Jumamosi, 15 Oktoba 2016

JAMBO LA TANO (KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

JAMBO LA TANO
(KATIKA MAMBO 10 YANAYOMNYIMA MWAJIRIWA YEYOTE UWEZO WA KUFIKIA UHURU WA KIPATO)

TUNAENDELEA:

Kwa neema ya Mungu naendelea ku-share mambo 10 (yani jambo moja kwa siku) yanayomnyima mwajiriwa uwezo wa kufikia UHURU wa kipato. Kwa maana nyingine ataendelea kuwa mtumwa wa kipato).

Na leo naendelea na sababu ya 5.

5. JAMBO LA TANO: HAKUJAWAHI KUWA NA  AJIRA SALAMA... (THERE'S NEVER BEEN THE SO-CALLED "JOB SECURITY", AND NEVER WILL THERE BE ANY)

Leo sianzi na swali. Naanza na ASSIGNMENT hahaaa. Usiseme hee shule tena? Usijali. Ni fupi tu.

(Assignment):
Kama wewe ni mwajiriwa mahali popote naomba chukua kalamu la karatasi. Kisha andika sababu 10 ambazo unadhani zinakupa UHAKIKA wa kumaliza huu mwaka ukiwa kwenye hiyo ajira. Huu mwaka tu. I'm serious. Write them down. Labda..

1. Mchapakazi
2. Mwaminifu na Mwadilifu
3. Una elimu kubwa zaidi
3. Bosi ni Ndugu Yako, (au mchepuko), nk
4. Una kipaji kimoja unique sana so lazima waendelee kukuajiri.
5.
6.
7.
8.
9.
10.

Andika usiache. Halafu ukimaliza kuziandika utagundua hakuna hata moja ambayo inakupa UHAKIKA kuwa ajira yako iko SECURE(salama).
None!

Huenda hukubaliani na mimi kwa sababu unazoziamini sana. Lakini ngoja nikupe sababu chache kwa nini JOB SECURITY IS A MYTH. Ni kitu kisichokuwa halisi.

(I). HUNA CONTROL NA MAWAZO YA BOSI WAKO.

Na katika ubinadamu kuna mengi. Anaweza asikupende tu. Kaamka na hasira zake akakuanzishia visa tu. Au kama ana mamlaka ya kukufuta akakufutilia mbali asubuhi. Unabisha? Kuna watu walifukuzwa kazi katika mazingira yasiyoeleweka. Yani bosi wako anawaambia wamiliki wa kampuni: MNANITAKA MIMI AU HUYU? Wamiliki wanaamua kukusacrifice wewe hata kama hawajaelewa? Unadhani haliwezi kutokea kwako?
Au unafuta katika Jina la Yesu. Basi sawa. Endelea kufuta bila maarifa. Unajua hata ukiwa unachora picha na penseli inabidi uwe una maarifa ya kuchora. Usitegemee kufuta tu. Ufutio utaisha na picha haiko. "Watu wangu wanangamizwa kwa kukosa maarifa" ~ hilo ni NENO la BWANA. Sasa wewe endelea kufanya Yesu kuwa "ufutio" wako utauona mwisho wake.

(II). HUNA CONTROL YA MAPATO YA SEHEMU YAKO YA KAZI

Inawezekana sasa hivi mnapata pesa pesa kidogo hivyo siyo shida kukulipa wewe huo mshahara. Ikitokea competition ya maana sokoni kampuni yenu ikakosa kuona faida cha kwanza wanaangalia wapi pa kupunguza MATUMIZI. Unaweza ukajikuta huna ajira na hutaamini. Naamini ushajipanga pa kuanzia.
Hapa ndipo ninaposhauri ukasome kitabu muhimu sana cha mtu anaitwa Dr. Spencer Johnson kiitwacho WHO MOVED MY CHEESE?
Utaelewa. Usije ukadhani ajira ni yako. Ajira ni ya mwajiri tu. Wewe umekodishwa kwa muda tu. Anytime mwenye nayo anaichukua. Afu na wewe utaanza kuuliza WHO MOVED MY CHEESE? Kweli? "Your" cheese?

Unaikumbuka UCHUMI Supermarket? Ilikuwa imeajiri watu wengi siyo. Ikafunga ofisi zake. Halafu inakuwaje sasa.
What about ada za hao watoto wako. Au ndo elimu bure! Kuna kitu cha BURE kweli dunia hii? It's not free. There's no free lunch wazungu wanasema. You'll somehow pay for it in a different way.
Think. It's still LEGAL to think.

Halafu mwingine akiona unaongelea sijui Uchumi Supermarket yeye anaona haimhusu. Anajisemea Kwanza Mimi Mwalimu. Ajira UHAKIKA. Unafikiri kutumbuliwa ni kwa Wakurugenzi tu na wakuu wa mikoa? Umesahau methali ya MWENZAKO AKINYOLEWA.....

(III). HUNA CONTROL NA UWEPO WA MWAJIRI AU BOSI MPYA

Kumetokea mara kadhaa makampuni kwa sababu kadha wa kadha yameuzwa au kuingia ubia. MERGERS AND ACQUISITIONS. Huwezi kuzuia. Hapo unajikuta chini ya bosi mpya au mwajiri (kampuni) mpya.

Kuna kampuni inaitwa Yahoo! Sijui kama kuna kijana wa mtandaoni asiyeijua. Ilikuwa MAARUFU. Wakitengeneza pesa nyingi. Wakiajiri watu wengi. Siku moja BILL GATES (MICROSOFT) akaamua kuwa itakuwa dili nzuri akiwanunua. Kwa sababu uwezo anao akawanunua. Yani unanua kampuni na wafanyakazi wake wote. What happened later? Unajua? Kama hujui ni kwamba baada ya kununua Yahoo! MICROSOFT wakaona wana mzigo mkubwa sana wa waajiriwa. Wakaamua kupunguza waajiriwa 800!!!! Wengi kati yao wakiwa waliokuja kutoka Yahoo!. Hapo unalipwa stahiki zako unaenda. Sasa security ipo wapi? Hivi kama Bill Gates anapunguza watu 800 hujiulizi.

Juzi juzi hapa kwetu kuna kampuni maarufu ya Africa Barrick Gold (ABG) maarufu kama Barrick ambayo iliuza baadhi ya hisa zake kwa ACACIA na hivyo kuipa ACACIA uwezo wa kufanya baadhi ya maamuzi kuhusu ajira. Watu wamepoteza ajira katika mazingira hayo.

Sasa nini kinaweza zuia Vodacom au Tigo au Twiga Cement au ITV au TCC (Sigara) au CRDB wasifikie huko. Soma alama za Nyakati. NBC iliuza baadhi ya hisa zake kwa ABSA Bank ya South Africa na ABSA hisa zao nyingi zinamilikiwa na BARCLAYS BANK ya Uingereza. Sasa hapo nani mmiliki wa NBC? Afu wewe hutaki kusoma THE WRITING ON THE WALL.
Stanbic Bank ilikuja Tanzania kwa kununua MERIDIAN BIAO kuna watu wakipoteza kazi enzi hizo.
Unajua mwenye hisa nyingi Fastjet ni nani?
TBL je?
Vodacom je?
Unajua nani mwenye hisa nyingi?
Unajua maamuzi yake anafikiria nini kichwani?

See. So, ajira ni a sort of gambling. Kamari. Hujui hata keshokutwa tu kama ajira yako itakuwa salama.

Sasa Uhuru wa kipato hapo hauwezi kuja kamwe.

Unakumbuka transition ya kutoka SHOPRITE kwenda NAKUMATT? Siku hizi naona kuna wakenya mle wameajiriwa kwa kazi ya kuoka mikate. Sijui kama wote waliokuwa Shoprite wamepata nafasi Nakumatt.

Wakati nakuja jijini kulikuwa na hoteli maarufu sana SHERATON, baadaye mmiliki akabadilika akaitwa MOVENPICK, baadaye akaja mwingine ROYAL PALM, saivi yupo mwingine SERENA. Hivi kinachomzuia Serena kuajiri mtu mpya kwenye nafasi yako ni kipi? Ask yourself.

(IV). HUWEZI KUJUA MAAMUZI YA SERIKALI KUHUSU SEHEMU YAKO YA KAZI AU AJIRA YAKO

Kuna mtu alijua kuna uhakiki wa vyeti ungekuja?
We unajua baadaye watahakiki nini?

Serikali inaweza kulipiga marufuku shirika unalofanyia kazi kwa madai ya kujihusisha na labda USHOGA. Hapo ajira yako vipi?
Sijui magazeti na redio vikifungiwaga kwa muda usiojulikana huwa ajira zinakuwaje? Wanaendelea kulipwa mshahara bila kuzalisha?
Serikali inaweza kuja na maamuzi ya kurasimisha jambo au kuharamisha jambo ambalo likaathiri ajira yako moja kwa moja.
Au kuanzisha sheria ya kuajiri watu waliopita JKT kwanza na waliopo kazini waende JKT pia ndo waendelee na ajira. Utakataa?
Au huamini kuwa hilo linaweza kutokea?
Kwani mjadala wa FAO LA KUJITOA uliwahi kufikiria kuwa utakuwepo?
Nini kinazuia serikali kufuta ajira za shirika fulani na kuajiri upya? Sasa hapo undugu wako na bosi ndo utajua. Kama rais anaweza kumtaja mke wa Waziri kung'ang'ania ajira itakuwa wewe na huyo bosi ambaye ni ndugu yako?
Unategemea undugu?
Serikali ikifanya maamuzi ya kubadilisha wakuu wote wa idara zote nyeti ukapata bosi mpya?
Unategemea nini
Kipaji?
Uadilifu?
Hujui kuna watu hata uadilifu wako hawana time nao. Hawakutaki tu wewe. Licha ya uadilifu.

(V). HUNA CONTROL NA TEKNOLOJIA KUREPLACE AJIRA YAKO

Unafahamu kitu kinaitwa teknolojia. Basi welcome to the future.

Kuna watu walikuwa wameajiriwa kwenye call box miaka ya nyuma. Kuna makondakta wanapoteza kazi kwa mfumo wa mwendo kasi. Tunakoenda dunia hii ni treni za umeme madereva mpo? Ulaya sasa  kuna electric cars.
Watoto wanaosomea urubani kuna ndege hazina rubani now.
Kuna DRONES now..
Nani kati yetu aliwaza miaka 20 iliyopota kuhusu drones.
ThreeD videos?
Sasa hivi teknolojia imefikia unaweza kupima damu yako au mapigo ya moyo kwa kutumia Application kwenye simu yako!
Sisi huku bado watu wanafanya kazi ya kuajiriwa kujaza mafuta kwenye magari Petrol Station.
Teknolojia imeshaondoa hizo vitu nchi za wenzetu. It's a matter of time huku  kwetu yatafika.
Nchi za wenzetu kuna mahali hotelini ukienda restaurant ni self-service hakuna hata mhudumu wa eti akupakulie. No, unapakua mwenyewe ukimaliza kula vyombo unaweka kwenye conveyer belt vinapelekwa kwenda kuoshwa na machine.
Sasa wale mnasomea kuajiriwa kwenye Restaurant Mahotelini...
Subiri uone siku tukiwa na angalau umeme wa uhakika ndo mambo mengi yataibuka hujawahi kuona. Ajira nyingi miaka 20 ijayo hazitakuwepo. Technology is taking over baby! Sasa unasemaje una uhakika na ajira yako wakati teknolojia ikibisha hodi tu ajira yako inakuwa past tense.


Kazi nyingi za kufanywa na binadamu zinaenda kuwa replaced na computer. Unadhani komputer haiwezi nini sasa hivi?

~ Kupika?
~ Kuendesha gari?
~ Kupanga mafaili?
~ Kupiga muhuri?
~ Kutegua mabomu?
~ Kufagia na kufuta vioo?
~ Kushona nguo?
~ Kupokea wageni?
~ Kufanya interview?
~ Kuendesha ndege?
~ Kuongoza magari barabarani?
~ Kupakua mizigo bandarini?
~ Kufanya utafiti wa wapi kuna madini na wapi kuna udongo wenye rutuba?
~ Kuandaa risala?
~ Kutambua mhalifu?
~ Kujua kitu anachowaza mtu?
~ Kufanya auditing?
~ Kuandaa ripoti?
~ Kutoa tahadhari (prediction) kuhusu hali ya hewa au ujio wa Tsunami?
~ Kutangaza mpira?
~ Au kumoderate mdahalo?
~ Kupokea simu?
Kwani unapopiga simu na kuambiwa sijui bonyeza nyota.. Unadhani ni MTU yule? Si automation tu. Na majibu unayapata.


Kuna mtu akisoma baadhi ya vitu hapo juu anashangaa anasema aah wapi?
Huamini kuwa one day computer itafanya virtually everything? Basi hujaijua computer ninayozungumzia hapo juu. Tunaongelea computer mbili tofauti kama huamini kuwa in future mtu anaweza kuingia benki na kusiwe na mhudumu hata mmoja wala hata mlinzi!!! Welcome to the microchip world bruh!
Nahmean?
Sasa hivi watu wanatengeneza BURGER maabara. Hahaaaa. Watu wana gari isiyo na Dereva.
Anyway.

Fanya hivi ingia FACEBOOK kaangalie page inaitwa #FUTURISM. Usiache. Utapata picha dunia inaelekea wapi..

Sasa..
Ukitoka kwenye hiyo page ujiulize ajira ngapi zitapotea kwa computer kufanya vitu vyote hivyo kwa UFASAHA bila kukosea hata kidogo au kwa advancement hiyo ya teknolojia?
Uliwahi kuwaza mwaka 1999 wakati wa Floppy Disks kuwa kuna siku tutakuwa na kichip kidogo kinaitwa memory card chenye uwezo wa kutunza kumbukumbu za sheria zooote za nchi na regulations zake na ka-chip kenyewe kako kama ukucha tu.!!

Sasa piga mahesabu miaka 20 ijayo.

That's the future we are facing.  But most of us are so enstranged to the reality we do face. Total strangers to reality.
Teknolojia itaondoa walioajiriwa shambani, kiwandani mpaka sokoni. Sasa wataenda wapi? Ndo ujue Mungu alichoweka ni KAZI si AJIRA. Coz ajira ikiwa haipo still things can go. With technology.

Sasa ukikaa katika ajira mpaka siku uambiwe hatukuhitaji kwa sababu tumeleta hii mashine inaweza kufanya kazi zako kwa usahihi sijui utaendelea kufuta kwa Jina la Yesu? Maarifa.
Afu vijana wanasoma BANKING AND FINANCE wakaajiriwe kama Bank Tellers wakati sasa hivi kuna ATM za mpaka kuweka hela benki dunia hii.
Bill Gates ana mradi wa Tsh Trilioni 150 wa kuangamiza mbu duniani ili kuondoa Malaria kabisa. Sasa kama umeajiriwa shirika la kudeal na malaria hiyo ndo future yako.

Sasa basi kwa mazingira hayo ya kutokuwa na control ya source yako ya income (ajira) sahau kuhusu financial freedom. It just can't happen in that setup. Kupata uhuru wa kipato unapaswa kuwa na uwezo wa kucontrol source yako ya income.

Anyway.
Hayo ni baadhi ya mambo machache tu yenye lengo la kukupa picha ya hali halisi kuhusu AJIRA. Kwamba ajira haina usalama wowote kama unavyodhani. Kama wewe pia umeajiriwa kwa kigezo cha ajira kuwa na job security.

Lakini katika pita pita zangu huku na kule nimekuwa nikikutana na waajiriwa wakisema:
"Mwenzako nina ajira angalau nina UHAKIKA wa kuingiza kitu". Kama swala ni UHAKIKA wa kuingiza kipato basi utakuwa hujajua vizuri kitu kuhusu ajira. Ieleweke kwamba siko hapa kukwambia acha kazi. That's your business. Mimi nipo kukwambia kwa nini ajira siyo mfumo sahihi wa kukupeleka kwenye uhuru wa kipato. So kama financial freedom si ndoto yako wala usihofu sana kuhusu haya unayoyasoma hapa. Wewe ambaye unajisemea saivi kuwa cha msingi mkono uende kinywani. Wewe unayedhani uliumbwa ili kupeleka mkono kinywani. Wewe usijali sana kuhusu unayoyasoma hapa. Endelea kuwa na uhakika wa kupeleka mkono kinywani.

But bottomline is...
Kama ulisoma makala zangu hizi toka mwanzo utaanza kuona kuwa zote kuanzia ile ya kwanza hadi hii ya 5 zinafanya kazi kinyume cha MWAJIRIWA. Ziunganishe utaelewa vizuri. Again..Don't read them in isolation.

Na bado zingine 5. Dah siku kweli hazigandi.
Endelea kuwa na mimi.

But kwa leo hicho ndiyo kikwazo cha 5 cha kumzuia mwajiriwa asifikie kamwe FINANCIAL FREEDOM. Ule MTAA WA UHURU (WA KIPATO).
Leo naishia hapa. Kesho kwa neema ya Mungu nitaendelea na LIMITING FACTOR YA SITA.

Kwa maswali. Maoni. Critique. Ushauri. Au kujifunza zaidi nk.
SMS, WhatsApp and Calls: +255752366511
WhatsApp Only: +255788366511
Blog: andreamuhozya.blogspot.com

Barikiwa Sana!

Semper Fidelis my People,

Semper Fi,

Andrea G. Muhozya
Dar es Salaam, Tanzania,
East Africa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni