Ijumaa, 21 Oktoba 2016

JAMBO LA KUMI NA LA MWISHO (KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

JAMBO LA KUMI NA LA MWISHO
(KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

TUNAENDELEA:

Kwa neema ya Mungu naendelea ku-share mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia UHURU wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Na leo naendelea na sababu ya 10 na ya mwisho.

10. JAMBO LA 10: WAAJIRIWA WENGI HUISHIA KUWA WAOGA (MOST EMPLOYEES END UP BEING COWARDS)


SO WE ARRIVE.... Siku kumi za kujifunza pamoja.

Leo tutajifunza jambo la mwisho

Zamani nilikuwa nikijiuliza kwa nini wale watu ambao walikuwa na USHAWISHI (influence) sana shuleni ama vyuoni kwa nini wakiajiriwa ni vigumu sana kuwasikia tena. Mtu ambaye alikuwa akiitisha mgomo vijana wenzake Chuo kizima au shule nzima watu wanagoma mpaka wakati mwingine wanasababisha taifa zima kujadili hilo suala lakini akiingia kwenye ajira si rahisi kumsikia tena.
Wala kukuta akipewa cheo kikubwa labda.

Nikaja kugundua kuwa setup ya mfumo wa ajira ilivyo japokuwa inafanana na mfumo wa shule kwa maana ya ratiba lakini kuna tofauti kubwa ya PRINCIPAL au HEADMASTER na mtu anayeitwa BOSS aisee. Yani Principal wa chuo anaweza kuwa hata na elimu ndefu na umaarufu mkubwa nchi nzima lakini haogopwi kama mtu anayeitwa BOSS hata kama boss mwenyewe hata shule hakwenda ila ndo boss. Hapana chezea AJIRA.


Ni watu wachache sana... EXTREMELY FEW PEOPLE... ambao wako katika ajira na wana ujasiri katika mambo wanayoyaamini. Wengi wanapoajiriwa wanajifunza kuwa waoga. Bosi akiingia ofisini wengine hata mazungumzo yanakatayanakata
. Au mwajiriwa akiitwa ofisini kwa bosi yani automatically anajiset kuappear "vizuri" wakati alikuwa tu okay. Wengi hiyo inakuwa si kwa sababu eti heshima bali WOGA tu. Yani bosi akiingia ofisini ni shida...

~ wengine wanaweza kutetemeka hata kama kwa nje kajikaza. Anavibrate ndani kwa ndani. We jiulize kama wewe ni Mwalimu hivi Mama Ndalichako akitinga hapo shuleni bila taarifa hali itakuwaje. Woga. Kwani mmeua MTU nyie?

~ wengine hata anaweza kushindwa kuongea vizuri. Angalia Waziri akitembelea mahali hasa kwa idara zilizo chini yake.

~ wengine anaweza kutamani atoke katika mazingira hayo.

Confidence inaanza kuondoka taratibu.
Mwishowe wanahitimu katika UOGA.
Wanakuwa waoga wa vitu vingi.

~ Waoga wa kuomba kuongezewa maslahi.
~ Waoga wa kuondoka kazini kutafuta maslahi kwingine hata kama ni ajira nyingine
~ Waoga kabisa wa kujaribu kutafuta maisha katika mifumo mingine ya fedha nje ya mfumo wa ajira kama ujasiriamali au biashara. Yani aneshakuwa ADDICTED to kuishi kwa mfumo wa ajira tu.
~ Waoga wa kutoharibu kazi kwa sababu ya kuogopa itakuwaje akiambiwa kazi imeisha.


Mtu huyu anaanza kupoteza vitu muhimu:

1. Kwanza anapoteza UJASIRI.. Self confidence and hata self esteem.

2. Pili anapoteza HONESTY....hawezi kusema ukweli hadharani. Ila bosi akiondoka ndo unamsikia eti.."To be honest....." Hahaaaa

3. Mwisho anapoteza INDEPENDENCE OF THINKING.
Yaani hata angekuwa na mawazo au opinion tofauti vipi atasikilizia kwanza wenzake wanawazaje. Wanatakaje. Anaanza kuwa victim wa GROUP THINKING. Anasahau Mungu alituumba individually. Anasahau kuwa kuna vitu vya kukubaliana na wengine lakini when it comes to matters of PRINCIPLES zako unatakiwa usimame imara unshakable ukisimamia principles zako. Bosi akisema unaobey.


Kama wewe ni mwajiriwa jiulize hujawahi kucompromise principles zako kwa sababu ya kulinda "KIBARUA" chako? Kwamba unaamini hiki si sahihi hata aje nani na ukasimama imara kulinda msimamo wako! Come what may! Je ndivyo ulivyo katika ajira yako? Kwamba you can tell your boss to their face kuwa jambo fulani si sahihi hata kama itakuwaje ilimradi si sahihi?
Thubutu!

Ndo hii sasa kwamba kwa sababu kuna BOSS. MASTER. Hapo unajikuta unaCOMPROMISE kwa sababu mfumo huo umempa control yeye ya kudetermine mambo mengi juu yako. Unaogopa KUHARIBU kazi. Unaanza kujiuliza:

~ Watoto watakula nini?
~ Kodi ntalipaje?
~ Mkopo ntaumaliziaje?

Is that the mind of a free person?

Na wenzako "wanaokutakia mema" wanakuita kando wanakwambia "Aah, we huyu bosi mwache kama alivyo. We unadhani sisi hatuoni kuwa anakosea? We potezea tu atajiona mjinga"
Unapotezea.
Una compromise.

Hatimaye unakuwa miongoni mwao. Unakuwa muoga kabisa. Hata kama ulikuwa wewe ndo unaendesha migomo vyuoni.
End of your story.
Coz MAFAHALI WAWILI HAWAFANYI NINI.....?


And so..ndo hivyo...

Na kwa kuwa mada yangu katika hizi makala ilikuwa ni kuhusu uhuru wa kipato...then sababu hii ya mwajiriwa husika kuwa mwoga, na kuishi kwa hofu inamnyima uwezo wa kufikia FINANCIAL FREEDOM. Why? Kwa sababu uhuru wowote ule huwa mtu hapewi, huwa anautafuta na kuupata. Hata uhuru wa kisiasa w kifikra na hata huu wa kipato. No one will give it to you. Unapaswa kujifunza UKWELI kuhusu mfumo ambao wewe upo. Je mfumo uliopo wewe kuna mtu yeyote ambaye unaweza kuwa na access naye ambaye ametumia huo mfumo wa ajira akafikia uhuru wa kipato? Kwamba hahitaji tena kwenda kazini ili kuingiza pesa labda aende tu sababu working is a mark of NOBILITY? Je yupo unayemjua ambaye alimake FORTUNE kupitia ajira ili walau ukajifunze kwake? Jipe jibu.
Na kama yupo je wewe na yeye mpo katika footing sawa? Tafuta kujua ukweli.


TRUTH shall set you FREE.


And so I rest my case, for now. Nimezungumza mawazo yangu kwa siku 10 sasa. Naamini nimetimiza wajibu wa kutoishi na mawazo muhimu bila kuwashirikisha wengine ambao huenda yanaweza kuwasaidia.

Na kama ulisoma makala zangu hizi toka mwanzo utaanza kuona kuwa sababu zote nilizoelezea kuanzia ile ya kwanza hadi hii mwisho zinafanya kazi kinyume cha MWAJIRIWA linapokuja suala la kufikia uhuru wa kipato. Ziunganishe utaelewa vizuri. Again..Don't read them in isolation.

Na mpaka hapo nimefikia mwisho wa mfululizo wa makala hizi.

Asante sana kwa kuwa nami tangu mwanzo mpaka leo.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS, WhatsApp and Calls: +255752366511
WhatsApp Only: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com

Barikiwa Sana!


Semper Fi great people,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni