Alhamisi, 27 Oktoba 2016

IT TAKES "A LITTLE EXTRA" TO MAKE A DREAM COME TRUE


Katika zawadi kadhaa nilizowahi kupata maishani mwangu ambazo zilibadilisha maisha yangu moja wapo ni kadi ya kunitakia mafanikio mema katika mitihani yangu ya kumaliza kidato cha sita.

Kadi hiyo niliipata kutoka kwa walezi wangu Mr & Mrs Senga Kabipi aka baba na mama Laurent Kabipi. Nikiwa nimepitia mabonde na milima hadi kufikia kipindi cha mimi pia kuikabili NECTA ya Form VI, kadi hiyo ilikuja  katika kipindi muafaka sana ambacho nilikuwa nikihitaji binadamu yeyote wa kunitia moyo na kuniambia nitafanikiwa. Ninakumbuka daima nilivyotiwa nguvu na kitendo tu cha kupewa ile kadi. It was so powerful!

Hata hivyo ni maneno yaliyoandikwa kwenye hiyo kadi ambayo yalinifanya niikumbuke zaidi ile kadi hadi leo. Yalisema hivi:

Dear Andrea,

It takes A LITTLE EXTRA..

A LITTLE EXTRA COURAGE

A LITTLE EXTRA HOPE

A LITTLE EXTRA BELIEF

A LITTLE EXTRA PUSH

A LITTLE EXTRA STEP

It takes A LITTLE EXTRA EFFORT...

....TO MAKE A DREAM COME TRUE.

Wishing you all the best in your exams,

Yours,

Mr & Mrs Kabipi.

That was it. So baada ya kufurahi nikaanza kujiuliza kuhusu ujumbe huo. Nikawaza kweli eti. Huu ujumbe mbona unanipa mawazo tena. Bado siku mbili kufanya NECTA. Nimeshasongoka miaka miwili mizima nimejiandaa nimeshajiamini kuingia kwenye NYAMBIZI la Makongo High School. Afu naambiwa #EXTRA tena? Lakini moyoni nikasema Mungu huenda ameniletea ujumbe muhimu mno kunisaidia si tu kwa mitihani yangu bali hata maishani. Nikaazimia kufanya hiyo extra. Walimu walisema usisome hadi siku ya pepa mi nikasema nitafanya EXTRA. Sitaenda kwenye mtihani wowote bila kufanya EXTRA. Nilifanikiwa kufanya vema mitihani yangu na nilishukuru kwa zile EXTRA nilizofanya kipindi chote cha wakati wa NECTA.

Ni miaka mingi imepita now na nimekuja kugundua kumbe ndoto nyingi hufia mlangoni. Maono mengi hufia karibu na kuzaliwa. Mafanikio ya watu wengi hushindwa kuwafikia kwa sababu tu ya kutofanya kitu EXTRA. Just some little extra stuff. Angalia watu wote waliofanikiwa duniani katika kila eneo. Iwe ni siasa, michezo, dini, biashara nk. Wote kuna kitu kidogo tu EXTRA wanafanya. Kuna wakati nilisikia kuwa Cristiano Ronaldo alikuwa wakimaliza mazoezi kocha akiwaruhusu kuondoka yeye anabaki anaanza kufanya mazoezi kidogo EXTRA. Huenda ikawa penalties au free kicks etc. Kidogo tu. Afu ndo anaondoka. A little EXTRA. Sets him apart.

Angalia wanamuziki waliofanikiwa. Siyo kipaji tu. Vipaji viko lukuki. Lakini nani yuko tayari kufanya that little EXTRA. Akae studio kwa muda extra kidogo. Akienda gym kwa ajili ya mazoezi ya pumzi basi azidishe muda kidogo tu EXTRA. Akifanya mazoezi ya vocals afanye kwa muda kidogo tu EXTRA. Nitajie ni nani na utakuta ni ambaye tayari ni jina kubwa kabisa!

Angalia watu wengi wanaopanda vyeo makazini kihalali. Wamefanya kitu kidogo EXTRA. Huwezi kufanya EXTRA halafu Mungu akakuacha. Never. Uwe mpagani uwe mnini kanuni za mafanikio si za dini ni tabia inayobidi kujengwa.

Angalia wafanya biashara waliofanikiwa lazima utakuta kuna hicho kitu EXTRA katika maisha yao. Anaamka mapema kidogo au kulala late kidogo. Siyo late akiwa anatuma katuni katuni WhatsApp no. Labda anasoma kitu fulani EXTRA. Au anasaidia wengine a little EXTRA. Kuna kitu EXTRA Dewji amefanya, siyo suala la kurithi. Wamerithi wangapi?

Angalia watu wanaokuwa wahubiri wa kimataifa. Utakuta kuna kitu anafanya EXTRA. One more EXTRA foreign language. Maombi kidogo EXTRA. Kufunga kidogo EXTRA. Kusoma NENO kidogo EXTRA. Nk. Hata Mtume Paulo ana nyaraka nyingi kuliko mitume wengine kwa sababu ya hiyo EXTRA.

So swali la kujiuliza kwa wewe unayetaka kufanikiwa maishani ni hili: NI KITU GANI EXTRA UNAFANYA AMBACHO WENGINE HAWAFANYI? Kama huna any little EXTRA basi utakuwa wa kawaida. Just ordinary. Just any Thom, Dick and Harry. Afu kila siku unajiambia  "MUNGU ALINIUMBA KUWA EXTRAORDINARY" Ni kweli kabisa. Lakini Mentor wangu mmoja alisema  tofauti kati ya ORDINARY na EXTRAORDINARY ni hiyo EXTRA tu. Ukiondoa EXTRA katika EXTRAORDINARY unabaki na ORDINARY. Sasa kama unakiri uliumbwa kuwa EXTRAORDINARY halafu huna kitu EXTRA unachofanya daily basi mtajuana na muumba wako ambaye bado amekupa uhai hadi sasa.

Azimia leo kufanya hizo EXTRA ndogo ndogo. You will definitely become EXTRAORDINARY.

Don't forget,

IT TAKES "A LITTLE EXTRA" TO MAKE A DREAM COME TRUE.

Barikiwa sana.

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
#o752366511
Tanzania,
East Africa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni