapchat au WhatsApp ungeutumia vizuri mbona ungesaidia watu wengi mno! Hivi unadhani Mungu atakusahau wakati anaona unatumia muda wako vizuri kujifunza mambo muhimu? Lakini vijana wengi ninawaona humu kwenye mitandao wakikuta mada kama hizi wengine wanatukana wengine much know, wengine wanaignore tu wanataka kila post iwe inaongelea vitu soft soft tu. Tunazalisha taifa la walalamishi na crybabies! Watoto wadogo wanajifunza kwa kuona. Wasomi wengi vyuo vikuu ni walalamishi na crybabies. Shame! Ndo maana unashangaa mtu anamaliza chuo akitaka kwenda kusambaza CV anaomba nauli kwa wazazi. Yani kama elimu ya Chuo Kikuu inashindwa kukuzalishia nauli wewe itamsaidia nani sasa? Utasikia eti. Ah sasa bro sijapata kazi si unajua tena. Ulalamishi tu. Si ukafundishe hata tuition? It's a shame! Wasomi ndo wanaenda kuwa watendaji. Wabunge. Unashangaa analalamika tu.
Why?
Soft generation.

I'm telling you utakuwa mbunge au waziri na utaondoka hukumbukwi. Coz you did not touch lives. You were not successful. Coz ulikuwa whiner and such a sorry crybaby maisha yote. Ndo unashangaa mtu mzima anaachishwa kazi anaanza kulia hadharani. Eti ntaishije? It's a shame. And that's a representation of what our society is beginning to look like!

You need to be TOUGH.
Tough for the dreams you have.
Tough for your children.
Tough for others.
Tough for your nation.
Tough for the world.
Tough for God!
Tough for YOURSELF.
Mungu hakukuumba uje ulie toka unazaliwa mpaka unakufa. Mungu alikupa uwezo wa ku-withstand every tough situation. Lakini umechagua kulialia. Yani umekuwa mtu wa: Ooh yani sijui nianzie wapi? Khaa! Yani utadhani mwili wako umekufa ganzi kuanzia shingoni kwenda juu!


Stop being too soft.
Kama uko kwenye soft generation bonyeza kitufe cha EXIT haraka sana. Toka humo.
Learn to be tough and to fight for what you want. Siyo kulalamika. Ain't nothing gonna change because you whine or complain. Achana na kutukana serikali haikusaidii.
That's being a CRYBABY! Success is never for crybabies. I told you that already.
Achana na kufollow page za watu wanaolalamika na kukasirika every day. Haikusaidii kusikiliza crybabies.

Amua kusema kuanzia leo sitaki kulalamika. Wala kusikiliza malalamiko.
But I will fight for my dreams.
I will fight for my success.
I will soldier on and toughen up mpaka nifanikiwe.
Coz I have the DNA of God.
The DNA of success.

Amua kwamba kuanzia leo nikikosa kitu nachotaka sitakasirika wala kulalamika bali nitakuwa mbunifu na kuwaza upya ili nikipate hicho nilichotaka. Anza kujifunza tabia ya kuwa tough minded. Jifunze hata kwa machinga. Akitembeza vitambaa watu 10 mfululizo kawaonyesha na wote hawanunui hakati tamaa na kurudi nyumbani baada ya lisaa. Anajua atauza tu.

Success is not for soft people.
And never for crybabies.
TOUGHEN UP MY FRIEND!

If you belong to the soft generation then you can as well kiss your success goodbye and forget about being successful. Be it at school, or in business or your relationship; be it in politics, sports or whatever endeavour - success is for tough people.

Amua kuwa imara! No matter what.
Uninstall the software of whining and complaining. Weka mpya ya kuwa imara na kung'ang'ana.

THEN AND ONLY THEN WILL YOU BECOME SUCCESSFUL!

Badilika!

Barikiwa!

Kwa mawasiliano zaidi au maswali, ushauri, appointments contact me via:

WhatsApp only: +255788366511
Sms + Calls: +255752366511

Blog: www.andreamuhozya.blogspot.com


Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.

Jumapili, 13 Novemba 2016

JINSI YA KUZALISHA MUDA ZAIDI ILI KUPATA FEDHA ZAIDI


Yes. Unaweza kushangaa mtu anawezaje kuzalisha muda zaidi wakati umefundishwa kuwa muda kila mtu anapewa masaa 24 tu kila siku. Sasa unaweza kuwa unajiuliza je utazalishaje muda zaidi. Utautoa wapi? Ndo siri za mafanikio hizi sasa ndugu yangu. Zimefichika machoni pa wengi. Mpaka ufanye bidii ya kuzitafuta.

Sasa tunaanza na kipengele hiki cha kucreate muda ambacho  matajiri wengi ndo wanakitumia.

Ni kwamba unaweza kufanya hivyo kwa kununua muda wa wenzako. Yaani kuna mtu ana muda wa masaa 24 kama wewe lakini yeye hana kitu chochote cha kufanya na huo muda ila ana maarifa mengi tu labda kayapata chuo kikuu nk mfano amesomea utunzaji wa kumbukumbu au utunzaji wa fedha. Na yeye hana hizo fedha kwa sasa kwa hiyo elimu yake haimsaidii chochote kama asipopata pa kuitumia. Kwa hiyo wewe tajiri mwenye fedha zinazotakiwa kutunzwa au kusimamiwa unamnunua huyo mtu kwa muda fulani kwa siku. Unampa majukumu (job description) ya kuzisimamia pesa zako kila siku saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni. Anasimamia utajiri wako wa milioni 900 usipotee. Na unamlipa laki 5 kwa mwezi. Hii ndiyo situation ya ajira. Hana cha kufanya na elimu yake anaishi kwa CV. Akiona kwako wewe mshahara mdogo anaenda CRDB anawaambia ana experience ya kufanya kazi kwako wewe Bakhressa. Wao CRDB wanampa ajira awasaidie kusimamia fedha za shareholders (wamiliki) wa benki. Hii ndo ajira. Kwa hiyo basi, ukiweza kununua muda wa masaa tisa tisa ya watu 100 tofauti kwa wakati mmoja it means utakuwa umeongeza muda wako wa uzalishaji  mara nyingi sana. Coz kimahesabu watu 100 wakikufanyia kazi kwa masaa 9 tu kila mmoja kwa siku ina maana utakuwa umepata masaa 900 ya uzalishaji ndani ya masaa 24 ambayo Mungu amekupa. Huyu uliyenunua muda wake yeye amefanya kazi masaa 9 tu kwa siku wewe umefanyiwa kazi ya masaa 900 kwa siku hiyo hiyo moja. Hivi lini atalingana na wewe? Maana itamchukua huyo mtu siku 100 za kufanya kazi kwa masaa 9 kufikisha masaa 900 ya uzalishaji. Lakini ndani ya hizo siku 100 wewe tajiri utakuwa umeshafanyiwa kazi ya jumla ya masaa 90,000! Na itamchukua huyo mtu bila kujali elimu yake siku 10,000/- kufikisha hayo masaa. Yaani takribani miaka 27 ya kufanya kazi kwa mwajiriwa ndiyo inaweza   kumpa utajiri anaozalisha Bakhressa kwa siku 100 tu. Sasa mwambie mwajiriwa mambo kama haya uone. Haelewi kabisaa...! Kisa ni bank teller wa "XYZ Bank". Anafurahia kuvaa uniform za kampuni kubwa. Au ni mhasibu wa "XYZ Clearing and Forwarding" au ni Mwalimu wa "XYZ International School". Unadhani kwa nini tajiri anafungua biashara kila kukicha? Ili anunue muda wa watu wengine weengi zaidi.

Lakini njia hii inakulazimu uwe na mtaji mkubwa ndipo uweze kuajiri watu wengi kiasi hicho. Nadhani utakubaliana na mimi kwa hili.

But kuna namna nyingine ya wewe kuzalisha muda mwingi wa kukuzalishia kipato cha ziada yaani njia ya pili ya kutengeneza hii TIME LEVERAGE yaani kuDUPLICATE muda wako wa uzalishaji zaidi!! Kumbuka ukibakia tu umeajiriwa au kujiajiri mwenyewe unaweza kufanya kazi kuanzia leo mpaka miaka 27 ijayo yaani mwaka 2043 na itakuwa hujawa Dewji au Bakhressa. Hivi utawezaje kumfikia mtu anayeingiza labda milioni 1 na laki 1 hivi kama faida kwa siku moja wakati wewe kwa saa moja unalipwa  tsh 1850/- kwa siku kama elfu 16 hivi yaani laki 5 kwa mwezi! Coz anakupa kiujira tu kidogo.
Ndo yaleyale. Faida yake ya siku moja ni mshahara wako wa miezi miwili. Faida yake ya siku kumi ni mshahara wako wa miezi 20 yaani mwaka mmoja na miezi 8! Mwaka mmoja na miezi 8 hizo ni siku takribani 600. Unaongelea yeye kuwa ameshatengeneza Tshs 600,000,000!! Milioni 600 ndani ya mwaka mmoja na miezi 8 tu.  Ambazo wewe utafanya kazi mpaka kustaafu na mwanao atafanya kazi mpaka atastaafu na mjukuu wako pia... Niendelee? Ndani ya huo muda yeye ameshapata faida ya 600 million!

Wanafunzi. Kama wewe ni mwanafunzi na unasoma ujumbe huu take it very serious. Usibweteke na hiyo degree unayosomea ya usimamizi wa fedha za wengine halafu uanze kuishi kwa kusambaza CV yaani bila plan nyingine yoyote maishani mwako. Elimu yote hiyo itakuwa haina manufaa kama ni kwa ajili ya kwenda kumfanyia mtu kazi maisha yako yote. Watoto wako nao waje wakasome elimu kama yako nao wakamfanyie mtu mwingine maisha yao yote. Wajukuu zako hivyo hivyo. Vitukuu... Vilembwe..
Wanafunzi wengi huwa ni wabishi. Wamesoma "elimu ya juu" wengine "wanafanya" masters. Hahaaa. Kuna tofauti ya "kuchukua" degree na "kufanya" masters. Hizi mbwembwe hizi jamani. Haya huyu mtu anawaza kuwa anajua sana vitu vingi. Kumbe anajua tu definition za economics na matajiri hawazijui hizo definition ila wanajua uchumi wenyewe na ndo wanaushikilia. Wanafunzi fungueni macho. Anza kujiandaa mapema. Usitamani tu kuajiriwa kupitia kiasi ndo mpaka baadhi ya dada zetu wanatoa rushwa ya mwili ili aajiriwe tu.

Jifunze haya mambo! Usikae kuchat chat tu na kutumiana vikatuni vya ajabu ajabu. Unachekacheka tu mwaka mzima sasa unaenda kwisha ushatumiwa vikatuni kibao mwenzako anatengeneza milioni 600. Unachat chat wenzako wanatengeneza hela. Unataka ukafanye masters ili mshahara upande. Unacheza au?

Anyway...
Kama uko interested kufahamu haya mambo kiundani hususan njia rahisi ya wewe kuzalisha muda zaidi ili kupata kipato zaidi basi njoo kwa WhatsApp  #o788366511 au #o752366511.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa

Jumamosi, 12 Novemba 2016

KUANZIA LEO HUTAKOSA MTAJI WA KUANZA BIASHARA


Kila siku watu wananitafuta wanataka kujifunza biashara. Lakini wengi wao wanasema shida ni kukosa ➡ ➡

Mimi huwa nawaaambia kuwa mtaji (pesa) siyo shida kabisa. Tatizo ni kukosa WAZO SAHIHI la biashara. So tafuta wazo sahihi la biashara.

Why?

Well kwa sababu ukipata WAZO SAHIHI la biashara pesa zina kawaida ya kuwa na "KIHEREHERE" cha kufata WAZO SAHIHI lilipo. Ndo maana watu wote waliofanikiwa walianza bila pesa! Hata Donald Trump alianza bila pesa ila akakopa kwa baba yake.
Jeff Bezos alianza bila pesa.
Facebook walianza bila pesa.
Google walianzia gereji tena kwenye gereji (parking) ya mama mwenye nyumba wao, hawakuwa na hela ila walikuwa na WAZO SAHIHI.
Bill Gates alianza na WAZO SAHIHI kuuza software.

Wewe una WAZO gani sasa? Unawaza kufungua saluni au kuuza CD za muziki? Kuuza mbao? Kuuza nyumba? Kuuza magari? Vyakula? Kufanya Network Marketing? Kubuni software au Application fulani fulani? Haina shida. Whatever utaamua kufanya kuna kitu muhimu kuangalia. Je hiloni wazo sahihi la biashara KWAKO?

Likishakuwa sahihi kwako hela itakuja tu.

Hii ni kwa sababu WAZO likiwa sahihi unaweza kwenda kwa mtu ambaye hujawahi kutarajia kumfata kumwambia akupe mtaji na atakupa! Na hata akawa hajaelewa kila kitu still akakupa! Kwa hiyo kuanzia Leo usihangaike na mtaji. Mimi ni shahidi wa jambo hili katika safari yangu ya biashara na ujasiriamali.

So... Hangaika kwanza kujua unachotaka kukufanya ni SAHIHI KWAKO?

KANUNI NI HII (THE AGM's PRINCIPLE OF START-UP CAPITAL ATTRACTION):

"WAZO LIKIWA SAHIHI KWAKO INA MAANA KUNA SULUHISHO FULANI UNALETA KWA WANADAMU WA MAHALI FULANI KWA WAKATI HUO. PESA ZITATOKA ZITOKAKO KUKUFATA WEWE ILI KUKUWEZESHA KUTIMIZA KUSUDI HILO LA KUTATUA HIYO SHIDA YA WATU"

The whole universe will conspire to bring the money you NEED to get started. That's very important.


SWALI MUHIMU NI HILI:

Sasa utajuaje kuwa WAZO fulani la Biashara ni sahihi KWAKO? Hapa nakupa kanuni yangu nyingine.
(Hii nimeiita THE AGM's PRINCIPLE OF DETERMINING THE RIGHT BUSINESS IDEA). This one ni threefold. Ina vitu vitatu: THINKING, TALKING  and STARTING. Tunaanza kimoja kimoja. Ili ujue kuwa ulichonacho ni THE RIGHT BUSINESS IDEA vitu vitatu vitatokea kwako. Visipotokea ujue hiyo business idea siyo yako! Ni sahihi kwa mtu mwingine. Au siyo sahihi kwako kwa sasa.

Je, ni vitu gani hivyo?

1. YOU CAN'T STOP THINKING ABOUT IT.


Yaani hilo wazo la biashara ukishakutana nalo litakujaa kwenye fikra (mind/heart) kwa namna ya tofauti sana kiasi kwamba utakuwa consumed na hilo wazo kila uendako. Hii ni muhimu sana kujichunguza. Huwezi kuwa na wazo sahihi la biashara halafu eti likawa halipo kichwani kwako siku nzima unaendelea na mambo yako siku nzima huiwazi kabisa hadi baadaye. Au mpaka mtu akuulize eti. Aisee. Ukiwa na wazo sahihi litakuwa kichwani all the time.

Katika kufundisha kwangu biashara niliwahi kwenye Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) na katika kuongea na wanafunzi nikajikuta ninaongea na kijana mmoja ambaye incidentally alikuwa ndo raisi wa wanafunzi. Na katika kubadilishana naye mawazo one of the things alichoniambia ni kuwa yeye huwa anatest rafiki zake kama akiwapa idea fulani kuhusu mambo ya wanafunzi labda mfano kuanzisha mradi wa kusaidia wanafunzi wenye ulemavu nk anasema akikupa hiyo idea wewe mwanafunzi mwenzake halafu usipomtafuta ndani ya wiki nzima basi hilo jambo alilokwambia halijaingia akilini mwako sawa sawa. Hiyo ndo test yake. Na hapo hatakuuliza tena. Wow!

Brilliant young man! Now anamiliki App maarufu inaitwa SOMA APP. Google hiyo kitu umwone alipofika.

Ndo hivyo hivyo sasa. Ukiona umepata wazo fulani la biashara halafu halizunguki kichwani mwako mchana na usiku ni dalili kuwa si la kwako.
Na si kwamba ni wazo baya. Ah-ah! Ni zuri ila tu siyo sahihi kwako tu. Hiyo ni test ya kwanza.
Jipime.


2. YOU CAN'T STOP TALKING ABOUT IT.

You just can't!


Mentor wangu amekuwa akinikumbusha kitu kwamba Biblia inasema kimtokacho mtu ni kile kiujazacho moyo wake( Out of a heart's OVERFLOW the mouth speaketh). So kitu kinachomtoka mtu iwe ni lugha (kiswahili, kiingereza au kimarangu) or aina ya lugha yake (ya kistaarabu, matusi, nk) vinaonyesha tu huyu mtu mind/spirit yake imejaa nini?

Sasa hata katika hili la mtaji. Kanuni ama test ya pili ni kwamba kwa kuwa wazo litakuwa litakuwa limejaa in your mind/heart/spirit kiasi cha kwamba ndo hicho hicho unafikiria kila wakati. Yani WAZO hilo la biashara limejaa mawazoni mwako kiasi kwamba ukinywa maji unaliona kwenye glass!!! Basi kitakachofuata ni kuwa kila ukiongea utataka uliongelee. Na utaanza kushangaa unataka tu kuwa karibu na watu wanaoweza kukufeed taarifa sahihi kuhusu hilo wazo. Hutataka kukaa karibu na watu wasioweza kukupanua zaidi kuhusu wazo lako. Hutakaa tena karibu na watu wanaoweza kukucheka au kukukatisha tamaa. Maana utakuwa huivi nao tena. Hata kama ni WAZAZI au ndugu. Utashangaa unataka kampani ya watu wanaongelea biashara biashara zaidi kuliko kuongelea Trump kashinda kweli au bado wanahesabu kura. Sijui utabiri ulikuwa wa uongo au wa ukweli. Utajikuta hizo habari hazikuvutii tena. I'm telling you, ukishapata WAZO SAHIHI la biashara likakukaa sawa sawa kichwani basi lugha yako itachange AUTOMATICALLY.

Are you hearing what I'm telling you?

Na kuna watu utawaboa mno. Maana kimtokacho mtu ni kile kiujazacho moyo wake. Na wewe na wao sasa mioyo/mind zenu zimejawa na kuwa consumed na vitu tofauti! You can't stop talking about your business idea. Hilo la pili.
Twende la tatu.

3. YOU CAN'T WAIT TO GET STARTED

Hili ni muhimu zaidi.

Utafika mahali huoni haja ya kuishi bila kulifanya hilo WAZO kuwa halisi. Yani utahangaika kama mama mjamzito akikaribia kujifungua. Coz you are PREGNANT. Na ujauzito wako wa hiyo idea yako haufichiki tena kila anayekujua anafahamu. Na sasa utafikia hatua una UTUNGU wa kuzaa.

Siyo wewe. Ni idea inataka kuja. Utakosa amani moyoni bila kuona hiyo idea ikiwa halisi. Wa kukuita kichaa watakuita kichaa. Wa kukucheka ndo muda wao huu maana unahangaika kama kuku anayeanza kutaga kwa mara ya kwanza yani hata kwenye bustani atataga. Ndo hapa nimekwambia Google walianzia garage. Facebook walianzia bwenini. Si unasikia Bakhressa alianzaje? Wa kukukatisha tamaa wataongeza juhudi utadhani wako muda wa majeruhi. Hiki ni kipindi huwezi kutulia. Na hapa sasa imani inakuwa KALI sana kama vile umekuwa kichaa. Yani ndo hapa ukiambiwa shuka kwenye boti utembee juu ya maji unashuka fasta! Utawaza baadaye. Imani kali! Hapa ndo watu huwa wanapata mitaji wa njia ambazo hakuwahi kuzifikiria kuwa atakuja kufanya siku moja. Hapa mimi binafsi napafahamu sana. Yani ni unakuwa na CONVICTION kiasi kwamba hata ukimfata mtu kumwomba mtaji anaweza kukusikiliza moyo ukamchoma tu bila sababu hata hajakuelewa vizuri akakupa.
Are following me?


HAPA ndipo watu wengi wanalia eti ooh "sina mtaji". Nani kakwambia mtaji ni shida my friend? Shida ni WEWE!! Huna conviction moyoni. So hata ukiongea na mtu kuhusu IDEA ya biashara unayotaka kuifanya mtu haoni kabisa kama unachotaka kufanya kinatoka moyoni mwako. Unaongea EMPTY words! Mdomo tu unaongea. Moyo haupo. Na hili limewakosesha watu wengi fedha za kuanzia kwa kutokuwa na conviction.

Sikia ndugu mpendwa.. Watu wenye uwezo wa kukupa mtaji huwa hawasikilizi mdomo wanasikiliza SPIRIT yako inasemaje? Wanajua mdomo ukiwa unaongea na MOYO ukiwa unaongea. Kuna tofauti. Kama maneno unayotamka kuhusu why unamwomba hela yakiwa empty atajua tu. Na yakiwa yanakuja na CONVICTION pia atajua.


*Case Studies:*
Jifunze kwa wawili hawa

(i) Joe Kusaga alipotaka kuanzisha Clouds FM alienda kuomba hati ya nyumba ya baba yake ili akakope pesa benki. Na wakampa hati bila kujua huko mbele itakuwaje. Why? Kwa sababu ya CONVICTION aliyokuwa nayo moyoni. Jaribu wewe sasa uone hao wazazi kama hawajakuitia Dr Chris Mauki aje akupe ushauri wa KISAIKOLOJIA!

(ii.) Jeff Bezos wa AMAZON DOT COM.

Huyu alipotaka kuanzisha mtandao wa kuuza vitabu kwa njia ya internet hakuwa na hela akawaomba wazazi wake wampe pensheni yao aanzishie biashara. Can you imagine? Hivi wewe ukiwafata wazazi wako leo ukawaomba pesheni yao hapo ndo wamestaafu eti wakupe wewe huyo ukaanzishe biashara.. Hivi wataona empty words au wataona moyo wako wote uko consumed na hilo WAZO SAHIHI la biashara? Jeff wazazi walimuuliza umesema unataka pensheni yetu sisi, ukaanzishe biashara kwenye internet? Internet ndo nini? Enzi hizo hata wazazi wake hawajui internet ni nini. Ni kama wewe tu bibi yako au hata mzazi kijijini hajui internet sijui blog sijui tovuti afu leo umwambie"Baba hizo hela ulizouza korosho mi naomba ninataka kufungua TOVUTI!!!" Hahaaaa. Imagine! Sasa Jeff wazazi  hawakumwelewa lakini walimpa PENSHENI. Why? Because ALIKUWA NA WAZO SAHIHI, na likawa limejaa kwenye MIND yake and akawa hawezi kuacha kuwaza wala kuliongelea na alipoongea na wazazi wake moyo wake wooote ulikuwa juu ya MANENO yake. Walimpa aisee. Bila kumwelewa.


Sasa huwa nakutana na watu hasa vijana wanalialia tu. Anasema "nimeongea na ba mkubwa anipe mtaji nikafungue saluni hata hajanielewa!" Kweli? Are you sure uliongea kutoka moyoni halafu hakuelewa?

Mwingine anasema: "Nimepata WAZO la biashara nimemwambia mama mdogo anipe mtaji hata hajanielewa". Sasa ndugu yangu unaomba mtaji huku unang'ata kucha utadhani unaongea na boyfriend kweli huyo mama mdogo atakuelewa?

Mwingine anasema Oh "nimeongea na mume wangu anipe tafu kidogo kuhusu mtaji wala hata hanielewi". No my friend. Wewe ndo hujajielewa upo wapi katika utayari wao mumeo siyo shida. Huna conviction.. Unaongea na mtu kuhusu mtaji as if unaongea naye kuhusu nauli ya bajaji. Huna passion. Kwani ukiomba nauli au ada kwa mzazi unahitaji PASSION yoyote? No. Lakini kama ukidhani ukiongea naye hivyo hivyo kuhusu mtaji atakupa utashangaa ada ya milioni tatu alilipa ila mtaji wa laki tano au saba hakupi!!! Why? Huna CONVICTION. Maneno yako hayana uzito unaoweza kumchoma mtu  moyoni. And that is YOUR problem. Mtu anayekupa mtaji kipimo chake pekee ni HOW SERIOUS ARE YOU. Akiona hauko setious anakujibu tu "sina hela" au "ngoja baadaye". Ukioma unaambiwa NGOJA na wewe unaridhika ujue ni kweli ulistahili kunyimwa mtaji. Huwezi kuwa na ujauzito wa kujifungua afu mtu akwambie ngoa usijifungue leo ngoja kesho.
So how come wazo lako limefikia muda wake halafu mtuwingine ambaye wazo hilo si lake akwambie SUBIRI na wewe usubiri kweli?

Nakupa elimu ADIMU hapa. Izingatie sana. Ni elimu nyeti sana..

So usiseme "sina mtaji". No my friend. Mtaji si kazi yako. Ni kazi ya watu wengine. Mtaji unaweza kutoka kwenye mshahara, au kukopa kwa mtu au kuuza kitu cha thamani ulichonacho. Wanunuzi watapatikana bila wewe kuelewa imekuwaje. Yes ukiwa consumed na idea yako utauza anything even everything. Yani hata simu unaweza kuuza ili ukusanye pesa upate pa kuanzia zingine utaomba huko mbele kwa mbele.

But problem nya watu wengi sana sana ni kuwa hawana PASSION na wazo la biashara alilonalo. Nikiongelea kuuza simu hapo unajisemea aah broh we nipe idea nyingine tu ya kupata mtaji. Kuna mtu alinijibu hivyo ati. See?

Inawezekana inanibidi nikukumbushe mfano wa yule jamaa kwenye Biblia. Aliona hazina mahali kwenye shamba la mtu. (That's a business idea). Au unaionaje wewe? Hiyo kitu ilimconsume mpaka alienda kuuza kila alichokuwa nacho akaenda kununua lile shamba.
Bila kuchelewa. Huenda wakati anauza mkewe aligombana naye. Lakini baadaye akawa very wealthy.

Kwa hiyo mimi huwa nawaambia watu hasa vijana kwamba ukiona unashidwa kupata MTAJI dunia ya Leo ujue either:

1. HUNA WAZO SAHIHI LA BIASHARA

na kama unalo basi ni kuwa

2.  HALIJAKUJAA SAWASAWA KIFIKRA

Likijaa sawasawa utamfata hata Dewji na appointment utapata na atakupa huo mtaji hata ungekuwa milioni 40 anakupa. Lakini sasa akikusikiliza je ataona maneno ya mtu ambaye yuko consumed na idea yake kutoka moyoni au ataona maneno tu ya mtu anaomba pesa kinyonge kinyonge?

Money is not a problem. YOU are the problem. Watu wa kukupa mtaji unataka au kununua vitu vyako unavyouza ili upate mtaji wapo lukuki!


Ila wanachohitaji ni CONFIDENCE wakati unaomba hiyo hela. Siyo UNYONGE na kuonewa huruma.

Ukifuata ushauri wangu huo hutokaa ukose mtaji wa kuanzia biashara.


Kwa maoni, ushauri, critique, au Appointment.



Thank you and God bless,

Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa.
WhatsApp only: +255 788 366 511
SMS/Calls:  +255 752 366 511