Jumapili, 13 Novemba 2016

JINSI YA KUZALISHA MUDA ZAIDI ILI KUPATA FEDHA ZAIDI


Yes. Unaweza kushangaa mtu anawezaje kuzalisha muda zaidi wakati umefundishwa kuwa muda kila mtu anapewa masaa 24 tu kila siku. Sasa unaweza kuwa unajiuliza je utazalishaje muda zaidi. Utautoa wapi? Ndo siri za mafanikio hizi sasa ndugu yangu. Zimefichika machoni pa wengi. Mpaka ufanye bidii ya kuzitafuta.

Sasa tunaanza na kipengele hiki cha kucreate muda ambacho  matajiri wengi ndo wanakitumia.

Ni kwamba unaweza kufanya hivyo kwa kununua muda wa wenzako. Yaani kuna mtu ana muda wa masaa 24 kama wewe lakini yeye hana kitu chochote cha kufanya na huo muda ila ana maarifa mengi tu labda kayapata chuo kikuu nk mfano amesomea utunzaji wa kumbukumbu au utunzaji wa fedha. Na yeye hana hizo fedha kwa sasa kwa hiyo elimu yake haimsaidii chochote kama asipopata pa kuitumia. Kwa hiyo wewe tajiri mwenye fedha zinazotakiwa kutunzwa au kusimamiwa unamnunua huyo mtu kwa muda fulani kwa siku. Unampa majukumu (job description) ya kuzisimamia pesa zako kila siku saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni. Anasimamia utajiri wako wa milioni 900 usipotee. Na unamlipa laki 5 kwa mwezi. Hii ndiyo situation ya ajira. Hana cha kufanya na elimu yake anaishi kwa CV. Akiona kwako wewe mshahara mdogo anaenda CRDB anawaambia ana experience ya kufanya kazi kwako wewe Bakhressa. Wao CRDB wanampa ajira awasaidie kusimamia fedha za shareholders (wamiliki) wa benki. Hii ndo ajira. Kwa hiyo basi, ukiweza kununua muda wa masaa tisa tisa ya watu 100 tofauti kwa wakati mmoja it means utakuwa umeongeza muda wako wa uzalishaji  mara nyingi sana. Coz kimahesabu watu 100 wakikufanyia kazi kwa masaa 9 tu kila mmoja kwa siku ina maana utakuwa umepata masaa 900 ya uzalishaji ndani ya masaa 24 ambayo Mungu amekupa. Huyu uliyenunua muda wake yeye amefanya kazi masaa 9 tu kwa siku wewe umefanyiwa kazi ya masaa 900 kwa siku hiyo hiyo moja. Hivi lini atalingana na wewe? Maana itamchukua huyo mtu siku 100 za kufanya kazi kwa masaa 9 kufikisha masaa 900 ya uzalishaji. Lakini ndani ya hizo siku 100 wewe tajiri utakuwa umeshafanyiwa kazi ya jumla ya masaa 90,000! Na itamchukua huyo mtu bila kujali elimu yake siku 10,000/- kufikisha hayo masaa. Yaani takribani miaka 27 ya kufanya kazi kwa mwajiriwa ndiyo inaweza   kumpa utajiri anaozalisha Bakhressa kwa siku 100 tu. Sasa mwambie mwajiriwa mambo kama haya uone. Haelewi kabisaa...! Kisa ni bank teller wa "XYZ Bank". Anafurahia kuvaa uniform za kampuni kubwa. Au ni mhasibu wa "XYZ Clearing and Forwarding" au ni Mwalimu wa "XYZ International School". Unadhani kwa nini tajiri anafungua biashara kila kukicha? Ili anunue muda wa watu wengine weengi zaidi.

Lakini njia hii inakulazimu uwe na mtaji mkubwa ndipo uweze kuajiri watu wengi kiasi hicho. Nadhani utakubaliana na mimi kwa hili.

But kuna namna nyingine ya wewe kuzalisha muda mwingi wa kukuzalishia kipato cha ziada yaani njia ya pili ya kutengeneza hii TIME LEVERAGE yaani kuDUPLICATE muda wako wa uzalishaji zaidi!! Kumbuka ukibakia tu umeajiriwa au kujiajiri mwenyewe unaweza kufanya kazi kuanzia leo mpaka miaka 27 ijayo yaani mwaka 2043 na itakuwa hujawa Dewji au Bakhressa. Hivi utawezaje kumfikia mtu anayeingiza labda milioni 1 na laki 1 hivi kama faida kwa siku moja wakati wewe kwa saa moja unalipwa  tsh 1850/- kwa siku kama elfu 16 hivi yaani laki 5 kwa mwezi! Coz anakupa kiujira tu kidogo.
Ndo yaleyale. Faida yake ya siku moja ni mshahara wako wa miezi miwili. Faida yake ya siku kumi ni mshahara wako wa miezi 20 yaani mwaka mmoja na miezi 8! Mwaka mmoja na miezi 8 hizo ni siku takribani 600. Unaongelea yeye kuwa ameshatengeneza Tshs 600,000,000!! Milioni 600 ndani ya mwaka mmoja na miezi 8 tu.  Ambazo wewe utafanya kazi mpaka kustaafu na mwanao atafanya kazi mpaka atastaafu na mjukuu wako pia... Niendelee? Ndani ya huo muda yeye ameshapata faida ya 600 million!

Wanafunzi. Kama wewe ni mwanafunzi na unasoma ujumbe huu take it very serious. Usibweteke na hiyo degree unayosomea ya usimamizi wa fedha za wengine halafu uanze kuishi kwa kusambaza CV yaani bila plan nyingine yoyote maishani mwako. Elimu yote hiyo itakuwa haina manufaa kama ni kwa ajili ya kwenda kumfanyia mtu kazi maisha yako yote. Watoto wako nao waje wakasome elimu kama yako nao wakamfanyie mtu mwingine maisha yao yote. Wajukuu zako hivyo hivyo. Vitukuu... Vilembwe..
Wanafunzi wengi huwa ni wabishi. Wamesoma "elimu ya juu" wengine "wanafanya" masters. Hahaaa. Kuna tofauti ya "kuchukua" degree na "kufanya" masters. Hizi mbwembwe hizi jamani. Haya huyu mtu anawaza kuwa anajua sana vitu vingi. Kumbe anajua tu definition za economics na matajiri hawazijui hizo definition ila wanajua uchumi wenyewe na ndo wanaushikilia. Wanafunzi fungueni macho. Anza kujiandaa mapema. Usitamani tu kuajiriwa kupitia kiasi ndo mpaka baadhi ya dada zetu wanatoa rushwa ya mwili ili aajiriwe tu.

Jifunze haya mambo! Usikae kuchat chat tu na kutumiana vikatuni vya ajabu ajabu. Unachekacheka tu mwaka mzima sasa unaenda kwisha ushatumiwa vikatuni kibao mwenzako anatengeneza milioni 600. Unachat chat wenzako wanatengeneza hela. Unataka ukafanye masters ili mshahara upande. Unacheza au?

Anyway...
Kama uko interested kufahamu haya mambo kiundani hususan njia rahisi ya wewe kuzalisha muda zaidi ili kupata kipato zaidi basi njoo kwa WhatsApp  #o788366511 au #o752366511.


Semper Fi,


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania
East Africa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni