Jumatatu, 29 Mei 2017

KIPAWA CHAKO NA JINSI YA KUKITUMIA KUTIMIZA MALENGO YAKO KIUCHUMI

(MAKALA HII ILIANDIKWA MAY 30 2017)

Na Andrea G. Muhozya 

:::::::::::::::::::::::::::::::::::

Habari ya leo kijana wa kitanzania. Mungu  ni mwema tuko hai hadi leo.
Naomba muda wako kidogo tuendelee kujifunza zaidi pamoja leo.

::::::::::::::::::::::::::::::::::::

Yes...

Mungu aliweka kipawa ndani ya kila mmoja wetu. Ili usife njaa wala usife maskini.

Hata hivyo tunapozungumzia KIPAWA yaani TALENT watu wanachanganya sana mambo, wanaita tu KIPAJI.

Ndo utasikia kuna eti "SHULE ZA VIPAJI MAALUMU" wakati pale wanachomaanisha ni shule za watu waliopata maksi nyingi labda. Wameleta tafsiri mbovu ya hata hivyo "vipaji".

Tafsiri sahihi ya TALENT  ni kitu kinachoitwa KARAMA. Yaani simply ni kitu cha ziada ambacho mtu anacho cha kipekee ambacho mara nyingi wengine hawana. Uwezo fulani alionao mtu wa kufanya jambo muhimu ambao watu wengine hawana. Kila binadamu ana cha kwake.

Hapa tunaweza kupata aina mbali mbali za VIPAWA au UWEZO WA KIPEKEE huo:

Mfano:

1. Kipawa cha Kuongea vizuri
(Orators wazuri wako hapa kama kina Mwalimu Nyerere. Yani akiongea mnapenda hadi uongeaji wake tu yani. Comedians wazuri na watangazaji kama kina Charles Hilary wako hapa. Yani anavyoongea tu unatamani kipindi chake kisiishe)

2. Kipawa cha Kuandika vizuri
(Ukisoma novel kama Windmills of the Gods ya SIDNEY SHELDON utaelewa maana ya kipawa cha kuandika.
Ana kitu cha kipekee akipewa "pen and paper". Mhe. January Makamba ni mmoja wapo watu miongoni mwetu ambao wana karama hii. Yani akiandika article inakuwa tu ya kipekee from title to conclusion. Huenda ndo maana alikuwa muandaaji wa speeches za Rais Kikwete. Karama. Kipawa. Kipaji)

3. Kipawa cha Uongozi
Unajua watu kama Gandhi?
Yes. Yani anaweza kufanya wananchi wakubali kulala kwenye reli ili kuzuia treni la mkoloni lisipite na wakalala. Anaweza kufanya shule nzima mkagomea chakula. Anaweza pia kufanya msitishe mgomo.  Wafanyabiashara wakubwa wana hii karama.
Hata Yesu alipokuwa duniani alikuwa na hii karama. Yani anaweza kukukuta uko kazini kwako akakwambia tu "FOLLOW ME" na ukaacha kila kitu. Ukamfata.
Hawa ni watu hata kama hatoki familia inayojulikana lakini anakuja kufanya nchi nzima imfate kwa mazuri au yasiyo mazuri.  Napoleon Bonapatre. Unamkumbuka? Margareth Thatcher alikuwa na karama ya uongozi plus ungangari. Na wengine.
Unashangaa hizi nguvu anapata wapi? Nguvu imejificha kwenye karama tu.
Kuna viongozi wa vyama vya siasa hana elimu ndefu kama wengine wala hahangaiki nayo lakini ukimstudy anaweza kufanya watu lukuki wafanye anachotaka.  We unasema ati ana kismati.  What's kismati. Kipawa hicho.. Talent.

4. Kipawa cha Uimbaji.
Wimbo ule ule lakini akiuimba yeye watu wanaweza kushangilia mwanzo hadi mwisho na wakampa na standing ovation wakati wengine hawakupewa yote hayo. Mtu ana sauti nzuri utadhani koo lake lilitengenezwa baada ya mwili wake kuumbwa yani likaumbwa kivyake. Kuna watu kanisani wakiimba huwa najikuta natamani wimbo usifike mwisho. Huwa wananifanya nitamani zaidi mbinguni sema tu sijamaliza kazi kubwa Mungu aliyonipa hapa duniani. Ndo kwanza ninaanza. Lakini mtu anaimba mpaka unahisi ukiitikia utamharibia wimbo vile. Hivyo yani..

Sasa watu wengi wanajua hiki tu ndo kipaji. Au kipaji cha michezo. Basi.

5. Kipawa cha Uchezaji:
Hapa napo ndo wengi wanaishia like I just said.
Lakini kuna vipawa vingi zaidi ya michezo na kuimba kama tulivyoona hapo juu na tutakavyoona hapa chini.

Na hata hapa kwenye michezo kuna kipawa cha kila aina ya mchezo.
(Mfano kuna kipawa kwenye soccer, kwenye football, basketball, racing (ya magari au ya farasi, mitumbwi, pikipiki, baiskeli, nk), riadha, boxing, kung-fu, weight lifting, mieleka, kuogelea, cricket, tennis, kuteleza kwenye barafu au kwenye maji yaani skiing, chess, hockey, golf, gymnastics, na mingine mingi. Kuna tofauti ya Messi na Phelps)
See? Sasa huku kwetu watu wengi wanajua Mbwana Samatta na Hashimu Thabeet basi.

6. Kipawa cha uigizaji
Umesema nani Kanumba? Hujakosea.  Alikuwa na something EXTRA.  Hiyo extra hiyo. Ndo kipawa.
Kuna yule mama mnaijeria yule. MAMA G.

Akiigiza kama Mama Mkwe utamkubali yani utasikia kila anayetazama ile filamu anasema "Huyu mama ana roho mbaya huyu".
Anaigiza hadi unahisi ndivyo alivyo. Hiyo ndo maana ya KITU CHA ZIADA. Kipawa. Mtu hadi anafanana na anachoigiza.

7. Kipawa cha Uchoraji.
Kina Ibra Washokera. Kina Masoud "Kipanya" na wengine. Yani akichora hata kama ni kikatuni tu kikawa hakina maneno utaona tofauti tu. Unakumbuka katuni ya Kingo. Lol. James Gayo huyo. Hazina maneno lakini ujumbe unafika.Kipawa.

Yani nimeona Kingo toka niko mtoto. Ilikuwa inafikirisha sana afu ukiielewa unaona jinsi mchoraji alivyo na kitu cha ziada.

8. Kipawa cha Kufikiri (thinking).
Tofautisha kufikiri na kuwaza. Sizungumzii kuwaza maana kuwaza kila mtu anawaza ila ni wachache wanafikiri. Kuwaza unaweza kuwa huna hela ukajaa mawazo. Mi nazungumzia KUFIKIRI (THINKING).
Kuna watu wana karama hii. Ukimpa afikirie kitu analeta jibu lenye something EXTRA.
Ulishasikia kitu kinaitwa THINK TANK? Mara nyingi kwenye think tanks kuna watu wenye kitu cha ziada kwenye kufikiria.  Yani ukimpa issue ya mchanga wa dhahabu anaweza kukupa solution ndogo tu na ikawa ndo the most effective. Ana karama mwenzako.

9. Kipawa cha Ubunifu (creativity).
Hata wachoraji, watunzi wa vitu nk hii pia wanayo.
But hapa naongelea wabunifu.  Ndo unaona wanabuni magari,
wabunifu wa mitindo ya mavazi, wa matreni, midege ya ajabu, simu hizi na computers nk. Mifumo mbali mbali kama android, MPESA, max malipo, Uber etc. Creativity tu hapo. Sasa mwingine anaweza kukaa miaka nane hajaweza kubuni kitu cha maana. Mwingine mpe nusu saa tu. Inatosha.

10. Kipawa cha Kumbukumbu
(hapa ndo wanafunzi wanofaulu vizuri wapo. Anaweza akasikiliza kidogo tu darasani lakini akakumbuka every detail hata ambavyo mlikuwa mnahisi hakuvisikiliza kwa makini. Na nyie mpaka mmemrekodi mwalimu na notes mmeandika na maswali mmeuliza lakini "pepa" ikija anafaulu yeye zaidi yenu. Ana something EXTRA linapokuja suala la kumbukumbu.
Nk..
Wewe utaomba Roho wa Mungu akukumbushe vitu kwenye mtihani mwenzako hata hajui kuomba labda. Lakini anapata "A" wewe unaondoka na karai.
Kumbuka kipawa alipewa na Mungu. Na wewe una cha kwako labda michezo.  Ndo hivyo.

SASA TUENDELEE..
Nadhani hadi hapo unaweza kuona Michael Jordan alikuwa wapi, na Diamond Platnumz  yuko wapi, Ronaldo na Messi na kina Mbwana Samatta wako wapi, Roger Federer yuko wapi, Tiger Woods yuko wapi, na Les Brown yuko wapi Dan Brown yuko wapi, Jack Chan alikuwa wapi, Kanumba alikuwa wapi, Michael Phelps yuko wapi, Alexander Bell, Mohammad Ali na kina Tyson walikuwa wapi katika hizo hapo juu. Nk.

Yaani Tyson hakujaribu kulazimisha kuimba, Ronaldo hajalazimisha kuchora, Diamond hajalazimisha kuogelea. Kuna siku nilisema Dan Brown anajiandikia zake vitabu hajalazimisha kuongea kama Les Brown na Les Brown naye hakujaribu kuandika stori za kuvutia kama za Dan Brown na wote wamekuwa multi-millionaires.


TALENT YAKO NA MAFANIKIO KIUCHUMI

Ni ujinga kumwonea wivu mtu anayefanikiwa kupitia kipawa chake ilhali kila mtu alipewa cha kwake. Muhimu ni wewe kutafuta cha kwako my friend.

Talent ni njia kubwa mno ya kuweza kukupa pesa nyingi na kukufikisha katika utajiri. Leo hii Michael Jackson alishafariki lakini bado analipwa mamilioni, lakini watu lukuki wako hai na hawajui senti tano wataipata wapi...

Lakini angalia watu kama Michael Jordan na kina Lionel Messi, Cristiano Ronaldo, na wengineo. Angalia waigizaji kama Tyler Perry na kina Samuel Jackson au Angelina Jolie uone wanavyopata pesa nyingi mno kupitia vipawa vyao.

Siwezi kutaja kila mwenye kipawa hapa maana hatutamaliza. Michezo tu pale juu nimetaja mingi mingi na hiyo ni michezo hatujaongelea vipawa vingine  kama vipawa vya thinking and creativity (ubunifu)  ambao hawa ndo wanabuni mitindo ya mavazi, ya magari, ya ndege na computer na simu na drones nk lakini pia ndo wanabuni solution za migogoro mikubwa ya kati ya mataifa. Hawa nao wanatengeneza pesa nyingi mno. Mfano mtu anayebuni gari la Rolls Royce au Bentley au Ferrari nk hao wanatengeneza pesa nyingi na hawachezi mpira wala hawaimbi R n B au pop!

Tatizo la watu wengi hasa huku kwetu ni kuwaza kuwa vipaji ni mpira na nyimbo na bongo movie basi. Yani kama hajui kuimba wala kucheza wala kuigiza basi. Katoto kakiimba kama Ali Kiba eti ndo kana kipaji.  Kali Kakichora chora ukutani kila siku katakemewa eti kanachafua nyumba.

Lakini point ya msingi hapa ni kuwa kipawa kinaweza kumpa mtu utajiri mkubwa. Kuna wanamichezo wanapesa nyingi mno. Kuna watu wa vipaji wengi wana pesa nyingi. Kuna watu wanalipwa mpaka dola laki 7 kuongea mahali. Yaani kwa saa moja. Imagine! Hiyo ni kama Tshs BILIONI MOJA NA MILIONI 400!!! Kwa saa! Sasa si unaona kipawa kinavyoweza kukufikisha mbali? So usingángáne tu na Bachelor of Law kama niliyosoma mimi. Dan Brown kitabu kimoja tu kinaweza kumpa dola milioni 10. Yaani BILIONI 20+! Hivi unaelewa? One BOOK. Sijui INFERNO sijui DIGITAL FORTRESS.

What’s your TALENT? Usidharau nguvu ya kipawa chako. Mungu atakushangaa na ATAKUADHIBU. Trust me. You MUST FIND OUT ni nini Mungu alikupa. Hakuna ambaye aliumbwa bila kupewa kitu EXTRA. Kila mtu anacho. Ndo wenzetu Ulaya wakikijua kwa mtoto wao wala hawahangaiki eti akasome "vidudu" afu aende primary school asome rundo la vitu kisha aende sekondari asome vitu kibao bado high school bado chuoni.  Wakati kumbe yeye mngempeleka kuendeleza kipawa cha kupiga mbizi tu kwenye mabwawa angetangaza nchi na umaskini kwenu ingekuwa bye bye. Lakini mlitaka tu awe daktari. Au mhasibu. Halafu sasa amekuwa what next? Ndo unakuta yeye akiwa kazini anawaza weekend ifike kuna mechi ya bonanza akacheze. Kipawa kilipotezwa.

Usidharau hii. Ukiitumia unaweza kufika bungeni na ikulu mpaka hata UN na wala form four hukumaliza. Wengine wamesoma mpaka maktaba inawajua na ikulu wanapasikia tu.


CONDITIONS ZA KIPAWA CHAKO KUKUFIKISHA KATIKA MAFANIKIO KIUCHUMI

Sasa hapa ndipo shule ilipo. Vipawa pia vina mahitaji yake.

1. Ubora wa team yako.

Moja ni kuwa ili kipawa kikuletee utajiri inahitaji TEAM WORK. Yaani lazima uwe na team ya watu wanaokuhandle wewe na mambo yako yote. Mfano angalia mtu kama Cristiano Ronaldo au Messi. Hafungi magoli bila team work. Yaani anategemea vipaji na creativity ya watu wengine kwenye team ili afike mbali zaidi. Ukimuweka Messi timu kama Mtibwa Sugar (no offense) hatawika kama anavyowika huko aliko maana huko aliko amezungukwa na professionals na watu wenye creativity na vipawa vya aina ya kwake pia.


Lakini pia Ronaldo au Messi ana kocha wa mazoezi binafsi, ana mshauri wa kisaikolojia anamlipa yeye, ana Manager wake binafsi, mwanasheria wake binafsi, ana mtaalamu wa chakula anayemshauri ale nini asile nini (huyu siyo mpishi ni mtaalamu tu yani nutritionist), ana daktari wake binafsi na wa timu pia yupo. Maana ukitegemea daktari wa timu afu akawa kwa mchezaji mwingine itakuawaje? Ana mtu wa mitindo mfano kinyozi na stylist wa mavazi kabisa,  ana mwalimu wa kufundisha mtoto wake nyumbani, ana designer wa nyumba na wafanyakazi wa nyumbani kama wapishi, watu wa usafi, gardeners, nk.

See? Haya yote watu hawajui wanapomshabikia Ronaldo au Messi au Tiger Woods. Au wanapoona analipwa pesa nyingi.

Sasa kama unataka kutumia kipawa kuufikia utajiri inabidi ufundishwe ukweli kama hivi. Usije ukaenda tu Bongo Star Search halafu hujui WHAT IT TAKES kukupelea kwenye mafanikio makubwa kupitia kipawa chako. Inahitaji investement kubwa mno. Na NIDHAMU YA MAZOEZI KUBWA SANA.

Na bahati mbaya sasa investment hii indo inakuwa tena BURDEN kwa mwenye kipawa maana ana watu wengi wa kuwalipa. Inakuwa MZIGO MKUBWA mno. So unashangaa mtu analipwa paundi 365,000 kwa wiki moja tu (yani $468,000/- yaani Tshs BILIONI MOJA) anazipeleka wapi? Unahisi ukizipata wewe utakuwa tajiri. No. Nilishasema hauwi tajiri kwa kupata hela nyingi ila kwa kuwa na MINDSET ya utajiri kwanza. Na kuhakikisha fedha inapita kwenye mfumo wa kuzaa tena.

Unaweza kusema hawa hela zao wanazitumia vibaya..no. Licha ya kununua majumba na magari ya kifahari na kufanya masherehe nk  lakini pia wanalipa watu wengi mno. Kama nilivyoainisha hapo juu. Tena hapo nimeweka vitu general tu. Na bado kodi ni kubwa balaa. 

Kwa hiyo kama una kipawa cha kuongea kama Joel Nanauka (Public Speaking) unataka kuwa kama kina Les Brown ama una kipaji cha kuandika pia kama mimi (Writing) na unataka kuwa kama kina Dan Brown ama kama kina John Maxwell basi unapaswa kujua kuna TEAM inahitajika. Nani atakuwa mentor wako? Nani atakuwa mtunza fedha wako? Nani atakuwa trainer wako. Mentor na trainer ni watu wawili tofauti. Kina Les Brown walijiandikisha katika madarasa ya DALE CARNEGIE ambaye alikuwa mtaalamu wa kufundisha kitu kinachoitwa Public Speaking.

Sikiliza... Dan Brown mpaka amalize kuandika novel moja anaweza kusafiri nchi 10 kukusanya data na kufanya mikutano na watu maarufu duniani na inamgharimu pesa nyingi na muda mwingi kuandaa manuscript hadi iandikwe.

Nani atakuwa MANAGER WAKO? Wa kuorganise wapi ukaongee na ulipwe shilingi ngapi nk. Usije ukawa wewe ndo kila kitu.  Messi hakufanya hivyo. Aliandaliwa.  Nani anakusaidia kujiandaa?

Changamoto kubwa ya watu wenye vipawa huku kwetu na hata duniani ni kuwa wanafanya kila kitu wao wenyewe. Kwa hiyo anakuwa hana tofauti tu na mtu aliyejiajiri. Anakuwa kama jongoo miguu mingi lakini spidi kidogo. Kipaji kikididimia naye anaishia hapo.
Lakini ukimtaka Les Brown aje Tanzania  sasa huongei naye yeye unaongea na watu wake. Yeye sasa ni TAASISI.
Hilo ni jambo la kwanza la kuzingatia. Tengeneza team around your talent. Skilled people. Uwalipe.

2. Vipawa vingi vina muda fulani tu.
Yes.
Changamoto ya pili ni timeframe. Hasa kwa wanamichezo. Kwa mchezo kama Soccer kuna muda wake. Umri ukienda mwili unakataa. Unastaafu bila kupenda. Tofauti na uandishi kwamba umri unavyokwenda ndo unazidi kuwa bora zaidi na zaidi.

Mbwana Samatta ana miaka chini ya 10 hivi ya kuhakikisha ameshatimiza ndoto ya kucheza timu kubwa maana vijana wadogo wenye  vipawa vikubwa ni wengi kwenye ulimwengu wa soka kwa hiyo anatakiwa ajitahidi mno. Kwa sasa ana miaka 24. Miaka mitano ijayo mwaka 2022 atakuwa na miaka 29. Hapo mwili umeanza kuchoka na wenye vipaji wadogo zaidi watakuwa wameshaibuka wengi. Ni vigumu kukuta bado akicheza timu kubwa Ulaya mwaka 2025. See? Huo ndo ukweli. Kina Msuva na Kichuya watakuwa wapi?  Ni lazima wafikirie.
Lakini Masudi Kipanya anaweza kuwa bado anachora kipanya chake mpaka hata 2050.
Ni muhimu kujua kipawa chako timeframe yake imekaaje.

3. Vyanzo vingi vya mapato.

Cha tatu ni kuwa lazima uwekeze maeneo mengine usitegemee kipawa chako tu. Katika wanamichezo wote ni Michael Jordan tu ambaye amefikisha utajiri wa dola BILIONI MOJA. Yani ndo yuko kwenye Forbes List ya binadamu  matajiri duniani. Nazungumzia athletes (wanamichezo kama mpira riadha nk) ni yeye tu bilionea. Yani yuko level kama ya Mo Dewji kwa utajiri. Si mchezo ujue.. lakini hii ni kwa sababu analipwa kwa matangazzo na ana miradi mingine zaidi na zaidi. Kwa hiyo kina Messi siju Ronaldo bado sana kufikia NETWORTH ya dola bilioni moja. Ndo maana unasikia Ronaldo kafungua mradi huu ama ule.

Ndo maana unaona kijana kama Diamond anawekeza kwenye sijui pafyumu, internet, radio stations (added) na mambo mengine. Ukisubiri hela za matamasha tu na mechi nk kuna siku kipawa kitaisha makali yake. Kipawa kina life span yake maana hata wewe mwenyewe una life span yako. Angalia watu hapa kwetu kama Mr. Nice. Walipata pesa nyingi lakini hana washauri hana plans hana team ya professionals wa kumshauri cha kufanya matokeo yake SEASON YAKE ilipopita akapotea. Juma Kaseja na Mrisho Ngassa season imepita. Kina Bombi wachekeshaji season imepita. Emanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji) amekwenda kwenye kilimo na biashara ya chakula na security na uchimbaji madini. Anatambua kuwa kuna siku Ze Comedy itakuwa hahiwiki tena. Sijui kama inawika tena kwanza.

Swali la kujiuliza je wewe una kipawa gani? Na umeshaanza kukifanyia kazi? Au bado? Una umri gani? Kipawa chako watu waliofanikiwa nacho walitumia MUDA GANI kufikia utajiri? Usiende tu.


GOOD NEWS IS UNAWEZA KUANZA SIFURI

Uzuri ni kwamba hata kama huna shilingi unaweza kuanza hapo ulipo. Mimi nimeanza kuandika 2013 kupitia hii mitandao ya kijamii. Sikuhitaji pesa. Labda bando tu.

Lakini pia nillianza kuandika kitabu changu cha kwanza 2015 ambacho nilikimaliza mwaka huo huo ila toka hapo nakirekebisha na kukipeleka kwa watu wenye mafanikio na upeo zaidi yani kuongeza ideas na kurekebisha na naamini itakuwa ni moja ya best books duniani.
Kiko kwa lugha ya kiingereza. It's a book for the nations. Nitakipublish miaka ijayo kwa neema ya Mungu kwani ninayafanyia kazi pia yale niliyoyaandika mwenyewe kuthibitisha usahihi wake katika kuleta matokeo.

Lakini pia mwaka jana October 2016 nilianza kozi ya Public Speaking na kuongeza uwezo mzuri zaidi wa kiingereza mpaka sasa naendelea nayo na kila siku nafanya mazoezi ya kiingereza na ya kuzungumza kwa sababu pia nina kipawa cha kuongea.
Kwa hiyo najiandaa tu zaidi. Siku nikifika kwenye World Economic Forum kuongea niweze kufikisha ujumbe kwa usahihi na kuwe na hiyo intelligibility.

Point ni kwamba. Nilianza hapo nilipo. Ni watu wanaoniambia kuwa naweza kuandika "vizuri". Mi napokea na kushukuru na kutendea kazi..
Nikienda mahali kuongea ni watu wanaoniambia kuwa naweza kufanya vizuri pia eneo hilo.
Point ni kuwa nimeanza nilipokuwa. Bila kitu. Na wewe unaweza kwa kipawa chako ulichonacho. Haijalishi nani anavuma sasa usiogope. Mentor wangu alisema one day kuwa ukitazama nje mchana kuna kunguru na ndege wengi tu wote wanaruka kuna mpaka mbu na vipepeo.  Vyote vina ruka na hakuna kinachosema "mbona nakosa nafasi ya kurukia". Smart man. So usiwaze kuhusu hilo.  Unaweza pia.

Lakini lazima uzingatie yale mambo matatu niliyoyasema pale juu: yaani team work na timeframe na kuwekeza kwenye vitu vingine.

Na pia lazima uzingatie kwamba ili uweze kukifanya kipawa chako kuwa biashara itahitaji uwe vitu vitatu: yaani bidhaa au huduma, system na team. Hili ni somo linalojitegemea.

Ukitambua kipawa chako unakuwa umetambua kama 50% ya kitu ambacho Mungu alitaka ufanye huku duniani.  Maana kipawa kitalitumikia KUSUDI. Na ukitambua kipawa chako ukaki develop basi hutakufa njaa wala hutakufa maskini. Mungu ali-make sure hilo amelifanya kabla hujaja duniani. Usimwangushe!

So ukisema SINA MTAJI Mungu anakuangalia tu. You have something in you.

Vipawa viko vingi. Usilazimishe kipawa cha kuimba huku wewe una cha kuigiza. Usilazimishe cha kuchekesha kumbe una cha kufikiri.

Tambua kipawa chako pasi na shaka. Ujue kabisa mimi niliwekewa hiki.


OK BYE..

Niishie hapo kwa sasa na  naamini utapa mwanga zaidi ili kujua uanzie wapi kama unataka kuitumia njia hii kuufikia utajiri. Ni imani yangu kuwa umejifunza kuhusu njia hii na wewe kama wewe unaweza kuona kama inakufaa au la.

Ila utaona tu kuwa siyo shortcut. Usijaribu kuwa tajiri kwa short cut. It takes time!

Asante sana kwa kuwa hapa na karibu kwa maswali maoni michango zaidi nk.

Much Love!


Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.
WhatsApp #o788366511
Blog: www.andreamuhozya.blogspot.com
May 30, 2017.

Maoni 2 :

  1. Asante, Kwa ujumbe mzuri

    JibuFuta
  2. Me, pia ninakipaji cha kuandika(writing) and I wish one day kila familia itakuwa unasoma kitabu changu. Asante

    JibuFuta