Jumanne, 11 Oktoba 2016

MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO

MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO


UTANGULIZI:

Nina siku 10 kuanzia leo ambazo kwa neema ya Mungu nitashare mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia uhuru wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Ninapozungumzia uhuru wa kipato ninachomaanisha ni uwezo wa kufikia hatua pesa ikawa siyo tena kikwazo cha kufanya chochote unachotaka kufanya. Mfano ukihitaji kununua kitu chochote basi pesa isiwe ndo kikwazo. Mfano unahitaji kununua labda gari lolote mfano LANDROVER la make yoyote mfano RANGE ROVER la rangi yoyote mfano RANGE NYEUPE (ranla mwaka wowote mfano toleo la mwaka ujao 2017 basi kikwazo kisiwe ni pesa. Huo ndio uhuru wa kipato. Ni mfano tu. Au unahitaji mwanao asome shule yoyote yenye ada yoyote hata kama ada ni milioni 30 kwa mwaka kikwazo kisiwe pesa. Kama unataka kununua kiwanja au nyumba nchi hii mkoa wowote labda hapa Dar mahali popote labda Masaki au Oyster bay basi kikwazo kisiwe pesa. Hiyo ndiyo Financial Freedom ninayoelezea hapa. Au unataka siku moja umiliki Private Jet. Kikwazo kisiwe pesa.

Ndo nasema kuna mambo 10 yanayomzuia Mwajiriwa kutoweza kufikia UHURU WA KIPATO.


1. JAMBO LA KWANZA:
KUINGIZA KIPATO LAZIMA UWE NA UWEPO KUFANYA KAZI. (YOU MUST SHOW UP PHYSICALLY)


Sasa hili ni jambo la kwanza ambalo waajiriwa wengi huwa hawalitilii maanani. AJIRA ni mfumo mmojawapo wa kutengeneza kipato. Mfumo mwingine ni BIASHARA.

Sasa ajira kama mfumo wa kutengeneza kipato ni mfumo unaohitaji uwepo wako katika eneo lako la kazi ili uweze kutengeneza fedha. Kwa hiyo unalazimika kubadilishana muda wako wa maana (PRODUCTIVE HOURS) kumpa mtu ambaye anahitaji umfanyie jambo fulani kwa kubadilishana na fedha. Sasa kama umeajiriwa naomba nikuulize maswali machache..


SWALI LA KWANZA:
Huoni tatizo katika hilo la wewe kuuza muda wako? Huoni tatizo kuuza kitu ambacho huwezi kukirejesha tena (A NON-RENEWABLE RESOURCE) na wewe kupewa kitu ambacho unaweza kukipata tena (RENEWABLE RESOURCE)? Yes. Muda unaouuza huwezi kuupata tena. Kama umeshauza muda wa masaa 9 kwa siku tano kwa juma kwa muda wa miaka 10 hadi sasa jiulize kama huo muda unaweza kuurejesha tena. Afu unalaumu nchi inauza madini (non renewable resource kama wewe) kwa bei chee kwa njaa ya miaka michache? Are you kidding me?

Hellooo...

Mfano ulianza kazi ukiwa na miaka 30 sasa una miaka 40. Je muda huo wa miaka 30-40 ambapo ndo una nguvu nyingi za mwili na akili iliyoanza kukomaa vizuri na creativity ya hali ya juu na uwezo wa kufanya mambo mengi mapya je unaweza kuurudisha? Jibu ni HAPANA. Muda huo ulishauuza for good! Ni kama almasi za Mwadui. It's gone forever. Miaka kadhaa ijayo ardhi ya mwadui nk itabaki macho kodo!

SWALI LA PILI:
Je fedha ulizotengeneza kwa kipindi chote ulichoajiriwa mfano Tshs milioni 2 hivi ya GROSS SALARY kwa mwezi (hata kama ulianza na mshahara wa 1m or less tufanye tu flat rate ya 2m a month) kwa miaka 10 yani total ya Tshs milioni 240 kwa miaka 10, je hiyo pesa ni impossible kuitengeneza pasipo kuajiriwa? Yani wewe unaona huna uwezo kabisa kabisa wa kuzalisha GROSS income ya Tshs milioni 240 ndani ya miaka 10 kwa njia zingine zozote (halali) bila ajira? Kumbuka hiyo milioni 240 hujapata yote. Kuna ambayo iko NSSF utapewa siku ukifika miaka 55 kama sheria itapitishwa. Is it true kuwa pasipo ajira uliyonayo huwezi kuzalisha pesa ulizowahi kuzalisha toka siku umeajiriwa hadi leo? Au umekuwa brainwashed kuamini kuwa huwezi? Yani kama mwajiri wako ameweza kupata na hana elimu kama ya kwako wala mawazo kama ya kwako wala hajui hata definition ya materminology uliyosoma huko shuleni wala hana kiingereza kama cha kwako cha BabbroJahansen sijui Babbro nini. Wala hana cheti cha Chuo Kikuu wala hata hakumbuki mara ya mwisho darasani alisoma topic gani. Kama huyo kaweza na wewe huwezi basi hiyo ndo tafsiri ya wewe kuwa BRAINWASHED. Na kwa sababu uko brainwashed basi you're not receptive of new ideas. Mindset closed. Na ndo hujui kuwa kitendo cha kupata kipato kwa kulazimika kwenda kufanya kazi kwanza huoni kama ni shida. Hujafahamu kuwa unaweza wewe huyo huyo ukabuni kitu kipya kwa muda wa miezi 6 tu au hata ikikuchukua mwaka au hata miaka mitano na baada ya hapo ukaanza kuingiza kipato 24/7 kama MaxMalipo. Wengine wenu mmeajiriwa mna uwezo wa kuzalisha Tshs milioni 240 kwa mwaka mkiamua. Au hata kwa mwezi mmoja tu. Wengine nyinyi ndo solutiin ya matatizo ya watoto yatima au maji vijijini. Mna miradi mikubwa kichwani but umekaa hapo. Unafurahi kuitwa Meneja Mauzo wa..... Au IT SPECIALIST wa naniliu Tanzania Limited. Nipo hapa kukupa nguvu mpya kuanza safari ya kubuni au kufanya kitu kipya (mfano biashara) ambacho kina POTENTIAL ya siku moja kuja kukupa pesa hata ukiwa umelala is a SIGNIFICANT STEP IN THE RIGHT DIRECTION. Kuliko kuendelea kufanya kitu ambacho hakina hiyo potential kamwe. Kama huniamini mimi fanya hivi:

JIFUNZE KWA MUNGU
Kwa mujibu wa Biblia Mungu aliumba kila kitu kwa SIKU SITA tu. (Mwanzo 2:1) Alichokifanya alivipa tu hivyo vitu uwezo wa ku"REPRODUCE" (Mwanzo 1:28+29).
That's a system ambayo Mungu alitaka tujifunze. Kwamba siyo lazima uumbe kila siku. Unaweza kuumba kwa siku 6 tu na after that ukapumzika (siyo kwa kuwa umechoka no. Bali kwa kuwa umeshaweka SYSTEM ya kukupa results unazotaka. Veeery *SMART.* Isn't it?

Kampuni unaibuni once. Biashara unaianza once. Mradi unauanza once. Hiyo once inaweza kukuchukua six days or even six years etc. But ukishauanza unajenga tu SYSTEM. It is POSSIBLE. Matajiri wanamuiga Mungu. Maskini  sijui wanamuiga nani hata...
Seriously. Maana hata kwenye eneo la #utoaji kuna tofauti sana kati ya makundi haya mawili. Think about it.

So kwa nini usifanye kama Mungu? Create something once and put a system ambayo itakufanya upate kipato 24/7 mpaka siku ukifa wanaendeleza wanao ulipoishia nk. Sasa wewe kila siku unadai unafanya kazi kwa sababu ya Junior. Ooh Junior mwanangu sitaki apate shida. Ok sawa. Sasa hiyo ajira ukifa huyo Junior ndo atapewa kazi yako? Uliona wapi? Umejiandaaje sasa? See. Unatiririka. Sawa. Very good. Endelea tu.

SWALI LA TATU KWAKO:
Tunaendelea. Je hiyo Tshs Milioni 240 uliyoipata ndani ya miaka 10 kwa mfumo wa ajira imeshakupa angalau DALILI yoyote ya kwamba kuna siku utakuwa na Uhuru wa kipato pia? Maybe miaka 10 ijayo tena? Kwamba kwa mfumo huo wa AJIRA utaweza kusomesha mtoto wako shule atakayopenda hata kama ni IST na siyo unayoweza kuafford? Nk. Kuna hiyo dalili? Au unaendelea kutiririka tu kwa sababu "NDO MAISHA BANA". Kweli? Think about it.

Hii ndo shida ya kwanza (first limiting factor) wasiyoiona waajiriwa wengi. Ni wachache mno wanaoona kuwa ni shida. Kwamba pesa haiji hadi uende to a SPECIFIC PLACE ukaperform SPECIFIC DUTIES kwa a SPECIFIC TIME ndipo pesa iingie.

Uliwahi kujiuliza itakuwaje kama utaondoka kwenye mfumo wa kulipwa kwa masaa 9 na ukaweza kulipwa kwa masaa 24? Kama bwana Zuckerberg ambaye analipwa 24/7 awe amelala amesafiri, nk. Kuwaza kuwa ili uingize kipato lazima uende "ofisini" ni traditional thinking ambayo ndo inatafuna jamii hasa vijana wadogo ambao sasa wanasoma ili wakaajiriwe.  Mfumo wa ajira ni an financial dead end.

Usione watu wanahangaika na matikiti na kufuga kuku. Inaweza isimfikishe mbali but ndo hicho nilichosema ni *SIGNIFICANT STEP IN THE RIGHT DIRECTION.* Anajifunza. Huwezi kulingana Nate mawazo huyo. Unajua kitu kipya. Wengine anahitaji tu msaada wa mtaji zaidi au mafunzo muhimu ya kumsaidia. Wewe upo tu kazi yako kucheka. Umesahau *FAINALI UZEENI*. Sikia ndugu. Ukiona mjasiriamali anahangaika usimcheke. Huenda anaumba dunia yake. Na bado yuko "siku ya kwanza" ndo ameumba tu usiku na mchana. Bado huoni kama ksumba cha maana. I tell you wait and see. Salute kwa fighters wote. Keep going. Keep "umbaring" your dunia!💪🏻💪🏻💪🏻

BOTTOMLINE
Bottomline ni kuwa kuingiza kipato kwa mwajiriwa kunategemea yeye KWENDA kufanya kazi. Usikariri. Mungu aliumba Adam, Adam akazaana huko mbeleni. System. Kuzaana ni SYSTEM ya Mungu ya kuumba. Sasa wewe unataka KUUMBA kipato kila siku hadi siku unastaafu? Ukiacha kuumba no kipato. Why? Coz huna system. umesahau kuwa wewe unaoperate kwenye SYSTEM ya mwajiri wako. Ambaye anaweza asije kazini na kipato kikaendelea kuingia kwake. Kaweka system. Wewe ndo ADAM NA HAWA wake. Unareproduce kwa niaba yake.
Amejifunza kwa Mungu.
Wewe umejifunza kwa nani my friend. Mungu huyo huyo?

Hiyo ndiyo kikwazo cha kwanza cha kumzuia Mwajiriwa asifikie kamwe FINANCIAL FREEDOM.
Leo naishia hapa. Kesho kwa neema ya Mungu nitaendelea na LIMITING FACTOR YA PILI.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS and Calls: +255752366511
WhatsApp: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com.

Barikiwa!


Semper Fi


Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni